UJENZI WA MIUNDO MBINU YA VIWANJA VYA MICHEZO UZINGATIE JINSIA.
NA ASIA MWALIM KATIKA Nchi nyingi siku hizi miundo mbinu ya viawanja vya michezo huzingatia mambo mengi ikiwemo vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji ili watu wa rika zote na jinsia tofauti waweze kuvitumia viwanja hivyo bila ya matatizo. Kwa bahati mbaya hapa kwetu vigezo hivi havijapewa umuhimu unaostahiki kwenye viwanja vidogo vidogo na vinavyotumika kwa ajili ya mazoezi na mechi za kirafiki. Ni hali ya kusikitisha na hili kwa kiasi kikubwa imekua inachangia wanawake na wasichana kujiona wanatengwa na kudhalilishwa na kwamba wanakosa haki zao za kibinaadamu. Zanzibar imebarikiwa viwanja vingi vya michezo mjini na vijijini lakini unapofuatilia kwa karibu utabaini miundo mbinu hiyo sio rafiki kwa watoto wa kike na mara nyengine huwa sababu ya vitendo vya udhalilishaji kwao. WANAFUNZI WA KIKE Ashura Omar Majaaliwa mwanafunzi wa darasa la nne skuli ya msingi Salim Turky, anasema anapenda michezo tofauti ingawa katika mazingira ya skuli ...