KIONGOZI MWANAMKE ANAEONGEZA KASI YA MAENDELEO KATIKA MKOA WAKE NDANI YA KIPINDI KIFUPI CHA UONGOZI. Uboreshaji wa huduma Muhimu za kijamii ikiwemo Maji, Skuli, Masoko Na vituo vya Afya. Usimamiz bora uwajibikaji i na utayari wa utendaji kazi waelezwa kuchagia kasi hiyo

NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA 

NI KIPINDI Cha Miaka Miwili ( 2) Tangia Rais wa Zanzibar  Dk Hussein Ali Mwinyi  Kumteua  Salama Mbarouk khatib Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Kushika Nafasi hiyo ambapo Mnamo Siku yaTarehe  1/12/2020 Alimteua Rasmi kushika   nafasi hiyo.

Ni Salama Mbarouk khatib ni Mwanamke  1  Pekee alieteuliwa  katika Serikali ya Awamu ya nane ya Mapinduzi ya Zanzibar kati ya Wakuu wa Mikoa 5 waliopo  Zanzibar ambapo ni sawa na asilimia  20 ya viongozi wote ambao wameshika nafasi hiyo kwa wanawake . 

Zanzibar ina jumla ya Mikoa 5   Mitatu  kati ya hiyo inapatikana kisiwani Unguja na Miwili iliyosalia ikiwa ipo kisiwani Pemba. 

  Mabadiliko makubwa yanaendelea kujitokeza katika Mkoa Wa Kaskazini Pemba katika kipindi Kifupi  cha Miaka Miwili. 

Miingoni Mwa Mabadiliko hayo ni pamoja na Ujenzi  wa Matangi ya kuhifadhia Maji,  Vituo vya Afya, Skuli, Umeme pamoja na Miundo Mbinu ya Barabara.

 Mkoa wa kaskazini Pemba umeundwa na wilaya 2 Wete Na ile ya  Micheweni. 

Kaskazini Pemba ni moja kati ya Mikoa Miwili ambayo inaongoza kwa idadi kubwa ya watu  Zanzibar  Kati ya Mikoa 5 ilyopo ambapo kwa mujibu wa Takwimu za Sensa  ya watu na makazi Mkoa huo una jumla ya watu   272, 091, Wanaume wakiwa  ni 131,484, Na wanawake  140,607, Sawa na Ongezeko la Asilimia 2.3 ukilinganisha na Takwimu za Sensa ya watu na makazi mwaka 2012 ambayo ilikiwa na Asilimia   1.5. 

Kwanini Kasi ya Maendeleo katika kipindi kifupi! 
 
" Tunasimamiwa na kiongozi Sahihi ambae ana maono ya Kuifikisha mbali kimaendeleo Mkoa huu, Usimamizi bora wa Majukumu  Tuliyopangiwa kufuata sheria, kuendana na  kasi ya Mabadiliko  Ambayo Dk Mwinyi Rais wa Zanzibar anaitaka Mashirikiano, kutii Maagizo tunayopewa kama wasaidizi wa Serikali, Lakini pia Kupokea ushauri vipi tutaleta mabadiliko  katika utendaji ni kitu cha kipekee kwetu. "

 Alisema  Hamad Omar Bakar ambae pia ni  Mkuu wa Wilaya ya Wete. 
             HAMAD OMAR BAKAR   DC  WETE 

" Tunapewa Maelekezo  na kiongozi wetu Tunafuata  Tunafanya kazi kwa Moyo mmoja  kusudi tu kuonesha Jamii na Taifa  kama kasi ya Mabadiliko sehemu yeyote ile ni  utayari wala siyo Jinsia".

" Tunakaa tunatafakari mambo mabli mbali Mazuri ambayo yataleta maendeleo kwa Jamii Yataondosha usumbufu kupata Huduma Bora kwa Wananchi Wetu. 

 Alisema Mgeni Khatib Yahya  Mkuu wa wilaya ya Micheweni. 
                 MGENI KHATIB YAHYA - DC MICHEWENI 

UPATIKANAJI WA HUDUMA YA MAJI KASKAZINI AWALI NA  SASA. 

 katika  kipindi Cha Miaka  3 iliyopita upatikanaji wa Huduma ya Maji  Safi na Salama Mkoa wa Kaskazini Pemba Ulikuwa ni asilimia 46  katika Miji na vitongoji vyote ambayo yalikuwa yanapatikana kwa wananchi wote. 

Licha ya Hatua mbali mbali kuchukuliwa lakini upatikanaji wa Maji haukuongezeka kutokana na Miundo mbinu kuwa Midogo ambayo hulazimika kutoa Maji kwa Mgao katika Maeneo Mengi ya Mkoa huo. 

"Moja kati ya Vitu ambavyo nilivipa kipaumbele kuona vinapata ufumbuzi wa kudumu ni huduma ya Maji kwa Wananchi Wangu ni kutokana na Umuhimu wake  hii, Lakini pia nilikuwa najua kwa undani  shida hii ilivyo kwa  vile nilibahatika kuogoza wilaya  za Mkoa huu kabla.
  
"Kuvuja kwa Pakacha ni Nafuu kwa Mbebaji.

" Kulitolewa Fursa Kusemea changamoto za Mikoa  baada ya kuwepo Fedha zile zilizotolewa kwa ajili ya ahueni ya uviko"

 "kwa vile ni kitu ambacho kiliniumiza nilitafakari sasa vipi nitalipatia Ufumbuzi suala hili niliitumia fursa hiyo. 

" Niliwashirikisha wasaidizi wangu tulipeleka Maombi Kwa Serikali kuu ili tusaidiwe suala hili na Mengine . 

Nilifanikiwa Miradi yote ambayo tumeomba imebahatika kutokana na hoja zilizokuwa na Mashiko".  Alisema Salama Mbarouk khatib. 

   SALAMA MBAROUK KHATIB   - RC KASKAZINI PEMBA. 

"Tuliomba kusaidiwa miradi mbali mbali  Elimu, Afya Maji, Barabara, Pamoja na  Masoko  Kaskazini hatukuachwa nyuma tuliletewa Miradi inayotekelezwa kupitia Fedha za ahueni ya uviko 19 Kiukweli nasubutu kusema Tulupendelewa kuoata miradi Mingi Katika Mkoa wangu. 

" Kupatikana Maji kwa Mgao katika baadhi ya Maeneo ndani ya Mkoa wangu ni suala ambalo linanikosesha Usingizi   sababu naelewa waathirika wakubwa ni Wanawake na watoto juu ya hili 

"Alieleza kuwa Mgao huo umetokana na kuongezeka  kwa matumizi na uhitaji wa  maji kwa  wananchi wake  huku Miundo mbinu ya kufikisha maji   ikiwa ni Midogo.

"Katika maeneo mengi Visima  na Mabomba yanayotumika ni  ile iliyowekwa Zamani , na Uhitaji wa Maji ni Mkubwa ukilinganisha na sasa,  tunaendelea na kulipatia ufumbuzi suala hilo ikiwemo Ubadilishwaji wa Mabomba  kwa kushirikiana  na mamlaka yenye dhamana ya kusimamia hili .

 Alisema   Ujenzi unaendelea huku vikiwa vipo  baadhi ya visima ambavyo vilifanyiwa uharaka  ili kusaidia kuongeza upatikanaji wa huduma hiyo katika baadhi ya maeneo na vimeanza kutumika. 

" Upatikanaji wa Maji katika Mkoa Wangu hadi sasa ni sawa  asilimia  54 ambapo awali ulikuwa ni asilimia 46.

  Vipo vijiji ambavyo Mgao wake ni kwa uchache Matarajio ni kufikisha asilimia 100  kwa upatikanaji wa maji safi na salama   katika miji na vijiji vyote baada ya kukamilika kwa ujenzi  wa Matangi na Visima hivyo.

 Suleiman Anass Massoud  ni  Afisa Uhusiano kutoka mamlaka ya Maji Zanzibar zawa Pemba alisema kuwa    Jumla ya Matangi Matatu (3)  Visima 11 pamoja na ubadilishaji Mambomba  Mapya yenye upana wa nchi 4 na mengine nchi 11 na nusu unaendelea katika Mkoa huo.

" Awali Kaskazini Yote ilikuwa inatumia Tangi  1 na visima visivyozidi  vitatu 3  kusambazia Maji, Mabomba  ya  nchi Moja na nusu  Mengine 1 na nusu  ndiyo yalikuwa yapo kwa sasa  tumebadilisha" . 

" Tangi linalojengwa  Kilindini Shehia ya Wingwi Wilaya ya Micheweni, Ambalo litakapokamilika litasaidia kuondosha usumbufu huo kwa vijiji vya Shumba Mjini,  Majenzi Chamboni na  vijiji jirani. 

Tangi la Limani Shehia ya  Kipange Ambalo linatarajiwa kunufaisha  Vijiji vya kipange,Limani, Makangale,Mkia Wa Ng'ombe,Mnarani, Kiuyu Pamoja na  Ukarabati wa Tangi la Gando Wete ambalo litakaokamilika litasaidia kunufaisha   Vijiji vya Gando  Raha, Madaniwa, Mtemani, Mleteni Sambamba na maeneo ya visiwa vya fundo pamoja na uvinje.
 
 VIONGOZI WA SHEHIA WANANSEMAJE JUU YA HILI LINALOENDELEA KWA SASA LA UBADILISHWAJI NA UJENZI WA MATANGI NA VISIMA! . 

 Rahila Ramadhan Juma Sheha wa Shumba Viamboni  Micheweni Pamoja na Mrisho Juma Mtwana Sheha wa Shehia ya Mtemani Wete  kwa nyakati tofauti walisema huduma ya maji inayopatikana katika  Shehia zao ni ya Mgao  jambo ambalo Linapelekea usumbufu kwa wananchi kutokana na kukosa huduma hiyo ipasavyo .

"Tunaona Mabadiliko kuna Mabomba yamelazwa Misingi inachimbwa  tunaamini muda si mrefu   Maji yatakuwepo, Miaka ya nyuma uo  Mgao tulikuwa hatupati walau saivi tunapata kwa Mgao na  tunamatarajio ya kupata bila Mgao karibuni.  

" Uhitaji wa Huduma za kijamii bila usumbufu si jambo la hiari katika jamii yeyote ile, Idadi kubwa ya watu inapelekea kuongezeka kwa uhitaji na matumzi mengi ya Maji pamoja na huduma nyengine za kijamii. 

 Shehia yangu Imekombolewa na Wanawake kuna kijijikinaitwa Mleteni kilikuwa hakijulikani kabisa Hakukuwa na Huduma yeyote Muhimu  Mpka tuifate mbali lakini kwa Sasa imefunguka kimaendeleo Huduma za Afya zimefika Kwa karibu zaidi na Barabara ipo njiani  kuletwa Alisema Shaaban Salum Mtwana Sheha wa shehia ya Kisiwani . 

JEE MATUMAINI YA WANANCHI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO  KWA KIONGOZI WAO YAPOJE! 

 Fatma Ramadhan Said,  Safinia  Issa Pamoja na Asha Abass ni wakaazi wa Wete  walisema  hatua hizo zilizofikiwa zimeanza kuleta Mabadiliko ambayo yatapelekea kuboresha huduma za kijamii, kukuza maendeleo ya kiuchumi  kwa wananchi  pamoja na kuondoa usumbufu wa kufata huduma bora  nje ya wilaya hiyo. 

"Niseme kuja kwa Miradi hii ya uviko katika Mkoa wetu ni mafanikio  bila shaka mpka serikali kuu imeamua kutuletea miradi hii  viongozi wetu waliomba kwa nia njema kwetu walipeleka malalamiko  bila kupeleka wao sSerikali kuu isingejua kama kuna Matatizo, kwaio tunaimani itakapokamilika tutanufaika sisi na vizazi vyetu. 

" Kiukweli tuna matumaini kuona  Ujenzi wa hospitali  ile ya Micheweni umefikia hatua kubwa sasa umeanza kumaliza  itatusaidia sisi akina mama kutuondoshea usumbufu, Mrundikano wa Wagonjwa lakini kurahisisha  huduma za Matibabu tunaamini  hata huduma ambazo awali tulikuwa tunazikosa mwazo sasa tutazipata ni jambo la furaha. 
 
 Sleiman Said Ali ambae ni Mjasirimali Soko la wete 
 Alisema kuwa matumaini aliyonayo  mara baada ya kuona hatua kubwa zilizofikiwa katima ujenzi wa miradi hiyo ikiqemo soko la wajasirimali katika wikaya yake ni makubwa ambapo amesema itasaidia kupata bidhaa kwa urahisi na kwa uhakika pindi atakapozihitaji
  KUSHOTO   -  MJASIRIAMALI WA  VIUNGO.    SLEIMAN SAID ALI  AKIZUNGUMZA  NA MWANDISH WA HABARI HIZI. 

"Dhamira  Njema ya serikali kwa wajasirimali ni kuona tunapata soko la uhakika kuweka na kuuza bidhaa zetu tunaimani kubwa ujenzi wa soko itakapokamilika utakuwa Mkombozi wetu" . 

 Msimamizi mkuu wa  wa miradi ya maenedeleo ambayo inatekelezwa kupitia fedha za ahuweni ya  uviko 19  Mkoa wa kaskazini Pemba Amesema hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa miradi hiyo itakayotumika kwa wananchi ipo ukingoni kukamilika na kukabidhiwa kwa serikali. 

 Msimamizi huyo  wa  ambae ni Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib  Alisema uongozi wake utaendelea kutoa mashirikiano yakutosha katika kuona miradi hiyo inakamlika kwa wakati na kutumiwa  na  wananchi kuleta  maendeleo ikiwa na ubora kama matumaini ya wananchi wake yalivyo juu ya miradi hiyo.

   Miradi hiyo ni ujenzi wa Masoko ya  Wajasiriamali, Skuli Majia miradi ya ujenzi wa Hospitali. 

"Wilaya ya Wete eneo la Kifumbi kai, Pamoja na Soko la wajasiriamali Tumbe wilaya Ya Micheweni  Mkoa wa Kaskazini Pemba,  ambayo hii itakapokamilika  wajasiriamlai zaidi ya 154 watanufaika  kutokana na kupata sehemu rasmi za kuuza bidhaa zao na kupelekea kuleta tija na ukombozi kwa taifa. 

Alieleza kuwa Mradi wa Maji safi na Salama kupitia ujenzi wa Matangi  ambao unatekelezwa katika  eneo la Kilindini, Wilaya ya Micheweni, Kipange wilaya Wete Sambamba na ukarabati wa tangi eneo la Raha, wilaya hiyo ambapo itakapokamilika miradi hiyo kutasaidia kundoa tatizo la maji katika maeneo mbali mbali. 

Aidha Alisema miradi ya Afya inayotekelezwa katika  wilaya ya Micheweni  ni Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambapo kukamilika kwa ujenzi huo kutaipa hadhi Hospitali ya Cottage Micheweni na kuwa hadhi ya wilaya Pamoja na ujenzi wa hosptali ya wilaya ya Wete ambao mradi wake unatekelezwa eneo la Kinyasini Wilaya ya wete.
 
 
           JENGO LA HOSPITALI  MPYA YA WILAYA
 
Hata hivyo Salama alisema Mradi wa mwisho ambao unatekelezwa katika wilaya yake kupitia fedha za uviko 19 ni mradi wa Elimu ambao ni ujenzi wa skuli mpya pamoja na ukarabati wa  Madarasa. 

"Skuli za kisasa   kupitia miradi hii ya uviko ambayo katika Mkoa wangu inajengwa pale Jadida Wete ambayo ni msingi lakini pia  Makangale mnarani, awali hazikuwepo  u Madarasa mapya, na skuli kisiwa cha kojani, Gando, kiuyu Mbuyuni  Matangatuani, Maziwani, sambamba na ukarabati wa skuli za MchinaTumbe Pamoja na Konde
  JENGO JIPYA SKULI YA SIZINI WILAYA YA MICHEWENI 

Miradi hiyo  ina thamani ya shilingi Bilioni 1. 2  imekamilika kwa asilimia  99  ambapo Kwa mujibu wa Takwimu za  Taarifa za Ajira  kutoka  Taasisi binafsi Mkoa wa Kaskazini Pemba  jumla ya watu  1,049   wamenufaika kwa kupata  ajira  binafsi   kupitia  ujenzi  wa miradi hiyo  ya Covid 19  huku   vijana   wakiwa ni ,  410,  234 , kati yao  275  kutoka  wilaya ya Wete  wanaume  145  wanawake 130, Huku wilaya ya  Micheweni  vijana 49 wanaume 47 na wanawake  2, Sambamba na Ajira zisizo rasmi   639  ikiwa ni pamoja na kupata  utaalamu wa kufanya shughuli mbali mbali, kukuza Biashara  na kujipatia kipato katika kipindi cha miaka  miwili . 
            JENGO NI SOKO LA WAJASIRIMALI TUMBE 

Sio tu Miradi ya Covid ambayo inajengwa na kusimamiwa bali   miradi mikubwa ambayo itakuwa fursa kwa wajasirimali  Zanzibar

Tulikuwa na maeneo ambayo ni ya wazi mengi  ambayo kwa asilimia kubwa sasa  yameanza kutumiwa kueta maendeleo kwa wananchi Tunaendelea na ujenzi wa kiwanda Cha Mwani, Viwanda viwili vya Maji tayari vimeanza kutumika zote hizo ni fursa ambazo zipo katika Mkoa kwa sasa awali zilikuwa hazipo.  Alisema Rc  

Kuimraika kwa huduma za kifedha Mkoa wa Kaskazini Pemba Ambapo katika kipindi Cha miaka mitano iliyopita  huduma hizo zilikuwa  ni  chache  huku baadhi ya maeneo zikikosekana kabisa. 

 " Kuna tawi la CRDB  tunatumia kuhifadhia pesa zetu wengine tumeunga akaunt kupitia hilo tawi zamani tulikuwa hatuna  hata io akaunt Fedha zetu zipo salama tunatembea kwa amani bila kuogopa  amhaturandi na fedha mifukoni. Aliongeza Sleiman Said Ali.

 Wapo Waliodiriki kusema kuwa "Tunatamani Awe na mamlaka ya juu zaidi  au ahudumu kwa muda mrefu Mkuu wetu ili tuone Mageuzi mazima ya kiuchumi sio Kaskazini tu Hata Zanzibar Nzima Alisema  Zawadi  anapambana sana  kwajili ya wananchi. 

 Mwisho












Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI