WAATHIRIKA WAKUBWA UKOSEFU WA HUDUMA YA MAJI NI AKINA MAMA BAADHI YA VIJIJI WALIA KUKOSA HUDUMA.

Na AMINA AHMED MOH’D 

Wananchi wanalalamika kukosa huduma ya maji safi na salama kwa muda wa miezi mitatu sasa licha ya kufika mmlaka husikakuomba msaada  wa kupatiwa ufumbuzi suala hilo.

 Wakizungumza baadhi ya kina mama katika kijiji cha kichanjaani  shehia ya Dodo Pujini wilaya ya mkoani  mkoa wa kusini pemba wamesema kukosa huduma hiyo  kwa kipindi  cha miezi mitatu kumekuwa usumbufu  jambo ambalo hulazimika kusitisha  baadhi y shughuli zao ikiwemo kilimo  . 

 Akina mama hao wameiomba serikali pamoja na viongozi wao wa jimbo  kuwasaidia kulipatia ufumbuzi    suala hilo ambapo wamesema licha ya kukosa huduma hiyo kwa ajili y shughuli zao lakini pia husababishia usumbufu wa kuifata  masafa ya mbali huduma  hiyo. 

 " Tunaiomba serikali ituangalie wananchi wake  tunasumbuka  vikuta vya  mifereji vimeshakauka maji tukikosa kupeleka dumu mbili mbli   hapa kwenye kisima hichi cha Msikiti  bhasi ndoo hatujsalimika na  kichwani  kil siku Alisema Mastura Ali Mkaazi wa kichanjaani. 

Aidha  kwa upande wake  Fatma Salum  Amesema kuwa kukosa huduma hiyo   kwa muda mrefu sasa hulazimika kusitisha huduma za kilimo. 

"Maji  tumekuwa sikuizi hatulimi hata mboga mana ndo htuna maji   kukosa mji kila kiu kimekuwa kigumu  mana shughuli za kiuchumia zimesimama kil kitu tununue mpka majani y mboga" 
 
 "Tunayafata mabondeni maji sisi na watoto wetu   visimani hatari kama nini dunia hii iliyojaa udhalilishaji  wkati mwengine watoto wakike wanaenda peke yao  kufuata maji  Viongozi tusaidieni  maji ndio kila kitu kwa binaadamu Alisema Bi suria Juma." 

 Kwa upande wa   akina baba  kijijini humo wamesema kuwa  wamekuwa wakichukua hatua mbali mbali kulipatia ufumbuzi sul hilo ikiwa  ni pamoja na kufika mamlaka husika kuomba usaidizi juu ya suala hili linalowakbili kijijini humu". 

Akizungumzia suala hili sheha wa shehia ya Dodo Pujini  Ramadhan  Farhan  Farjala  amekiri kuwepo kwa tatizo hilo  katika badhi ya meneo ndani ya shehia yake ambapo amesema uongozi wa shehia   umechukua jitihada mbali mbali ikiwemo kulipfikisha suala hili katika uongozi wa wilaya.

"Ni kweli vijiji  vitatu katika shehia ya Dodo  Havina huduma ya mji miezi mitatu sasa Chanjaani, kwaGombe, pamoja na kichanjaani    na tatizo tulilifikisha kwa wahusika ambao ni zawa wamesema tatizo ni kuharibika kwa mchikikichi katik kisima kinachosambazia maji katika maeneo hayo  na waliahidi  wanalifanyia kazi suala hilo lakini ni miezi mitatu sasa inaenda kuwa mwezi wa nne". 
 
Aidha  sheha huyo amesema kuwa  wamelipeleka suala hili kwa uongozi wa wilaya kwa kupatiwa ufumbuzi zaidi.

Hata hivyo ameiomba serikali pamoja na mamlaka husika  kusiaidia kulipatia ufumbuzi suala la kukosekana kwa huduma ya maji katika vijiji hivyo. 

 Harakati za kumtafuta mkurugenzi wa mamlaka ya maji   pemba  juu ya  suala hili zinaendelea .

Na tutakujuza zaidi. 

Mwisho
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI