RASIMU YA KANUNI YA HIFADHI YA JAMII ZSSF SEKTA ISIYO RASMI WADAU WATOA MAONI YAO

Na Amina Ahmed Moh’d, Pemba

 KAIMU Mkurugenzi  Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Pemba  Said Maalim Said Amefungua Mkutano wa Siku moja   ambao umejadili Rasimu ya kanuni ya Hifadhi ya Jamii kwa Sekta isiyo juu ya  Kuchangia katika Mfuko  wa hiari  ambao umewashirikisha wadau mbali mbali  kutoka Sekta isiyo rasmi kiswani humo. 
   SAID MAALIM SAID  - K/ MKURUGENZI ZSSF PEMBA 

 Akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake Chake  Kaimu huyo amesema kuwa ZSSF itaendelea kupokea na kuyafanyia kazi  mapendekezo ya wadau hao kwa lengo la kuimarisha  Kanuni hiyo ambayo itakapokamlika itakuwa na manufaa zaidi kwa wadau wa sekta hiyo  isiyo rasmi. 

 Amesema   Serikali inatambua Mchango mkubwa unaotolewa na sekta hiyo   jambo ambalo limepelekea Kuanzisha kwa Mfuko wa uchangiaji wa hiari  ili kuweza kuwasaidia kufaidika na hifadhi inayotolewa. 

 "ZSSF imetayarisha hii kanuni ili kuona vipi itasaida kuboresha na kuwapa fursa wenzetu ambao hawapo katika mfumo rasmi  waweze kufaidika katika sekta hii, hivyo kutoa  kwenu, Michango itakayosaidia kuboresha kutasaidia kuwawezesha Kuchangia katika mfuko wa hiari  ambao utawasaidia kunufaika na kupata faida mbali mbali kma wadau wa sekta Binafsi". 

Amesema Lengo la Serikali ni kuwezesha watumishi wa Sekta isyo rasmi  kuingia na kujiunga katika Mfuko wa kuchangia kwa hiari Wa ZSSF na kuweza kufaidika katika mambo mbali mbali. 

"Serikali  inatambua Mchango wa Wadau binafsi katika Maendeleo ya Taifa, Mh Rais anasema kila siku Jinsi gani tutaweza Kuwainua wenzetu wa sekta Zisizo rasmi ambao zaidi ya Asilimia 60  waajiriwa wake ni  wengi  jambo ambalo limepelekea   kuwaangalia kwa jicho la karibu zaidi kwa vile wanafanya kazi kubwa kwa Serikali".
 
 Kwa upande wake   Mtendaji wa Mfuko wa Hiari ZSSF Rajab  Haji Machano amesema kuwa lengo la Kukusanya Maboresho kutoka kwa Wadau hao ni kutekeleza Ahadi ya Serikali juu ya kutoa Hifadhi  ya jamii kwa watu wote  na kuweza kufaidika na mfuko Huo. 

"Kama ambavyo  wenzetu ambao ni wafanyakazi waliomo katika sekta Rasmi ambao wanatambulika na Mfuko huu na kufaidika nao katika mambo mbali mbali  ikiwemo  kupata Pencheni ya ustaafu, Mikopo ya Elimu na faida nyengine mbali mbali ndivyo ambavyo tunataka sekta isiyo rasmi nayo iweze kufaidika kutokana na kazi kubwa wanayoifanya. 

Akipokea Maoni ya maboresho kutoka kwa wadau hao mara baada ya kuwasilisha  rasimu  hiyo yenye Sehemu 12  Mwanasheria kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF Daud  Juma  Sleiman Amesema kuwa ZSSF itayafanyia kazi Mapendekezo ya maboresho hayo yaliotolewa   ili kuweza kuongeza tija kwa watumishi wa sekta isiyo rasmi. 

Wakitoa  maoni Yao juu ya kanuni hiyo baadhi ya wadau hao Akiwemo, Fatma Maruzuku Khamis, Asila Omar Sleiman Pamoja na Ulfat Sultan Yussuf wameuomba Ungozina Usimamizi wa mfuko huo wa hiari kuendelea kutoa Elimu kwa vijana  Katika Maeneo mbali mbali ili kuweza kufikia malengo yaliokusudiwa katika kuwasaidia wafanyakazi wa sekta isiyo rasmi. 
"Vijana wengi mitaani wamejiajiri  wenyewe kwa kufanya shuguli mbali mbali kuna wanaoendesha boda boda wanaouza biashara ndogo ndogo na wengine wengi, Ili kuona na wao wanakuwa wanufaika wa kuchangia mfuko huu wa hiari naiomba ZSSF Iwafikie kuwapa Elimu hii  waliwengi huko mitaani hawajui kama kuna fursa hii yenye faida kwao, na wao kuweza kujua lakini pia kuweza kutoa maoni yao wasikose fursa hii "

Kanuni ya Rasimu hiyo  ya Hifadhi ya jamii kwa Sekta isiyo rasmi imejadiliwa na kutolewa Mapendekezo ya Maboresho na Wadau mbali mbali  kutoka  Sekta isiyo Rasmi ikiwa ni pamoja na Wanasheria wakujitegemea, Wajasiriamali, pamoja na wafanyakazi kutoka Sekta mbali mbali zisizo rasmi kisiwani Pemba . 

Mwisho
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI