PEMBA PRESS CLUB YATOA NENO KWA WAANDISHI WA HABARI.

Na AMINA AHMED MOH’D. 

WAANDISHI wa Habari  Kisiwani Pemba wameaswa  kufuata maadili  ya uandishi wa habari   kwa kufanya kazi zao wakiwa makini hasa wanapotumia mitandao ya kihamii ili kuepusha migogoro .

Ushauri huo umetolewa na Mwenyekiti Mstaafu wa Club ya waandishi wa habari Pemba PPC Said Moh'd Ali   alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano mkuu maalumu ulioandaliwa na Club hiyo uliofanyika katika ukumbi  wa Maktaba Chachani Chake Chake.

Alisema  iwapo waandishi watafuata maadili na kutumia taaluma  yao ipasavyo  kutaepusha migogoro katika jamii ambayo inaweza kuchangia uvunjifu wa amani. 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Klabu hiyo Bakar Mussa Juma  Amewataka waandishi wa habari ambao hawajawa wanachama kujiunga na club hiyo ili kuwasogeza karibu na wenzao. 

Akisoma  maazimio ya club hiyo  kwa mwaka 2023  imeweka mikakati ya kuboresha  shughuli za club hizo kwa maslhi ya jamii. 

Mkutano huo pamoja na mambo mengine umejadili mambo mbali mbali ikiwemo  maazimio ya UTPS Sambamba na kukabidhi utambulisho maalum wa kutumiwa na waandishi wa habari wapya waliothibitishwa na Club hiyo. 

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI