Posts

Showing posts from July, 2026
Image
  KUVUNJIKA KWA NDOA NA HATARI ZA WATOTO WA   KIKE KUKATISHA NDOTO ZAO   Na HABIBA ZARALI PEMBA NDOTO za watoto wengi wa kike huanza kujengwa tangu wakiwa wadogo. Wengine hutamani kuwa madaktari, walimu, wanasheria au wataalamu watakaosaidia familia zao na taifa kwa ujumla. Hata hivyo, kwa baadhi ya watoto wa kike, ndoto hizo zimekuwa zikififia na hatimaye kutoweka kutokana na changamoto zinazotokana na kuvunjika kwa ndoa za wazazi wao. Ingawa talaka huonekana kuwa mwisho wa uhusiano wa wanandoa, ukweli ni kwamba athari zake huendelea kuonekana kwa muda mrefu katika maisha ya watoto. Watoto wa kike ndio huonekana kubeba mzigo mkubwa zaidi, wakikabiliwa na hatari ya kuacha shule, kuozeshwa mapema, kukosa malezi bora au kushindwa kufikia ndoto walizojijengea tangu utotoni. Katika Mkoa wa Kaskazini Pemba Wilaya ya Micheweni na maeneo mengine, simulizi za watoto wa kike walioathirika zinaonesha namna migogoro ya kifamilia inavyoweza kubadili kabisa mweleke...