UHABA WA VITUO VYA POLISI WILAYA CHAKE CHAKE NI SABABU INAYOCHANGIA KUWEPO KWA VITENDO VYA UHALIFU NA UVUNJIFU WA HAKI ZA BINAADAMU .

NA  AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 

Chake Chake ni wilaya iliyopo katika  Mkoa wa Kusini Pemba  Zanzibar Tanzania  ambayo kwa mujibu wa sensa ya  mwaka 2012  ina idadi ya wakaazi 97,249 na anuani za makazi  74200 . 

Hadi kufikia mwaka huu 2022 wilaya hiyo ina jumla ya shehia 32 ambazo wakaazi  wake hulazimika  kutumia kituo kimoja pekee  cha Polisi   katika kuripoti  matukio mbali mbali ya kihalifu ikiwemo  udhalilishaji, wizi wa mazao  mifugo pamoja na kesi mbali mbali   huku  baadhi ya  wananchi wakikwazika  zaidi kukifikia kituo hicho bila kujua hatima na ufumbuzi wa suala hilo.
                             MJI WA CHAKE CHAKE

Licha ya baadhi ya  wananchi hao  waliowengi  kuwa  na matumaini  kusogezewa kwa karibu   vituo vya polisi  katika shehia zao. 
" Tuna matumani  na serikali pamoja   na watu wenye uwezo  kutusaidia kutuongezea vituo  wilayani kwetu na kwa vile tukionana na viongozi  tunalalamika   suala hili ni imani yetu watalipa uzito suala hili"Alisema Pascal Mkubwa  mwanaharakati  wa   dini  juu ya kupinga udhalilishaji wa kijinsia. 
Aliendelea kuzungumza  na  habari hizi maalum kuongeza kuwa  
" Tupo tayari kujitolea  nguvu zetu  kufanikisha ujenzi wa vituo vya polisi endapo wadau watajitokeza tupo tayari tushike pauro tubebe mabero   sisi uwezo wa kujenga hatuna lakini uwezo  kujitolea nguvu kusaidia tuko tayari". 

"Suala hili linarudisha nyuma mapambano dhidi ya udhalilishaji  na  Matukio mengi   huishia njiani kutokana na wahusika kuwa mbali na vyombo vya sheria." Alisema  kiongozi huyo mkaazi wa Gombani chake chake. 

 Baadhi ya wananchi wanasema kuwa   umbali huo umbali  wa vituo vya polisi katika maeneo yao ni chanzo cha kufanyika suluhu  na kuishia majumbani baadhi ya kesi za udhalilishaji zinazojitokeza. 

" Suluhu zinapita majumbani  kesi za udhalilishaji lakini ingekuwa vituo vipo karibu   matukio yakitokea yanaripotiwa uongo mtu anogopa kusuluhisha  kwa vile itakuwa tayari ashapeleka kesi  atahofia kumaliza kesi mjumbani lakini saivi mtoto anasoma skuli  kadahlilishwa  kesi hayendi popote anakatishwa masomo anaolewa siku mbili anaudishwa  haki yake ya kusoma ashaikosa na kwa mume hajakaa. alisema  Bi Saumu Ali   mkaazi wa Ole. 

"   Watoto sikuizi  wazazi hawatuogopi tena unamkataza kitu hichi kibaya anafanya hicho hicho   wilaya nyengine zikiona mtoto kawa msugu anapelekwa polisi ijapo kutishiwa kama alikiwa haendi skuli ndio inakuwa dawa anaogopa  kiupande wetu hilo ni gumu tunawaacha tu mana mpka ukifunga safari  kuenda uko kituoni  si leo". 

Tunaibiwa mifugo yetu inachinjwa  usiku   huko huko tulikoilaza  mtu ata akipiga kelele muibaji anaacha kisu  na mapolo apo apo anakimbia  Tusubiri asubuhi tuende Kutoa tarifa polisi  mana uwezo wa kuenda kwa  miguu kutoa taarifa  hatuna  kituo mpka uende chake mjini    ".

" Tunamuomba Rais wetu wa zanzibar atusaidie   kusogeza huduma hizi karibu kutuondolea usumbufu  tunaoupata sisi akina mama  mifugo  yetu inaibiwa tunakosa haki zetu kutokana na kushindwa kufikia kwa wakati sahihi vituoni kutoa taarifa za kuibiwa". 

"Binafsi  mwanzoni mwa mwaka huu nimeibiwa ng'ombe wangu  akachinjwa  lakini  kesi nikaenda polisi siku moja zilizobakia sijaenda kufuatilia mpka kesho  inabaki kumbukumbu tu nilichoka kwenda na kurudi kila siku Nimerudia nyuma kimaendeleo " .

Ni maneno ya bi Asha Bakari Juma mkaazi Wa Kijiji Cha  Simaongwe Shehia ya Mjini Ole wilaya ya chake chake.

 "Haki za binaadamu hazipo  zinakosekana kabisa kuna nyakati tumekuwa tukiogopa hata kukatisha njia na watoto Vurugu za vyombo vya miguu miwili nyakati za jioni na usiku  wale hawana  kofia ngumu, wale wanaendesha wanavyojua" . 

"kwa sababu hakuna polisi vijana  wanapoteza nguvu  ajali barabara  wengine wanakufa wengine wanakatika viungo huku kwetu zaidi, kungekuwepo na kituo hakuna kijana angeendesha chombo ovyo akapita mbele ya kituo anajua atachukuliwa hatua lakini hakuna anafanya anavyojiskia ". 

" Serikali  tunaomba itusaidie huki wesha kuwekwe kituo na sehemu nyengine zenye barabara za ndani  vijana wanapoteza maisha kizembe wallah. 

"Bi Mkasi Haji Mkaazi wa Wesha. Kwa upande wake Mzee Hassan Yakoub alisema kuwa  Baadhi ya vijana wasiopenda amani wamekuwa wakiutumia mwanya huo kufanya vitendo vya uhalifu .

" Wanajua kama kwa mda huu naweza kuiba nikakimbia  bila konekana   na hata nikionekana  ata nikifikishwa polisi sio leo wala kesho naweza nikababaisha  nikaachiwa huru madhali hawakunikamata pale pale".

"Tunaomba  Tusogezewe karibu vituo vya polisi Sababu  vitendo vya  uhalifu vinavunja amani   na  watu hujichukulia sheria mikononi   mwao kwa vile vyombo vya sheria  havipo karibu yao". Alisema  Mzee huyo mkaazi wa ole. 
 
Hemed Abeid Hemed  Ni sheha wa shehia ya Mbuzini wilaya ya chake chake amesema kuwa shehia yake ni moja kati ya shehia ambayo serikali inahitaji kuweka kituo cha polisi  ili kudhibiti usalama wa watu wa aina mbali mbali. 

 "Mbuzini ndio shehia ambayo ina  lango kuu  la kuingilia na kutokea chake chake hapa ndio kuna umuhimi mkubwa wa kuwepo kituo cha polisi kudhibiti uhlifu Tunaiomb serikali na wahisani  itusaidie  suala hili tunataka chake chake ambayo  haina uhalifu". 

Bi mafunda hamad Rubea Sheha wa shehi ya Madungu anasema  Matukio  mengi ya kiuhalifu yanayoripitiwa kwake yamekuwa na urahisi kufikishwa kituoni kutokana na kuwa karibu na kituo hicho kwa upande wake jambo ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa   kupungua kwa vitendo vya uhalifu ikiwemo wizi wa mazao na mifugo. 

"Kesi dha udhalilishaji  zinaporipotiwa  kwangu  dakika tumezifikisha kituoni ufuatliaji unaanza zinapelekwa mahakamani  hazina nenda uje ambayo itawasumbua wananchi wangu labda mtu hna nauli anamudu kuenda kituoni hata kwa miguu ni jambo la kujivuna kuwa karibu na kituo, lakini hata uhalifu  sio mara nyingi kuskia kumeibiwa nguo mara mifugo mara mazao ni vile tu  shehia ipo karibu na kituo cha polisi ". 

kila siku zinavyozidi wakaazi wilaya ya chake chake wanazidi kuongezeka  katika maeneo ya miji na vijiji na hii inasababishwa na  kuwepo kwa mjii mkuu wa kibiashara wilayani humo ambao  takribani wilaya  zote  zilizopo kisiwani Pemba Hulazimika kufuata mahitaji mengi  katika mji huo.

Kwa upande wa Ofisi Ya Mkurugenzi wa Mashtaka  Mkoa wa kusini Pemba  imesema  inapokea  kesi nyingi zaidi za makosa na  vitendo mbali mbali  vya uhalifu h kutoka wilaya ya  Chake Kuliko wilaya ya Mkoani. 

"Wilaya ya Chake tunapokea kesi nyingi zaidi kuliko Wilaya ya Mkoani na zinatokea kesi na jalada linaletwa Ofisini lakini  kutokana na ushahidi kuwa dhaifu tunaelekeza kufungwa kutokana na kukosa ushahidi zipo ambazo Walifunguwa  kshindwa kurudi tena  kufuatilia Zipo kesi ambazo aliefanya kosa hajulikani alieripoti kaja siku moja tu harudi tena". 

"Sababu zinaweza kuwa nyingi zinazopelekea tofauti hiyo kiwilaya kwanza  Wilaya ya Chake ina idadi kubwa ya watu kuliko mkoani lakini Wilaya ya Chake ni Wilaya yenye mji kuliko mkoani, na wilaya zote ambazo zina miji makosa ni mengi kuliko ambazo hazina miji kifupi mjini makosa ni mengi na wahalifu ni wengi". 

Sababu nyengine ni "Wilaya ya Chake ina upungufu wa vituo vya Polisi, kipo kimoja tu tofauti na Wilaya ya Mkoani yenye Vituo vitatu vya Polisi, pia inapelekea kupungua kwa makosa endapo vituo vikiwa karibu na wahalifu kwani huingiwa na hofu lakini pia  Jamii zinazoishi wilaya ya Mkoani wanaishi kijamii kwa maana wengi ni ndugu tofauti na Wilaya ya Chake yenye wahamiaji wengi". Alisema Wakili wa serikali  kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Ali Amour Makame Aliookuwa akizungumza na mwandishi wa makala hii maalumu "

Kwa upande wa jeshi la Polisi  limesema kuwa licha ya changamoto hiyo Hulazimika kutumia   Askari wakaguzi  ambao wamekuwa mbadala wa kuimarisha ulinzi na usalama  katika shehia ambazo zipo mbali na kituo hicho cha polisi" Tunao maafisa wakaguzi kutoka jeshi la polisi  ambao tumewaweka maalum katika  kila  shehia kuona kwamba wanaimarisha  na kutoa mashirikiano   juu ya kutatua changamoto mbali mbali katika kuimarisha ulinzi" 

" Changamoto iliyopo kwa sasa ni uhaba wa askari hao 
jambo ambalo tunalishughulikia  kuona kwamba wanatosheleza kwa vile kutokana na uhaba huo  askari mmoj hulazimika kusimamia shehia zaidi ya tatu".

" Kuhusu Suala la vituo ni jambo la Jamii husika watakapoona kuna ulazima wa kuwepo Jeshi halitosita kupeleka askari vituoni humo ni jambo la kukaa na kujadilina uongozi wa wilaya kuona namna gani wanafanikisha hilo sababu  jukumu letu ni kuimarisha ulinzi na usalama naaskari wetu wapo tayari". 

Alisema  Kamishna Wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad. 

Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake  Abdalla Rashid Ali amekiri na kusema  kuwa Suala la uhaba wa vituo vya polisi katika wilaya yake lipo  ambapo tayari  Umeanza kulifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kulifikisha suala hilo uongozi wa mkoa kujadiliwa zaidi. 

    ABDALLA RASHID ALI - MKUU WA WILAYA YA CHAKE                                          CHAKE PEMBA. 
"Masheha waliowengi  mara kwa mara katika vikao vyetu wamekuwa    wakiliwasilisha   suala hili na wilaya tumeshafanya juhudi za kulifikisha suala hili uongozi wa juu zaidi kupatiwa ufumbuzi ". 

Aidha Mkuu wa wilaya huyo alisema kuwa  kamati ya ulinzi  na usalama ya wilaya inajukumu la kuhkikisha masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo ya utawala yanaimarika mda wote wilaya na mkoa. 

" Wenye dhamana ya usalama  ni wananchi wote kwa ujumla wao licha ya serikali kuweka taasisi za kusimamia masuala ya kiusalama  miongoni mwao ni jeshi la polisi Tunashukuru  jeshi hilo linatoa mashirikiano vizuri katika kudumisha ulinzi  na usalama wa kulinda na mali na raia wake". 

Alisema " kutokana na ukuaji wa miji, na ongezeko la idadi ya watu  kwa wilaya yetu ya chake chake sasa ivi bado tuna kituo kimoja tu cha polisi, katika hatua hiyo miji yetu kutanuka zaidi, watu kuongezeka, harakati za kiuchumi za kijamii pia kukua, ni kiri kuwa kituo hichi hakitoshelezi hivyo  ni wazi kuwa ipo haja ya kuongeza vituo  hivyo ili kudhibiti  zaidi usalama . 

 Alisema kuwa bado uongozi wa wilaya mpaka sasa haujafanikisha suala hilo  la ujenzi  wa vituo vyengine vya polisi katika maeneo mbali mbali ya mji wa chake chake. 

"Tayari ndani ya wilaya yetu tumebahatika kupata barabara kubwa hii yabole kengeja ambayo imekuwa na tija kubwa  na wananchi wameanza kuvutika kuanza kuishi katika ukanda wa barabara hiyo na bado utakuta kutok hapo ole mpka kufika kengeja bado hakuja kuwa na kituo cha polisi ni maeneo muhimu ambayo pia yana umuhimu na ulazima wa kuwepo na  kituo". 

Katika hatua nyengine mkuu wa wilaya huyo Alisema kuwa Serikali ya wilaya tayari imetenga maeneo maalum ambayo itakuwa tayari kuyatumia kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi katika wilaya hiyo endapo serikali itaridhia   na  wadau watajitokeza kujenga vituo hivyo katika wilaya yake. 

 Aidha amesema  uongozi wa wilaya  unaendelea  kuzungumza na wadau na wazalendo wa nchi hii ili kupata msaada wa kujengewa  vituo vya polisi katika badhi ya maeneo muhumu na yenye ulazima wa kuwepo  vituo vya polisi  . 

Tunaendelea vizuri na mazungumzo kwa wadau wanaopenda amani na maendeleo kuona na wao wanatoa nhuvu zao katika kutusaidia jambo hili na mmoja ameahidi  kushirikiana kupata kituo katika maeneo ya wilaya yetu. 

 Aidha Mkuu wa wilaya  amesema kuwa endapo wilaya hivyo itaweza kupata  vituo vingi vya polisi  kutasaidia kudhibiti uhalifu  unaoendelea kutokea katika maeneo mbali mbali. 

" Chake Chake  ina zaidi ya bandari Zisizo rasmi 88  ambazo wahalifu huzitumia  katika  kufanya mambo ya kiuhalifu jeshi la Polisi linaendelea kudhibiti na kukamata  wahalifu wanaotumia  maeneo hayo  lakini endapo kutakuwa na vituo vya uhakika   kutarahisisha zaidi kudhibiti uhalifu". 

"Wezetu wilaya ya Mkoani wana vituo  vingi  hata kasi yao ya kudhibiti vitendo vya kihalifu inaongezeka  maeneo yao ya bandari kuna kituo, Kengeja, Mtambile  na mote humo ukaguzi unakuwa unafanyika mda wote na unazuilika unapotokezea kwa upande wa mashariki kituo kipo karibu  magharibi lakini pia center ya mji kipo kituo karibu,kadhalika wete na micheweni Alisema". 

Alindelea kisema kuwa " Chake Chake ina shehia 32na tunampango wa kuongeza shehia  kituo kipo mjini  lakini kuna maeneo ambayo ufikiaji wake ni mgumu kwa mfano  mgelema,  kilindi Ndagoni ni mbali na yote ni maeneo ambayo ni maeneo ambayo kuna bahari, kote huko kwa umuhimu wake kunastahiki kabisa kuwa na vituo vya polisi  endapo kutakuwa na uwezekano kujengwe vituo itakuwa ni hatua nzuri ya kudhibiti uhalifu usiingie na usitokee katika wilaya. 

 Mkuu wa Wilaya huyo  amewataka wananchi kutosita kuisadia serikali na jeshi la polisi kudhibiti vitendo vya kihalifu badala yake watoe Taarifa   endapo watabaini kuwepo kwa vitendo viovu katika jamii zao.

Aidha Aliwaomba  wadau mbali mbali kujitolea kusaidia kuongeza vituo    vya polisi katika wilaya yake. 

" Tuko Tayari kutoa mashirikiano  kwa yeyote atakaekuwa tayari kusaidia suala hili la ujenzi wa vituo vya polisi katika wilaya yetu ikiwa ni wadau wa kupinga udhalilishaji, kulinda haki za binaadamu watu binafsi kikundi cha watu  taasisi za fedha   na wasamaria wema  wajitokeze kufanikisha  kupunguza changamoto hii lengo ni kuona tunaendeleza mapambano ya kudhibiti uhalifu wa aina mbali mbali. "

Wilaya ya Chake Chake ina shehi 32 Ambazo ni  Shehia ya  Wara, Kichungwani, Chanjaani, Matale,  Kilindi, Kibokoni, Uwandani, Ng'ambwa, Wawi, Mchanga Mrima, Ndagoni, Wesha, Birikau, Madungu, Shungi, Msingini, Chachani, Mgelema,  Tibirinzi, Kwale, Michungwani, Gombani, Vitongoji, Mfikiwa, Mgogoni, Ole, Mjini ole, Mbuzini, Mvumoni, Pujini, Chonga Pamoja na Chanjmjawiri. 
                     MTAA    WA CHACHANI  CHAKE CHAKE 


              MTAA WA  AFRIKANA CHAKE CHAKE 
              MTAA WA     MADUNGU CHAKE CHAKE 
Shehia zote hizo zimekuwa zikiendelea kuishi kwa wasi wasi endapo vitajitokeza viyendo vya kihalifi nyakati za usiku ambapo  Wananchi  wengi wanaoishi   katika baadhi y vijiji vilivyomo  shehia   hizo hushindwa kuripoti matukio ya kiuhalifu huku wengine kuripoti matukio mara moja  bila kuyafuatilia sababu ikiwa  ni umbali wa vituo vya Polisi. 

  Suala hili hupelekea kukosa haki zao muhimu huku watoto  vijana na wanawake  wakiendelea kukosa haki zao muhimu kutikana na kufanyiwa  vitendo vya kikatili ikiwemo udhalilishaji jambo ambalo hupelekea kuvunjwa  sheria mbali mbali ya usalama wao Huku shehia moja ya Madungu  ikibakia kuwa Salama   Juu ya mapamabo dhidi ya uhalifu. 

Mwisho. 

Comments

  1. Ni kweli kabisa Chake chake hilo ni tatizo watu wamekuwa free sana yani ao Boda boda Mati one ndio zaidi Bara bara mpya ndo hakufai kazi wanakata wenzao miguu tu usiku Pujini kwa kupiga misere na mavespa Kijengwe tu .

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI