Posts

Showing posts from December, 2022

KIONGOZI MWANAMKE ANAEONGEZA KASI YA MAENDELEO KATIKA MKOA WAKE NDANI YA KIPINDI KIFUPI CHA UONGOZI. Uboreshaji wa huduma Muhimu za kijamii ikiwemo Maji, Skuli, Masoko Na vituo vya Afya. Usimamiz bora uwajibikaji i na utayari wa utendaji kazi waelezwa kuchagia kasi hiyo

Image
NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA  NI KIPINDI Cha Miaka Miwili ( 2) Tangia Rais wa Zanzibar  Dk Hussein Ali Mwinyi  Kumteua  Salama Mbarouk khatib Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Kushika Nafasi hiyo ambapo Mnamo Siku yaTarehe  1/12/2020 Alimteua Rasmi kushika   nafasi hiyo. Ni Salama Mbarouk khatib ni Mwanamke  1  Pekee alieteuliwa  katika Serikali ya Awamu ya nane ya Mapinduzi ya Zanzibar kati ya Wakuu wa Mikoa 5 waliopo  Zanzibar ambapo ni sawa na asilimia  20 ya viongozi wote ambao wameshika nafasi hiyo kwa wanawake .  Zanzibar ina jumla ya Mikoa 5   Mitatu  kati ya hiyo inapatikana kisiwani Unguja na Miwili iliyosalia ikiwa ipo kisiwani Pemba.    Mabadiliko makubwa yanaendelea kujitokeza katika Mkoa Wa Kaskazini Pemba katika kipindi Kifupi  cha Miaka Miwili.  Miingoni Mwa Mabadiliko hayo ni pamoja na Ujenzi  wa Matangi ya kuhifadhia Maji,   Vituo vya Afya, Skuli, Umem...

PEMBA PRESS CLUB YATOA NENO KWA WAANDISHI WA HABARI.

Image
Na AMINA AHMED MOH’D.  WAANDISHI wa Habari  Kisiwani Pemba wameaswa  kufuata maadili  ya uandishi wa habari   kwa kufanya kazi zao wakiwa makini hasa wanapotumia mitandao ya kihamii ili kuepusha migogoro . Ushauri huo umetolewa na Mwenyekiti Mstaafu wa Club ya waandishi wa habari Pemba PPC Said Moh'd Ali   alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano mkuu maalumu ulioandaliwa na Club hiyo uliofanyika katika ukumbi  wa Maktaba Chachani Chake Chake. Alisema  iwapo waandishi watafuata maadili na kutumia taaluma  yao ipasavyo  kutaepusha migogoro katika jamii ambayo inaweza kuchangia uvunjifu wa amani.  Kwa upande wake Mwenyekiti wa Klabu hiyo Bakar Mussa Juma  Amewataka waandishi wa habari ambao hawajawa wanachama kujiunga na club hiyo ili kuwasogeza karibu na wenzao.  Akisoma  maazimio ya club hiyo  kwa mwaka 2023  imeweka mikakati ya kuboresha  shughuli za...

Zoezi la Usafi Hospitali ya Chake Chake

Image
Na AMINA AHMED     MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali  leo ameongoza zoezi la  ufanyaji wa usafi katika hospitali ya wilaya Chake Chake lilioandaliwa na Bodi ya mapato Zanzibar ZRB ikiwa ni muendelezo wa mwezi wa kurejwsha shukurani kwa mlipa kodi.  Akizungumza   na watendaji wa ZRB mara baada ya kumalizika kwa zoezi hilo Mkuu wa Wilaya huyo Amesema kuwa suala la usafi katika Hospitali lina umuhimu mkubwa kwa afya ya wagonjwa, wauguzi na watu wengi wanaofika katika maeneo hayo .  Amesema kuwa   kuwepo kwa mazingira safi  kutasaidia kupatikana afya  bora kwa wananchi ambao wao ndio walipaji wa kodi zinazosaidia  kuleta Maendeleo.  Mapema Mkurugenzi wa Bodi ya Mapato Zanzibar ZRB  Pemba Jamal Hassan Jamal amesema ZRB itaendelea kuunga mkono upatikanaji wa huduma bora za kijamii kupitia kodi wanazolipa kwa kurejesha shukurani. Kwa upamde wake Daktari dhamana Hospitali ya Chake Chake Dr...

DC CHAKE ATOA NENO KWA WATENDAJI WA ZRB.

Image
Na Amina Ahmed Moh’d - PEMBA  MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Abdalla Rashid Ali amesema uhusiano nzuri baina ya Bodi ya Mapato Zanzibar(ZRB) na Wafanyabiashara utatanua wigo katika kuongeza katika ukusanyaji wa Mapato. Mkuu wa Wilaya huyo ameyasema hayo leo huko Katika ukumbi wa ZRB Gombani alipokuwa. akizungumza na Wafanyabiashara wa kisiwani Pemba ikiwa ni katika wiki ya kurejesha shukurani na furaha kwa mlipa kodi. Amesema wao kama viongozi wanajukumu ya kusimamia mipango ya serikali watatumia nafasi zao kuwaunganisha wafanyabiashara  na ZRB ili kila mmoja aweze kutekekeza majukumu yake kwa ufanisi bila ya kuwepo kwa mivutano. Mapema Mkurugenzi wa ZRB Pemba Jamal Hassan Jamal amewataka wafanyabiashara kuondelea kulipa kodi kwa hiari. Wakizungumza kwenye mkutano huo baadhi ya wafanyabiashara wa kisiwani Pemba wameendelea kuomba kuondoshewa changamoto zilizopo ikiwemo kodi kubwa ambazo ni kikwazo kwa maendeleo yao Pamoja na michango uliotolewa n...

MWAKILISHI JIMBO LA BUBUBU WAJADILI MIRADI YA MAENDELEO NA WANANCHI WAKE.

NA MWANDISHI WETU UNGUJA.   UKUSANAYAJI  wa maoni kwa wananchi wa jimbo la bububu utasaidia kujuwa aina ya miradi itakayowanufaisha wananchi kimaendeleo Hayo yamebainishwa na Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Mhe Mudrik Ramadhan Soraga baada ya mkutano wake na wananchi wa jimbo hilo ili kukusanya maoni ya wananchi kuhusiana na miradi wanatohitaju kutekelezewa huku shehia ya bububu Wilaya ya Magharib A Unguja.   Amesema ziara hizo zimekuwa zikifanyika mara kwa mara ndani ya jimbo lake kupitia kamati yake zenye lengo la kuibya miradi itokanayo na maoni ya wananchi kwa ajili ya utekelezaji ili kuboresha maisha ya wananchi ikiwemo wazee, vijana na watoto ndani ya jimbo hilo  Ameongeza kuwa kufuatia maoni waliyoyakusanya kutoka kwa wananchi hao kamati yake itayachukulia kwa umuhimu mkubwa na anaamini yatasaidia kutekeleza ahadi alizoahidi wakati alipokuwa akiomba nafasi hiyo sambamba na kuomba mashirikiano ya wananchi katika utekelezaji huo “Kupitia maoni haya naamini tutaibu...

Watumishi wa umma wapewa neno

WATUMISHI WA UMMA  WAMETAKIWA KUFUATA MUONGOZO NA KANUNI ZA KAZI KATIKA UTEKELEZAJI WA KAZI  ZAO ILI  KURAHISISHA SHUGHULI ZA KUKUZA ZA MAENDELEO  NA KUPELEKEA KUIMARIKA KWA UKUAJI  WA UCHUMI NCHINI. AKIZUNGUMZA WAKATI AKIFUNGUA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA AFISI YA RAISI KAZI UCHUMI NA UWEKEZAJI HUKO UKUMBI WA AJIRA WA OFISI HIYO MWANAKWEREKWE KAMISHNA WA KAMISHENI YA KAZI RASHID KHAMIS  OTHUMAN AMESEMA MABADILIKO HAYO YANAWEZA KUFIKIWA KWA HARAKA  ENDAPO KUTAKUWEPO NA MASHIRIKIANO YA PAMOJA BAINA YAO AMESEMA KUWA NI VYEMA KWA KILA MTUMISHI KUHAKIKISHA ANATEKELEZA WAJIBU WAKE ILI KUONA MALENGO YA SERIKALI YA KUWA NA WATUMISHI BORA YANAFIKIWA NA KULETA MAFANIKIO HIVYO AMEWWTAKA  WAFANYAKAZI  HAO KUJIFUNZA ZAIDI  KATIKA MASUALA YA SHERIA  ZA KAZI  HATUA AMBAYO  ITASAIDIA  KULETA  MATOKEO MAZURI  HAPO BAADAE  NA KUJENGA UFANISI  AMESEMA  NI WAJIBU  KWA KILA MTUMISHI  KATIKA SEKTA YA UMMA...

MAKAMU WA PILI ATOA AGIZO ZAWA

Image
Na AbdulRahim Khamis Unguja   MAKAMU Wa  pili wa Rais w Zanzibar Hemed Sleiman Abdulla  ameutaka Uongozi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kuisimamisha mara moja Kampuni ya Ms/Sapphire Engineering (t) Limited) pamoja na kufuta Mkataba baada ya kuidanganya Serikali kwa kuchelewesha kufikisha Tangi la maji eneo la Raha Gando Mkoa wa Kaskazini Pemba.   Mhe. Hemed ameeleza hayo katika Kikao kazi cha kujadili maendeleo ya Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kilichofanyika Makao Makuu ya Mamlaka hiyo Mayugwani Jijini Zanzibar.   Amesema kitendo  cha kuidanganya Mamlaka hiyo kuhusu kuchelewesha kufikisha Tangi hilo ni kitendo cha kuonesha udhaifu wake katika kazi hizo na kueleza Mamlaka husika kuchukua hatua za kisheria.   Amesema Serikali imetenga fedha nyingi kwa kuwafikishia Huduma ya Maji Safi na Salama  wananchi wake kwa muda wote na kushangazwa kuona baadhi ya watu kwenda kinyume na Juhudi hizo.   Mhe. Hemed ameitaka Mamlaka hiyo kupitia mik...

Wana CCM wampokea kwa vishindo Dk Mwinyi

NA HANIFA SALIM, PEMBA MAKAMU Mwenyekiti wa (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewahakikishia wananchi wa kisiwa cha Pemba, kwamba katika miaka mitatu ijayo ataweka juhudi maalumu za ziada kuhakikisha ahadi zote alizoziweka zinatekelezwa.  Dk. Mwinyi alisema, atahakikisha atakaporudi kwa wananchi katika kipindi cha kampeni ahadi alizoziweka amezitekeleza, huku akiahidi kutumia nguvu zake zote katika kuwatumikia wananchi wa Visiwa vya Zanzibar. Aliyasema hayo katika mkutano wa ndani wa mapokezi ya Makamu mwenyekiti wa (CCM) Zanzibar, Kisiwani Pemba uliofanyika katika kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake chake.  Alieleza, kwa mujibu wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) anatakiwa atekeleze ahadi alizizoweka kwani ndio mkataba wake na wananchi, itakapofika 2025 wananchi watakua wanahitaji majibu ya ahadi alizowapa. Alisema, nchi haiwezi kupata maendeleo bila ya uwepo wa amani, utulivu, umoja, mshik...

MKUU WA MKOA KASKAZINI PEMBA AKABIDHI MSAADA WA CHAKULA KWA FAMILIA 100 ZENYE HALI NGUMU KANGAGANI AWAHAMASISHA KUDAI RISITI ZA KIELECTRONIKI.

Image
Na AMINA AHMED MOH’D.  MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib Amewataka wananchi  kutoa mashirikiano kwa Bodi ya Mapato Zanzibar ZRB  Kwa kudai risiti za kielectroniki wanaponunua bidhaa  mbali mbali ili bodi hiyo  iweze kukusanya kodi kwa usahihi  kutoka kwa wafanya biashara   kodi ambazo  zitasaidia kuleta maendeleo kwa Wananchi Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi  wa kijiji cha kangagani  katika ghafla ya kupoeana kukabidhi msaada wa chakula uliotolewa na  na Bodi ya mapato Zanzibar kwa familia 100  zenye Hali ngumu kijijini humo ikiwa ni  Wiki maalum ya kurejesha shukurani kwa walipa kodi nchini.  Amesema iwapo wananchi watatoa mashirikiano na kuunga mkono  Ununuaji wa bidhaa kwa kudai risiti za kielektronik kutasaidia kudhibiti upotevu wa kodi  na kutumika kodi hizo katika ujenzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo unguja na Pemba na kutumika kwa maslahi ya Ta...

MBINU BORA ZINAHITAJIKA KUHAMASISHA JAMII

Image
NA FATMA SULEIMAN- PEMBA.  KATIBU Mkuu Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo bi  Fatma Khamis Rajab amewataka wadau wa lugha ya kiswahili kubuni mbinu bora na katika kuhamasisha jamii na kupata wadau wengi ili kuinyanyua zaidi lugha hiyo pamoja na  kuunga mkono juhudi za raisi wa Zanzibar katika kukikuza kiswahili ndani na nje ya nchi. Ameyasema hayo wakati akiahirisha Kongamano la 6 la Kiswahili la Kimataifa liloambatana ziara maalum ya kutembelea sehemu za kihistoria huko Mnara wa Kigomasha Shehiya ya Makangale Mkoa wa Kaskazini Pemba. Aidha Katibu mtendaji BAKIZA Bi Saade Mbarouk ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana kujitoa katika kujifunza kiswahili kwani Baraza lina mpango wa kuanzisha mafunzo ya kiswahili kwa wageni jambo litakalosaidia kupata fursa hasa kwa vijana.   Akitaja mchango wa mabaraza ya kiswahili Konsolata Mushi Katibu Mtendaji BAKITA amesema mabaraza yameweza kuleta tija kwani yanasimamia maendeleo ya matumizi ya lugha hiyo kikanda...

MKURUGENZI ZRB PEMBA JAMAL HASSAN JAMAL ATOA ELIMU KWA WAFANYA BIASHARA WETE

Image
Na AMINA AHMED MOH’D    PEMBA.  MKURUGENZI wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) Pemba, Jamal Hassan Jamal amewataka wafanya biashara waendelee kuiunga mkono serikali yao ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kulipa kodi kwa mujibu wa utaratibu na sheria zinavoelekeza. Aliyasema hayo mara baada ya kuwatembelea wafanya biashara wa Mji wa Wee , ambapo ni utaratibu wao kila ifikapo Disemba ya kila mwaka kupita kwa wafanya biashara kutoa shukurani na kusikiliza changamoto, ushauri na maoni yao juu ya utendaji kazi wa ZRB. Amesema, wafanya biashara wa Mji wa Wete kwa  asilimia kubwa wamefurahishwa na ujio wa watendaji wa ZRB ambapo wamefahamu kwamba bodi inafanya kitu kizuri cha kurejesha shukurani kwa wafanya biashara. "Kiukweli tumefikia sehemu nzuri ZRB na wafanya biashara, tumechukua changamoto zao zinazotokana na sheria zetu za kodi, viwango vya tozo ambazo wanalipa, nyengine zinatokana na uwelewa mdogo ambapo tumechukua nafasi ya kuwapa elimu",alisema. Aidha alisema, mbali ya kup...

WAFANYA BIASHARA WAFURAHISHWA NA MASHIRIKIANO WANAYOYAPATA KUTOKA BODI YA MAPATO ZANZIBAR ZRB.

Image
Na AMINA AHMED MOH’D          Jamal Hassan Jamal - Mkrugenzi   ZRB  Pemba  . WAFANYA biashara wa bidhaa mbali mbali  Katika Mji Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba wameishukuru Bodi ya Mapato Zanzibar ZRB  kwa kuendelea kuwapa elimu  Mashirikiano pamoja na  maelekezo mbali mbali ya  ulipaji wa   kodi kwa njia sahihi  .   Wametoa Shukurani hizo walipokuwa wakizungumza mara baada ya kutembelewa na kupewa Elimu  na Ofisa kutoka bodi  hiyo ikiwa ni shamra shamra za  wiki ya Mlipa kodi  .  Wamesema Masirikiano hayo wanayoyapata kutoka kwa bodi hiyo  yanasaidia kupata ufumbuzi wa changamoto mbali mbali zonazohusu ulipaji wa kodi  pamoja na utumiaji wa mashine na utowaji wa Risiti za Kielectroniki .  "Tunapata mashirikiano katika kutatua changamoto mbali mbali zinazohusu biashara zatu lakini ulipaji wa kodi   tunapata Elimu inayosai...

LICHA YA JUHUDI KUCHUKULIWA NA VIONGOZI WA SHEHIA GOMBANI BADO WALIA KUKOSA HUDUMA YA MAJI MIEZI SABA SASA .

Image
NA AMINA AHMED MOH’D  UKOSEFU wa huduma ya maji katika Baadhi ya Maeneo Shehia ya Gombani wilaya Ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Waathirika wakubwa ni wanawake na watoto. Harakati hizi Mapema leo Asubuhi zilifika ili kuthibitisha kilio  hicho na kamera za Habari hizi zikawaanasa Baadhi ya watoto wakitembea masafa marefu  huku wakiwa na ndoo kichwani wakitoka kuifata huduma hiyo  Katika eneo la Msikiti Uliopo karibu na Ofisi za Serikali Huku wengine wakionekana kuelekea huko  kuifata huduma hiyo. Sheha wa Shehia ya Gombani Subira  Abdalla Juma akizungumza na habari  hizi Alisema kuwa Upatikanaji wa huduma ya Maji katika shehia hiyo umekuwa  mkubwa licha ya   ya Uongozi wake kuchukua  hatua mbali mbali. "Tatizo hili la ukosefu wa Maji  Safi na Salama  Gombani si baadhi ya Maeneo tu nasubutu kusema ni Gombani nzima  hapo mwanzo yalikuwa yanapatikana walau baadhi ya maeneo lakini  saivi ni mote inakar...

MAKAMU WA PILI WA RAIS ATOA NENO KWA WAZAZI.

Image
Na - ABDULRAHIM KHAMIS WAZAZI na Walezi Nchini wametakiwa kushirikiana katika Malezi ya pamoja ili kupata kizazi chenye Maadili Mema. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Hemed Suleiman Abdulla alitoa wito huo wakati akiwasalimia Waumini wa Masjid Salummka  Miti Ulaya alipojumuika nao katika Ibada ya Sala ya Ijumaa.   Amesema Zanzibar ilisifika kwa Mila na Desturi njema zilizojengeka kwa  Jamii kulea Watoto kwa pamoja ambapo jamii ya sasa imekosa malezi hayo hatua ambayo inapelekea kupata kizazi kilichokosa maadili.   Aidha amesema  Uislamu umeelekeza namna ya kulea watoto kupitia kitabu kitukufu cha Qur-ani pamoja na Hadithi za Mtume Muhammad (S.A.W) jambo ambalo jamii ya wazanzibari ikikishika Kitabu hicho itaweza kupata Kizazi kitakachoshika Qur-ani. Alhajj Hemed ameongeza kuwa miongoni mwa jukumu la wazazi ni kulea watoto na kuwakuza katika makuzi mema jukumu ambalo siku ya Kiama kila mzazi ataulizwa na Allah Mtukufu namna alivyolea watoto wake.   A...

Viongozi wa chama waaswa na Jeshi la Polisi.

Image
Na Amina Ahmed Moh'd. JESHI la polisi Mkoa wa kusini Pemba  limewashikilia na kuwahoji  watu wawili  kwa tuhuma za kutoa maneno ya  uchochezi na  matusi  dhidi ya   viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya  kupinga uteuzi wa Mkurugenzi  Mkuu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Ndugu Thabit Idarous faina na kusambaza kashfa  na maneno hayo katika mitandao ya kijamii .  Watu hao  ambao  ni Salum Abdalla Herezi (maarufu Mwalim  Herezi ) ( 65 ) ambae ni mjumbe  wa kamati ya uongozi jimbo la Mtambile  Kupitia  chama cha ACT wazalendo mkaazi  wa Mjimbini  wilaya ya Mkoani  pamoja   Nachia  Ali Jamali ( 39)   mjumbe   wa kamaati ya fedha jiombo la Chamabani  kupitia chama hicho  mkaazi wa wambaa Mkoa wa Kusini Pemba. Akitoa  Taarifa kwa  waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa kusini Pemba  ACP Abdalla Hussein Mussa alis...

MIKAKATI ILIYOUNDWA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI KASKAZINI PEMBA YAZAA MATUNADA WANANCHI WAPATA UELEWA KUYARIPOTI YANAPOJITOKEZA.

Image
NA - AMINA AHMED   MOH’D  - PEMBA.      MASHIRIKIANO  yanayotolewa katika kusimamia mikakati maalum ilionazishwa  na Serikali ya Mkoa wa kaskazini Pemba juu  ya  kupambana na vitendo vya uhalifu  kwa miaka Miwili sasa imesaidia kuongeza uelewa kwa wanajamii juu  ya kuripoti matukio ya udhalilishaji wa kijinisia yanapojitokeza  katika maeneo ya miji na vijiji  mkoani humo.   Akizungumza na habari hizi maalum Kuelekea kilele cha siku 16 za kupinga udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto duniani Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini  Pemba Salama Mbarouk khatib   Alisema  usimamizi na mashirikiano yanayoendelea kuoneshwa  katika utekelezaji wa mikakati hiyo  iliyowekwa  imesaidia   kukuza uelewa wa wanajamii  ndani ya mkoa huo ambao kwa sasa wamekuwa na muamko mkubwa wa kuyaripoti matukio ya udhalilishaji katika vyombo vya sheria na kuchukuliwa hatua .  ...

Siku 16 za kupinga udhalilishaji wa kijinsia. Jeshi la polisi lafanya haya.

Image
Na- Abel Paul Arusha.    JESHI   la Polisi la Mkoa wa Arusha limetoa huduma ya matibabu na ushauri wa kiafya katika kituo cha AST maalumu kwa ajili ya kuwalea wazee wanaoishi katika mazingira magumu Jijini Arusha.   Mwenyekiti wa mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Arusha (TPF NET) Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP MARY KIPESHA amebainisha kuwa  kupitia mtandao huo wametoa msaada wa vitu mbalimbali pamoja na huduma ya kiafya ikiwa mwendelezo wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mkoani humo.   ACP Kipesha amesema mbali na kutoa msaada huo, katika siku hizo 16 za kupinga ukatili amebainisha kuwa wametoa  elimu katika shule, hospitali, nyumba za ibada, masoko pamoja na stendi za mabasi ambapo jamii imepata uelewa wa kutosha.   Mkurugenzi wa Kituo hicho Bi. Ester Njau amelishukuru Jeshi hilo kwa kutoa matibabu kwa wazee wanaoishi katika kituo hicho ambapo amebainisha kuwa matibabu hayo pamoja na vitu mbalimbali vilivy...

Shamra shamra kuelekea siku ya Rushwa

Na Fatma Suleiman Pemba.  Tarehe 9 Disemba duniani kila mwaka huadhimisha siku ya Kupambana na Rushwa   ambapo serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kupitia ZAECA inaungana na Mamlaka nyengine  katika kupinga  Vitendo hivyo vya Rushwa na Uhujumu uchumi.  Katika kuelekea siku hio zaeka  Mkoa wa Kusini  Pemba imefanya matembezi  yaliyokuwa na lengo la uhamasishaji wananchi juu ya kupinga vitendo vya Rushwa na Uhujumu Uchumi.  Katika matembezi hayo yaliyoanzia benk Chake Chake hadi Uwanja Gombani yaliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Chake Abdalla Rashid Ali ambapo vikundi vya Mazoezi  na  wananchi pia walishiriki.    Akizungumza mara baada ya matembezi hayo Mkuu wa Wilaya ya chake chake Abdalah Rashid Ali amesema matembezi hayo ni muhimu saba kwani yanaunga mkono jitihada za serikali za kupambana na rushwa visiwani hapa Kaimu kamanda wa zaeka mkoan WA kusini Pemba amesema wamejipanga kuhakikisha wanafikia ma lengo ya kupambana n...