WADAU MBALI MBALI WAJADILI RASIMU YA KANUNI ZA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII ZANZIBAR ZSSF JUU YA FAO LA FIDIA YA KUUMIA KAZINIILI KUFANYIWA MABORESHO (SKIMU)

NA- AMINA AHMED MOH’D, PEMBA. 

OFISA  Mdhamini Ofisi ya Rais kazi, Uchumi Na Uwekezaji Pemba Dk Fadhila Hassan Abdalla amefungua Mkutano maalum wakujadili rasimu  ya  Kanuni za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar Zssf juu ya Fao la Fidia ya Kuumia kazini  (SKIMU) Ambao umeshirikisha wadau kutoka Taasisi  Mbali mbali. 
  
 
Katika Ufunguzi huo Mdhamini Huyo Amewataka Wadau hao kujadilia na kutoa Mapendekezo yao ambayo yatasaidia kuboresha na kuongeza   ufanisi  na uboreshwaji wa huduma bora kwa Wafanyakazi wanapopata dharura hizo za kuumia kazini.

Alisema kuwa Lengo la Serikali la kuwajali watumishi wa umma litazidi kufikiwa iwapo wadau hao wataweza kujadili kwa pamoja   na kutoa Mapendekezo ambayo yataboresha huduma hiz za dharura ambazo zimekuwa kilio kikubwa  kwa wafanyakazi  na watumishi ambao wamekuwa wakikosa haki  hiyo ya kulipwa Fidia.

Awali  Akizungumza  na wadau hao   Kaimu Mkurugenzi wa  Zssf Pemba  Said Maalim Said Amesema kuwa Mfuko huo utaweza  kusimamia majukumu yake ya kuondoa  usumbufu  unaowapata wafanyakazi kwa kusimamia  upatikanaji wa Fidia hiyo  kwa Muda na wakati Stahiki iwapo wadau hao  Wataweza kutoa Maoni ya pamoja  katika kanuni hiyo.
 Wakitoa maoni Yao juu ya kanuni hiyo baadhi ya wadau hao Akiwemo, Juma Ali Makame kutoka  Wizara ya Afya kitengo  cha Usalama  kazini, Saida Abdalla Bakari  kutoka Shirika la Bima Zanzibar, Sifuni Ali Juma kutoka mwamvuli wa Asasi za kiraia Pemba  Pacso, Wameomba mfuko huo kurekebisha  mapungufu katika baadhi ya kanuni hizo ikiwa ni pamoja      Kuweka mbinu mbdala za kulinda na kuzuia Ajali, kutolewa fidia ndani ya kipindi cha ugonjwa, Kuiweka   sambamba na kuweka mchanganuo  ambao utaonesha kima cha mwanzo na  ukomo wa fidia  hizo   Sambamba na kuiweka  Kanuni hiyo kuwanufaisha  Wafanyakazi wa  Taasisi binafsi.

 Mkutano  huo Uliofanyika Katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Pemba  Umekusanya wadau   kutoka  wizara ya Afya, Jeshi la Polisi, Wadau kutoka Wizara ya Kazi uwezeshaji,  Wadau wa sheria kutoka Wizara  katiba na Sheria, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Ofisi ya Wakfu na mali ya  amana,    shirikisho la Vyama vya Wafaya kazi pamoja na wakala wa matukio ya huduma Za kijamii Zanzibar ambapo jumla ya kanuni yenye vipengele nane juu ya  rasimu hiyo ya   ya Mafao ya Kuumia kazini ( SKIMU). 
 Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI