Umuhimu wa Lishe Bora kwa Makuzi ya Awali ya Mtoto
NA,Amina Ahmed
Lishe bora ni msingi wa afya na
maendeleo ya mtoto.
Katika kipindi ambacho mtoto yupo chini ya
umri wa miaka mitano, mwili na akili
hukua kwa kasi kubwa, na hatua hii
huonekana ukuaji wa mtoto katika maeneo
mbali mbali , afya mwili, pamoja na akili. Tafiti za afya ya jamii zinaonyesha
kuwa karibu nusu ya vifo vya watoto chini ya umri wa miaka mitano hutokana na
ukosefu wa lishe bora.
Lishe si suala la hiari bali ni
uwekezaji wa maisha ya mtoto na jamii kwa ujumla.uwekezaji ambao humuandaalia
kesho iliyo bora mtoto.
JEE kwanini
Lishe Bora ni Muhimu kwa Makuzi
ya Awali ya Mtoto?
Ukuaji wa
Mwili
Protini,
wanga, mafuta, vitamini na madini huchangia ukuaji wa mifupa, misuli na viungo.
Lishe bora
huimarisha nguvu na uwezo wa mtoto kushiriki michezo na shughuli za kila siku.
Maendeleo ya
Akili
Virutubisho
kama chuma, omega-3 na vitamini B huchangia ukuaji wa ubongo na uwezo wa
kujifunza.
Siku 1,000
za mwanzo (kutoka ujauzito hadi miaka miwili) ni kipindi cha dhahabu kwa
maendeleo ya akili na kinga ya mwili.
Kuimarisha
Kinga ya Mwili
Vitamini
A, C, D na madini kama zinc huimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa ya
utotoni.
Lishe duni hudhoofisha kinga na kuongeza hatari ya maradhi ya mara kwa mara.
Kuzuia
Utapiamlo ambao ni Utapiamlo
ni hali ya kiafya inayotokea pale mtu kukosa lishe bora ya kutosha na
kupelekea :
- Upungufu wa virutubishi (kama protini, vitamini,
madini).
- Lishe isiyo sahihi (kula vyakula visivyo na
uwiano mzuri wa virutubishi).
- Lishe kupita kiasi (kula chakula kingi kisicho
na afya, kinachoweza kusababisha unene kupita kiasi na magonjwa
yasiyoambukiza),utapiamlo ni tatizo la lishe linaloweza kuathiri ukuaji,
afya, na uwezo wa mwili kufanya kazi vizuri jambo ambalo husababisha kudumaa kwa ukuaji na
matatizo yasiyorekebishika baadaye maishani.
Lishe
sahihi husaidia kuepuka udumavu na upungufu wa damu kwa watoto.
|
Aina za Vyakula Bora kwa Watoto wa awali |
||||||||||||||||||||||||||||
|
Inashauriwa kumuandalia chakula cha
Asubuhi mtoto alie chini ya umri wa miaka miatano kama vile ,Uji wa nafaka (mtama, ulezi au
mahindi) uliopikwa kwa maziwa,Tunda moja kama ndizi, embe,papain a matunda
mfano wa hayo.
Huku
Mchana aweze kula vyakula kama vile ,Wali au ugali pamoja na mboga za majani mchicha na nyenginezo),Kipande cha samaki au
nyama ndogo dagaa au supu ya mdagaa samaki kulingana na uwezo wa mlo wa siku. Pamoja na e cha juisi ya
matunda safi.
na kwa wale ambao wanautaratibu wa
kula jioni inashauriwa kwa mtoto
aliechini ya umri wa miaka 5 kula vyakula kama vile Viazi vilivyochemshwa au mikate ya ngano,Mayai au dengu kwa
protini pamoja na Mboga za rangi tofauti (karoti, nyanya, pilipili hoho).
Huku
vitafunwa bora kwa mtoto vibaki kuwa ni
Parachichi,
karanga au maziwa ya mtindi,Matunda madogo kama chungwa au apple.
Ratiba hii inahakikisha mtoto
anapata virutubisho vyote muhimu kwa ukuaji wa mwili, akili pamoja na kinga ya
mwili.
CHANGAMOTO
KWA WALEZI NA WAZAZI
Ukosefu wa uelewa: Wazazi wengi hawana elimu ya
kutosha kuhusu lishe sahihi.
Umaskini: Familia nyingi hukosa uwezo wa
kupata vyakula vyenye virutubisho kamili.
Mila na desturi: Baadhi ya jamii hupuuza ulaji wa
vyakula fulani kwa watoto, jambo linalozidisha utapiamlo.
Lishe bora kwa makuzi ya awali ya mtoto ni nguzo ya afya na maendeleo ya maisha
yake yote kwani inahakikisha ukuaji wa mwili, maendeleo ya akili, na kinga ya
mwili. Familia, jamii na serikali zinapaswa kushirikiana kuhakikisha watoto
wanapata chakula chenye virutubisho kamili.
Kila sahani yenye lishe bora ni
hatua ya kujenga kizazi chenye afya, chenye uwezo wa kujifunza na kuchangia
maendeleo ya taifa.
# Mtoto Kwanza
aminaahmedmohd735@gmailcom
MD digital

Comments
Post a Comment