WATENDAJI WIZARA YA KILIMO PEMBA WAASWA

Na   ALI MASSOUD KOMBO. 

AFISA Mdhamin wizara ya Kilimo Pemba,  Inginia IDRIS HASSAN ABDULLAH, amewataka watendaji wa wizara yake kuwajibika vyema katika nafasi zao pamoja na kusimamaia nidhamu za wanaowaongoza,ili kufikia malengo ya taasisi.

Afisa mdhamin Inginia  Idris ameyasema hayo wakati wa kikao cha kawaida pamoja na  wakuu wa maidara na vitengo mbali mbali vya wizara ya kilimo kilichofanyika katika Afisi za wizara hiyo Weni, Wete Pemba.


Aidha IDRIS, amekemea ukataji wa miti ovyo usiozingatia uhifadhi wa mazingira na kuwahimiza watendaji wake kusimamia sheria zilizopo katika kuilinda rasilimali za misitu nchini, sambamba na kupiga vita uvunwaji  wa mazao machanga. 

Kwa upande wao, watendaji wa wizara hiyo walioshiriki katika kikao hicho walikubali kuwepo kwa mapungu yanayoikabili sekta ya kilimo na hivyo kuahidi kuyafanyia kazi ili kuona Sekta hio inapiga hatua mbele.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI