Posts

Showing posts from June, 2023

USHIRIKISHWAJI WA VIJANA WANAWAKE KATIKA SIASA,NGAZI ZA UONGOZI NA MAAMUZI.

Image
Na Riziki Abdalla KATIKA  karne ya 21, adhma ya kufikia usawa wa kijinsia imekuwa ni agenda inayotiliwa mkazo kimataifa na kitaifa kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika ngazi za uongozi na za maamuzi hususani ndani ya vyama vya siasa.  Takwim u zinaonesha kuwa idadi ya wanawake imekuwa ikiongezeka zaidi kuliko ya wanaume. Katika sensa ya mwaka 2022, Zanzibar ina jumla ya watu 1,889,773  kati ya hao wanawake ni 974,281 sawa na asilimia 52 ya  watu wote. Takwimu hizi zinaonesha kwa kiasi gani suala la kuzingatia ushirikishwaji wa wanawake katika mambo ya maamuzi na uongozi ni jambo lisiloweza kuepukika.  Pamoja na uwepo wa idadi kubwa ya wanawake bado ushiriki wao katika ulingo wa uongozi umekuwa ni mdogo sana , ila dhana hii imeanza kufanyiwa mageuzi makubwa kupitia Jimbo la Fuoni Katika Jumuiya Ya Umoja Wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kuwa na idadi kubwa ya viongozi wanawake hususani katika nafasi ya katibu kuanzia matawi, wadi ...

WANAWAKE PEMBA WAASWA KUJIKOMBOA KICHUMI KUPITIA BIASHARA YA UREMBO SALUNI.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA,     0719859184  WANAWAKE Kisiwani Pemba Wameaswa kuzichangamkia Fursa zinazopatikana kupitia  Biashara ya  Urembo,  ili kuweza kujipatia Kipato na kupata fursa za kuwajiri   wengine  kusaidia Serikali kuondokana na  mzigo wa Utegemezi .    Ametoa Ushauri huo Leah Uswage  Stephano  alipokuwa akizungumza na Habari hizi  juu ya Fursa za kujiajiri kupitia kazi ya urembo huko Katika Ofisi  yake  ya Ususi, na urembo wa akina mama   Iliyopo Mtaa Wawi Gereji  Wilaya Chake Chake Pemba.     LEAH USWAGE - MJASIRIAMALI BIASHARA YA UREMBO.   Amesema Bado  wanawake wengi kisiwani Pemba wamekuwa Wakiipuza fursa inayopatikana kupitia Kazi za  Urembo katika Saluni   licha ya kuwa na  Faida Ambazo zinaweza  kuwakomboa  kichumi na kuzalisha fursa nyengine za kuondokana na utegemezi.  Wanawake wezangu Moj...

RASIMU YA KANUNI YA HIFADHI YA JAMII ZSSF SEKTA ISIYO RASMI WADAU WATOA MAONI YAO

Image
Na Amina Ahmed Moh’d, Pemba  KAIMU Mkurugenzi  Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Pemba  Said Maalim Said Amefungua Mkutano wa Siku moja   ambao umejadili Rasimu ya kanuni ya Hifadhi ya Jamii kwa Sekta isiyo juu ya  Kuchangia katika Mfuko  wa hiari  ambao umewashirikisha wadau mbali mbali  kutoka Sekta isiyo rasmi kiswani humo.      SAID MAALIM SAID  - K/ MKURUGENZI ZSSF PEMBA    Akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake Chake  Kaimu huyo amesema kuwa ZSSF itaendelea kupokea na kuyafanyia kazi  mapendekezo ya wadau hao kwa lengo la kuimarisha  Kanuni hiyo ambayo itakapokamlika itakuwa na manufaa zaidi kwa wadau wa sekta hiyo  isiyo rasmi.   Amesema   Serikali inatambua Mchango mkubwa unaotolewa na sekta hiyo   jambo ambalo limepelekea Kuanzisha kwa Mfuko wa uchangiaji wa hiari  ili kuweza k...

ELIMU JUU YA ATHARI ZA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA YAFIKA KWA WANAFUNZI SKULI YA SEKONDARI UWELENI

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA  ZAIDI ya Wanafunzi 200 wa Skuli ya  Sekondari Uweleni Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba  wamefikiwa na kupewa Elimu Juu ya  Sheria, Na Athari mbaya  za Matumizi na Uuzaji wa Dawa za kulevya kutoka kwa Maafisa  kutoka Mamlakaya kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kisiwani humo  Ikiwa   ni muendelezo wa  Shamra  shamra za Kuelekea siku ya Kupiga  vita Biashara  ya Uuzaji na utumiaji wa Dawa za Kulevya inayoadhimishwa kila ifikapo June 26  Duniani kote .  Akitoa Elimu  ya Kisheria kwa Wanafunzi hao  Kamanda Wa Wilaya Kutoka Mamlaka hiyo Ahmed  Khamis Kombo  Amewataka wanafunzi hao kutoa Taarifa kwa Uongozi wa Skuli  kwa wazazi, endapo watabaini kuwepo kwa viashiria vya uuzwaji, Uwepo, pamoja utumiwaji wa Madawa hayo katika maeneo yao yaliyoawazungukua ikiwemo maeneo ya  Skuli .    Kamanda Ahmed Khamis alisema  kuwaambia Wanafunzi hao...

JESHI LA POLISI LAWASHIKILIA WATATU KWATUHUMA ZA WIZI WA SARUJI ZA MIRADI YA SERIKALI USIKU WA MANANE

  NA OMAR HASSAN –  Unguja                                                       Watu watatu wanashikiliwa katika kituo cha Polisi Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja kwa tuhuma za wizi wa saruji paketi 27 iliyokuwa ikitumika katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Mwera Pongwe Wilaya ya Kati.  Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari huko Makao Makuu Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja Kamishna msaidizi wa Polisi ACP GAUDIANUS FELISIAN KAMUGISHA amesema kuwa Juni 18,2023 majira ya saa 07:30 Usiku Askari Polisi wa kituo cha Polisi Tunguu wakiwa katika doria walifanikiwa kuwakamata watu watatu wakiwa na gari Z.350 HH ikiwa imepakia mifuko hiyo ya saruji ambayo inatiliwa mashaka huwa ni ya wizi. Aliwataja watu hao kuwa ni Saleh Ali Bakar (25)   ambae ni dereva wa gari hiyo ,Seif Khamis Mati (2...

WATENDAJI WIZARA YA KILIMO PEMBA WAASWA

Na   ALI MASSOUD KOMBO.  AFISA Mdhamin wizara ya Kilimo Pemba,  Inginia IDRIS HASSAN ABDULLAH, amewataka watendaji wa wizara yake kuwajibika vyema katika nafasi zao pamoja na kusimamaia nidhamu za wanaowaongoza,ili kufikia malengo ya taasisi. Afisa mdhamin Inginia  Idris ameyasema hayo wakati wa kikao cha kawaida pamoja na  wakuu wa maidara na vitengo mbali mbali vya wizara ya kilimo kilichofanyika katika Afisi za wizara hiyo Weni, Wete Pemba. Aidha IDRIS, amekemea ukataji wa miti ovyo usiozingatia uhifadhi wa mazingira na kuwahimiza watendaji wake kusimamia sheria zilizopo katika kuilinda rasilimali za misitu nchini, sambamba na kupiga vita uvunwaji  wa mazao machanga.  Kwa upande wao, watendaji wa wizara hiyo walioshiriki katika kikao hicho walikubali kuwepo kwa mapungu yanayoikabili sekta ya kilimo na hivyo kuahidi kuyafanyia kazi ili kuona Sekta hio inapiga hatua mbele.

WAZIRI TAMISEMI AAGIZA KUSIMAMISHWA KAZI WENGINE KUONDOLEWA WANAOSABABISHA UPOTEVU WA MAPATO.

WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa Serikali za mitaa na Idara Maalum za SMZ, Mh Masoud Ali Mohammed, ameagiza kusimamishwa kazi na wengine kuondolewa, wasimamizi wakuu wa mapato na usafi katika Manispaa na Mabaraza ya miji. Akizungumza katika kikao maalum Afisini kwake Vuga, amesema hatua hiyo ya kuondolewa na kusimashwa kazi kwa wasimamizi hao ni kutokana na serikali kotoridhishwa na hali ya usafi wa mji, na upotevu wa mapato katika mabaraza ya miji Pemba. Agizo jengine la Serikali ni kuondolewa waendesha bodaboda katika maeneo ya michenzani na kuhamishiwa eneo la maegesho maduka mapya darajani Souk, sambamba na kuhamishiwa katika soko la welezo  wafanyabiashara ndogo ndogo maeneo michenzani na mwembetanga. Aidha waziri Masoud ameagiza kwa kamati za ulinzi na usalama za wilaya kusimamia Opersheni maalum za kupambana na kuwadhibiti wahalifu wanaondesha vitendo vya uporaji na kuwajeruhi wananchi wasio na hatia. Katika kikao hicho kilichowashirikisha wakuu wa mikoa, Wakuu w...

MBUNGE AAHIDI KUZIOATIA UFUMBUZI CHANGAMOTO HIZI ZINAZOWAKABILI WANANCHI NDANI YA MUDA MFUPI

Image
Na  -  Abdalla Amour  Mbarouk, Pemba. Mbunge wa bBnge la Afrika Mashariki Tanzania kupitia Chama Cha Wananchi CUF Mashaka Khalfani Ngole ameahidi kuzipatia ufumbuzi baadhi ya kero za skuli ya Msingi Makongeni Mtambwe kusini Mkoa wa Kaskazini Pemba. Ahadi hizo amezitoa wakati alipo guswa na kero za skuli hiyo zilizo wasilishwa kwa njia ya Risala iliyo somwa na mmoja ya walimu wa skuli ya Makongeni mbele ya mbunge huyo alipofika skulini hapo katika ziara yake ya Chama kisiwani Pemba. Katika Risala hiyo imeelezwa kua skuli hiyo imepata mafanikio mengi na makubwa ikiwemo kufaulisha wanafunzi na kuongezeka kwa idadi ya walimu skulini hapo lakini bado inakabiliwa na changamoto kadhaa ambazo hazijapatiwa ufumbuzi  ikiwemo ukosefu wa umeme,uhaba wa madarasa, ukosefu wa huduma ya maji safi, uzio na vifaa vya kisasa kama vile kompyuta na uhaba wa vyoo skulini hapo. Akihutubia baadhi ya wananchi na wanafunzi waliohudhuria mkutanoni hapo mbunge huyo pekee...

YAJUE USIYOYAJUA KUHUSU ALIEKUWA RAIS, CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE KAMPASI YA KARUME .

Image
Na Riziki Abdalla, Unguja.  TUNAPOZUNGUMZIAharakati za mwanamke na uongozi hatumaanishi tu katika nyanja za siasa ama kiuchumi bali pia katika nyanja za kitaaluma ikiwemo shule za msingi, sekondari na hata vyuo vikuu.  Na leo mwandishi wa makala hii anaeleza nadharia finyu zilizozunguka vichwa vya watu wengi wakiwemo wanafunzi wa vyuo vikuu wakidhani ya kuwa mwanamke hawezi kuwa kiongozi katika nafasi ya uraisi eti tu kwa jinsia yake.  Na je? Unajua nadharia hii ilifutwa baada ya chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kampasi ya karume Zanzibar kupata raisi wa kwanza mwanamke na kuleta maendeleo chanya hususani kwa wanawake wenziwe?  “Nilikumbana na kebehi nyingi sana kipindi ambacho nilitia nia ya kugombania nafasi ya uraisi katika chuo changu lakini sikukata tamaa na nilibaki na msimamo wangu’’ alisema Mariam Khamis Abdulla ambae aliongoza chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Zanzibar kwa nafasi ya urais kwa muda wa mwaka mmoja kuanzia 2020 – 2021. M...

ZINA MOLA, USHIRIKA ULIO LETA UKOMBOZI WA MAENDELEO KWA WANAWAKE KIJIJI CHA ZIWANI, FEDHA ZA HAKIBA NA UZALISHAJI WA BIDHAA, BORA KWA MUDA MFUPI TANGIA KUANZISHWA KWAKE.

Image
Na, AMINA AHMED MOH’D - PEMBA      0719859184  WAJASIRIAMALI WA  USHIRIKA wa Kikundi Cha Zina Mola  kikichopo Pembeni ya Muangaza Ziwani wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba  kinachojishughulisha na Usarifu wa Vibdhaa za Udongo  wamesema Kumekuwa na Mafanikio makubwa katika kujikomboa na Umasikini  Tangia kuanzishwa kwa Ushirika huo Mwaka 2020.   Wakizungumza Huko katika Eneo lao maalum la kusarifu  Udongo kwaajili ya kutengeneza bidhaa mbali mbali Baadhi ya Wanaushirika huo  Akiwemo Hamida  Juma Amour wamesema kuwa Wanawake wengi wa  kijiji cha Pembeni ya Mwangaza, kwa Asilimia kubwa wakubwa na wadogo kwa sasa wanajishughulisha na kazi hiyo ya ufinyazi, jambo  Ambalo limezaish  ajira kwao na watu wengine na kujipatia kipato. "Wanawake wa kijiji hichi hutumia muda wao mwingi kwa ajili ya kufanya kazi hiyo, ambayo huwapatia kipato cha kuendeleza maisha yao ya kila siku binafsi nimekuwa ...

WANANCHI WAPONGEZA JUHUDI ZINAZOENDELEA KUFANYWA NA SHEHA WAO NI BAADA YA KUPATIWA UFUMBUZI JUU MASUALA YANAYOWAUMIZA VICHWA KILA SIKU KATIKA MAENEO MBALI MBALI YA VIJIJI NA MITAA YAO.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA  WANANCHI Wa  Shehia Ya Wawi  wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Wamempongeza Sheha wa Shehia hiyo kwa Juhudi mbali mbali anazoendelea  kuzifanya kwa wakazi wake ikiwa ni pamoja na Kusaidia kupata Elimu Juu ya Masuala   ya Kisheria jambo ambalo  awali lilikosekekana na kupelekea Kuongezeka kwa changamoto mbali mbali za kijamii Ikiwemo migogoro .   Wakizungumza  na Habari hizi Baadhi ya Wananchi hao Akiwemo Juma Muhammed Tamimu, Fatma Muhammed Abdallah, Raya Khamis Omar pamoja na Khamis Muhammed Khamis  wamesema kuwa  Jitihada hizo Zimekuwa Chachu ya Wananchi mbali mbali katika Shehia hiyo  kuanza kuzitambua Sheria mbali mbali  na kuzitumia katika kutatua changamoto zinapojitokeza kwa Uweledi.    "Kikubwa sisi  wanajamii tuendelee kushirikiana vya kutosha  na sheha wetu tu, Amekuwa mstari wa mbele kuona nakuhakikisha  ile migogoro isiyokwisha  kutokana na...

BIASHARA YA KUKU WA KIENYEJI FURSA VIJANA WAASWA KUCHANGAMKIA

Image
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba   ( (0719859184   MJASIRIAMALI Anaejishughulisha na Ufugaji wa kuku wa kienyeji  Mgogoni  Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba Amina Juma Salum amewaasa vijana na akina mama kutozipuuza fursa za ujasiriamali ambazo huanza na mtaji mfogo badala yake kuziendeleza ili ziweze kuwaletea ukombozi wa kiuchumi.  Ametoa ushauri huo alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa Habari hizi  juu ya Fursa  alizozipata na kuwa msaada kwa wengine  baada ya kuamua kwa  mjasirimali wa Ufugaji wa kuku wa kienyeji kwa kipindi kifupiakiwa ni mnufaika wa mradi wa kunusuru  kaya masikini TASAF chini ya Mfuko wa Maendeleo ya jamii Tanzania.  Amesema ni vyema vijana hususan wanawake kuzitumia fursa  wanazozipata kwa kuanzisha shughuli mbali mbali ikiwemo ufugajii kwa vile waliowengi wamekuwa wakiizembea na kuona haileti tija jambo ambalo ni kinyume na mitazamo yao.  "Fursa yeyote hata ya mtaji wa shili...

UDHALILISHAJI BADO SUALA LINALOPASUA VICHWA VYA WADAU MBALI MBALI PEMBA

Image
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba  WANANCHI wa maeneo ya Mwambe Pemba wamesema bado wanakabiliwa na changamoto kadhaa katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia na ajira za utotoni ni pamoja na muhali na wanajamii kutokuwa na umoja na mashirikiano. Wakizungamza na waandishi wa Habari katika mkutano wa wadau wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji na utumikishwaji wa watoto katika Ofisi za KUKHAWA Chake Chake, wamesema kumekuwepo baadhi ya wanajamii ambao wanashindwa kutoa mashirikiano pindi vinapotokea vitendo viovu jambo ambalo linapelekea kuongezeka kutokea kwa vitendo hivyo. Kwa upande wake mkurugenzi wa jumuiya kupunguza umasikini na kuboresha Hali za wananchi 'KUKHAWA' Hafidh Abdi Said, amesema wameamua kushirikiana na waandishi wa Habari katika mradi wa KATAA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO kwani waandishi wa Habari ni wadau muhimu katika kuibua na kupambana na vitendo vya udhalilishaji na utumikishwaji wa watoto. Nae mratibu wa chama...

KUTANA NA VIJANA WA KIKE WALIYOAMUA KUVUNJA UBAGUZI WA KIJINSIA KATIKA SEKTA YA KILIMO

Image
Na Masoud Juma, Unguja. “KUTOKANA na ukosefu wa ajira, kwa hiyo baada ya kuona fursa ya kilimo na hapo tulikua tushapata mafunzo, tukaamua kujitoa majumbani na kuanza kujikita katika sekta hiyo ili tuweze kupata maendeleo” anasema Subira. Nchini Tanzania sekta ya kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi wake, watu wengi hujiajiri katika sekta hiyo lakini kwa bahati mbaya si wanawake wengi wamejitokeza katika kufanya shughuli za kilimo Marekebisho ya kiuchumi yamesaidia sana kufungua sekta ya kilimo kuanzia kwenye usindikaji, usafirishaji na uuzaji wa bidhaa za kilimo yameifanya sekta hii kukua na kuwa na maslahi makubwa kwa wananchi. Hali imekua tofauti kwa kijana Zainab Zubeir Juma na wenzake kwani wao wameamua kuitumia fursa ya kilimo kama ndio mkombozi wao na Zainab nae amesaidia sana kushawishi wanawake wenzake ambao hawakuwahi kufikiria kujikita katika sekta hiyo kujiunga nae katika shughuli za kilimo na kujipatia kipato. Zainab aliamua kujiingiza katika kikundi kinachojuli...

ALIEKOMBOA WANAWAKE KUTOKANA NA UMASIKINI NI MUANZILISHI WA KIKUNDI CHA “TUPO WENYEWE”.

Image
Na Masoud Juma, Unguja. NI KIPINDI kirefu kilichopita ilikua si rahisi kuona wanawake wakijishughulisha na shughuli zozote za kiuchumi hapa visiwani Zanzibar. Hata baada ya kuanza kuingia kwenye shughuli za kiuchumi bado wanawake hawakuwa katika ajira rasmin, ambapo kwa mujibu wa kituocha taifa cha takwimu ni asilimia sitini ya wanawake wote wanajishughulisha na ajira zisizo rasmin. Katika kuhakikisha kuwa anajikomboa kiuchumi bi Subira Khamis Ali mkaazi wa Bumbwini Misufini aliamua kujishughulisha na kazi za ususi wa mikoba, vipepeo na makawa na kuviuza sehemu mbali mbali zenye uhitaji. Baada ya kuona kuwa anafaidika kwa kiasi na kupata ari na moyo wa upambanaji bi Subira aliamua kuanzisha kikundi cha ujasiriamali cha wanawake ambacho kinajishughulisha na masuala hayo ya ususi kinachojulikana kwa jina la TUPO WENYEWE. Kikundi hicho chenye jumla ya wanachama 12 ambapo makazi yake yapo wilaya ya Kaskazini B kijiji cha Bumbwini Misufini wanasema pamoja na kujipatia kipato lak...

UONGOZI WA DR SAMIA ULIVYOCHANGIA KUTATUA CHANGAMOTO 11 ZA MUUNGANO.AMBAZO ZILIKUWA SUGU

Image
Ushirikiano wa kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar umefanikiwa kuleta mafanikio makubwa katika maeneo tofauti ikiwemo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa. Katika kipindi chote cha ushirikiano huo, serikali hizo zimefanikiwa kusimamia utekelezaji wa mambo ya Muungano kwa ufanisi mkubwa na kwamba hatua hiyo inathibitishwa na mafanikio yaliopatikana kwa kipindi kifupi cha serikali ya awamu ya sita baada ya kuingia kwa uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Najma Murtaza Giga ambaye ni Mbunge wa viti maalum kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa kama kiongozi mwanamke ambaye anayeongoza vikao vya Bunge katika muhimili huo anajitokeza kuonyesha hisia zake zenye imani na uwezo mkubwa wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika eneo la mafanikio la Muungano. Giga ambaye kwa sasa anatumikia kwa kipindi cha pili tangu Bunge la1,  anasema Rais Samia ni m...

WADAU MBALI MBALI WAJADILI RASIMU YA KANUNI ZA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII ZANZIBAR ZSSF JUU YA FAO LA FIDIA YA KUUMIA KAZINIILI KUFANYIWA MABORESHO (SKIMU)

Image
NA- AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.  OFISA  Mdhamini Ofisi ya Rais kazi, Uchumi Na Uwekezaji Pemba Dk Fadhila Hassan Abdalla amefungua Mkutano maalum wakujadili rasimu  ya  Kanuni za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar Zssf juu ya Fao la Fidia ya Kuumia kazini  (SKIMU) Ambao umeshirikisha wadau kutoka Taasisi  Mbali mbali.       Katika Ufunguzi huo Mdhamini Huyo Amewataka Wadau hao kujadilia na kutoa Mapendekezo yao ambayo yatasaidia kuboresha na kuongeza   ufanisi  na uboreshwaji wa huduma bora kwa Wafanyakazi wanapopata dharura hizo za kuumia kazini. Alisema kuwa Lengo la Serikali la kuwajali watumishi wa umma litazidi kufikiwa iwapo wadau hao wataweza kujadili kwa pamoja   na kutoa Mapendekezo ambayo yataboresha huduma hiz za dharura ambazo zimekuwa kilio kikubwa  kwa wafanyakazi  na watumishi ambao wamekuwa wakikosa haki  hiyo ya kulipwa Fidia. Awali  Akizungumza  na wadau hao   Ka...

JUMLA YA VIKUNDI 42 VYA KIJALUBA VIMEPATIWA VITENDEA KAZI KWA AJILI YA KUANZA KWA UTEKELEZAJI WA MRADI

Image
Na- ASHA AHMED    VIKUNDI 42 vya Unguja na Pemba vimekabidhiwa visanduku maalum ambavyo vimekusanya vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuanza rasmi utekeleza wa mradi wa Kijaluba. Akizungumza na wahusika wa vikundi hivyo, mratibu wa mradi huo kutoka TAMWA Zanzibar Nairat Ali, alisema kwa upande wa Unguja wana jumla ya vikundi 20 na kwa upande wa Pemba ni 22 ambavyo awamu hii ya majaribio itakuwa na vikundi 42. Aidha alisema ili kuona kuwa vikundi hivyo vinaendelea kufanya kazi zao walizokusudia katika mradi huo wamekabidhi visanduku kwa ajili ya watu kuanza kuweka hakiba (hisa) ili kuweza kujiimarisha kiuchumi. Alisema katika vitendea kazi vilivyokabidhiwa ni pamoja na kalkuleta ambazo zitawasaidia katika kupanga mahesabu yao, buku kwa ajili ya kuhifadhia taarifa zao, vibuku vidogo vidogo kwa kila mwanachama, na kufuli tatu kwa ajili ya usalama wa kisanduku, mistari, kalamu, wino wa kufutia na muhuri kwa ajili ya kuonesha idadi ya hisa alizonazo mwanachama. Msaidi...

WANANCHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM WASIFIA UWAJIBIKAJI WA DIWANI JIMBO LA CHAMBANI

Image
NA - AMINA AHMED MOH’D, PEMBA  0719859184    MWAKILISHI wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo Amewataka Wanawake  Kuongeza Mshikamano na kuwa kitu kimoja ili kuweza kuitetea Zanzibar  na Kuongeza Ufanisi katika Maendeleo ya Wanawake Na Watoto. Akizungumza na Habari hizi  katika Ukumbi Wa baraza la Mji Chake Mwakilishi huyo Alisema Maendeleo ya Wanawake  Visiwani yanaweza kufikwa Endapo wataendelea kuzidisha mshikamano na kuungana mkono katika  kutafuta Fursa mbali mbali  ambazo zinaweza kuwa Chachu ya kusaidia wengine.  Alisema Wapo ambao wamekubali kujitoa kwajili ya maendeleo  ya Wanawake Wenzao kwa Kutafuta fursa za Uongozi Lakini kutokana na Kuosa Mshikamano  kwa Wanaume ambao huendelea kuwalisha dhana potofu baadhi ya Watu Hupelekea  Kukosa nafasi hizo na kuendelea kubakia kwa wanaume na kushindwa kuzitumia katika Kupata ufumbuzi wa Masuala yanayiwakabili.  "Kuna Dhana hii ambayo  Wanawake wen...

USAWA WA KIJINSIA KWENYE VYOMBO VYA MAAMUZI NDIO NYENZO MAMA YA WANAWAKE NA UONGOZI.

Image
NA , RIZIKI ABDALLA- UNGUJA  "MOJA ya nyenzo mama ya kuwawezesha wanawake katika kufikia asilimia 50 kwa 50 katika harakati za uongozi ni kuwepo na usawa wa kijinsia kwenye vyombo vya maamuzi". Amesema hayo ndugu Khamis Ali Rashid ambae ni Mratibu wa mradi wa kuwainua wanawake kiuongozi (SWIL- Strengthen Women In Leadership) kwa upande wa ZAFELA katika muendelezo wa kuwajengea uwezo wanawake katika masuala ya kiuongozi uliofanyika katika ukumbi wa ZSSF  Kariakoo Mjini Zanzibar. Muendelezo huo umewakutanisha wanawake mbalimbali wa vyama vya siasa vya Zanzibar ikiwemo CCM, CUF, CHADEMA, UDP, ACT WAZALENDO na vyenginevyo kwa lengo la kujadili mikakati na  mbinu mbalimbali za kuweka mazingira rafiki kwa wanawake kushiriki kwenye masuala ya uongozi na demokrasia ili kuweza kufikia malengo yao pamoja na kutathmini changamoto wanazokumbana nazo katika harakati za kujipanga kwenye kuwania nafasi za uongozi na jinsi ya kuzitatua changamoto hizo. "Ni vyema tukajadili k...