ZAWA YA WATAKA WANANCHI WALIOLALAMIKA KUKOSA HUDUMA HIYO KUVUTA SUBRA TATIZO LINASHUGHULIKIWA.

NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA

 Mamlaka ya maji Zanzibar zawa  kisiwani pemba imesema inendelea na zoezi la usafirishaji wa mabomba   makontena  na  pampu  kutoka kisiwani unguja ili  kupeleka na  kuendeleza harakati  za uboreshaji  na ubdilishaji wa mabomba na mashine  katika baadhi ya maeneo ambayo yanayokosa  pamoja na kupata kwa mgao huduma ya maji . 

Mamlaka hiyo imewataka wananchi kisiwani humo kuendelea kusatahimili  kutokana na kukosa huduma ya maji safi na salama katika meneo yao  ambapo imesema mamlaka hiyo inaendelea kulipatia ufumbuzi  suala hilo ili waweze kupata huduma hiyo bila ya usumbufu kama ilivyokuwa awali.

Akizungumza na habari hizi  kwa  niaba ya mkurugenzi wa mamalka hiyo kisiwani pemba Ofisa Mahusiano  mamlaka ya maji zawa   Sleiman  Anass Massoud  amesema  mamlaka inaendelea kufuatilia upatikanaji wa mashine   itakayosaidia kufikisha maji katika vijiji hivyo  jambo ambalo tayari limefanikiwa kwa hatua kubwa hadi kufikia sasa. 

"Tunaendelea na utaratibu tu wa usafirishaji wa vifaa  ili  kuweza kurejesha huduma ya maji pamoja  na mashine zilizounguwa  kufungwa mpya
 katika baadhi ya visima vilivyoungua mashine" 

"Lakini pia tunaendelea kutekeleza miradi ambayo itakapomalizika  itakwenda kumaliza kabisa tatizo la maji kisiwani pemba kwa maeneo yote".

" Ni kweli  Tatizo lipo katika vijiji hivyo na  sababu ni mashine iliyopo katika kisima kilichopo chambani kwa popo  ambayo ndicho kinachopeleka maji katika maeneo  ya kwa gombe  kichanjaani pamoja na maeneo jirani imeharibika   lakini mamlka  inaendelea kulipigia mbio kulipatia ufumbuzi  suala hili  "

Amesema  Tayari mashine zipo bandarini   katika makontena ambapo mara zitakapofika kisiwani pemba moja kati ya mashine hizo itatumika katika kisima hicho. 

  Aliongeza kuwa" Kuthibitisha kwamba suala la kukosa huduma ya maji wananchi wetu sisi mamlaka linatukosesha raha  tumemuomba Makamo wa pili wa rais  kutusaidia kufunguliwa kwa urahisi makontena ambayo yana vifaa vya  maji  vilivyotoka oman ambayo  yapo bandarini   vifanyiwe urahisi  vitolewe na viweze kugawiwa  vitakavyoletwa pemba viletwe na vitakavyobaki unguja vibakie 

"Na mkurugenzi wetu hivi ambavyo tunaongea yupo unguja anashuhulikia suala  hilo   ili wananchi wasiendelee kuteseka maji ndio uhai Alisema".

" Aliongeza kuwa  Mashine iliharibika na kuungua tulitengeza  kuona kama itakubali   tuweze kuirudisha lakini haikukubali  tena hivyo zipo mashine ambazo  zimeagizwa na mda wowote kutoka sasa zitafika kisiwani pemba  kwajili ya visima mbali mbali  moja kati ya visima hivyo ni  kisima cha popo kilichopo Chamabani" . 

Aidha alisema  kuwa  Mamlka haikuwa na namna nyengine juu ya suala hilo kutokana na mashine iliyoharibika kutokubali kupandisha maji kupeleka katika vijiji hivyo licha ya matengenzo iliyofanyiwa. 

 "Mashine iliharibika mia fil mia  ililazimika ipatikane kama ile iliyoungua  ambayo ni  11kilowat tu kusafirishia maji tulijarivu kuingiza mashine kubwa haikukubali tukaitoa ndio mana tatizo likadumu kwa muda wa miezi  sasa kwa vile ililazimika kupatikana mashine  (Pampu) kma  ile  tunasubiri kuipokea tu kisiwani pemba kuweza kuwatatulia shida hiyo.
  
Alisema  ni kweli  maji ndio kitu muhimu katika harakati za kila siku ambapo  amewaahidi wanachi hao kutegemea   mambo mazuri kutoka mamlka ya maji  ambapo amesema lich  hatua hizo lakini pia  katika maeneo yao ujenzi wa tangi kubwa la maji unaendelea ambapo utakapokamilika  utasaidia  juwaondoshea shida ya maji wananchi wote. 


 Aidha Afisa huyo ametaja baadhi ya meneo ambayo  mamlka inaendelea kuyasimamia kupata ufumbuzi kumaliza tatizo la kukosa hudua ya  maji safi na salama kutokana na kupata maji kwa mgao huku mengine y kikosa kabisa  kisiwani pemba katika wilaya ya chake chake wete  micheweni na mkoani 


ambapo ameyataja maeneo hayo kuwa ni pamoja na  kichanjaani, Chanjani, kwa Gombe, Pujini dodo, Kilimni  banaani madungu chanjaani, Chuchuu, Shaurikani, Mjana pweza, Matale, kitwea, Mtangani Mtambile Chambani,  pandani, Makangale, Kiuyu maziwa ngombe pamoja na kiuyu mjini 

Katika hatua nyengine Afisa huyo amesema kuwa mamlaka hiyo inaendelea na ujenzi na  uchimbaji na uboreshaji wa  visima vya maji  pamoja ma ujenzi wa matangi  ili kuendelea kuwapatia huduma bora zaidi wananchi  maeneo ya miji vijiji. 

"Tunaendelea kubadilisha mabomba kuchimba visima pamoja na kulaza mabomba mapya   takriban maeneo yote  ya wilaya kisiwani pemba na hii ninkutokana na kuongezeka kwa matumizi ya maji yatakayisaidia  kuondoa usumbufu maeneo hayo nikiyoyataja na maeneo mengine. 

"Yapo mabomba ambayo kutokana na kuongezeka mahitaji kwa sasa yamekuwa hayatoshelezi, mengine ni bomba chakavu  jambo ambalo linasababisha baadhi ya vijiji hivyo kupata maji kwa mgao.  " 

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI