WAFANYA BIASHARA WAFURAHISHWA NA MASHIRIKIANO WANAYOYAPATA KUTOKA BODI YA MAPATO ZANZIBAR ZRB.

Na AMINA AHMED MOH’D 
       Jamal Hassan Jamal - Mkrugenzi   ZRB  Pemba  .

WAFANYA biashara wa bidhaa mbali mbali  Katika Mji Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba wameishukuru Bodi ya Mapato Zanzibar ZRB  kwa kuendelea kuwapa elimu  Mashirikiano pamoja na  maelekezo mbali mbali ya  ulipaji wa   kodi kwa njia sahihi 

 Wametoa Shukurani hizo walipokuwa wakizungumza mara baada ya kutembelewa na kupewa Elimu  na Ofisa kutoka bodi  hiyo ikiwa ni shamra shamra za  wiki ya Mlipa kodi 

Wamesema Masirikiano hayo wanayoyapata kutoka kwa bodi hiyo  yanasaidia kupata ufumbuzi wa changamoto mbali mbali zonazohusu ulipaji wa kodi  pamoja na utumiaji wa mashine na utowaji wa Risiti za Kielectroniki . 

"Tunapata mashirikiano katika kutatua changamoto mbali mbali zinazohusu biashara zatu lakini ulipaji wa kodi   tunapata Elimu inayosaidia katika masuala ya biashara., Awali tulikuwa tunawakimbia tukisikia wanakuja tu  tulikuwa tunaona kama ni usumbufuni kwa sababu Hatukuwa na uelewa  lakini mashirikiano yao leo hii tunajifunza mambo mbali mbali mfano mashine Alisema Abdi Abdalla Omar Mfanya Biashara Konde. 

Hata hivyo  wafanya biashara hao  wameiomba bodi hiyo kuwasaidia kuwatatulia baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikirudisha nyuma harakati zao 
Tunaomba mtusaidie kupunguza changamoto ya usafirishaji wa mizigo lakini tunaomba mtuwekee usawa kwa ulipaji kodi kuwe na asilimia sawa isiwe wengine wanapata ndogo wengine kubwa kwa bidhaa moja, Alisema Muhammad Gharib Moh’d. 

Akizungumza   Mkurugenzi wa Bodi hiyo pemba  Jamal Hassan Jamali  Alisema Bodi hiyo itaendelea kutoa elimu  kwa wafanya biashara ili kuzidisha uelewa juu ya Ulipaji kodi pamoja na kuzipatia ufumbuzi baadhi ya Changamoto zilizotolewa na wafanya biashara ambazo kwa kiasi kikubwa zinahitaji uelewa zaidi  ili kuacha kuona kama ni changamoto.

"Tupo Hapa  Micheweni leo  Katika Mji huu wa konde ikiwa ni Wiki ya Mlipa kodi  Maofisa wetu kwa pamoja tunatoa elimu kwa wafanya biashara lakini pia tunabadilishana mawazo na walipa kodi wet, wamefurahi  kwa ujio huu lakini pia wametupa changamoto zao na sisi tumezichukua kuona vipi tunabadilisha uelewa kwa kile ambacho wamehisi kwao ni Changamoto  Alisema Mkurugenzi. 

 Wiki ya Mlipa kodi  licha ya kuwatembelea wafanya Biashara katika maduka mbali mbali  lakini pia inatarajia kutoa msaada wa kibinaadmu katika hositali ya Abdalla Mzee Mkoani, Pamoja na kutoa misaada kwa familia mbali mbali  ambazo zinaishi katika mazingira magumu . 


  MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI