Posts

UJENZI WA MIUNDO MBINU YA VIWANJA VYA MICHEZO UZINGATIE JINSIA.

 NA ASIA MWALIM  KATIKA Nchi nyingi siku hizi miundo mbinu ya viawanja vya michezo huzingatia mambo mengi ikiwemo vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji ili watu wa rika zote na jinsia tofauti waweze kuvitumia viwanja hivyo bila ya matatizo.   Kwa bahati mbaya hapa kwetu vigezo hivi havijapewa umuhimu unaostahiki kwenye viwanja vidogo vidogo na  vinavyotumika kwa ajili ya mazoezi na mechi za kirafiki.   Ni hali ya kusikitisha na hili kwa kiasi kikubwa imekua inachangia wanawake na wasichana kujiona wanatengwa na kudhalilishwa na kwamba wanakosa haki zao za kibinaadamu.   Zanzibar imebarikiwa viwanja vingi vya michezo mjini na vijijini lakini unapofuatilia kwa karibu utabaini miundo mbinu hiyo sio rafiki kwa watoto wa kike na mara nyengine huwa sababu ya vitendo vya udhalilishaji kwao.   WANAFUNZI WA KIKE Ashura Omar Majaaliwa mwanafunzi wa darasa la nne skuli ya msingi Salim Turky, anasema anapenda michezo tofauti ingawa katika mazingira ya skuli ...

KIPATO DUNI KWA WANAWAKE KINAZUIA USHIRIKI WAO KATIKA MICHEZO.

  NA ASIA MWALIM  NCHI nyingi duniani zina mabadiliko makubwa katika soka la wanawake ambapo wachezaji wanapata malipo mazuri na kuwafanya kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolipwa vizuri katika soka.   Katika nchi kama marekani kupitia ligi kuu ya soka la wanawake (NWSL) wachezaji wengi wanawake wanapata mishahara inayofikia hadi dola milioni 1 kwa mwaka, lakini kwa soka la wanawake hususan visiwani Zanzibar hali ni tofauti kabisa kwenye suala la malipo.   Hali ya kipato kwa wachezaji wanawake nchini Zanzibar ni mbaya sana huku wengi wakikosa mikataba rasmi na kulipwa kiasi kidogo cha fedha, ingawa Tanzania bara inaonekana kuwa bora kidogo kutokana na uwepo wa ligi kuu ya wanawake inayotoa fursa za kifedha.   Zanzibar ina historia ndefu ya soka lakini soka la wanawake limeanza kupata umaarufu zaidi katika miaka ya hivi karibuni, hivyo kufanya baadhi yao kukosa mishahara na wengine kulipwa kiwango cha chini kabisa.   Kwa mfano wachezaji wengi Zanzibar wanapata...

ATHARI ZA KUTOWASHIRIKISHA WANAWAKE MICHEZO.

ASIA MWALIM  WANASOKA  wengi wanawake kutoka Zanzibar wanatamani kufikia angalau viwango vya wenzao kutoka Tanzania Bara, ambako soka la wanawake linaonekana kufanya vizuri. Mwaka 2016, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilianzisha ligi kuu ya wanawake ambayo imeendelea kufanyika na msimu wa mwisho wa 2023/2024 timu ya Simba Queens waliibuka mabingwa. Ikumbukwe kuwa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni 17 kati ya hayo lengo namba 5 linazungumzia “Usawa wa Jinsia” hii ina maana ya ushirikishwaji na ushirikiano kwenye kufanikisha usawa wa jinsia kwa upande wa wanaume, wavulana wanawake na wasichana. Kutowashirikisha watoto wa kike katika michezo kuna sababisha athari mbaya ambazo zinaweza kudumaza maendeleo yao ya kimwili, kiakili, na kijamii. Ni muhimu kuhakikisha wasichana wanapata nafasi sawa katika michezo ili waweze kufikia uwezo wao kamili. Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania -Zanzibar (TAMWA-ZNZ), ni mmoja wa wadau wanaojaribu kukabiliana na changamo...

MATUMAINI YA WANAWAKE KWENYE MICHEZO YANATEGEMEA MIFUMO SHIRIKIKISHI.

NA ASIA MWALIM MATUMAINI ya wanawake kwenye michezo yanategemea mifumo shirikishi ambayo yanawapa nafasi ya kushiriki kikamilifu, kujifunza na kukua kama wanamichezo “Huwezi kumwambia mgeni apite wakati mlango wa nyumba yako ukiwa umeufunga” Maneno yanapokua asilimia 90 lakini vitendo ni asilimia 0, hatuwezi kusema tuna mifumo Shirikishi ambayo inayowajumuisha wanawake katika maamuzi, mipango, na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za michezo. Ni wakati sasa kwa wadau mbali mbali wa michezo na jamii kushirikiana katika kuweka mifumo shirikishi kwenye sekta ya michezo ili kufikia usawa wa jinsia kwenye michezo. Mifumo shirikishi inatoa matumaini makubwa kwa wanawake katika michezo kwa kuimarisha ushiriki wao, kutoa fursa za maendeleo, na kuboresha mazingira ya ushindani.  Kwa hivyo ni muhimu kuimarisha mifumo hii ili kuhakikisha kwamba wanawake wanaweza kufikia malengo yao katika ulimwengu wa michezo. WACHEZAJI WAKIKE Mchezaji Kidawa Kheri Hamad na kapteni wa timu ya mpira wa miguu y...

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.

Image
 NA ASIA MWALIM  MARA nyingi tumeshuhudia uzinduzi wa mipango mikakati kwenye masuala mbali mbali ikizinduliwa,  lakini ukifatilia kwa karibu utabaini utekelezaji wake haufikii lengo husika.   Kwa kuwa utekelezaji wake hauzingatiwi, huo huwa wakati kwa baadhi ya watu kutokujali kutekeleza yalioelezwa kutokana kutochukuliwa hatua yoyote.   “Huwezi kumwambia mgeni apite wakati mlango wa nyumba yako umeufunga” huu ni wakati sasa serikali, wadau mbali mbali wa michezo na jamii kushirikiana katika utekelezaji wa mpango mkatati jumuishi wa michezo ili kufikia dhana ya kuanzishwa kwake na kila mmoja kunufaika na fursa za michezo.   Kwa muda mrefu kundi kubwa la wanawake na wasichana walishindwa kushiriki michezo ipasavyo kutokana na changamoto kadhaa ambazo hazina usalama kwao kushiriki michezo.   Hali hiyo ni miongoni mwa vikwazo vinavyowakabili baadhi ya wanawake wanaojitokeza kushiriki michezo, hatimae kuvunja ndoto zao ya kuibua vipaji kwa kut...

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Image
NA AMINA AHMED PEMBA. WANANCHI katika  Manispaa ya Mji wa chake chake na Vitongoji vyake walilazimika kuchelewa kakika harakati zao za kujitaftia riziki baada ya usafiri uliozoeleka kwa siku za hivi karibuni wa Bajajj kutoonekana au kuonekana chache kwenye viunga tofauti mapema leo Machi, 6, 2025. Baada ya hali hiyo kushika kasi huku wananchi wakipigwa na butwaa, mnamo Majira ya saa 3 Asubuhi  Gari za Daladala ikiwemo za Ole Kianga kuanza kuchukua Abiria hao na kuanza kuwasafirisha. Hata hivyo wakizumzia kutoonekana katika vijiwe vyao kubeba abiria baadhi ya waendesha Balaji walisema kuwa walilazimika kushiriki katika kikao  cha  dharura  kwa ajili ya kujadili  unyanyasaji wanaopata katika mamlaka za serikali ikiwemo Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kupitia mamlaka ya usafirishaji. Wamesema Mawasiliano na Baraza  MawasilianoJuu kile walichodai kuwa Wamechoshwa na Udhalilishaji wanaofanyiwa na Mamlaka hizo mb...

WAKULIMA KIUYU WALIA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI

Image
Wakulima wa kilimo mseto katika shehiya ya kiunyu Minungwi wamesema baado wamekuwa wakikabiliana na changamoto ya Majichuvi kwenye maeneo mbali mbali katika shehia hio.  Kaulihio imetolewa na Fatma Shabani Mohamed kwaniaba ya wakulima katika shehiya ya kiuyu Minungwini ambaye piya ni Mwalimu   wa Wakulima anaejulikana kama TOT wakati alipokuwa akizungumza na wandishi wahabari juu  ya kutaka kuzifahamu changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabiya ya nchi katika ahehiya hio. Amesema baado wapo wanajamii hawanauwelewa wakutosha juu ya kuzijuwa athari zitokanazo na mabadiliko ya Tabiya ya nchi jambo ambalo linapelekeya kurudishanyuma maendeleo ya wakulima na wanaoishi pembezoni mwabahari. Akizitaja changamoto hizo nipamoja na kupanda kwa Maji chuvi mpaka majumbani ikiwahukoseaha wananchi kwenda kufanya kazi za kujipatia kipato. Nae sheha wa shehiya ya chwale Mchanga Said Salim amesema lichayakutolewa elimu ya kukabiliana na Mabadiliko ya Tabiya ya nchi lakin...