Viongozi wa chama waaswa na Jeshi la Polisi.

Na Amina Ahmed Moh'd.

JESHI la polisi Mkoa wa kusini Pemba  limewashikilia na kuwahoji  watu wawili  kwa tuhuma za kutoa maneno ya  uchochezi na  matusi  dhidi ya   viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya  kupinga uteuzi wa Mkurugenzi  Mkuu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Ndugu Thabit Idarous faina na kusambaza kashfa  na maneno hayo katika mitandao ya kijamii .

 Watu hao  ambao  ni Salum Abdalla Herezi (maarufu Mwalim  Herezi ) ( 65 ) ambae ni mjumbe  wa kamati ya uongozi jimbo la Mtambile  Kupitia  chama cha ACT wazalendo mkaazi  wa Mjimbini  wilaya ya Mkoani  pamoja   Nachia  Ali Jamali ( 39)   mjumbe   wa kamaati ya fedha jiombo la Chamabani  kupitia chama hicho  mkaazi wa wambaa Mkoa wa Kusini Pemba.

Akitoa  Taarifa kwa  waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa kusini Pemba  ACP Abdalla Hussein Mussa alisema  watu hao ambao ni wafuasi wa chama cha ACT wazalendo  wameshikiliwa siku ya tarehe 10  kwa nyakati tofauti  kufuatia doria maalum iliyofanywa na jeshi hilo  katika maeneo mbali mbali ya Mkoa huo  ikiwa ni  harakati maalum za kuendelea kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo tofauti  ndani ya Mkoa huo.
         ABDALLA HUSSEIN MUSSA   -ACP KUSINI PEMBA.

 Alisema  kuwa mnamo  siku ya tarehe 5/12 / 2022 majira ya saa nne mpka saa sita za mchana  katika ofisi za  chama cha ACT wazalendo  eneo la Mtambile   Mkoa wa kusini Pemba wakiwa   katika kikao cha ndani   ya chama hicho viongozi hao walitoa maneno ya kashfa  na matusi   dhidi ya viongozi wa chama cha Mapinduzi  na kusambaza katika mitandao ya kijamii Jambo ambalo ni kosa.

Aidha jeshi  hilo limesema  bado linaendelea na upelelezi juu ya suala hili na  mara jeshi litakapokamilisha upelelezi huo litakapofanikisha upelelezi huo hatua nyengine za kisheria zitachukuliwa ikiwemo kufikishwa mahakamani wale wote watakaotiwa hatiani Juu ya uchochezi  pamoja na usambazaji wa kashfa hizo katika mitandao ya kijamii.

Aidha Jeshi La polisi Mkoa wa kusini Pemba limewataka  Viongozi wa  vyama vya siasa  Kutumia vyema uhuru na  fursa iliyotolewa kufanya mikutano ya ndani kwa kuzinagatia sheria  kanuni na taratibu ya ufanyaji wa mikutano hiyo.

 Katika hatua nyengine kamanda huyo Alisema kuwa hali ya ulinzi na usalama katika Mkoa huo inendelea vyema  kutokana na mashirikiano yanaoendelea kutolewa na wananchi .

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI