Tumieni Maji kwa uangalifu

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amewataka Wananchi wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani kuwa na matumizi mazuri ya maji wakati huu wa kiangazi kwa kuwa kina cha maji kwenye chanzo cha Mto Ruvu kimepungua kwa asilimia kubwa. 

Makalla akiwa kwenye ziara ya kutembelea chanzo cha maji cha Ruvu juu na chini amesema upungufu wa maji kwenye chanzo cha maji cha Mto Ruvu umesababishwa na ukosefu wa mvua za vuli na uwepo wa kipindi kirefu cha kiangazi. 

"Sote tulitarajia kuwepo kwa mvua za vuli kwa kipindi hiki ambazo zingesaidia kuongeza kiasi cha maji kwenye Mto Ruvu na kuwezesha upatikanaji wa maji kwa Wananchi”

"Lakini kulingana na utabiri wa Mamlaka ya hali ya hewa ambao ulieleza kuwa kutakuwa na kipindi kirefu cha kiangazi, imesababisha kupungua kwa maji, hivyo kutakwepo na mgao wa maji kwenye maeneo ya mijini” 

"Uzalishaji wa maji kwenye chanzo cha Mto Ruvu ni lita milioni 466 kwa siku lakini kwa sasa uzalishaji umepungua mpaka lita milioni 300 sawa na asilimia 64”
#MillardAyoUPDATES

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI