MKUU WA MKOA KASKAZINI PEMBA AKABIDHI MSAADA WA CHAKULA KWA FAMILIA 100 ZENYE HALI NGUMU KANGAGANI AWAHAMASISHA KUDAI RISITI ZA KIELECTRONIKI.

Na AMINA AHMED MOH’D. 

MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib Amewataka wananchi  kutoa mashirikiano kwa Bodi ya Mapato Zanzibar ZRB  Kwa kudai risiti za kielectroniki wanaponunua bidhaa  mbali mbali ili bodi hiyo  iweze kukusanya kodi kwa usahihi  kutoka kwa wafanya biashara   kodi ambazo  zitasaidia kuleta maendeleo kwa Wananchi

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi  wa kijiji cha kangagani  katika ghafla ya kupoeana kukabidhi msaada wa chakula uliotolewa na  na Bodi ya mapato Zanzibar kwa familia 100  zenye Hali ngumu kijijini humo ikiwa ni  Wiki maalum ya kurejesha shukurani kwa walipa kodi nchini.

 Amesema iwapo wananchi watatoa mashirikiano na kuunga mkono  Ununuaji wa bidhaa kwa kudai risiti za kielektronik kutasaidia kudhibiti upotevu wa kodi  na kutumika kodi hizo katika ujenzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo unguja na Pemba na kutumika kwa maslahi ya Taifa .

Awali akizungumza Mkurugenzi  wa ZRB Pemba Jamal Hassan Jamal amesema   msaada huo uluotolewa na bodi hiyo  ni katika kurejesha shukurani kwa walipa kodi  ambao ni  wananchi . 

 Nao baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wameishukuru ZRB kwa kuwapatia msaada huo ambapo wamewataka kuendeleza Utamaduni huo wa kuwakumbuka walipa kodi wao ambao wanaishi katika Mazingira Magumu maeneo mbali mbali. 
 Msaada uliotolewa kwa wananchi hao  ikiwa ni wiki ya furaha na  kurejesha shukurani kwa walipa kodi  ni Sukari, Mchele, Unga pamoja mafuta ya kupikia ambapo mapema asubhi wafanya biashara mbali mbali  waliofika katika ofisi za  bodi hiyo Gombani chake chake walijmuika pamoja na wafanya kazi wa bodi hiyo katika shehehe maalum ya kuwashukuru walipa kodi .

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI