MIKAKATI ILIYOUNDWA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI KASKAZINI PEMBA YAZAA MATUNADA WANANCHI WAPATA UELEWA KUYARIPOTI YANAPOJITOKEZA.

NA - AMINA AHMED   MOH’D  - PEMBA. 
  
 MASHIRIKIANO  yanayotolewa katika kusimamia mikakati maalum ilionazishwa  na Serikali ya Mkoa wa kaskazini Pemba juu  ya  kupambana na vitendo vya uhalifu  kwa miaka Miwili sasa imesaidia kuongeza uelewa kwa wanajamii juu  ya kuripoti matukio ya udhalilishaji wa kijinisia yanapojitokeza  katika maeneo ya miji na vijiji  mkoani humo.

  Akizungumza na habari hizi maalum Kuelekea kilele cha siku 16 za kupinga udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto duniani Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini  Pemba Salama Mbarouk khatib   Alisema  usimamizi na mashirikiano yanayoendelea kuoneshwa  katika utekelezaji wa mikakati hiyo  iliyowekwa  imesaidia   kukuza uelewa wa wanajamii  ndani ya mkoa huo ambao kwa sasa wamekuwa na muamko mkubwa wa kuyaripoti matukio ya udhalilishaji katika vyombo vya sheria na kuchukuliwa hatua . 
  SALAMA MBAROUK KHATIB - MKUU WA MKOA             KASKAZINI PEMBA 

"Mara tu Nilipoteuliwa  kushika nafasi hii ya Mkuu wa Mkoa  Disemba  1 / 2020  nilitafakari namna gani naweza kupambana   na suala la udhalilishaji wa kijinsia  katika Mkoa wangu ". 

 "Nilianzisha kamati ya mkakati  ya kushughulikia Udhalilishaji  wa kijinisia kwa wanawake na watoto ambayo  inashirikisha  jeshi la polisi,   Mahkama, Mkurugenzi wa Mashtaka, wakuu wa wilaya Wete na Micheweni, Viongozi wa Dini, Masheha, Waandishi wa Habari, maafisa kutoka Mamlaka ya kupambana na Rushwa na Uhujumu Uchumi,  wizara ya Afya,kituo cha Mkono kwa Mkono, lakini pia wadau mbali mbali ambao wamo katika mapambano ya udhalilishji wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto ambapo kwa pamoja tumekuwa tukuchukua  hatua mbali mbali za kiutendaji kila mmoja kwa nafasi yake nikiwa kama mwenyekiti wa kamati hiyo lengo ni  kupunguza kasi ya wimbi hili la udhalilishji ili kuona linaondoka katika Mkoa wetu". 

Mkuu huyo Alitaja hatua hizo za kiutendaji ambazo zinazoendelea kuchukuliwa na kamati  hiyo ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kwa kufaya mikutano inayozungumzia masuala ya udhalilishaji,  kufuata maelekezo ya serikali Kuu  kuelekeza nguvu ya kulimaliza suala la udhalilishaji kwa pamoja,  kuhamasisha jamii kuyatolea taarifa matendo  ya udhalilishaji yanapojitokeza, kutolea ushahidi  na kufika mahakamani  baada ya kujtokeza matokeo ya udhalilishaji lakini pia kuepuka muhali na kuwaficha wahalifu wanaofanya matendo ya udhalilishaji. 

"Mikakati ilisimamiwa na inaendelea kusimamiwa vyema kila mmoja kwa nafasi yake   jambo ambalo limepelekea kuongezeka  idadi ya matukio ya  vitendo vya ubakaji na ulawiti, ambavyo vinaripotiwa  ukilinganisha na miaka iliyopita nyuma wananchi walikuwa hawayaotolei taarifa kutokana na kukosa uelewa juu ya atahari ya vitendo hivyo  ."

" Wanaotenda makosa hayo wanashtakiwa na sheria  zinapowatia hatiani wanapewa adhabu kwa mujibu wa makosa yao wapo amba wanatumikia chuo cha mafunzo  cha miaka 30 wapo miaka  15 ni kwa mujibu wa sheria ilivyowatia hatiani,hii ni moja kati ya mafanikio makubwa yaliofikiwa ya kupambana na vitendo hivi katika Mkoa wa kaskazini Pemba".

Aidha alisema kuwa  Mikakati mengine iliyowekwa katika kamati hiyo ni kusimamia ufikishwaji wa kesi katika vituo vya polisi na kusimamia kufunguliwa majadala ili ziweze kufikishwa  kwa mkurugenzi wa mashtaka na kuweza  kufikishwa Mahakamani pamoja na kusimamia ili kuhakikisha zinafanyiwa uchunguzi. 

  Hata hivyo Salama Amewataka madakatari  wanaofanya uchunguzi kwa watoto wanaofanyiwa udhalilishaji   kutoa ushahidi juu ya kile ambacho wamekiona  na kuacha tabia ya kusema kuwa ni wazoefu ili kuharibu ushahidi. 

 Alieleza kuwa   Kamati hiyo itaendelea Kushirikiana  na taasisi binafsi pamoja na serikali katika kuona kesi hizi hazikai kwa muda mrefu  kupatiwa hukumu zinapofika mahakamani. 

Aidha mkuu wa mkoa huyo alisema kuwa kamati hiyo inaendelea na utaratibu maalum wa kufanya tathmini ya hatua zilizofikiwa katika mapambano hayo ambapo  alisema Mkuu wa mkoa huyo Alisema   kuwa  mpka sasa  kamati mkakati hiyo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza  vitendo vya udhalilishaji  ikiwemo mimba  za umri  mdogo. 

 Aidha Aliwataka wanakamati  na wananchi katika mkoa huo  kusimamia wajibu wao katika mapambano hayo  ili kuendelea kubaini kasoro zilizopo ambazo zinahitaji kuchukuliwa hatua katika kumaliza vitendo vya idhalilishaji. 

 "Kila mmoja  kwa nafasi yake atimize wajibu wake tutaweza kuona kipi kinahitaji nguvu ya ziada  katika kuendeleza mapambano haya ili yamalizike katika mkoa  huu. 

Nao baadhi ya wananchi katika  Mkoa huo  Wamemshukuru Mkuu wa mkoa huyo kwa jitihada anazoendelea kuzifanya katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji ambapo wamesema jamii imeanza kuelewa  madhara ya udhalilishaji, rushwa muhali  jambo ambalo limebadilisha uelewa kwa wanajamii waliowengi na kuendelea kuyaripoti yanapojitokeza. 
Harakati za kupata takwim  sahihi juu ya  mwenendo wa kesi za udhalilishaji  katika mkoa huo  zinaendelea . 

Mwisho
 
 


 




 

 








Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI