ELIMU JUU YA ATHARI ZA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA YAFIKA KWA WANAFUNZI SKULI YA SEKONDARI UWELENI

NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA

 ZAIDI ya Wanafunzi 200 wa Skuli ya  Sekondari Uweleni Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba  wamefikiwa na kupewa Elimu Juu ya  Sheria, Na Athari mbaya  za Matumizi na Uuzaji wa Dawa za kulevya kutoka kwa Maafisa  kutoka Mamlakaya kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kisiwani humo  Ikiwa   ni muendelezo wa  Shamra  shamra za Kuelekea siku ya Kupiga  vita Biashara  ya Uuzaji na utumiaji wa Dawa za Kulevya inayoadhimishwa kila ifikapo June 26  Duniani kote.

 Akitoa Elimu  ya Kisheria kwa Wanafunzi hao  Kamanda Wa Wilaya Kutoka Mamlaka hiyo Ahmed  Khamis Kombo  Amewataka wanafunzi hao kutoa Taarifa kwa Uongozi wa Skuli  kwa wazazi, endapo watabaini kuwepo kwa viashiria vya uuzwaji, Uwepo, pamoja utumiwaji wa Madawa hayo katika maeneo yao yaliyoawazungukua ikiwemo maeneo ya  Skuli .

   Kamanda Ahmed Khamis alisema  kuwaambia Wanafunzi hao wakike  na Wakiume kuwa " Sheria  ya kudhibiti na kupambana na Dawa za kulevya Zanzibar, ambayo ni sheria namba 8   ya mwaka 2020, 2021,Katika kifungu cha 26 kinaekeza ivi"( Endapo Ndani ya Skuli, ama  Taasisi  nyengine yeyote  au Mazigira ambayo yaeizunguka Taasisi hiyo, ikipatikana Dawa za kulevya, na Endapo watumiaji wa Taasisi hiyo ni watu ambao watakuwa chini ya Umri wa Miaka 18  Adhabu  yake   itakuwa ni kifungo kisichopungua miaka 30, kwa Wasimamizi au wamiliki wa  hizo Taasisi  )  "Jee Wanafunzi mtapenda  kuona  Mwalimu wenu Mkuu anafungwa  kwa kuona  viashiria bila kutoa Taarifa kwenu  kama jibu hapana bhasi niwaase mutoe Taarifa  ili Uongozi wa Skuli  uweze kutoa Taarifa kwa Mamlaka husika. 

 Akitoa Mada juu ya Athari ya matumizi  na Biashara ya Daawa za kulevya   Ali Yussuf Ali  ambae ni Afisa Kutoka Mamlaka hiyo Kisiwani humo  Pamoja na Mambo mengine Aliwataka wanafunzi hao  kuendelea kuchukua Tahadhari  juu ya kadhia mbali mbali za kiafya ambazo zinatokana Matumizi ya Dawa za kulevya. 

 "  Dawa ya kulevya  ya aina yeyote inakuwa na  kemikali ambayo ikiingia katika  Mwili wa binaadamu inakwenda kuathiri  Mwili wa kiumbe hai  na kuharibu mambo yoote ikiwemo fikra mawazo kumbukumbu na mawazo, hata kwa ile ladha tu ni sawa na mtu ambae amewahi kuonja ladha ya embe mbichi au limau   hawezi kuisahau tuiwache ili tujiepushe  na kupata Athari hizo mbaya". 


" Katika mazingira yetu kadhia hizi zipo zimetuzunguka,  wapo ambao  wanaotumia  Madawa haya kutokana na  sababu mbali mbali   Vijana wazee hata Watoto Wakike n, Muelekeo Umebadilika  hawako salama juu ya kadhia hii Madhara yae ni makubwa  tuepuke vishawishi ambavyo  vitatupelekea Kujiungiza huko. "

 Nao  Baadhi ya wanafunzi hao  waliopatiwa Elimu hiyo  Akiwemo Amina Abdalla Shamte, Ramla Halfan Juma, Fathiya Mzee Muhammed, Hasina Muhammed Abdalla pamoja na Adil  Muhammed  Ali  licha ya kupatiwa Elimu hiyi wameiomba Mamlaka hiyo   kuwapatia Ufafanuzi kwa baadhi ya maswali yao ambayoyalikuwa yakiendelea kuwaumiza kichwa kwa kukosa uelewa Wa Elimu ya Madawa ya kulevya,ikiwemo namna gani mamlka hiyo inadhibiti uungiaji  wa madawa ya kulevya. 

Akizungumza kwa niaba ya Uongozi wa Skuli ya  Sekondari Uweleni  Mwalimu Msaidizi wa Skuli hiyo  Kamis Muhammed Ussi amesema Elimu hiyo juu ya Athari za Madawa ya kulevya iliyotolewa kwa wanafunzi hao itasaidia katika kujikinga na kujiepusha na Ushawishi  wa kujiingiza katika kundi hilo. 

"Hii ni Mada kabisa ya somo la civics  Kwa vile imetolewa  kwa uwazi na upana kwa wanafunzi leo kutasaidia kuimarisha na kukuza uelewa wao  Juu ya  kujikinga na Masuala haya ya Madawa, Tumefarijika na tuiombe mamlakaiendekee kutumbuka kwa elimu hii kila baada ya muda. 
     
 Shamra shamra hizo   pia zinaendelea kupita katika Maeneo  ya Shehia mbali mbali kutoa elimu Ambapo awali, Shehia Ya Bopwe wilaya ya  Wete , Skuli ya kengeja,  pamoja na Kutembelea kutoa elimu zaidi kwa Familia ambazo zinawatu wenye uraibu zimefikiwa kuoewa elimu Juu ya  Athari za Matumizi uuzaji   wa Dawa za kulevya kwa kufanya mikutano ya wazi. 

 Mwisho



Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI