Posts

Image
  KUVUNJIKA KWA NDOA NA HATARI ZA WATOTO WA   KIKE KUKATISHA NDOTO ZAO   Na HABIBA ZARALI PEMBA NDOTO za watoto wengi wa kike huanza kujengwa tangu wakiwa wadogo. Wengine hutamani kuwa madaktari, walimu, wanasheria au wataalamu watakaosaidia familia zao na taifa kwa ujumla. Hata hivyo, kwa baadhi ya watoto wa kike, ndoto hizo zimekuwa zikififia na hatimaye kutoweka kutokana na changamoto zinazotokana na kuvunjika kwa ndoa za wazazi wao. Ingawa talaka huonekana kuwa mwisho wa uhusiano wa wanandoa, ukweli ni kwamba athari zake huendelea kuonekana kwa muda mrefu katika maisha ya watoto. Watoto wa kike ndio huonekana kubeba mzigo mkubwa zaidi, wakikabiliwa na hatari ya kuacha shule, kuozeshwa mapema, kukosa malezi bora au kushindwa kufikia ndoto walizojijengea tangu utotoni. Katika Mkoa wa Kaskazini Pemba Wilaya ya Micheweni na maeneo mengine, simulizi za watoto wa kike walioathirika zinaonesha namna migogoro ya kifamilia inavyoweza kubadili kabisa mweleke...

UMUHIMU WA VITUO VYA TUTU KWA MAKUZI YA MTOTO

Image
Katika miaka ya mwanzo ya maisha ya mtoto ndipo msingi mkubwa wa ukuaji wake hujengwa. Mtoto mdogo anahitaji mazingira yatakayomsaidia kukuza akili, afya, hisia na uwezo wa kuwasiliana na watu wanaomzunguka.  Vituo vya TUTU vimekuwa sehemu muhimu katika kuhakikisha watoto wa umri wa awali wanapata malezi na elimu inayowaandaa kwa maisha yao ya baadaye. Najua bado unajiuliza Tutu  ni nini lakini kamwe katika masikio lako sio neon geni TUTU ni kifupi kinachotumika kumaanisha Taaluma ya Uangalizi na Ujifunzaji wa Watoto Wadogo. Vituo vya TUTU ni sehemu maalumu zinazotoa malezi, uangalizi na elimu ya awali kwa watoto wadogo kabla ya kuanza elimu rasmi ya msingi. Vituo hivi vinalenga kumsaidia mtoto kukua vizuri katika maeneo mbalimbali ikiwemo ukuaji wa akili, lugha, afya, hisia, tabia na mahusiano na watoto wengine. Katika vituo vya TUTU watoto hujifunza kupitia michezo, nyimbo, hadithi, mazoezi ya ubunifu na shughuli zinazolingana na umri wao. Lengo kubwa la TUTU ni kuhakikisha ...

IJUWE NAFASI YA BABA NA MSAADA KWA MAKUZI YA MTOTO WA AWALI

Image
NA , Amina Ahmed Moh-d Ikiwa  Dunia inaendelea kuadhimisha siku ya Baba Duniani   , kwa kutambua  mchango wake katika Nyanja zote za maendeleo  ,Makala hii imeona ipo haja ya  kuendelea kuikumbusha jamii ya Zanzibar  Nafasi ya baba katika malezi ya awali ni msingi wa ustawi wa taifa.  Ushiriki wa baba si wa kifamilia pekee iwapo utasimamiwa ipasavyo bali ni bali ni wa kijamii na kitaifa katika maendeleo endelevu yanayotokana na uwekezaji katika rasilimali watu. Miongoni mwa  faida kubwa zinazopatikana katika kesho bora ya mtoto ambayo ndio taifa la kesho iwapo Baba atachangia katika maendeleo ya akili na tabia njema za mtoto, akimfundisha usawa, maadili na nidhamu ni kusirki nae kikamlifu katika makuzi yake  ya awali . Hadi sasa  Zanzibar inaaminika kuwa bado jamii ya akina baba ina uelewa mdogo kuhusu malezi ya awali licha ya kampeni mbali mbali za uhamasishaji kutolewa na wizara ya Afya ZNZ kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa ...

PACSO YATETA NA WANANCHI KOJANI

Image
MTANDAO wa Asasi za kiraia wa Pemba (PACSO) umeandaa mkutano maalumu kwa wananchi wa Kisiwa kidogo cha Kojani wenye lengo la kuiwezesha jamii kupata uwelewa mpana juu ya masuala ya kisheria na haki za binaadamu. Mkutano huo uliowashirikisha wananchi wa Kisiwa cha Kojani umeandaliwa na jumuiya PACSO kwa ufadhili wa shirika la UNDP na kufanyika huko ukumbi wa skuli ya msingi Kisiwani humo. Akizungumza na wananchi Mkurugenzi Mkuu wa PACSO Pemba Mohamed Najim Omar katika mkutano huo alisema, mpango huo una lengo la kuiwezesha jamii kupata ufahamu wa kisheria na haki za binaadamu. "Jamii zetu bado zina changamoto nyingi na baada ya kuliona hili tumeamua kuandaa mpango wa kupita kwenye jamii kutoa taaluma ya kuwawezesha watu ufahamu juu mambo haya, elimu zinatolewa nyingi lakini na sisi pia tumeona kuja haja ya kuwafikia", alisema.  Aidha alisema, kutokana na kujitokeza masuala mbali mbali ya unyanyasaji wa kijinsia, watoto kudhalilishwa, wanawake, watu wenye ulemavu na hata wazee ...

UMUHIMU WA LISHE BORA KWA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO

Image
  Lishe bora ni msingi wa afya na maendeleo ya mtoto. Katika kipindi cha chini ya miaka mitano, mwili na akili hukua kwa kasi kubwa. Tafiti zinaonyesha karibu nusu ya vifo vya watoto hutokana na ukosefu wa lishe bora. Lishe si hiari bali ni uwekezaji wa maisha ya mtoto na jamii.    JEE KWANINI LISHE BORA NI MUHIMU KWA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO?  Ukuaji wa Mwili   Protini, wanga, mafuta, vitamini na madini hujenga mifupa na misuli.   Huimarisha nguvu na uwezo wa mtoto kushiriki michezo.   Maendeleo ya Akili   Chuma, omega-3, vitamini B huendeleza ubongo na uwezo wa kujifunza.   Siku 1,000 za mwanzo ni kipindi cha dhahabu kwa maendeleo ya akili.   Kuimarisha Kinga ya Mwili   Vitamini A, C, D na zinc huimarisha kinga dhidi ya magonjwa.   Lishe duni huongeza hatari ya maradhi ya mara kwa mara.    KUZUIA UTAPIAMLO Utapiamlo hujumuisha:   Upungufu wa virutubishi   Lishe isiyo sah...

Umuhimu wa Lishe Bora kwa Makuzi ya Awali ya Mtoto

Image
  NA,Amina Ahmed    Lishe bora ni msingi wa afya na maendeleo ya mtoto.  Katika kipindi ambacho mtoto yupo chini ya umri wa  miaka mitano, mwili na akili hukua kwa kasi  kubwa, na hatua hii huonekana  ukuaji wa mtoto katika maeneo mbali mbali , afya mwili, pamoja na akili. Tafiti za afya ya jamii zinaonyesha kuwa karibu nusu ya vifo vya watoto chini ya umri wa miaka mitano hutokana na ukosefu wa lishe bora. Lishe si suala la hiari bali ni uwekezaji wa maisha ya mtoto na jamii kwa ujumla.uwekezaji ambao humuandaalia kesho iliyo bora mtoto. JEE  kwanini  Lishe Bora ni Muhimu  kwa Makuzi ya Awali ya  Mtoto?  Ukuaji wa Mwili Protini, wanga, mafuta, vitamini na madini huchangia ukuaji wa mifupa, misuli na viungo. Lishe bora huimarisha nguvu na uwezo wa mtoto kushiriki michezo na shughuli za kila siku.   Maendeleo ya Akili Virutubisho kama chuma, omega-3 na vitamini B huchangia ukuaji wa ubongo na uwezo wa ku...

UJENZI WA MIUNDO MBINU YA VIWANJA VYA MICHEZO UZINGATIE JINSIA.

 NA ASIA MWALIM  KATIKA Nchi nyingi siku hizi miundo mbinu ya viawanja vya michezo huzingatia mambo mengi ikiwemo vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji ili watu wa rika zote na jinsia tofauti waweze kuvitumia viwanja hivyo bila ya matatizo.   Kwa bahati mbaya hapa kwetu vigezo hivi havijapewa umuhimu unaostahiki kwenye viwanja vidogo vidogo na  vinavyotumika kwa ajili ya mazoezi na mechi za kirafiki.   Ni hali ya kusikitisha na hili kwa kiasi kikubwa imekua inachangia wanawake na wasichana kujiona wanatengwa na kudhalilishwa na kwamba wanakosa haki zao za kibinaadamu.   Zanzibar imebarikiwa viwanja vingi vya michezo mjini na vijijini lakini unapofuatilia kwa karibu utabaini miundo mbinu hiyo sio rafiki kwa watoto wa kike na mara nyengine huwa sababu ya vitendo vya udhalilishaji kwao.   WANAFUNZI WA KIKE Ashura Omar Majaaliwa mwanafunzi wa darasa la nne skuli ya msingi Salim Turky, anasema anapenda michezo tofauti ingawa katika mazingira ya skuli ...