WANANCHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM WASIFIA UWAJIBIKAJI WA DIWANI JIMBO LA CHAMBANI

NA - AMINA AHMED MOH’D, PEMBA  0719859184 

 MWAKILISHI wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo Amewataka Wanawake  Kuongeza Mshikamano na kuwa kitu kimoja ili kuweza kuitetea Zanzibar  na Kuongeza Ufanisi katika Maendeleo ya Wanawake Na Watoto.

Akizungumza na Habari hizi  katika Ukumbi Wa baraza la Mji Chake Mwakilishi huyo Alisema Maendeleo ya Wanawake  Visiwani yanaweza kufikwa Endapo wataendelea kuzidisha mshikamano na kuungana mkono katika  kutafuta Fursa mbali mbali  ambazo zinaweza kuwa Chachu ya kusaidia wengine.

 Alisema Wapo ambao wamekubali kujitoa kwajili ya maendeleo  ya Wanawake Wenzao kwa Kutafuta fursa za Uongozi Lakini kutokana na Kuosa Mshikamano  kwa Wanaume ambao huendelea kuwalisha dhana potofu baadhi ya Watu Hupelekea  Kukosa nafasi hizo na kuendelea kubakia kwa wanaume na kushindwa kuzitumia katika Kupata ufumbuzi wa Masuala yanayiwakabili. 

"Kuna Dhana hii ambayo  Wanawake wenyewe tumekuwa tukiiamini Kwamba hatupendani Jambo Ambalo  Naamini ni njama tu kutumika hii dhana  Lakini haina ukweli hivyo Wanawake Wenzangu niwaase Mashirikiano  katika Kuona Tunakuwa Wengi Katika Uongozi nyanja mbali mbali ili tujiletee Maendeleo. 

 Aidha Amewataka Wananchi Wa Jimbo la Chambani Kuendelea Kutoa Mashirikiano katika Kuzipatia Ufumbuzi Changamoto mbali mbali. 

 "Changamoto Nyingi Wananchi ndio ambao wanazijua Mashirikiano ambayo wananendelea kunipa kaika kuzioatia Ufumbuzi kama ambavto niliwaahidi, Niwatake Wasichoke bali wazidiahe Kuziibua na Kunifikishia Ili kuona tunazipatia Suluhu. 

 Wakizungumza na Habari hizi Baadhi ya Wananchama wa chama cha Mapinduzi CCM  Akiwemo Halima Juma Diwani Wamesema  Utendaji wa  Mwakilishi huyo katika  kusaidia Maendeleo na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo la Chambani ni wakupigia Mfano na kuigwa na Viongozi wengine. 

 "Tunapopokea au kuona taarifa za utekelezaji wa Ahadi  Kwa Viongozi wetu katika Majimbo tunakuwa Tunafarijika kwa sababu hiyo ndio nia Thabiti Ya Chama katika Kuona Wananchi waapata Maendeleo, na  Miongoni mwa Wawakilishi ambao Wanaiendea haki nafasi yao kwa kusaidia wananchi ni Mh Bahati. 

 Miongoni mwa Changamoto zilizopatiwa ufumbuzi na Mwakilishi hiyo jimboni kwake ni Pamoja na Maendeleo ya Elimu , Afya, Pamoja na Huduma ya Maji. 

Mwisho. 
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI