WATENDAJI WIZARA YA KILIMO PEMBA WAASWA

Na   ALI MASSOUD KOMBO. 

AFISA Mdhamin wizara ya Kilimo Pemba,  Inginia IDRIS HASSAN ABDULLAH, amewataka watendaji wa wizara yake kuwajibika vyema katika nafasi zao pamoja na kusimamaia nidhamu za wanaowaongoza,ili kufikia malengo ya taasisi.

Afisa mdhamin Inginia  Idris ameyasema hayo wakati wa kikao cha kawaida pamoja na  wakuu wa maidara na vitengo mbali mbali vya wizara ya kilimo kilichofanyika katika Afisi za wizara hiyo Weni, Wete Pemba.


Aidha IDRIS, amekemea ukataji wa miti ovyo usiozingatia uhifadhi wa mazingira na kuwahimiza watendaji wake kusimamia sheria zilizopo katika kuilinda rasilimali za misitu nchini, sambamba na kupiga vita uvunwaji  wa mazao machanga. 

Kwa upande wao, watendaji wa wizara hiyo walioshiriki katika kikao hicho walikubali kuwepo kwa mapungu yanayoikabili sekta ya kilimo na hivyo kuahidi kuyafanyia kazi ili kuona Sekta hio inapiga hatua mbele.

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.