LICHA YA JUHUDI KUCHUKULIWA NA VIONGOZI WA SHEHIA GOMBANI BADO WALIA KUKOSA HUDUMA YA MAJI MIEZI SABA SASA .

NA AMINA AHMED MOH’D 

UKOSEFU wa huduma ya maji katika Baadhi ya Maeneo Shehia ya Gombani wilaya Ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Waathirika wakubwa ni wanawake na watoto.


Harakati hizi Mapema leo Asubuhi zilifika ili kuthibitisha kilio  hicho na kamera za Habari hizi zikawaanasa Baadhi ya watoto wakitembea masafa marefu  huku wakiwa na ndoo kichwani wakitoka kuifata huduma hiyo  Katika eneo la Msikiti Uliopo karibu na Ofisi za Serikali Huku wengine wakionekana kuelekea huko  kuifata huduma hiyo.

Sheha wa Shehia ya Gombani Subira  Abdalla Juma akizungumza na habari  hizi Alisema kuwa Upatikanaji wa huduma ya Maji katika shehia hiyo umekuwa  mkubwa licha ya   ya Uongozi wake kuchukua  hatua mbali mbali.

"Tatizo hili la ukosefu wa Maji  Safi na Salama  Gombani si baadhi ya Maeneo tu nasubutu kusema ni Gombani nzima  hapo mwanzo yalikuwa yanapatikana walau baadhi ya maeneo lakini  saivi ni mote inakaribia  Miezo saba kama sio Mwaka.

" Napiga kelele kulisemea tatizo  kadri ya uwezo wangu kwa Viongozi wa juu, Mpka Serikali ya wilaya inatusaidia ilitoa ruhusa kuzibuliwa kwa Tangi Lililopo nyuma hospitali ya Chake Chake ili tupate Maji yalikuja siku mbili hayakuja tena" .

"Wawakilishi wetu na wabunge Tuliwatafuta tukawaelezea suala hili  walipofuatilia Zawa waliambiwa ni Transoma wakajitolea ikaletwaimefungwa siku mbili  halo ikawa ni ile ile tukaenda kuwalilia tena wakaambiwa Mchikichi wametuletea lakini kiukweli nao haukusaidia mana tuliambiwa umeharibika hatujajua bado tatizo ni nini Gombani mana Tumeshajitahidi na visima vipo vingi lakini maji hatupati.

Aidha Subira Alisema kuwa   usumbufu huo wa kukosa huduma ya Maji kijiji kizima cha Gombani ni takribani Mwezi wa Saba  Sasa ambapo wananchi wake hulazimika  kutafuta maji kwa majirani ambao wamechimba visima katika majumba yao Huku wengine kusubiri Lulu hiyo katika baadhi ya miferji ambayo yanatoa maji kwa baadhi ya wakati.

" Siku moja moja kuna baadhi ya nyumba mifereji yao hutoa maji apo tena watu hupigiana simu  wakaenda kupanga foleni watu hawamalizi yanakatwa ,,Wengine  wanapata maji kwa majirani ambao wamechimba visima  ndani mwao tena hiyo usiku, siku nyengine asubuhi, leo nyumba hii kesho ile  binafsi mimi mwenyewe namaliza mitaa kufuata maji apa kidutani kuna nyumba moja tu inayotoka maji.

Alieleza kuwa Shehia ya Gombani  yenye wakaazi 4835  ambao wao ni wanawake  na watoto wamekuwa wakishindwa kufanya shughuli zao kwa wakati kutokana na usumbufu huo .

 Wakizungumza baadhi ya wakaazi wa kijiji cha  Madina    Shehia ya Gombani wameiomba serikali kutolifumbia macho tena suala hili  na badala yake kuwatafutia njia ya kulimaliza Tatizo hili ambalo limeuwa kikwazo ha maendeleo. 
"Gombani ni shehia amayo ipo mjini kabisa vijijini hakuna shida ya maji ajabu  ipo hapa tu leo maji yanatoka kesho hayatoki inatuumiza sana hii, Watoto hawana muda na kucheza   lazima watusaidie kuyatafuta maji hatuna namna akina baba hawasubutu kutafuta kijio na Kuoanga foleni mzigo unatuelemea. Alisema Bi Rahma . 

Akizungumzia Suala hili Ofisa Uhusiano kutoka Mamlaka ya Maji Zanzibar zawa Ofisi ya Pemba Suleiman Anass Massoud Alisema kuwa Mamlaka hiyo inaendelea kulipatia ufumbuzi  tatizo la ukosefu wa Maji  Shehiaya Gombani na baadhi ya shehia jirani ili kuondoa shida kwa wananchi. 

" Nikiri kuwa mara kwa mara tumekuwa tukipokea taarifa kutoka  Shehia ya Gombani wakilalamikia ukosefu wa huduma ya maji Safi na Salama  nikiri hilo,  Viongozi wao wanatupigia mara kwa mara simu, Sio mara moja wala mara mbili ni kipindi sasa lakini naomba tufahamu kuwa  Sio Gombani yote kama inakosa maji, ni baadhi ya maeneo na Structure ya Gombani wanapata maji kwa vianzio tifauti yapo maeneo wanayopata maji kupitia Tangi la Machomane ambayo ni ya mgao , kuna baadhi wanapata kupitia kisima  cha Ng'ambwa na wegine wanapata Kupitia kisima cha Gomban Mchuwa,kwamana iyo utakuta inamapande mapande utokaji wake wa maji. 

Aidha Ofisa huyo alisema kuwa Tathmini ya jumla ya upatikanaji wa maji katika Shehia hiyo linaukubwa ambapo alisema kuwa  baadhi ya maeno yamekuwa  hayafikiwi  kwa sasa ni pamoja na Gombani Madina, Mchuwa, Gombani ya kati, Uwanja Mkongwe. 

Hata hivyo  Ofisa guto Alisema kuwa Mamlaka inaendelea na mipango miwili mikubwa ya kumaliza tatizo la ukosefu wa maji  Gombani.

"Kwanaz tumejaribu kubadilisha mtandao wa maji kutoka katikatangi la maji Gombani ambalo linapokea maji kutoka maeneo ya Ndagoni na wesha tumeunga bomba la nchi 4 Kusaidia Baadhi ya Sehemu ambapo kazi hii inasiku ya nne saivi, na tunatarajia kupata mrejesho kamili jumatatu kuona imefikia wapi  lengo kuweza kuona Mpango huo unasaidia kupatikana maji maeneo ya Gomban Madina ambayo imekuwa haipati na baadhi ya sehemu nyengine.
 
Aliendelea kuwa " Uhakika mkubwa ambao upo kwa Wakazi wa Gombani ni kuwa mamalka imekamilisha uchimbaji  wa visima3  kati ya visima 5 ambavyo vilikuwa vinahitajika, Bomba kubwa ambalo limepimwa kutoka maeneo ya Ng'mbwa Mpka kufika eneo la Gombani Getini, na bomba hilo litapokea maji kutoka katika visima hivyo vitatu vipya  ambavyo  tumevichimba  juzi, tayari vimeshakamilika, Tunachosubiri ni kupigwa mtaro, na hii kampuni ambayo tumikabidhi  kazi, tunamaliza taratibu hizi za utowaji wa tenda, kama miongozo ya Serikali inavyoelekeza zimejitokeza nyingi zimeomba kwaio tayark moja tumeshaona kuwa na muelekeo wa kupata tenda hiyo. 

Alisema kuwa baada ya kuanza kuchimbwa mitaro hiyo bomba hiyo itaanza kutoa huduma ya maji katika maeneo ya Mkoroshoni, Mkanjuni na Gombani  na  Kwale kuondoa kwa asilimia kubwa tatizo la Maji.

Aidha   Suleiman aliwataka wananchi Wa Gombani kuvuta subira na uenelea kupata maji hayo kwa Mgao na kuahidi kuwa Changamoto hiyo italata uhakika wa kumalizika  mwanzoni mwa January 2023.,Huku miradi mikubwa ya Maji ikiwemo Ujenzi wa matangi na Visima  inatarajiwa kuondoa tatizo la Ukosefu wa Maji  Pemba kumalizika Katika kipindi cha February Machi baada ya kukamilika kwa miradi mbali mbali inayoendelea kujengwa kwa Fedha za ahueni ya uviko 19 Kusini na Kaskazini. 

Mwisho
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI