WAANDISHI WAFUNDISHWA MBINU ZA KUJIKINGA NA UHALIFU WA MITANDAONI



NA A-MINA AHMED MOH’D -  PEMBA    

Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba wameaswa kuzidisha umakini katika utumiaji wa mitandao ya kijamii  ikiwa ni pamoja na kuweka ulinzi katika utumaji  wa taarifa zao ili zisiweze  kudukuliwa.


 Ushauri huo umetolewa na  Mwenyekiti wa Clabu ya waandishi wa Habari ksiwani Pemba Pemba Press Club  Bakar Mussa   Juma  Alipokuwa akifungua mafunzo ya Siku moja ya  Usalama Wa Mitandao (Digital Security) kwa waandishi wa habari wanaotumia zaidi  mitandao ya kijamii   katika kazi zao  yaliofanyika  katika ukumbi wa  ofisi hizo Misufini Chake Chake.
          BAKAR MUSSA JUMA- MWENYEKITI CLUB YA               WAANDISHI WA HABARI PEMBA ( PPC). 

Alisema   mitandao imekuwa ikipeleka ujumbe  kwa haraka  zaidi  kwa jamii    ukilinganisha na vyombo vyengine vya habari  vilivyopo  na kupelekea kutikuwepo kwa   usalama  kwa  waandishi wa habari   kutokana na baadhi ya wahalifu kutumia  mitandao  hiyo kwa kudukua taarifa  pamoja  kufanya uhalifu .

"Kudukuliwa  taarifa kwa mitandao ya kijamii  aidha za mwandishi mwenyewe lakini hata kazi za kihabari zinazofanywa na kutumwa katika mitandao , Pia unaweza kupata taarifa nyingi na ukazitumia   katika vyombo vyako vya habari lakini changamoto ikaja kuwa habari nyengine ni za uongo kwa vile   hujazifanyia uchunguzi  wa kina   na kuwa chanzo cha matatizo".

Aidha Amewataka  waandishi Hao  kuyafanyia kazi mafunzo watakayopatiwa  juu  ya  suala hilo la usalama wa mitandao ili kuweza  kujiweka salama  katika utumiaji wao.

 "Kujiepusha na  mitandao ambayo haiko Salama  kujiepusha kutofautisha fake news, kutasaidia kuwaepusha kujiingiza kwenye mashaka , kuweza kulinda taarifa zako tuyafanyie kazi mafunz haya tutakayo patiwa  leo  ambayo lengo lake ni kusaidia   kujua kuilinda na  kuitumia bila wasi wasi kwenu.Alisema. 

Kwa Upande wake  Mratibu  wa Club hiyo  Mgeni Kombo  Khamis aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kufikisha elimu watakayopatiwa  kwa waandiahi wengine ambao wamekosa fursa hiyo  kutokana na sababu mbali mbali. 
         MGENI KOMBO  - MRATIBU PEMBA PRESS CLUB. 

 Akitoa  Elimu ya Usalama wa mtandao   kwa waandishi hao mkufunzi  Aliepatiwa  Mafunzo hayo na Umoja wa Club za Waandishi wa Habari Tanzania UTPC Haji Nassor Muhamed pamoja  na mambo mengine   alisema kuwa usalama wa mtandao ni kujikinga  na hatari zinazoweza kujitokeza kwa watumiaji wa mtandao  katika kujikinga na hatari zilizokusudiwa na wahalifu na zisizokusudiwa.
HAJI NASSOR MUHAMED - MKUFUZI MAFUNZO DIGITAL SECURITY. 
 "kuna uhalifu katika mitandao ambao umepangwa na ule uliokuwa haukupangwa  yapo mavitu mbali mbali usiyahitaji unaweza ukayakuta katika simu au komputa yako  , masuala ya kufungilua email ya mtu kumuazima mtu mwengine, afungue, yote ni hatari ili ujikinge ni lazima ujue Usalama na ulinzi"Alisema.
 
 Waandishi hao walifundishwa mambo mbali  ya usalama wa mitandao ikiwa ni pamoja  na  Kujikinga dhidi ya hatari  (Safety) kujikinga  binafsi   ili kuweza kuwa salama katika matumizi ya mitandao kwa vyombo vya mitandao (Security)  Tathmini ya hali ya hatari pamoja na mbinu za kujua  program  hatarishi na zisizo hatarishi ambapo katika mafunzo hayo pia  waandishi hao wameaswa kujiunga na club ya waandishi wa habari ili kuweza kupata fursa mbali mbali. 


Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI