Tutaendela kudhibiti utoro wa skuli za msingi

Na AMINA AHMED MOH’D - PEMBA 

Uongozi wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba Umesema utaendelea kulisimamia vyema suala  la utoro  wa  wanafunzi wa skuli za msingi kwa kuendelea kukemea ajira za watoto  wilayani humo ili lisiendelee kujitokeza na kuathiri maendeleo ya elimu kwa watoto na kupelekea kukosa haki yao ya msingi kwa kukatisha masomo
Ameyasema Hayo Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni khatib Yahya  Alipokuwa akizungumza na habari hizi juu ya    maendeleo yaliofikiwa katika kuwarejesha skuli wanafunzi watoro wa skuli za msingi zilizomo katika skuli mbali mbali za wilaya hiyo.

Amesema  moja kati ya sababu iliyopelekea  kuwepo kwa  utoro wa wanafunzi wa skuli za msingi ktika baadhi ya skuli wilayani humo ni pamoja na ajira za watoto pamoja  kukosa mashirikiano  kwa waza jambo ambalo kwa sasa limepunguwa baada ya kuliwekea mikakati maalum.
 
"Tatizo kubwa la utoro kwa wanafunzi wa skuli za msingi  Wakati naingia hapa mwaka 2020 ilikuwa linasababishwa na watoto kutumikishwa kwa ajira mbali mbali, uchimbaji kokoto,  kupara samaki jambo ambalo ilinilazimu nikaze buti kulisimamia ili lisiwepo na nashkuru kwa sasa  limepunguwa na watoto waliowengi kwa sasa wamerudi skuli. "
Aidha Mkuu wa wilaya hiyo amesema kuwa kwa sasa utayari wa wazazi katika kudhibiti suala hilo umeongezeka  tofauti na ilivyokuwa awali. 

" Wazazi wameamka  katika wilaya yanhu  kuna wengine wao ndio wananipa taarifa  za watoto wanapowaona wanatumikishwa na hii imekuja baada ya kuweka mkakati kuwashirikisha na kujadiliana kwa pamoja katik kudhibiti suala la utoro  wameitikia wito tunafanya kazi kwa pamoja lengo letu limekuwa moja kuona kila mtoto anahaki yake ya kusoma nashukuru nimeweza kuwabadilisha mitazamo yao katika suala hili na sasa tunasaidiana kwa pamoja ". 
Alindelea kusema kuwa   kwa sasa maendeleo  ya wanafunzi waliorejeshwa skuli ni mazuri huku wengine wakiwa tayari wameanza kufanya mitihani yao ya ya madarasa mbali mbali.

" Watoto waliorudishwa skuli maeneo mbali mbali walikuwa wanaangaliwa  na kuwekwa madarasa kwa mujibu wa  hali ya ufaham wa masomo yao ulivyokuwa  wapo ambao walikuwa madarasa ya mitihani wengine madarasa ambayo si ya mitihani na wote wanaendelea vyema na masomo bila ya kuwa na vikwazo".
Hata hivyo mkuu wa wilaya huyo amewataka wazazi na walezi pamoja na waalimu kuendelea na mapambano hayo  kwa kuhakikisha wanafunzi walifanikiwa kurejeshwa skuli hawatoroki tena na wale ambao bado wapo mitaani kuwatolea taarifa ili waweze kurudishwa skuli  kupata haki zao. 

 "Watoto Tusiwamamie vyema wazazi tusiwatumikishe kwani wajibu  wa kutatua changamoto za watoto ni sisi wazazi  pia tufuatikie watoto kwa ukaribu zaidi , walimu tusimamie wajibu wetu   kama serikali ilivyituamini kwa kuwasimamia na kuwalinda wanapokuwa skuli ili waweze kupata elimu itakayosaidia wao  baadae. 

 Kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu wilaya ya micheweni mkoa wa kaskzini Pemba  bi Asya............. amesema kwa sasa suala la utoro kwa wanafunzi wa skuli za msingi  wilayani humo umepungua kwa kiasi kikubwa tofauti  na awali na hii imetokana na juhudi za mkuu wa wilaya hiyo  kufuatilia na kutoa mashirikiano  ya karibu katika kudhibiti suala hilo. 

"Utoro upo lakini ulipo sasa ni ule wa wiki siku mbili mwanafunzi hajaja tofauti na ile drop out  kabisa haonekani bila taarifa   mwaka miezi tunamshukuru mkuu wetu wa wilaya kwa suala hili anatusaidia sana kudhibiti utoro usiendelee.

  Jitihada za mkuu wa wilaya huyo katika kuwarudisha skuli wanafunzi watoro  zinaendelea vyema ambapo awali kabla ya  kuwa mkuu wa wilaya hiyo suala hilo lilikuwa kubwa katika wilaya hiyo ambapo  zaidi ya wanafunzi elfu saba   katika maeneo mbali mbali walikuwa nje ya skuli   ambapo kwa sasa  zaidi ya wanafunzi elfu moja wamerejea skuli huku mpango wa serikali ni kuwatafuta na  kuwarudisha wanafunzi elfu tatu   wa skuli za msingi kwa kipindi cha miaka mitatu ndani ya wilaya hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI