HALI ZA WAGONJWA WANAODAIWA KULA SAMAKI AINA YA BUNJU ZINAENDELEA VIZURI.

Na AMINA AHMED MOH’D  -PEMBA 
Uongozi  wa Hospitali ya Cottage Micheweni  Imesema  Hali ya Majeruhi waliolazwa  wanaodaiwa   kula  chakula cha baharini samaki  kinachodaiwa kuwa  na sumu  zinaendelea  vizuri  sambamba na  kuendelea vyema kupatiwa huduma  za mtibabu ili hali zao ziweze kurejea kama zilivyokuwa awali   .

Akizungumza na habari hizi Daktari dhamana hospitali ya Micheweni   Cottage Ali Hamad Sharif amesema kuwa  mpka sasa Hali zinaendelea vizuri licha ya kuwa bado Haijajulikana Rasmi aina ya  chakula na samaki waliokula  Watu saba wa familia moja  hiyo  na  kupata madhara hayo kutokana na  wahusika wenyewe kutoa taarifa za tofauti. 

  Hali zao mpka sasa zinaendelea vizuri Kwa. sababu wapo ambao alikuja  hawawezi kula lakini sasa wanaweza na huduma  za matibabu zinaendelea ila bado Hatujathibitisha  nakujua ni aina gani ya samaki wamekula hatujajua bado ni  bunju au ni kasa kwa vile  wanatoa maelezo tofauti  tofauti mara wanasema wamekula samaki mara wamekula maini    ya samaki kwaio tunaendelea na chunguzi kujua ni aina gani . 
 Alisema kuwa  wagonjwa  hao walifikishwa hospitali hapo  mnamo majira ya saa moja za usiku  wa kuamkia leo   baada ya kuhofia kula na uhisi mabadiliko ya afya zao tangia Saa saba za mchana. 

" Tumewapokea Wagonjwa hawa saa  moja na nusu  za usiku  walipata dalili  za kizungu zungu, kutapika, na wakajitafutia huduma ya mwazo wakiwa majumbani mwao   na katika hao watu saba walikuwa wanawake wawili na wanaume watano wote wa familia moja baba mama na watoto wake".

Daktari huyo Aliendelea kusema kuwa  Licha ya hali za wagonjwa hao kuendelea vizuri lakini wapo ambao kati yao hali zao bado   hazijatengamaa vyema  kutokana na wengine  hao kufika  hospitali hapo wakiwa  tayari wameishiwa  nguvu kutokana na  kutapika  sana pamoja na kulalamika kuumwa na viungo. 

   Awali akizungumza  Baba Mdogo wa Familia hiyo alisema  Alikuta tayari wamekula  chakula pamoja na kitoleo ambacho kiliwafanyia matatizo    na kuhofia baada ya mmoja wao kuhisi kizungu zungu  mda mchache baada ya kumaliza kula jambo ambalo lilikuwa likiendelea kwa wanafamilia wote.

" Walianza kushuku utowezi waliokula baada ya kuhisi kizungu zungu,  na Baba yao kutilia hofu   lakini wasi wasi zaidi ulikuja baada ya  kuona zile miba wlizokula wakazitupa kuku wadogo ambao walidona dona  na wao walikufa pale pale baada ya kula zile miba."

Aidha  aliendelea kusema    samaki aina ya bunju hutumika kama kitoweleo chengine jambo ambalo halikuwatia hofu wanafamilia hiyo  katika kukitumia kitoleo hicho.

" Walikula kwa kujua  ndio kwa sababu ni samaki kama kitoleo chengine ndio jina lake  bunju ila sio kwamba walijua kama atakuwa na atahari kwa  vile ni kitoleo cha kawaida na siku nyingi  leo tu labda imetokezea mistake  labada kal kitu labda  kala kitu cha sumu labada ayo maini yake yalikuwa ni machafu ndio wakadhurika.


Akizungumza kwa upande wake Baba Mzazi wa  Familia hiyo Alisema Alipata samaki hao bandarini alipokuwa katika harakati zake za kutafuta kitoleo  Kwa Ajili ya Matumizi Ya Nyumbani Kwake. 

"Nilipata Maini yale, Machali Chali, Vichwa Vidogo Vidogo Vya Bunju Lakini Baada ya kulikuta lile lishachunwa vizuri nikalichukua  Sikuhofia kwa sababu nishakula siku nyingi tu mambo kama hayo si chini ya miaka Lakini ni mtihani tu mwenyezimungu mja akishakuandikia lolote linakuwa,   
Hata hivyo Daktari huyo aliwataka wananchi kutoendelea kutumia samaki ambao tayari wanahofu kutokana na  kuwa na vinasaba amabavyo vina atahari kwa binaadamu ili kuepusha  Kuhatarisha usalama wa maisha yao. 

"Mara kwa mara kesi za ulaji wa samaki hawa   amabao wanavinasaba vyenye sumu mbaya endapo atatumia binaadamu  zinajitokeza wananchi waache kula     ni hatari kwao". 

  Kwa Mujibu wa Dakatari huyo dhamana alissema  Wanafamilia hao mmoja kati yao amepoteza maisha usiku wa saa tisa   mtoto mwenye umri wa miaka 5.

"Familia hiyo inatokea shehia ya tumbe Magharibi   kikunguni Mtaa wa Soko domo, na Said Omar Kassim amabae ni baba wa familia hiyo  Hali yake Bado anaendelea na matibabu licha ya kulalamika mara kwa mara kizungu zungu,  Jine Issa Abdalla Ambae ni mama wa familia hiyo yenye watoto watano   umri miaka 37 hali yake inaendelea vizuri, Abdul Majid Said Omar, Issa Said Omar, Hassan Said Omar, Muzna Said Omar, wote Wanaendelea na matibabu hospitalini hapo huku  Shafii Saidi Omar Akiwa tayari amepoteza Maisha mwenye umri wa miaka 5 .
Familia hiyo inaendelea kupata matibabu  katika hospital ya Cottage Micheweni  ambapo  Imefikishwa hospitlini hapo kwa kudaiwa kula samaki aina ya bunj

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI