WANANCHI WAPONGEZA JUHUDI ZINAZOENDELEA KUFANYWA NA SHEHA WAO NI BAADA YA KUPATIWA UFUMBUZI JUU MASUALA YANAYOWAUMIZA VICHWA KILA SIKU KATIKA MAENEO MBALI MBALI YA VIJIJI NA MITAA YAO.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA 

WANANCHI Wa  Shehia Ya Wawi  wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Wamempongeza Sheha wa Shehia hiyo kwa Juhudi mbali mbali anazoendelea  kuzifanya kwa wakazi wake ikiwa ni pamoja na Kusaidia kupata Elimu Juu ya Masuala   ya Kisheria jambo ambalo  awali lilikosekekana na kupelekea Kuongezeka kwa changamoto mbali mbali za kijamii Ikiwemo migogoro . 

 Wakizungumza  na Habari hizi Baadhi ya Wananchi hao Akiwemo Juma Muhammed Tamimu, Fatma Muhammed Abdallah, Raya Khamis Omar pamoja na Khamis Muhammed Khamis  wamesema kuwa  Jitihada hizo Zimekuwa Chachu ya Wananchi mbali mbali katika Shehia hiyo  kuanza kuzitambua Sheria mbali mbali  na kuzitumia katika kutatua changamoto zinapojitokeza kwa Uweledi. 
 
"Kikubwa sisi  wanajamii tuendelee kushirikiana vya kutosha  na sheha wetu tu, Amekuwa mstari wa mbele kuona nakuhakikisha  ile migogoro isiyokwisha  kutokana na sababu za kutokujua sheria bhasi  Haiendelei ni jambo la kiungwana ambalo ametusaidia na hatutolisahau, "

Tulikuwa tu nalalamika kuona baadhi ya wahalifu ambao tunawapeleka polisi usiku asubuhi wameachiwa Migigoro inaanza, lakini hatukuwa tunajua kama kumbe kisheria kuna haki ya dhaman, a hata kama mtu anaweza akawa muhalifu Tusingeyajua hayo kama wanajamii wa kawaida, na kama sio Sheha wetu  kufanya kazi kubwa ya kutafuta  wanansheria maalum, kuja kutusomesha  sheria Mbali mbali,ikiwemo sheria ya Jinai na Sheria ya Madai na  kupewa elimu  sisi wananchi wake". Alisema Juma Tamimu Mkaazi wa Wawi  Mtaa wa Msikiti kibegi. 

"Tunampongeza sana sana Mh Sheha wetu  Watu wengine wanaona kama hili suala ni dogo lakini kuumiza kichwa na kutaka kujua  kipi kinasababisha Changamoto  kwa wananchi na kutafuta  ( 40 )  wa tatizo linalorudisha nyuma Maendeleo  ni jambo la kuigwa na viongozi  wengine Kabisa.

"Tumeweza kujua mgawanyiko wa sheria mbali mbali zinazotuhusu, Tulikuwa tunakwenda tu kienyeji enyeji hatufahamu vipi Tufuatilie kesi Zetu lakini  Kuoutia yey me tumeweza kujua haki zetu ambazo zinatulazimu kisheria kuzidai  kuzitetea na kuzitafuta Tumefarijika sana" Fatma Muhammed Mkaazi wa  Shehia ya Wawi. 

 Khamis Muhammed Khamis Alieleza kuwa "Binafsi  Mpka umri huu niliofikia sikuwa na uelewa kabisa juu ya Masuala ya Ardhi nilikuwa naishi kibubusa tu kumbe kuna Sheria ya Ardhi  kuna mahali pakupeleka kesi za Ardhi Alichokifanya sheha kwa wananchi ni hazina  ya kuishi kwa kutafuta maendeleo ya kwetu wananchi  tu sio kitu chengine cha kuleta simtofahamu kikaturudisha  nyuma. 

"Tulikuwa tunaona vitu sawa sawa tu hatukuwa tunajua kama kuna sheria ya  Jinai na Sheria ya madai tulikuwa tunaona tumeshafanyia masuala mbali mbali ikiwemo Udhalilishaji tunaona ni kesi moja tu  leo hii watu wa shehia yetu  Takiban waliowengi wamekuwa na uelewa wa kutifautisha  Izo Sheria pia"Raya Khamis Omar. 

Akizungumza na na Mwandishi wa habari hizi sheha wa  wa  Shehia Hiyo Sharifa  Waziri Abdalla amesema kuwa  kutokana na vikwazo vingi ambavyo vilikuwa vinaendelea kumkosesha usingizi akiwa kama kiongozi mkuu wa kuisaidia Serikali Kufikia Maendeleo mbali mbali kwa  Wananchi wake katika Shehia ya Wawi, alibaini kuwa  kukosa Usaidizi  wa kutambua  na kuzitofautisha  Sheria ni moja kati ya Changamoto kubwa ambayo ilikuwa inawakabili wananchi wake. 
  SHARIFA WAZIRI ABDALLA, SHEHA WA SHEHIA YA WAWI 

"Nilipolibaini hilo nikaamua kwa moyo wangu Kujitolea kuisaidia jamii  kupata usaidizi wa kisheria, ndipo nilipoamua kumtafuta Msaidizi wa Sheria  aweze kunisaidia kutimiza hili, Nikaamua kuranda nae mtaa kwa mtaa kutoa Elimu  Kwa Makundi Mbali mbali  na kuwaelimisha juu ya Sheria mbali mbali  na Msaada wa Kisheria na waliowengi walinufaika na Elimu hiyo. "

" Aidha Niliomba Usaidizi maalumu kutoka Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria Chake Chake    kuandaa Mafunzo ya Siku 5  Kwa Gharama Zangu Mwenyewe   Ambayo yatawasaidia wasaidizi wangu kuzidisha Uweledi katika kusaidia Wananchi kupata ufumbuzi wa kisheria ."

Aidha Bi Sharifa alisema kuwa kwa sasa Wananchi waliowengi wamekuwa wakitoa Mashirikiano  mazuri kwa Msaidizi wa Sheria aliepo ndani ya Shehia hiyo katika kupata ufumbuzi wa Masuala mbali mbali. 
 
""Tumewapatia msaada wa kisheria kwa kuwapatia Elimu juu ya sheria mbali mbali ambazo moja kwa moja zimegusa Maisha ya wanajamii, Tumewafundisha  sheria ya Ardhi, Sheria ya mtoto, haki na wajibu  na Sheria mbali mbali za Madai na Jinai engo ni kuona jamii hi ya wawi ambayo wakaazi wake kwa asilimia kubwa ni wagen wa kuingia na kutoka wanaepukana na mizozo. Alisema Haji Nassor Muhammed Msaidzi wa Sheria Wawi. 

 Akizungumzia Suala Mkurugenzi wa Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Chake Chake ambae Pia ni  Kaimu mwenyekiti Bodi ya wadhamini Jumuia hiyo  Kassim  Ali Juma Amesema kuwa"  Sheha wa Shehia ya Wawi ni Shehia Pekee kati ya Shehia 32 zilizopo chake chake kufika katika Jumuia hiyo kuomba  kupatiwa Usaidizi na msaada kwa wananchi wake 

Hakuna  Uongozi wa Shehia hata moja Ukiacha Sheha  wa    Shehia ya Wawi Kuja kuomba Wataalam wa Sheria kuenda kupatiwa Elimu ya Msaada wa kisheria  kwa Wananchi wake yeye ni wa kwaza. 

Aidha Kassim amewaomba Masheha wa shehia nyengine kuiga Mfano huo katika kuona jamii Ya Chake chake inaondokana na Mizozo mbali mbali ya inayohitaji Msaada wa  kisheria.

 Shehia ya wawi  yenye wakaazi zaidi ya 5000  Awali ilikuwa ikikabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo mizozo ya Ardhi, wizi wa mazao na vitendo vya  Udhalilishaj, Mmongonyoko wa Maadili  Ambayo  hutokana  na wananchi waliowengi kushindwa  kupata msaada wa kisheria na kutojua sheria mbali mbali kutokana na Mwingiliano wa mara kwa mara wa wageni kutoka nje ya shehia hiyo kwajili ya kufanya  shuguli Mbali mbali.

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI