Posts

Showing posts from October, 2022

Tutaendela kudhibiti utoro wa skuli za msingi

Na AMINA AHMED MOH’D - PEMBA  Uongozi wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba Umesema utaendelea kulisimamia vyema suala  la utoro  wa  wanafunzi wa skuli za msingi kwa kuendelea kukemea ajira za watoto  wilayani humo ili lisiendelee kujitokeza na kuathiri maendeleo ya elimu kwa watoto na kupelekea kukosa haki yao ya msingi kwa kukatisha masomo Ameyasema Hayo Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni khatib Yahya  Alipokuwa akizungumza na habari hizi juu ya    maendeleo yaliofikiwa katika kuwarejesha skuli wanafunzi watoro wa skuli za msingi zilizomo katika skuli mbali mbali za wilaya hiyo. Amesema  moja kati ya sababu iliyopelekea  kuwepo kwa  utoro wa wanafunzi wa skuli za msingi ktika baadhi ya skuli wilayani humo ni pamoja na ajira za watoto pamoja  kukosa mashirikiano  kwa waza jambo ambalo kwa sasa limepunguwa baada ya kuliwekea mikakati maalum.   "Tatizo kubwa la utoro kwa wanafunzi wa skuli za msingi  Waka...

EPUKANANENI NA MIGOGORO.

NA OMAR HASSAN-   UNGUJA  JAMII IMETAKIWA KUFUATA TARATIBU ZA MANUNUZI YA ARDHI ILI KUEPUSHA MIGOGORO YA ARDHI INAYOSABABISHWA NA MATAPELI WANAUZA ARHI ZA WATU KWA NJIA YA UDANGANYIFU. WITO HUO UMETOLEWA NA KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR HAMAD KHAMIS HAMAD ALIPOKUA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA SHEHIA ZA MWANYANYA, SHARIFUMSA, KIBWENI NA MTONI HUKO UWANJA WA SKULI YA SHARIFUMSA MKOA WA MJINI MAGHARIBI ALIPOKUA AKISIKILIZA KERO ZA UHALIFU KATIKA SHEHIA HIZO.  AMESEMA KUMEKUA NA MATUKIO MENGI YA UTAPELI WA ARDHI KWA BAADHI YA WATU KUUZA ENEO MOJA LA ARDHI KWA WATU ZAIDI YA MMOJA NA BAADHI YA WATU KUUZA ARDHI AMBAZO SIO ZA KWAO KUNAKOSABABISHWA NA KUTOFUATA TARATIBU ZA MANUNUZI. KATIKA HATUA NYENGINE KAMISHNA HAMAD AMEWATAKA WANANCHI KUTOSHAWISHI KUTOA RUSHWA KWA ASKARI WA JESHI LA POLISI KWANI KUFANYA HIVYO NI KUCHOCHEA VITENDO VYA RUSHWA AMBAVYO VINAZUIA UWAJIBIKAJI NA HUKOSESHA HAKI ZA WANANCHI. AIDHA AMEELEZA KUWA ATAENDELEA KUWACHUKULIA HATUA ASKARI WA JESHI LA POLISI WA...

Teknologia ya Habari kuzidi kuimarika Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema ukamilikaji wa ujenzi wa minara 42 ya mawasiliano na vituo 11 vya Teknolojia, Habari,  Mawasiliano (TEHAMA) imefungua ukarasa mpya wa mawasiliano Zanzibar.   Ameyasema hayo leo mara baada ya kufungua kituo Cha TEHAMA kilichojengwa kupitia mfuko wa mawasiliano kwa wote (UCSAF) kilichopo Bwefum Mkoa wa Mjini Magharibi.   Pia, Rais Dk.Mwinyi amezindua mnara wa mawasiliano uliojengwa Kisakasaka wilaya ya Magharibi 'B'.   Rais Dk.Mwinyi  amesema kukamilika kwa vituo hivyo vitasaidia kuchochea ukuaji wa matumizi ya TEHAMA ambayo wananchi wengi watatumia kwenye shughuli za kila siku.   Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo 42 itaondoa malalamiko ya wananchi katika ukosefu wa huduma ya mawasiliano pamoja na kuwepo kwa hali ya usalama na mali za wananchi pamoja na wageni wanaoingia Zanzibar. 

WAANDISHI WAFUNDISHWA MBINU ZA KUJIKINGA NA UHALIFU WA MITANDAONI

Image
NA A-MINA AHMED MOH’D -  PEMBA     Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba wameaswa kuzidisha umakini katika utumiaji wa mitandao ya kijamii  ikiwa ni pamoja na kuweka ulinzi katika utumaji  wa taarifa zao ili zisiweze  kudukuliwa.  Ushauri huo umetolewa na  Mwenyekiti wa Clabu ya waandishi wa Habari ksiwani Pemba Pemba Press Club  Bakar Mussa   Juma  Alipokuwa akifungua mafunzo ya Siku moja ya  Usalama Wa Mitandao (Digital Security) kwa waandishi wa habari wanaotumia zaidi  mitandao ya kijamii   katika kazi zao  yaliofanyika  katika ukumbi wa  ofisi hizo Misufini Chake Chake.           BAKAR MUSSA JUMA- MWENYEKITI CLUB YA               WAANDISHI WA HABARI PEMBA ( PPC).  Alisema   mitandao imekuwa ikipeleka ujumbe  kwa haraka  zaidi  kwa jamii    ukilinganisha na vyombo vyengine...

Tumieni Maji kwa uangalifu

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amewataka Wananchi wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani kuwa na matumizi mazuri ya maji wakati huu wa kiangazi kwa kuwa kina cha maji kwenye chanzo cha Mto Ruvu kimepungua kwa asilimia kubwa.  Makalla akiwa kwenye ziara ya kutembelea chanzo cha maji cha Ruvu juu na chini amesema upungufu wa maji kwenye chanzo cha maji cha Mto Ruvu umesababishwa na ukosefu wa mvua za vuli na uwepo wa kipindi kirefu cha kiangazi.  "Sote tulitarajia kuwepo kwa mvua za vuli kwa kipindi hiki ambazo zingesaidia kuongeza kiasi cha maji kwenye Mto Ruvu na kuwezesha upatikanaji wa maji kwa Wananchi” "Lakini kulingana na utabiri wa Mamlaka ya hali ya hewa ambao ulieleza kuwa kutakuwa na kipindi kirefu cha kiangazi, imesababisha kupungua kwa maji, hivyo kutakwepo na mgao wa maji kwenye maeneo ya mijini”  "Uzalishaji wa maji kwenye chanzo cha Mto Ruvu ni lita milioni 466 kwa siku lakini kwa sasa uzalishaji umepungua mpaka lita milioni 300 sawa na asilimia ...

NABI BADO KOCHA YOUNG AFRIKANS (YANGA)

Image
Habari   Global Publisher  Tanzania  Uongozi wa Yanga unapenda kuwataarifu mashabiki na Wanachama wake kuwa Nasreddin Nabi, bado ni kocha mkuu wa timu yetu. Nabi alijiunga na Yanga April, 2021 na amekuwa na rekodi nzuri ya kuiongoza timu yetu kubeba Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita, bila kupoteza. Akizungumza na YANGA MEDIA, Mtendaji Mkuu wa Yanga, Andre Mtine amewaomba mashabiki na wanachama wa Yanga kufuatilia taarifa za uhakika za timu yao kupitia vyanzo rasmi vya habari vya klabu. “Niwaombe mashabiki na wanachama wetu kuwa na utaratibu wa kufatilia taarifa za klabu yetu kutoka kwenye vyanzo vyetu vya habari. “Tuna YANGA APP. Tuna Website ya Young Africans na kurasa zetu za mitandao ya kijamii ambazo zimekuwa zikitoa taarifa za klabu yetu na kwa wakati sahihi,” alisema Andre. Uongozi unamtakia kila la kheri kocha Nabi na benchi lake la ufundi kwenye maandalizi ya mchezo wa kesho wa Ligi Kuu dhidi ya KMC utakaopigwa saa 1:00 jioni kwenye uwanja wa B...

ZAWA YA WATAKA WANANCHI WALIOLALAMIKA KUKOSA HUDUMA HIYO KUVUTA SUBRA TATIZO LINASHUGHULIKIWA.

NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA  Mamlaka ya maji Zanzibar zawa  kisiwani pemba imesema inendelea na zoezi la usafirishaji wa mabomba   makontena  na  pampu  kutoka kisiwani unguja ili  kupeleka na  kuendeleza harakati  za uboreshaji  na ubdilishaji wa mabomba na mashine  katika baadhi ya maeneo ambayo yanayokosa  pamoja na kupata kwa mgao huduma ya maji .  Mamlaka hiyo imewataka wananchi kisiwani humo kuendelea kusatahimili  kutokana na kukosa huduma ya maji safi na salama katika meneo yao  ambapo imesema mamlaka hiyo inaendelea kulipatia ufumbuzi  suala hilo ili waweze kupata huduma hiyo bila ya usumbufu kama ilivyokuwa awali. Akizungumza na habari hizi  kwa  niaba ya mkurugenzi wa mamalka hiyo kisiwani pemba Ofisa Mahusiano  mamlaka ya maji zawa   Sleiman  Anass Massoud  amesema  mamlaka inaendelea kufuatilia upatikanaji wa mashine   itakayosaidia kufikis...

DIWANI AONDOA KERO YA VYOO SKULI WALIMU WAFURAHISHWA NA HATUA HIYO ALIYOICHUKUA.

Image
NA AMINA MASSOUD JABIR- PEMBA   Hatua zilizochukuliwa na Diwani Mwanamke wa Wadi ya Tibirinzi Chake Chake mkoa wa kusini Pemba kutatua changamoto ya Vyoo pamoja na Barabara kupitia fedha za mfuko wa jimbo katika Skuli ya michakaeni  imewafurahisha wazazi walezi, wanafunzi pamoja na waalimu wa  skuli hiyo     Wamesema hatua hiyo imesaidia kuboresha zaidi elimu na kupelekea maendeleo bora kwa wanafunzi wa jinsia zote kwani hapo awali mahudhurio yalikuwa tofauti kwa wanafunzi wa kiume na wakike waliofikia baleghe huku wanafunzi wenye ulemavu wakipiatia wakati mgumu. Wakizungumza na mwandishi wahabari hizi wanafunzi wenye ulemavu wa viungo  Samir Khamis Juma,  Latifa Haji Faki na wenye Ulemavu wa kuona  Amina Juma Omar na Raudhwat Mohammed AbdulRahman wamesema kutengenezwa kwa barabara kunawasaidia kufika Skuli mapema ukilinganisha na hapo awali. Kwa upande wao wazazi Halima Said Msiuna Hassan Khamis Othman wamesema kutengenezwa ...

Ahukumiwa kwa kumkashifu Rais

Image
 Habari  kwa hisani ya   Millard   Ayo Page  Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Simiyu imemuhukumu kifungo cha miaka saba Mtanzania Levinus Kidanabi (Chief Son's) baada ya kutiwa hatiani kwa makosa matatu ikiwemo kumkashifu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kupitia mitandao ya Kijamii. Mbali na hilo, pia Kidanabi ametakiwa kulipa faini ya Tsh.Mil 15 ambapo hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Matha Mahumbuga. Hakimu huyo amesema kuwa Mtuhumiwa huyo alitoa taarifa ya uongo kinyume cha sheria ya makosa ya kimtandao ya mwaka 2015, ambapo taarifa hiyo aliichapisha kupitia jukwaa la mtandao wa WhatsApp la 'Simiyu Breaking News' #MillardAyo   MAHAKAMANI

POLISI ZANZIBAR IMEWAKAMATA WATU 6 KWA TUHUMA ZA WIZI NA UNYANG'ANYI KWA WATALII NA WENGINE 29 KWA MAKOSA MBALI MBALI

Image
NA OMAR HASSAN NA SAID BAKAR - UNGUJA .         Jeshi Polisi Kamisheni ya Zanzibar linawashikilia watumiwa sita kwa wizi na unyang'anyi wa kutumia silaha za jaji dhidi ya watalii na wengine 29 kwa Makosa  mbali mbali. Hayo yamebainishwa na Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad huko kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja alipokua akisikiliza kero na changamoto za uhalifu za wananchi wa Kijiji hicho. Amesema watuhumiwa hao wamekamatwa kufuatia msako maalumu dhidi ya wahalifu katika maeneo ya kitalii unaoendelea kufanya na Jeshi hilo. Watuhumiwa waliokamatwa ambao wanatuhumiwa kuhusika katika matukio matatu ya kuwaibia wageni na kupatikana na baadhi ya vitu vya wageni ni pamoja na Hamidu Abdalla Hassan miaka 22 mkaazi wa Kibanda maiti, Mtumwa Jumanne Mtumwa miaka 32 wa Nyarugusu na Said Khalfan Said miaka 25  mkaazi wa Kizingo. Wengine ni Khelef Ali Khelef miaka 30 mkaazi Mwera, Mikidadi Ramadhan Idi miaka 45 mkaazi wa Sebleni na Juma Ajuwed...

HALI ZA WAGONJWA WANAODAIWA KULA SAMAKI AINA YA BUNJU ZINAENDELEA VIZURI.

Image
Na AMINA AHMED MOH’D  -PEMBA  Uongozi  wa Hospitali ya Cottage Micheweni  Imesema  Hali ya Majeruhi waliolazwa  wanaodaiwa   kula  chakula cha baharini samaki  kinachodaiwa kuwa  na sumu  zinaendelea  vizuri  sambamba na  kuendelea vyema kupatiwa huduma  za mtibabu ili hali zao ziweze kurejea kama zilivyokuwa awali   . Akizungumza na habari hizi Daktari dhamana hospitali ya Micheweni   Cottage Ali Hamad Sharif amesema kuwa  mpka sasa Hali zinaendelea vizuri licha ya kuwa bado Haijajulikana Rasmi aina ya  chakula na samaki waliokula  Watu saba wa familia moja  hiyo  na  kupata madhara hayo kutokana na  wahusika wenyewe kutoa taarifa za tofauti.    Hali zao mpka sasa zinaendelea vizuri Kwa. sababu wapo ambao alikuja  hawawezi kula lakini sasa wanaweza na huduma  za matibabu zinaendelea ila bado Hatujathibitisha  nakujua ni aina gan...

UHABA WA VITUO VYA POLISI WILAYA CHAKE CHAKE NI SABABU INAYOCHANGIA KUWEPO KWA VITENDO VYA UHALIFU NA UVUNJIFU WA HAKI ZA BINAADAMU .

Image
NA  AMINA AHMED MOH’D - PEMBA.  Chake Chake ni wilaya iliyopo katika  Mkoa wa Kusini Pemba  Zanzibar Tanzania  ambayo kwa mujibu wa sensa ya  mwaka 2012  ina idadi ya wakaazi 97,249 na anuani za makazi  74200 .  Hadi kufikia mwaka huu 2022 wilaya hiyo ina jumla ya shehia 32 ambazo wakaazi  wake hulazimika  kutumia kituo kimoja pekee  cha Polisi   katika kuripoti  matukio mbali mbali ya kihalifu ikiwemo  udhalilishaji, wizi wa mazao  mifugo pamoja na kesi mbali mbali   huku  baadhi ya  wananchi wakikwazika  zaidi kukifikia kituo hicho bila kujua hatima na ufumbuzi wa suala hilo.                              MJI WA CHAKE CHAKE Licha ya baadhi ya  wananchi hao  waliowengi  kuwa  na matumaini  kusogezewa kwa karibu   vituo vya polisi  katika shehia zao....

MASHIRIKIANO KUDHIBITI MAAFA KWA WATOTO YANAHITAJIKA.

Image
NA FATMA SULEIMAN - PEMBA Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mh. Leila Muhammad Mussa amewataka watendaji wa serekali kufanya kazi kwa mashirikiano  Ili kuwaepusha wanafunzi na maafa na kuwaacha  wakiwa katika mazingira salama ya kutafuta elimu. Waziri Lela ameyasema hayo Leo katika ziara yake ya siku moja katika Skuli ya uwandani msingi mara baada ya kutokea tatizo llililoshukiwa Kua lilitokana na wanafunzi kuchezea kemikali ambazo zimeshamaliza Muda wake wa matumizi. Amesema ni wajibu wa Kila mtendaji kusimamia ipasavyo majukumu yake katika kuhakikisha wanaweka mazingira mazuri na ya usalama kwa wanafunzi na kuacha kuwaeka wanajamii katika taharuki . Katika hatua nyengin waziri ameitaka ofisi ya Mkemia Mkuu kuondoa kemikali ambazo zimeshapitwa na wakati Ili kuwaeka wanafunzi katika mazingira salama na kuepusha taharuki kwa wanafunzi hao na jamii kwaujumla. Kwa Upangde wake Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Matar Zahor Masoud Amewapongeza watendaji wa ser...

TUSHIRIKIANE KUTOA TAARIFA ZA UHALIFU.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D   PEMBA Mkuu wa wilaya Ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuendelea kutoa mashirikiano katika kudhibiti vitendo vya uhalifu kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya sheria  husuan ni katika meneo  yenye bandari zisizo rasmi katika wilaya hiyo.  Amesema Mashirikiano wanayoendelea kuyatoa kwa serikali na jeshi la Polisi kuripoti taarifa za kiuhalifu zinazijitokeza imekuwa chachu ya  kudhibiti mali  za serikali zisiuzwe kinyemela ikiwemo Makonyo na karafuu. "Wananchi  wa kaazi  chake chake suala la kupambana na vitendo vya kihalifu  ni suala la kila mmoja wetu sio la serikali peke yake   mashirikiano mnayoonesha kupambana na masuala haya ni vyema tuyaendeleze kutoa taarifa serikali iweze  kuchukua hatua." Aidha aliwataka wananchi wanaokaa katika maeneo  ya bahari kutoa taarifa  za uingiaji wa wageni katika maeneo yao ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.  " wapo...

MJUE MWANAMKE WA KWANZA KUONGOZA KASKAZINI PEMBA HAIJAWAHI KUTOKEA NI IPI SIRI YAKE!.

Image
AMINA AHMED –PEMBA .    “... Mwenyezi Mungu amewaumba kutokana na nafsi moja...” (7:189) Wajibu na majukumu ya mwanamke ni kama ya mwanamume, na suala lake ni kama la mume yaani suala la haki, ujumbe na marejeo. Isitoshe, mustakbali wa kazi yoyote ni dini kwa njia moja au nyengine mwanamke naye ana kazi yake. Kuna kazi zingine ambazo hakuna awezaye kuzisimamia na kuzitekeleza ila yeye, kwa maana hiyo, huwezi kupata harakati zozote zenye kufaulu ila mwanamke atakuwa na fungu lake kubwa humo. “... Lau si waumini wanaume na waumini wanawake...” (48:25) Kazi inayompasa kufanya mwanamke wa kidini siyo zawadi anayopewa na mwanamume (akikataa kumpa, basi) bali ni miongoni mwa haki zake na ni miongoni mwa majukumu yake kwa hiyo ni juu yake atekeleze majukumu yake. Vinginevyo, hatakubaliwa atoe udhuru mbele ya Mwenyezi Mungu na Historia kwamba wanaume hawakumwachia atimize wajibu wake wala hawakumpa kazi ya kufanya kwenye utekelezaji huo. Kwa hivyo ni lazima mwanamke huyo ajihisabu kuw...

RADIO ELIMU KUPATA STUDIO ZAKE MUDA MFUPI KUTOKA SASA.

Image
 Amina Ahmed.  Baada ya  uongozi wahappy radio class kufanya ziara yake katika maeneo ya Mitambo ya radio elimu,  Studio inayotarajiwa kutumika kwa ajili ya kuendeshea shughuli mbali mbali za radio  pamoja na kutembelea  skuli inyotarajiwa  kisiwani pemba na hii ni baada ya kupokea mlalamiko ya kutokusiklikana kwa radio hiyo kisiwani pemba.  Picha za matukio mbali mbali  picha za matukio  Studio ambazo zinatarajiwa kutumika kwa ajli ya radio elimu 

WAATHIRIKA WAKUBWA UKOSEFU WA HUDUMA YA MAJI NI AKINA MAMA BAADHI YA VIJIJI WALIA KUKOSA HUDUMA.

Image
Na AMINA AHMED MOH’D  Wananchi wanalalamika kukosa huduma ya maji safi na salama kwa muda wa miezi mitatu sasa licha ya kufika mmlaka husikakuomba msaada  wa kupatiwa ufumbuzi suala hilo.  Wakizungumza baadhi ya kina mama katika kijiji cha kichanjaani  shehia ya Dodo Pujini wilaya ya mkoani  mkoa wa kusini pemba wamesema kukosa huduma hiyo  kwa kipindi  cha miezi mitatu kumekuwa usumbufu  jambo ambalo hulazimika kusitisha  baadhi y shughuli zao ikiwemo kilimo  .   Akina mama hao wameiomba serikali pamoja na viongozi wao wa jimbo  kuwasaidia kulipatia ufumbuzi    suala hilo ambapo wamesema licha ya kukosa huduma hiyo kwa ajili y shughuli zao lakini pia husababishia usumbufu wa kuifata  masafa ya mbali huduma  hiyo.   " Tunaiomba serikali ituangalie wananchi wake  tunasumbuka  vikuta vya  mifereji vimeshakauka maji tukikosa kupeleka dumu mbili mbli   hapa kwe...