TUSHIRIKIANE KUTOA TAARIFA ZA UHALIFU.



NA AMINA AHMED MOH’D   PEMBA

Mkuu wa wilaya Ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuendelea kutoa mashirikiano katika kudhibiti vitendo vya uhalifu kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya sheria  husuan ni katika meneo  yenye bandari zisizo rasmi katika wilaya hiyo. 

Amesema Mashirikiano wanayoendelea kuyatoa kwa serikali na jeshi la Polisi kuripoti taarifa za kiuhalifu zinazijitokeza imekuwa chachu ya  kudhibiti mali  za serikali zisiuzwe kinyemela ikiwemo Makonyo na karafuu.

"Wananchi  wa kaazi  chake chake suala la kupambana na vitendo vya kihalifu  ni suala la kila mmoja wetu sio la serikali peke yake   mashirikiano mnayoonesha kupambana na masuala haya ni vyema tuyaendeleze kutoa taarifa serikali iweze  kuchukua hatua."

Aidha aliwataka wananchi wanaokaa katika maeneo  ya bahari kutoa taarifa  za uingiaji wa wageni katika maeneo yao ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria. 

" wapo baadhi ya watu hutumia maeneo ya bandari zisizo rasmi  kuingiza na kusfirisha bidhaa lakini pia wageni kutoka meneo mengine wananchi msisite kutoa taarifa kama hizi zitasaidia kuimarisha usalama" .
     Abdalla Rashid Ali   Mkuu w wilaya ya Chake Chake

Alisema Mashirikiano hayo yanaendelea kuzaa matunda katika kudhibiti upotevu wa mali za serikali ambazo bila kudhibitiwa  na wananchi kutoa taarifa zingefanikiwa kupoyea na kupoteza pato la taifa. 

" Ni juzi tu tumewakamata baadhi ya wananchi  wasiopemdabkufuata sheria wakiwa na polo zaidi ya 80 za makonyo  Makavu wakiwa tayari wanayasafirisha kupitia bandari zisizo rasmi lakini wananchi walitoa  taarifa  askari wetu  wa kmkm pamoja na uongozi wa wilaya ulifika na kunusuru   ".

Katika Hatua nyengine Mkuu wa wilaya hiyo  Amewapongeza wananchi wa wilaya hiyo kwa kuendelea kutumia  Shirika la biashara la ZSTC kuuza  karafuu zao  kwa mujibu wa sheria.

" Niwatake wananchi waendeleze suala hili la uuzaji wa karafuu zao  katika  maeneo yaliwekwa na serikali  pia niwapongeze kuona wananchi wanayatumia vyema hadi sasa hakuna taarifa za kuwepo kwa waliokiuka agizo hilo nankuuza kimagendo.

 Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI