IJUWE NAFASI YA BABA NA MSAADA KWA MAKUZI YA MTOTO WA AWALI


NA,Amina Ahmed Moh-d

Ikiwa Dunia inaendelea kuadhimisha siku ya Baba Duniani   , kwa kutambua  mchango wake katika Nyanja zote za maendeleo  ,Makala hii imeona ipo haja ya  kuendelea kuikumbusha jamii ya Zanzibar  Nafasi ya baba katika malezi ya awali ni msingi wa ustawi wa taifa.

 Ushiriki wa baba si wa kifamilia pekee iwapo utasimamiwa ipasavyo bali ni bali ni wa kijamii na kitaifa katika maendeleo endelevu yanayotokana na uwekezaji katika rasilimali watu.

Miongoni mwa  faida kubwa zinazopatikana katika kesho bora ya mtoto ambayo ndio taifa la kesho iwapo Baba atachangia katika maendeleo ya akili na tabia njema za mtoto, akimfundisha usawa, maadili na nidhamu ni kusirki nae kikamlifu katika makuzi yake  ya awali .

Hadi sasa  Zanzibar inaaminika kuwa bado jamii ya akina baba ina uelewa mdogo kuhusu malezi ya awali licha ya kampeni mbali mbali za uhamasishaji kutolewa na wizara ya Afya ZNZ kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa malezi na makuzi ya awali kwa mtoto.


Shirika la kuhudumia watoto duniani  UNICEF linasisitiza siku 1,000 za mwanzo wa maisha ya mtoto kuwa kipindi muhimu zaidi, ambapo asilimia 80 ya ukuaji wa ubongo na mwili hukamilika.

Mpaka sasa Ukuaji wa watoto Zanzibar umefikia asilimia 47 ikilinganishwa na asilimia 51 Tanzania Bara, ikionyesha pengo linalohitaji juhudi za baba na mama kwa pamoja katika makuzi yake ya awali yenye mustakabali mzima wa makuzi bora kwa maendeleo yake .

Dira ya Maendeleo 2050 imeweka rasilimali watu kama nguzo kuu ya maendeleo hivyo rasilimali hiyo inahitaji maandalizi kuanzia hatua za awali za rasilimali hiyo ya mtoto  ambae ndio  rasilimali mtu.

 Ushiriki wa baba katika malezi unahusiana moja kwa moja na malengo ya kupunguza umasikini, kuongeza elimu bora na kujenga taifa lenye ustawi wa kijamii na kiuchumi. Malezi bora ya awali yanahakikisha Zanzibar inafikia hadhi ya hatuta kubwa  ifikapo mwaka 2050 kwa kujenga kizazi chenye afya na maarifa kitakachosaidia taifa hapo baadae.

Changamoto zinazokwamisha ushiriki wa baba ni pamoja na mila na desturi zinazomfanya baba aonekane kama mtoaji wa mahitaji pekee, ratiba za kazi zisizotabirika na ukosefu wa elimu kuhusu umuhimu wa nafasi ya baba, pamoja na migogoro ya kifamilia inayopunguza uwepo wa baba katika maisha ya mtoto.

Mapendekezo ya kuimarisha nafasi ya baba ni pamoja na elimu ya malezi kwa jamii nzima ili kubadilisha mtazamo wa kijamii, sera za kazi rafiki kwa familia zinazomruhusu baba kushiriki kikamilifu katika malezi, kampeni za kitaifa zinazosisitiza usawa wa majukumu ya malezi kati ya baba na mama, na ushirikiano wa taasisi za dini na jamii kuhamasisha baba kushiriki katika makuzi ya awali.

Nafasi  ya baba katika malezi ya awali ya mtoto Zanzibar ni nguzo ya ustawi wa taifa , Ushiriki wake huongeza ukuaji wa kihisia, kijamii na kielimu wa mtoto na kuchangia moja kwa moja maendeleo yake.

Kila baba ana wajibu wa kushiriki kikamilifu katika malezi ya mtoto wake, Ushiriki huu si wa kifamilia pekee, bali ni mchango wa kijamii na kitaifa. Baba anayeshiriki hujenga mtoto mwenye kujiamini, mwenye ustawi wa kihisia, na mwenye nidhamu na maadili bora.

Siku 1,000 za mwanzo za maisha ya mtoto ni kipindi cha dhahabu, Baba akishiriki kikamilifu, mtoto hukua kwa afya njema na maarifa thabiti. Ushiriki wa baba ni uwekezaji wa taifa, unaosaidia kufanikisha malengo ya Dira ya Maendeleo 2050 kwa kujenga kizazi chenye elimu, afya na maadili.

 Malezi si jukumu la mama pekee. Ushiriki wako ni wajibu wa heshima na ni urithi wa kizazi chenye ustawi wa kijamii na kiuchumi ni maneno ya Ali yahya Omar,mkaazi wa wawi  ambae alizungumza na mwandishi wa habari hizi ikiw a ni maoni maalum katika siku ya baba duniani 



#Mtoto Kwanza

 

Comments

Popular posts from this blog

UHABA WA VITUO VYA POLISI WILAYA YA CHAKE CHAKE BADO MLIMA MREFU KUDHIBITI UHALIFU VITENDO VYA UDHALILISHAJI NA UVUNJIFU WA HAKI ZA BINAADAMU.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.