Posts

UMUHIMU WA LISHE BORA KWA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO

Image
  Lishe bora ni msingi wa afya na maendeleo ya mtoto. Katika kipindi cha chini ya miaka mitano, mwili na akili hukua kwa kasi kubwa. Tafiti zinaonyesha karibu nusu ya vifo vya watoto hutokana na ukosefu wa lishe bora. Lishe si hiari bali ni uwekezaji wa maisha ya mtoto na jamii.    JEE KWANINI LISHE BORA NI MUHIMU KWA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO?  Ukuaji wa Mwili   Protini, wanga, mafuta, vitamini na madini hujenga mifupa na misuli.   Huimarisha nguvu na uwezo wa mtoto kushiriki michezo.   Maendeleo ya Akili   Chuma, omega-3, vitamini B huendeleza ubongo na uwezo wa kujifunza.   Siku 1,000 za mwanzo ni kipindi cha dhahabu kwa maendeleo ya akili.   Kuimarisha Kinga ya Mwili   Vitamini A, C, D na zinc huimarisha kinga dhidi ya magonjwa.   Lishe duni huongeza hatari ya maradhi ya mara kwa mara.    KUZUIA UTAPIAMLO Utapiamlo hujumuisha:   Upungufu wa virutubishi   Lishe isiyo sah...

Umuhimu wa Lishe Bora kwa Makuzi ya Awali ya Mtoto

Image
  NA,Amina Ahmed    Lishe bora ni msingi wa afya na maendeleo ya mtoto.  Katika kipindi ambacho mtoto yupo chini ya umri wa  miaka mitano, mwili na akili hukua kwa kasi  kubwa, na hatua hii huonekana  ukuaji wa mtoto katika maeneo mbali mbali , afya mwili, pamoja na akili. Tafiti za afya ya jamii zinaonyesha kuwa karibu nusu ya vifo vya watoto chini ya umri wa miaka mitano hutokana na ukosefu wa lishe bora. Lishe si suala la hiari bali ni uwekezaji wa maisha ya mtoto na jamii kwa ujumla.uwekezaji ambao humuandaalia kesho iliyo bora mtoto. JEE  kwanini  Lishe Bora ni Muhimu  kwa Makuzi ya Awali ya  Mtoto?  Ukuaji wa Mwili Protini, wanga, mafuta, vitamini na madini huchangia ukuaji wa mifupa, misuli na viungo. Lishe bora huimarisha nguvu na uwezo wa mtoto kushiriki michezo na shughuli za kila siku.   Maendeleo ya Akili Virutubisho kama chuma, omega-3 na vitamini B huchangia ukuaji wa ubongo na uwezo wa ku...

UJENZI WA MIUNDO MBINU YA VIWANJA VYA MICHEZO UZINGATIE JINSIA.

 NA ASIA MWALIM  KATIKA Nchi nyingi siku hizi miundo mbinu ya viawanja vya michezo huzingatia mambo mengi ikiwemo vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji ili watu wa rika zote na jinsia tofauti waweze kuvitumia viwanja hivyo bila ya matatizo.   Kwa bahati mbaya hapa kwetu vigezo hivi havijapewa umuhimu unaostahiki kwenye viwanja vidogo vidogo na  vinavyotumika kwa ajili ya mazoezi na mechi za kirafiki.   Ni hali ya kusikitisha na hili kwa kiasi kikubwa imekua inachangia wanawake na wasichana kujiona wanatengwa na kudhalilishwa na kwamba wanakosa haki zao za kibinaadamu.   Zanzibar imebarikiwa viwanja vingi vya michezo mjini na vijijini lakini unapofuatilia kwa karibu utabaini miundo mbinu hiyo sio rafiki kwa watoto wa kike na mara nyengine huwa sababu ya vitendo vya udhalilishaji kwao.   WANAFUNZI WA KIKE Ashura Omar Majaaliwa mwanafunzi wa darasa la nne skuli ya msingi Salim Turky, anasema anapenda michezo tofauti ingawa katika mazingira ya skuli ...

KIPATO DUNI KWA WANAWAKE KINAZUIA USHIRIKI WAO KATIKA MICHEZO.

  NA ASIA MWALIM  NCHI nyingi duniani zina mabadiliko makubwa katika soka la wanawake ambapo wachezaji wanapata malipo mazuri na kuwafanya kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolipwa vizuri katika soka.   Katika nchi kama marekani kupitia ligi kuu ya soka la wanawake (NWSL) wachezaji wengi wanawake wanapata mishahara inayofikia hadi dola milioni 1 kwa mwaka, lakini kwa soka la wanawake hususan visiwani Zanzibar hali ni tofauti kabisa kwenye suala la malipo.   Hali ya kipato kwa wachezaji wanawake nchini Zanzibar ni mbaya sana huku wengi wakikosa mikataba rasmi na kulipwa kiasi kidogo cha fedha, ingawa Tanzania bara inaonekana kuwa bora kidogo kutokana na uwepo wa ligi kuu ya wanawake inayotoa fursa za kifedha.   Zanzibar ina historia ndefu ya soka lakini soka la wanawake limeanza kupata umaarufu zaidi katika miaka ya hivi karibuni, hivyo kufanya baadhi yao kukosa mishahara na wengine kulipwa kiwango cha chini kabisa.   Kwa mfano wachezaji wengi Zanzibar wanapata...

ATHARI ZA KUTOWASHIRIKISHA WANAWAKE MICHEZO.

ASIA MWALIM  WANASOKA  wengi wanawake kutoka Zanzibar wanatamani kufikia angalau viwango vya wenzao kutoka Tanzania Bara, ambako soka la wanawake linaonekana kufanya vizuri. Mwaka 2016, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilianzisha ligi kuu ya wanawake ambayo imeendelea kufanyika na msimu wa mwisho wa 2023/2024 timu ya Simba Queens waliibuka mabingwa. Ikumbukwe kuwa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo ni 17 kati ya hayo lengo namba 5 linazungumzia “Usawa wa Jinsia” hii ina maana ya ushirikishwaji na ushirikiano kwenye kufanikisha usawa wa jinsia kwa upande wa wanaume, wavulana wanawake na wasichana. Kutowashirikisha watoto wa kike katika michezo kuna sababisha athari mbaya ambazo zinaweza kudumaza maendeleo yao ya kimwili, kiakili, na kijamii. Ni muhimu kuhakikisha wasichana wanapata nafasi sawa katika michezo ili waweze kufikia uwezo wao kamili. Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania -Zanzibar (TAMWA-ZNZ), ni mmoja wa wadau wanaojaribu kukabiliana na changamo...

MATUMAINI YA WANAWAKE KWENYE MICHEZO YANATEGEMEA MIFUMO SHIRIKIKISHI.

NA ASIA MWALIM MATUMAINI ya wanawake kwenye michezo yanategemea mifumo shirikishi ambayo yanawapa nafasi ya kushiriki kikamilifu, kujifunza na kukua kama wanamichezo “Huwezi kumwambia mgeni apite wakati mlango wa nyumba yako ukiwa umeufunga” Maneno yanapokua asilimia 90 lakini vitendo ni asilimia 0, hatuwezi kusema tuna mifumo Shirikishi ambayo inayowajumuisha wanawake katika maamuzi, mipango, na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za michezo. Ni wakati sasa kwa wadau mbali mbali wa michezo na jamii kushirikiana katika kuweka mifumo shirikishi kwenye sekta ya michezo ili kufikia usawa wa jinsia kwenye michezo. Mifumo shirikishi inatoa matumaini makubwa kwa wanawake katika michezo kwa kuimarisha ushiriki wao, kutoa fursa za maendeleo, na kuboresha mazingira ya ushindani.  Kwa hivyo ni muhimu kuimarisha mifumo hii ili kuhakikisha kwamba wanawake wanaweza kufikia malengo yao katika ulimwengu wa michezo. WACHEZAJI WAKIKE Mchezaji Kidawa Kheri Hamad na kapteni wa timu ya mpira wa miguu y...

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.

Image
 NA ASIA MWALIM  MARA nyingi tumeshuhudia uzinduzi wa mipango mikakati kwenye masuala mbali mbali ikizinduliwa,  lakini ukifatilia kwa karibu utabaini utekelezaji wake haufikii lengo husika.   Kwa kuwa utekelezaji wake hauzingatiwi, huo huwa wakati kwa baadhi ya watu kutokujali kutekeleza yalioelezwa kutokana kutochukuliwa hatua yoyote.   “Huwezi kumwambia mgeni apite wakati mlango wa nyumba yako umeufunga” huu ni wakati sasa serikali, wadau mbali mbali wa michezo na jamii kushirikiana katika utekelezaji wa mpango mkatati jumuishi wa michezo ili kufikia dhana ya kuanzishwa kwake na kila mmoja kunufaika na fursa za michezo.   Kwa muda mrefu kundi kubwa la wanawake na wasichana walishindwa kushiriki michezo ipasavyo kutokana na changamoto kadhaa ambazo hazina usalama kwao kushiriki michezo.   Hali hiyo ni miongoni mwa vikwazo vinavyowakabili baadhi ya wanawake wanaojitokeza kushiriki michezo, hatimae kuvunja ndoto zao ya kuibua vipaji kwa kut...