MJUE MWANAMKE WA KWANZA KUONGOZA KASKAZINI PEMBA HAIJAWAHI KUTOKEA NI IPI SIRI YAKE!.
AMINA AHMED –PEMBA .
“...Mwenyezi Mungu amewaumba kutokana na nafsi moja...” (7:189)
Wajibu na majukumu ya mwanamke ni kama ya mwanamume, na suala lake ni
kama la mume yaani suala la haki, ujumbe na marejeo. Isitoshe,
mustakbali wa kazi yoyote ni dini kwa njia moja au nyengine mwanamke
naye ana kazi yake.
Kuna kazi zingine ambazo hakuna awezaye kuzisimamia na kuzitekeleza
ila yeye, kwa maana hiyo, huwezi kupata harakati zozote zenye kufaulu
ila mwanamke atakuwa na fungu lake kubwa humo.
“...Lau si waumini wanaume na waumini wanawake...” (48:25)
Kazi inayompasa kufanya mwanamke wa kidini siyo zawadi anayopewa na
mwanamume (akikataa kumpa, basi) bali ni miongoni mwa haki zake na ni
miongoni mwa majukumu yake kwa hiyo ni juu yake atekeleze majukumu
yake.
Vinginevyo, hatakubaliwa atoe udhuru mbele ya Mwenyezi Mungu na
Historia kwamba wanaume hawakumwachia atimize wajibu wake wala
hawakumpa kazi ya kufanya kwenye utekelezaji huo.
Kwa hivyo ni lazima mwanamke huyo ajihisabu kuwa yumo kwenye
kutekeleza wajibu wake kwa kujitolea nafsi yake kwenye upande wa
mapambano kwa kuinua kiwango chake cha kifikra, kisiasa, kielimu,
kidini na kikazi.
Itoshe kuelezea umuhimu wa mwanamke katika Uislamu bali shauku yangu
ni kumuelezea Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib
ambae ni kiongozi mwanamke ambae sio rahisi kupata mfano wake katika
utendaji kazi, uthubutu lakini pia ujasiri alionao.
Unapozungunzia mkuu wa mkoa mwanamke kwa Pemba huwezi kuliacha jina
la Salama Mbarouk Khatibu kutoka na harakati zake za Uongozi na
aliedumu kwa muda mrefu katika Uongozi tokea awamu ya saba ya Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar.
Kiongozi huyu mwanamke anachukuwa mfano wa Mwanamke Hajar na Ibrahim (A.S)
Ambae alikuwa Mwanamke jasiri, mwenye nia safi aliyeihama nyumba yake
na nchi yake ili aende akaishi kando ya nyumba ya Mungu katika ardhi
kame isiyo na maji wala manyasi ili amwabudu Mungu pekee na ajitenge
na kuabudu watu.
Mfano huo ndivyo ulivyo kwa RC mama Salama Mbarouk Khatibu pale
anapoamuwa kutekeleza majukumu yake ya uongozi ndani ya mkoa wa
Kaskazini Pemba kwa vile hajali muda , juwa wala mvua ili akamilishe
lile alilopangiwa na Viongozi wake wakuu kwa mustakbali wa kuleta
maendeleo ya wananchi wa mkoa huo.
“...Mwenyezi Mungu amewaumba kutokana na nafsi moja...” (7:189)
Wajibu na majukumu ya mwanamke ni kama ya mwanamume, na suala lake ni
kama la mume yaani suala la haki, ujumbe na marejeo. Isitoshe,
mustakbali wa kazi yoyote ni dini kwa njia moja au nyengine mwanamke
naye ana kazi yake.
Kuna kazi zingine ambazo hakuna awezaye kuzisimamia na kuzitekeleza
ila yeye, kwa maana hiyo, huwezi kupata harakati zozote zenye kufaulu
ila mwanamke atakuwa na fungu lake kubwa humo.
“...Lau si waumini wanaume na waumini wanawake...” (48:25)
Kazi inayompasa kufanya mwanamke wa kidini siyo zawadi anayopewa na
mwanamume (akikataa kumpa, basi) bali ni miongoni mwa haki zake na ni
miongoni mwa majukumu yake kwa hiyo ni juu yake atekeleze majukumu
yake.
Vinginevyo, hatakubaliwa atoe udhuru mbele ya Mwenyezi Mungu na
Historia kwamba wanaume hawakumwachia atimize wajibu wake wala
hawakumpa kazi ya kufanya kwenye utekelezaji huo.
Kwa hivyo ni lazima mwanamke huyo ajihisabu kuwa yumo kwenye
kutekeleza wajibu wake kwa kujitolea nafsi yake kwenye upande wa
mapambano kwa kuinua kiwango chake cha kifikra, kisiasa, kielimu,
kidini na kikazi.
Itoshe kuelezea umuhimu wa mwanamke katika Uislamu bali shauku yangu
ni kumuelezea Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib
ambae ni kiongozi mwanamke ambae sio rahisi kupata mfano wake katika
utendaji kazi, uthubutu lakini pia ujasiri alionao.
Unapozungunzia mkuu wa mkoa mwanamke kwa Pemba huwezi kuliacha jina
la Salama Mbarouk Khatibu kutoka na harakati zake za Uongozi na
aliedumu kwa muda mrefu katika Uongozi tokea awamu ya saba ya Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar.
Kiongozi huyu mwanamke anachukuwa mfano wa Mwanamke Hajar na Ibrahim (A.S)
Ambae alikuwa Mwanamke jasiri, mwenye nia safi aliyeihama nyumba yake
na nchi yake ili aende akaishi kando ya nyumba ya Mungu katika ardhi
kame isiyo na maji wala manyasi ili amwabudu Mungu pekee na ajitenge
na kuabudu watu.
Mfano huo ndivyo ulivyo kwa RC mama Salama Mbarouk Khatibu pale
anapoamuwa kutekeleza majukumu yake ya uongozi ndani ya mkoa wa
Kaskazini Pemba kwa vile hajali muda , juwa wala mvua ili akamilishe
lile alilopangiwa na Viongozi wake wakuu kwa mustakbali wa kuleta
maendeleo ya wananchi wa mkoa huo.
SALAMA MBAROUK KHATIB RC / KASKAZINI PEMBA.
Makala hii maalum ilifunga safari hadi katika Ofisi za Mkoa wa
kaskazini Pemba alipo Mkuu wa mkoa Salama Mbarouk Khatib , lengo ni
kutaka kukujuza kiundani mwanamke huyo mfano wa kuigwa na
wanawake wengine wanaotaka kuwa viongozi bora na wenye kuleta
maendeleo katika jamii .
Baada ya kufika katika Ofisi hizo licha ya majukumu mengi aliyokuwa
nayo lengo liliweza kufikiwa baada ya kufanikiwa kupata kutenga
muda maalum kiongozi huyo na kutoka mashirikiano juu ya lile lengo
lililokusudiwa na makala hii.
Salama Mbarouk Khatib ni mwanamke pekee aliteuliwa kuongoza
mkoa wa kaskazini kwa mara ya kwa za kati ya wakuu wa mikoa 14
waliopita kabla yake.
Lakini pia ni Mwanamke pekee alieteuliwa kuongoza mkoa kati ya
wakuu wa mikoa watano waliopo Zanzibar katika awamu ya nane ya Rais
Dk, Hussein Ali.
Serikali ya awamu ya nane ilivyoweza kumuamini mwanamke na kumpa
nafasi mbali mbali za uongozi na ikiwa ni pamoja na kuongoza mikoa,
Wizara pamoja na taasisi mbali mbali huku ikiwa na katiba zote mbili
ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na ya Zanzibar zimempa nafasi sawa
mwanamke 50 kwa 50 ya uongozi wanawake na wanaume huku zikitekeleza
mkutano wa azimio la mkutano wa Beijing uliofanyika nchini China
takriban miaka 26 iliyopita.
Zanzibar ina jumla ya mikoa mitano mitatu kati ya hiyo inapatika
katika kisiwa na Unguja ambayo ni Mkoa wa mjini Magharibi, Mkoa wa
Kusini na Kaskazini Unguja huku kwa upande wa kisiwa cha Pemba ni
Kusini na kaskazini Pemba.
"Mh, Rais kwanza kafanya jambo kubwa na la maana kwa upande wangu
nimshukuru kwa dhati kwa kuniandikia historia hii maishani kwangu,
lakini pia kuniandikia historia mpya kaskazini Pemba,” alieleza.
Alisema yeye ni mkuu wa mkoa wa 15 kwa mujibu wa uteuzi , lakini
katika wakuu wa mikoa 15 wote waliopita walikuwa ni wanaume jambo
ambalo linaonesha mabadiliko na wanawake wenzake na hakuna cha
kuogopa ni muda wa mabadiliko sasa kikubwa ni kuona utendaji kazi
unafanyika .
Harakati za Salama Mbarouk Khatib zilianza mbali ambapo alisema
kuwa" siri kubwa niwaambie wanawake wenzangu kikubwa ni kujiamini na
tunapopata nafasi inatubidi tuitendee haki ipasavyo”, alieleza.
" Harakati zangu mimi zilianza mbali sana lakini siri kubwa ilikuwa ni
uthubutu nimekuwa natumia fursa ipasavyo ninapoipata niliwahi kuwa
mkuu wa wilaya Chake Chake nikawa mkuu wa wilaya ya Micheweni na mote
humo nilisimama kama kiongozi wala sikusimama kuhofia jinsia katika
utendaji wangu wa majukumu ", alisema RC.
Mashaallah, Allah amjaalie mafanikio mema, wepesi na utayari wake
katika utendaji kazi kabla ya kuteuliwa kuongoza nafasi hiyo
kumechangia kufika hapa alipo sasa ambapo kwani aliweza kuhudumu
katika nafasi mbali mbali wakati akiwa katika Wizara ya Wanawake na
watoto kwa sasa Ustawi wa jamii kama Ofisa Mipango.
" Nilikuwa najiamini na naitendea haki kazi niliopewa sekta
niliyopangiwa sikuwa na hofu wala woga pakutolewa maamuzi kama
kiongozi nilikuwa natoa, pakushauri nilikuwa nashauri pia nilikuwa
nasikiliza na kufanyia kazi maelekezo, na kufuata Sheria , Sera
pamoja na , miongozo ya serikali lakini zaidi sikuwa na hofu nahisi
hicho ndio kitu kilichopelekea leo kufika hapa nilipo", alisema.
Alieleza kuwa jukumu la uongozi alilonalo huku akiwa ni mke lakini pia
mama wa familia linatofautishika haliyaathiri utendaji kazi, hivyo
ni kusema maisha ya uongozi hayaathiri familia yake bali yanaongeza
heshima na mashirikiano jambo ambalo linazidi kumpa ari na nguvu ya
kufanya kazi kwa bidii.
" Mimi ni mama ambae nina mume na nina watoto serikali inanitegemea
lakini niseme kwamba kikubwa ni kujifahamu tu , unapokuwa Serikalini
wewe ni kiongozi ujuwe wewe ni kiongozi na unapokuwa nyumbani ujuwe
wewe ni mama ambae unastahiki kufanya majukumu yako na mimi nafanya
hivyo bila usumbufu wowote “, alieleza RC .
Alindelea kusema kuwa kama mama ana watoto wadogo huku ni mkuu wa
mkoa ambapo watoto wanataka huduma ya mama zaidi na mara nyingi
inakuwa anasafiri, kazi ni nyingi zaidi, lakini na wao wanajuwa kama
ni mama yao kwani anakuwa anajipanga a natoa mashirikiano nakuwa
karibu nao kila anapokuwa nyumbani.
Hata hivyo Bi Salama aliwataka wanawake wengine nchini kusimamia
maamuzi yao bila kuogopa vitisho ili kuonesha uwezo walionao katika
utendaji kazi.
" Katika kuwaaminisha wananchi kuamini utendaji kazi wako ni
kusimamia malengo yako na kutokukubali kurudishwa nyuma jambo hilo
litawafanya waweze kujenga imani ya kukuamini wewe unaweza kuongoza
bila kujali jinsia”, alieleza.
Anaeleza kuwa wananchi wameamka sasa hivi hawaangalii jinsia
wanaangalia utendaji kazi aliwaasa wanawake wenzake kutuogopa fursa
wasizichezee watufanye kazi kadri ya uwezo wao na suala hilo linaweza
kuwapa fursa wanawake kupata nafasi zaidi ya ukuu wa mkoa na
nyenginezo.
Alifahamisha licha ya watu wachache kumtia midomoni katika utowaji wa
maamuzi ya kiutendaji katika uongozi wake bi Salama hakulipokea
suala hilo kama ni kikwazo kwa upande wake anajiamini.
" Kuna baadhi ya watu wanaotaka wakuendeshe vile wanavyotaka wao kwa
maslahi yao binafsi jambo ambalo kwangu silipi kipaumbele naamua kwa
kufuata sheria na miongozo kwa maslahi ya taifa wao wanaishia
kunitupia majungu bi salama mkali haambiliki”, alifahamisha.
" Unapofanya kazi ndipo kasoro zinaonekana na ukikosa kasoro wewe sio
binaadamu kwahiyo nakubali kushauriwa lakini zaidi na angalia ule
ushauri ninaopewa je hautokweda kinyume na sheria za serikali, jee
una maslahi ya taifa, hautoathiri serikali ndipo naufanyia kazi
kikubwa ninachoangalia ni hicho", alisema.
Alieleza kuwa elimu inanafasi na na mchango mkubwa katika kuwa
kiongozi bora mbapo aliwataka wanawake kuendelea kusoma na kujifunza
mambo mbali mbali.
Alisema licha ya mashirika kupigania Women mwananmke na Uongozi bado
wanawake wengine hawajajua lengo la kupigania kupata haki hizi kuwa
ni kupata haki zetu ipasavyo ili wanawake kupata maendeleo.
Mgeni Khatib Yahya mkuu wa wilaya ya Micheweni alisema kuwa kiongozi
huyo ndie ambae alikuwa anajifunza mambo mengi kutoka kwakwe kabla ya
hajawa mkuu wa wilaya na hadi sasa anaendelea kupata ushauri na
kupokea mawazo mbali mbali kutoka kwa kiongozi wake huyo.
"Najifunza siku hadi siku mambo mazuri kutoka kwa Mh Salama
ananishauri ananipa maelekezo kama msaidizi wake na natekeleza
majukumu yangu vyema kwa kufuata nyao zake zaidi nakubali uthubutu na
namna anavyojiamini katika uongozi wake ,tunasaidiana kwa pamoja
kuleta maendeleo kumsaidia Rais wa Zanzibar , "anaeleza.
Wakizungumza baadhi ya wakaazi wa wete waliozungumza na makala hii
juu ya uongozi wa mkuu huyo wa mkoa akiwemo Bi Aziza Makame Abass
Mkaazi wa Limbani wilaya ya hiyo alisema kuwa jitihada zinazofanywa
na mku huyo wa wilaya katika kuleta maendeleo ya mkoa huo yanaonekana
na kila mtu ambapo aliiomba Serikali kumuacha aendelee kuishikilia
nafasi hiyo kwa miaka yote.
"Kwanza binafsi nampenda anavyofanya kazi nikisikiliza radio jamii
nisipomsikia jioni basi asubuhi nitamsikia anazungumzia jambo
lolote tunajuwa hasa wa kama tuna kiongozi sio wengine ambapo hata
kuwasikia kwa radio hatuwasikii anajitahidi Rais asituondolee tunu
hii wazazi tunaojuwa tunaifurahia”, alisema.
" Kile ni kipaji wanawake wengine wajifunze pale mana ni darasa la
namna ya mwanamke atakapoamua kuwa kiongozi vipi anatakiwa awe
kabisa,” alisema .
Mwananchi Salim Ali wa Wete ,anasema anazipongeza juhudi za kupata
viogozi wanawake zilizochukuliwa na mashirika na asasi mbali mbali
zilizopigania na zinazoendelea kumpigania mwanamke kupata haki na
fursa sawa katika uongozi ambapo ni pamoja Chama Cha waandishi wa
Habari wanawake Tanzania TAMWA Tanzania na Zanzibar.
Anafahamisha kuwa Zanzibar kwa sasa kasi ya wanawake kuingia katika
uongozi imeongezeka ukilinganisha na miaka iliyopita ambapo kwa
mujibu wa takwimu fupi iliyotolewa na Chama cha waandishi wa Habari
Tanzania TAMWA Zanzibar zilionesha kuwa idadi ya viongozi wanawake
katika Baraza la wawakilishi ni asilimia 36 ambayo ni sawa na
wanawake 28 kati ya wawakilishi 84 waliopata nafasi hiyo.
Anaeleza kwa Takwimu hizo bado haitoshi na wanawake hawajapata fursa
sawa za usawa wa kijinsia katika vyombo vya kutolea maamuzi utawala
na utowaji wa maamuzi katika ngazi za maamuzi.
BiSalama ametowa wito kwa wanawake wote nchini ambapo amewataka
kutotumia vibaya madaraka wanayoyapigania kuyapata badala yake
wayatendee haki, kwa kufanya kazi vizuri, kuwashirikisha wengine,
ujitathmini na kujiuliza masuali katika kila hatua ya utendaji.
"Tuige mazuri kutoka kwa wanawake wengine binafsi mimi ni mwanamke
pekee yangu lakini wakuu wa mikoa wenzangu ambao ni wanaume wanasema
katika vikao.
" Yule ni mwanamke lakini anapambana na mimi nilikuwa sijui hizi
taarifa lakini wanakuwa wanaiambia wengine wananipa hongera wengine
wananipigia kutaka ushauri wa kuleta maendeleo katika mikoa yao kwa
hiyo kimeeleweka kwamba kumbe mkuu wa mkoa wa kaskazini ni mwanamke
lakini anapambana na juhudi zinaonekana kwamba wanawake tunapopewa
fursa tunaweza kufanya kazi”, anaeleza .
Ni Wanawake 22 pekee ambao ni viongozi wakuu kati ya nchi na
mataifa ya nchi 123 kwa idadi hiyo bado jitihada zinahitajika katika
kuona mwanamke anapata fursa sawa katika vyombo vya maamuzi ili kupata
idadi kubwa zaidi Zanzibar naTanzaniabara pamoja na Mataifa mbali
mbali.
Hata hivyo kuna usemi kuwa “Hakuna kinachoshindikana chini ya jua”
usawa wa kijinsia katika ngazi ya maamuzi Uchumi, Siasa, Biashara,
elimu na majukumu ya kiutendaji inawezekana iwapo wanawake watapata
fursa sawa 50 kwa 50.
MWISHO.
kaskazini Pemba alipo Mkuu wa mkoa Salama Mbarouk Khatib , lengo ni
kutaka kukujuza kiundani mwanamke huyo mfano wa kuigwa na
wanawake wengine wanaotaka kuwa viongozi bora na wenye kuleta
maendeleo katika jamii .
Baada ya kufika katika Ofisi hizo licha ya majukumu mengi aliyokuwa
nayo lengo liliweza kufikiwa baada ya kufanikiwa kupata kutenga
muda maalum kiongozi huyo na kutoka mashirikiano juu ya lile lengo
lililokusudiwa na makala hii.
Salama Mbarouk Khatib ni mwanamke pekee aliteuliwa kuongoza
mkoa wa kaskazini kwa mara ya kwa za kati ya wakuu wa mikoa 14
waliopita kabla yake.
Lakini pia ni Mwanamke pekee alieteuliwa kuongoza mkoa kati ya
wakuu wa mikoa watano waliopo Zanzibar katika awamu ya nane ya Rais
Dk, Hussein Ali.
Serikali ya awamu ya nane ilivyoweza kumuamini mwanamke na kumpa
nafasi mbali mbali za uongozi na ikiwa ni pamoja na kuongoza mikoa,
Wizara pamoja na taasisi mbali mbali huku ikiwa na katiba zote mbili
ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na ya Zanzibar zimempa nafasi sawa
mwanamke 50 kwa 50 ya uongozi wanawake na wanaume huku zikitekeleza
mkutano wa azimio la mkutano wa Beijing uliofanyika nchini China
takriban miaka 26 iliyopita.
Zanzibar ina jumla ya mikoa mitano mitatu kati ya hiyo inapatika
katika kisiwa na Unguja ambayo ni Mkoa wa mjini Magharibi, Mkoa wa
Kusini na Kaskazini Unguja huku kwa upande wa kisiwa cha Pemba ni
Kusini na kaskazini Pemba.
"Mh, Rais kwanza kafanya jambo kubwa na la maana kwa upande wangu
nimshukuru kwa dhati kwa kuniandikia historia hii maishani kwangu,
lakini pia kuniandikia historia mpya kaskazini Pemba,” alieleza.
Alisema yeye ni mkuu wa mkoa wa 15 kwa mujibu wa uteuzi , lakini
katika wakuu wa mikoa 15 wote waliopita walikuwa ni wanaume jambo
ambalo linaonesha mabadiliko na wanawake wenzake na hakuna cha
kuogopa ni muda wa mabadiliko sasa kikubwa ni kuona utendaji kazi
unafanyika .
Harakati za Salama Mbarouk Khatib zilianza mbali ambapo alisema
kuwa" siri kubwa niwaambie wanawake wenzangu kikubwa ni kujiamini na
tunapopata nafasi inatubidi tuitendee haki ipasavyo”, alieleza.
" Harakati zangu mimi zilianza mbali sana lakini siri kubwa ilikuwa ni
uthubutu nimekuwa natumia fursa ipasavyo ninapoipata niliwahi kuwa
mkuu wa wilaya Chake Chake nikawa mkuu wa wilaya ya Micheweni na mote
humo nilisimama kama kiongozi wala sikusimama kuhofia jinsia katika
utendaji wangu wa majukumu ", alisema RC.
Mashaallah, Allah amjaalie mafanikio mema, wepesi na utayari wake
katika utendaji kazi kabla ya kuteuliwa kuongoza nafasi hiyo
kumechangia kufika hapa alipo sasa ambapo kwani aliweza kuhudumu
katika nafasi mbali mbali wakati akiwa katika Wizara ya Wanawake na
watoto kwa sasa Ustawi wa jamii kama Ofisa Mipango.
" Nilikuwa najiamini na naitendea haki kazi niliopewa sekta
niliyopangiwa sikuwa na hofu wala woga pakutolewa maamuzi kama
kiongozi nilikuwa natoa, pakushauri nilikuwa nashauri pia nilikuwa
nasikiliza na kufanyia kazi maelekezo, na kufuata Sheria , Sera
pamoja na , miongozo ya serikali lakini zaidi sikuwa na hofu nahisi
hicho ndio kitu kilichopelekea leo kufika hapa nilipo", alisema.
Alieleza kuwa jukumu la uongozi alilonalo huku akiwa ni mke lakini pia
mama wa familia linatofautishika haliyaathiri utendaji kazi, hivyo
ni kusema maisha ya uongozi hayaathiri familia yake bali yanaongeza
heshima na mashirikiano jambo ambalo linazidi kumpa ari na nguvu ya
kufanya kazi kwa bidii.
" Mimi ni mama ambae nina mume na nina watoto serikali inanitegemea
lakini niseme kwamba kikubwa ni kujifahamu tu , unapokuwa Serikalini
wewe ni kiongozi ujuwe wewe ni kiongozi na unapokuwa nyumbani ujuwe
wewe ni mama ambae unastahiki kufanya majukumu yako na mimi nafanya
hivyo bila usumbufu wowote “, alieleza RC .
Alindelea kusema kuwa kama mama ana watoto wadogo huku ni mkuu wa
mkoa ambapo watoto wanataka huduma ya mama zaidi na mara nyingi
inakuwa anasafiri, kazi ni nyingi zaidi, lakini na wao wanajuwa kama
ni mama yao kwani anakuwa anajipanga a natoa mashirikiano nakuwa
karibu nao kila anapokuwa nyumbani.
Hata hivyo Bi Salama aliwataka wanawake wengine nchini kusimamia
maamuzi yao bila kuogopa vitisho ili kuonesha uwezo walionao katika
utendaji kazi.
" Katika kuwaaminisha wananchi kuamini utendaji kazi wako ni
kusimamia malengo yako na kutokukubali kurudishwa nyuma jambo hilo
litawafanya waweze kujenga imani ya kukuamini wewe unaweza kuongoza
bila kujali jinsia”, alieleza.
Anaeleza kuwa wananchi wameamka sasa hivi hawaangalii jinsia
wanaangalia utendaji kazi aliwaasa wanawake wenzake kutuogopa fursa
wasizichezee watufanye kazi kadri ya uwezo wao na suala hilo linaweza
kuwapa fursa wanawake kupata nafasi zaidi ya ukuu wa mkoa na
nyenginezo.
Alifahamisha licha ya watu wachache kumtia midomoni katika utowaji wa
maamuzi ya kiutendaji katika uongozi wake bi Salama hakulipokea
suala hilo kama ni kikwazo kwa upande wake anajiamini.
" Kuna baadhi ya watu wanaotaka wakuendeshe vile wanavyotaka wao kwa
maslahi yao binafsi jambo ambalo kwangu silipi kipaumbele naamua kwa
kufuata sheria na miongozo kwa maslahi ya taifa wao wanaishia
kunitupia majungu bi salama mkali haambiliki”, alifahamisha.
" Unapofanya kazi ndipo kasoro zinaonekana na ukikosa kasoro wewe sio
binaadamu kwahiyo nakubali kushauriwa lakini zaidi na angalia ule
ushauri ninaopewa je hautokweda kinyume na sheria za serikali, jee
una maslahi ya taifa, hautoathiri serikali ndipo naufanyia kazi
kikubwa ninachoangalia ni hicho", alisema.
Alieleza kuwa elimu inanafasi na na mchango mkubwa katika kuwa
kiongozi bora mbapo aliwataka wanawake kuendelea kusoma na kujifunza
mambo mbali mbali.
Alisema licha ya mashirika kupigania Women mwananmke na Uongozi bado
wanawake wengine hawajajua lengo la kupigania kupata haki hizi kuwa
ni kupata haki zetu ipasavyo ili wanawake kupata maendeleo.
Mgeni Khatib Yahya mkuu wa wilaya ya Micheweni alisema kuwa kiongozi
huyo ndie ambae alikuwa anajifunza mambo mengi kutoka kwakwe kabla ya
hajawa mkuu wa wilaya na hadi sasa anaendelea kupata ushauri na
kupokea mawazo mbali mbali kutoka kwa kiongozi wake huyo.
"Najifunza siku hadi siku mambo mazuri kutoka kwa Mh Salama
ananishauri ananipa maelekezo kama msaidizi wake na natekeleza
majukumu yangu vyema kwa kufuata nyao zake zaidi nakubali uthubutu na
namna anavyojiamini katika uongozi wake ,tunasaidiana kwa pamoja
kuleta maendeleo kumsaidia Rais wa Zanzibar , "anaeleza.
Wakizungumza baadhi ya wakaazi wa wete waliozungumza na makala hii
juu ya uongozi wa mkuu huyo wa mkoa akiwemo Bi Aziza Makame Abass
Mkaazi wa Limbani wilaya ya hiyo alisema kuwa jitihada zinazofanywa
na mku huyo wa wilaya katika kuleta maendeleo ya mkoa huo yanaonekana
na kila mtu ambapo aliiomba Serikali kumuacha aendelee kuishikilia
nafasi hiyo kwa miaka yote.
"Kwanza binafsi nampenda anavyofanya kazi nikisikiliza radio jamii
nisipomsikia jioni basi asubuhi nitamsikia anazungumzia jambo
lolote tunajuwa hasa wa kama tuna kiongozi sio wengine ambapo hata
kuwasikia kwa radio hatuwasikii anajitahidi Rais asituondolee tunu
hii wazazi tunaojuwa tunaifurahia”, alisema.
" Kile ni kipaji wanawake wengine wajifunze pale mana ni darasa la
namna ya mwanamke atakapoamua kuwa kiongozi vipi anatakiwa awe
kabisa,” alisema .
Mwananchi Salim Ali wa Wete ,anasema anazipongeza juhudi za kupata
viogozi wanawake zilizochukuliwa na mashirika na asasi mbali mbali
zilizopigania na zinazoendelea kumpigania mwanamke kupata haki na
fursa sawa katika uongozi ambapo ni pamoja Chama Cha waandishi wa
Habari wanawake Tanzania TAMWA Tanzania na Zanzibar.
Anafahamisha kuwa Zanzibar kwa sasa kasi ya wanawake kuingia katika
uongozi imeongezeka ukilinganisha na miaka iliyopita ambapo kwa
mujibu wa takwimu fupi iliyotolewa na Chama cha waandishi wa Habari
Tanzania TAMWA Zanzibar zilionesha kuwa idadi ya viongozi wanawake
katika Baraza la wawakilishi ni asilimia 36 ambayo ni sawa na
wanawake 28 kati ya wawakilishi 84 waliopata nafasi hiyo.
Anaeleza kwa Takwimu hizo bado haitoshi na wanawake hawajapata fursa
sawa za usawa wa kijinsia katika vyombo vya kutolea maamuzi utawala
na utowaji wa maamuzi katika ngazi za maamuzi.
BiSalama ametowa wito kwa wanawake wote nchini ambapo amewataka
kutotumia vibaya madaraka wanayoyapigania kuyapata badala yake
wayatendee haki, kwa kufanya kazi vizuri, kuwashirikisha wengine,
ujitathmini na kujiuliza masuali katika kila hatua ya utendaji.
"Tuige mazuri kutoka kwa wanawake wengine binafsi mimi ni mwanamke
pekee yangu lakini wakuu wa mikoa wenzangu ambao ni wanaume wanasema
katika vikao.
" Yule ni mwanamke lakini anapambana na mimi nilikuwa sijui hizi
taarifa lakini wanakuwa wanaiambia wengine wananipa hongera wengine
wananipigia kutaka ushauri wa kuleta maendeleo katika mikoa yao kwa
hiyo kimeeleweka kwamba kumbe mkuu wa mkoa wa kaskazini ni mwanamke
lakini anapambana na juhudi zinaonekana kwamba wanawake tunapopewa
fursa tunaweza kufanya kazi”, anaeleza .
Ni Wanawake 22 pekee ambao ni viongozi wakuu kati ya nchi na
mataifa ya nchi 123 kwa idadi hiyo bado jitihada zinahitajika katika
kuona mwanamke anapata fursa sawa katika vyombo vya maamuzi ili kupata
idadi kubwa zaidi Zanzibar naTanzaniabara pamoja na Mataifa mbali
mbali.
Hata hivyo kuna usemi kuwa “Hakuna kinachoshindikana chini ya jua”
usawa wa kijinsia katika ngazi ya maamuzi Uchumi, Siasa, Biashara,
elimu na majukumu ya kiutendaji inawezekana iwapo wanawake watapata
fursa sawa 50 kwa 50.
MWISHO.
Comments
Post a Comment