WANAWAKE PEMBA WAASWA KUJIKOMBOA KICHUMI KUPITIA BIASHARA YA UREMBO SALUNI.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA,     0719859184


 WANAWAKE Kisiwani Pemba Wameaswa kuzichangamkia Fursa zinazopatikana kupitia  Biashara ya  Urembo,  ili kuweza kujipatia Kipato na kupata fursa za kuwajiri   wengine  kusaidia Serikali kuondokana na  mzigo wa Utegemezi . 

  Ametoa Ushauri huo Leah Uswage  Stephano  alipokuwa akizungumza na Habari hizi  juu ya Fursa za kujiajiri kupitia kazi ya urembo huko Katika Ofisi  yake  ya Ususi, na urembo wa akina mama   Iliyopo Mtaa Wawi Gereji  Wilaya Chake Chake Pemba.
    LEAH USWAGE - MJASIRIAMALI BIASHARA YA UREMBO. 

 Amesema Bado  wanawake wengi kisiwani Pemba wamekuwa Wakiipuza fursa inayopatikana kupitia Kazi za  Urembo katika Saluni   licha ya kuwa na  Faida Ambazo zinaweza  kuwakomboa  kichumi na kuzalisha fursa nyengine za kuondokana na utegemezi.

 Wanawake wezangu Moja kati ya Fursa  ambayo  imekuwa inaweza kutuingizia kipato ni biashara ya urembo kwa akina mama, kutokana na kuwa suala hilo ni la kila siku kwa rika zote  Tuichangamkie, Tusiibeze, 

"  Ususi wa Nywele, Mitindo mbali mbali, kubandika Wigi Kuweka dawa kufanya usafi wa kucha   Urembo wa Uso, kushonea Mawigi, Kusuka Mabutu, kuweka Dawa za nywele ,Kuchora na Nyenginezo ni Moja kati ya Biashara ambayo licha ya kuwa na  uhitaji mkubwa kwa wakinamama  Kisiwani Pemba Lakini bado fursa hiyo hawajaitumia Kuanzisha Saluni  na kujipatia Kipato.

 Sisi ambao sio wazawa hapa kisiwani Pemba ndio Ambao  Tumekuwa Tukilazimika  Kuziona hizi fursa, Na tunazitumia ipasavyo, tumeajiri na wengine kutoka nje ya Kisiwa hichi Na wao wanaendesha Familia zao kupitia kazi hizi biashara za urembo lakini wazawa bado hawajaona hii fursa. 

 Akizungumza kwa upande wake Tina James Mfanya kazi katika Saluni hiyo ya akina mam Amesema kuwa Kazi hiyo imekuwa msaada mkubwa katika  kuendesha maisha yake. 

"Nakidhi mahitai yangu na wadigo zangu, Natuma Pesa nyumbani Nawasaidia mahitaji mbali mbali Sikubweteka wala sikuogopa kuifata Pemba fursa hii ya Kazi yangu ya Urembo. 

Wakizungumza na habari Hizi Baadhi ya wanachi kisiwani Pemba Akiwemo Omar Khamis Mgando, Pamoja na Ismail khatibu   Wamesema kuwa  Dhana potofu juu ya Biashara ya urembo katika masaluni ndio inayopelekea Wanawake wengi kukosa kuitumia fursa hiyo. 

 Nao Baadhi ya wanawake waliozungumza na habari hizi khadija Seifu Ridhwan Amesema kuwa mara nyingi amekuwa  Anatumia Saluni Kufanya urembo katika nywele zake, na kupata matokeo mazuri. 

 Kupitia Biashara ya Saluni mfanya biashara huyo Amefanikiwa Kumiliki Mafridge 2 ambayo yanahifdhia samaki katika Duka lake  Vitoweo Vya baharini Samaki, kusomesha watoto wake sambamaba na kuendelea kuendesha familia yake kila siku katika mahitaji mbali mbali. 

Mwishi







Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.