Posts

Showing posts from May, 2023

TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI SKULINI, BILA HUDUMA YA MAJI, DAMPO NA VYUMBA MAALUM HAKUNA HEDHI SALAMA,NI HATARI KWA AFYA ZAO NA ATHARI KATIKA UFAULU WAO.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA. ( 0719859184)   IKIWA JANA  28 /5/ Dunia iliaadhimisha siku ya Hedhi  Salama bado kuna mengi yanahitaji kuangaliwa na wadau Serikali na wote wanaopenda Maendeleo bora ya Elimu kwa watoto wa kike kwa Shamra shamra mbali mbali ikiwemo kutoa Elimu  ya Afya ya uzazi kwa baadhi ya wanafunzi, kugawa Sabuni pamoja na Taulo zakike lakini bado kuna changamoto Nyingi ambapo zisipoangalia kwa jicho la Tatu na wadau pamoja na serikali kwakuwekewa mkakati Endelevu Kugawa Taulo kutoa Elimu na Sabuni hizo  hautokuwa Msaada kwa Wanafunzi Wakike Maskulin i.  Jee ni kwa namna gani yataweza kufikiwa Maendeleo ya Elimu ambayo itakuja kuwa mkombozi baadae katika maisha ya mtoto wa kike ni pamoja na kuwa na Afya imara mazingira salama na upatikanaji wa huduma muhimu ambazo zitasaidia kuondosha usumbufu wanapokuwa katika kipindi cha Hedhi. Wanafunzi wengi wakike ambao wamefikia umri wa baleghe ( kuvunja ungo) wakiwa katika hara...

UELEWA WA KURIPOTI MATUKIO YA UDHALILISHAJI WA KIJINISIA KATIKA JAMII UMEONGEZEKA, WANAMTANDAO WAPEWA MASHIRIKIANO NI BAADA YA KUANDALIWA NA TAMWA-ZANZIBAR KUIFIKIA JAMII.

Image
Na Amina Ahmed Moh’d, Pemba  ( 0719859184).  UELEWA katika  Kuripoti Matukio mbali mbali ya Udhalilishaji wakijinsia kwa wanawake na watoto yanapojitokeza katika Jamii kisiwani Pemba Imeelezwa kuongezeka baada ya wanachi kuendelea kutoa mashirikiano kwa wanamtandao  pamoja na kutumiaJukwaa la Habari kuripoti Matendo hayo yanapojitokeza.   Hayo yameelezwa na Wanamtandao wa kupinga udhalilishaji  wa Kijinsia Kisiwani Pemba katika Mkutano maalum wa kuwasilisha Ripoti ya Ufuatiliaji wa matukio ya ukatili na Udhalilishaji   walioifanya katika kipindi cha Miezi 5 kutoka maeneo mbali mbali  ya shehia za Kusini na Kaskazini Pemba.  Wamesema  awali Jamii ilikosa Imani juu ya Mtandao huo wa kufatilia Masuala hayo Lakini kwa sasa  uelewa umeongezeka na wanaendelea kupata Mashirikiano  katika kuendeleza mapambano  hayo.  " Jamiii, Walikuwa wanaona kama sisi hatuna nia ya kupambana na Udhalilishaji, lakini ki...

WANAFUNZI MADUNGU SECONDARI WAIPONGEZA TAASISI BAREFOOT COLLEGE INTERNATIONAL ZANZIBAR, KWA KUWAFANYIA MAZURI HAYA KUELEKEA SIKU YA HEDHI SALAMA , HUKU WAKIIBUA MENGINE YANAYOHITAJI MSAADA KATIKA KUIMARISHA AFYA ZAO NA KUTIMIZA MALENGO YAO WALIYOJIWEKEA. .

Image
NA AMINA AHMED MOH’D,    PEMBA   (O719859184).  KILA Ifikapo May  28 Dunia huadhimisha Siku Ya Hedhi Salama Ambapo Katika kuadhimisha Siku hiyo   Wanafunzi Wa Skuli ya Sekondari Madungu wameishukuru Taasisi ya Barefoot College International Zanzibar  kwa kusherehekea siku hiyo Pamoja nao  kwa kuwapatia Elimu ya Afya ya uzazi kwa Mwanamke sambamba na kuwagawia Taulo za kike, Nguo za ndani, pamoja  Sabuni ya Unga  ambapo Wanafunzi hao wamewataka  wadau wengine kuendelea kusaidia upatikanaji wa Elimu na vifaa hivyo ili kuimarisha Afya za watoto wakike katika Maskuli mbali mbali Mijini na Vijijini na kuwaondoshea usumbufu.     Wakizungumza  mara baada ya Kumalizika kwa Zoezi la utolewaji wa Elimu hiyo ya Afya, Ugawaji wa Taulo hizo Nguo za Ndani  pamoja Sabuni Baadhi ya Wanafunzi hao wamesema  iwapo Wadau kutoka taasisi na Mashirika Mengine wataungana pamoja na  Taasisi ya  B...

WANANCHI WAMPONGEZA KADUARA UTENDAJI WAKE JIMBONI WAAMUA KUMUITA TENA KUONGEZA KASI YA UJENZI WA MAENDELEO.

Image
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba (0719859184).  WAKAAZI wa Kijiji cha Madungu Kosovo Wilaya ya Chake Chake Wamemuomba Mwakilishi wa jimbo hilo Shaibu Hassan Kaduara  Kuendeleza Ujenzi wa Barabara aliyoanza kuijenga  Na kuwa Faraja kwa wakazi wa kijiji hicho  katika kurahisisha huduma zao mbali mbali, jambo ambalo awali halikuweza kufanywa na viongozi waliopita ndani ya jimbo hilo.  Wakizungumza baadhi ya Wakaazi hao wamesema Ujenzi  wa barabara hiyo  ulioasisiwa na Mwakilishi wao  wa jimbo la chake chake umesimama kwa Muda  huku kifusi kilichowekwa Awali kikianza kuburutwa na Maji baadhi ya Maeneo ya barabara hiyo kutokana na kusita kwa Ujenzi huo.  Wamesema Matumaini yao ni kukamilishwa kwa kiwango cha lami Barabara hiyo  ambayo licha ya kuwahaijakamlika lakini  inaendelea kuwa faraja kwawananchi wa kjiji hicho hado sasa.  "Mwakilishi wetu Amefanya jambo kubwa ambalo hatukuwahi kulitegemea , lakini yeye ameweza katu...

WANANCHI PEMBA WALIA KUKOSA HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA WAOMBA WADAU NA SERIKALI KUJITOKEZA KUWASAIDIA, WADAI KUKOSA MATUMAINI NA AHADI WANAZOPEWA NA ZAWA.

Na Amina Ahmed Moh’d, Pemba- (0719859184) BAADHI YA WANANCHI   Shehia ya Gombani wilaya Ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Wamemuomba Waziri wa Maji  , nishati na Madini, Zanzibar Shaib  Hassan kaduara kulipatia Ufumbuzi Tatizo la ukosefu wa Huduma ya Maji Safi na  Salama  katika Baadhi ya Vijiji ndani ya Shehia yao kwa Muda mrefu sasa ambalo limeshindwa kupatiwa ufumbuzi.   Wakizungumza na Habari hizi  baadhi ya wakaazi wa Gombani Wamesema kukosa huduma hiyo kwa muda mrefu   sasa bila muelekeo wa kuoatikana ufumbuzi tatizo hilo imekuwa  kukirudisha nyuma Matumaini yao katika kuipata huduma hiyo muhimu. " Tunawaomba wahisani wanaowajengea  Visima watu vijijini waje na Shehia ya Gombani wasiwekeze tu Vijijini,  tunausumbufu mkubwa kwa Muda mrefu sasa waje watusaidie, au Waziri mwenye dhamana  Kaduara  asilichukulie masihara hili suala Wananchi wake tunasumbuka sana na  Watoto, kila siku tunaambiwa kuna ...

WANAWAKE WAKONGWE HARAKATI ZA SIASA NA UONGOZI PEMBA WATOA NASAHA KUELEKEA 2025 KWA WANAWAKE WENYE NIA

Image
NA AMINA AHMED MOH’D  KATIKA kuhakikisha ushiriki wa wanawake katika vyombo vya maamuzi unaongezeka, wanawake wenye ndoto za kugombea uongozi wameshauriwa kuanza kujifunza kutoka kwa wanawake wanasiasa waliowatangulia ili kuongeza ujasiri na uthubutu wa kukabiliana na vikwazo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025. Ushauri huo umetolewa na wanasiasa wanawake wakongwe katika mkutano wa jukwaa la wanawake na uongozi lililoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari WanawakeTanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) na Ubalozi wa Norway kwa lengo la kuwaunganisha wanawake wanasiasa kutoka vyama mbalimbali vya siasa Pemba kubadilishana uzoefu na kuwajengea uwezo kuhusu ushiriki wao kwenye nafasi za uongozi na namna ya kukabiliana na vikwazo vinavyoweza kurejesha nyuma ufikiaji wa malengo ya wanawake kiuongozi. Mwana Masoud Ali, mbunge na mwakilishi mstaafu wa chama cha Wananchi CUF jimbo la Mtambwe Pemba, alisema ili wanawake wenye nia ya kugombea waweze kufanikiwa kiuongozi  ni lazima wat...

ZSSF PEMBA YATOA TAHADHARI KWA WASTAAFU , NI BAADA TA KUJITOKEZA MATAPELI KUTUMIA VIBAYA KAULI YA DK MWINYI KUONGEZA PENCHENI KUIINUA MGONGO.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA (0719859184).   UONGOZI wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar Zssf Pemba Umewataka Masheha  Kutoa Taarifa za uhalifu na Utapeli  zinazoendelea  Kujitokeza katika Shehia zao  Ambazo zinafanywa na baadhi ya watu ambao sio waaminifu  kwa  kutumia jina na mwamvuli wa mfuko huo  na kufanya  udanaganyifu kwa wazee wastaafu  wakidai  kuwa wanafanya usajili kwajili ya kupata Pencheni zao kwa haraka na kuwachukulia fedha .  Akizungumza na Waandishi wa Habari Kaimu Mkurugenzi Zssf Pemba Dk. Said Salim Maalim  Amesema watu hao  ambao wamekuwa wakipita katika maeneo mbali mbali ya kisiwa cha Pemba  wakiwaeleza wazee wastaafu  kuwa wao ni Wafanya kazi kutoka Hazina Zssf   na kujitambulisha katika Uongozi wa Shehia Na hatimae kupata ruhusa ya  kuingia Mitaani kufanya udanganyifu huo  limekuwa likijitokeza katika maeneo mbali mbali  hivyo Masheha kuend...

MWAKILISHI VITI MAALUM KUSINI PEMBA NEEMA KWA AKINA MAMA WAJASIRIAMALI.

Image
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba  Mwakilishi wa Viti Maalum kupitia Jumuiya ya Wanawake(UWT) Mkoa wa Kusini Pemba Leila Muhammed Mussa amekabidhi vyerahani 8 kwa wanawake na wanavikundi vya UWT Mkoa huo na vifaa vya ujenzi ikiwemo Bati 80 na Matufali 500 kwa ajili ya ujenzi wa maskani na ofisi Pamoja na Fedha . Akikabidhi vifaa hivyo huko Baraza la Mji Chake Chake  Leila amesema lengo la kukabifhi vyerahani hivyo kwa wanavikundi vya UWT ni kutaleta ukombozi wa Kimaendeleo kwa akina mama katika kujikwamua kiuchumi. Alisema kuwa vifaa vya ujenzi Vitasaidia kukamikishia na kuendeleza ujenzi wa Maskani na matawi ya chama kwenye yaliopo katika Maeneo mbali mbali Mkoa huo. Alisema wao kama viongozi walipata dhamana ya kuwawakilisha wanawake kupitia Jumuiya kwenye vyombo vya kutunga sheria na serikalini wanao wajibu wa kujengea uwezo wanachama wao waweze kujikwamua na umaskini. Aidha Waziri Leala aliwahimizwa wanavikundi waliopatiwa vyerahani hivyo kuvitumia ili waweze kuongeza k...

JAMII YATAKIWA KUWAPA MSAADA WA USHAURI NASAHA WAHANGA WA UKATILI WA KIJINSIA

Na Khamis Haji     Unguja.  BI FATMA HAMIS ALI  AMBAE NI MWANAHARAKATI WA KUPINGA VITENDO VYA UDHALILISHAJI KWA  WANAWAKE NA WATOTO AMESEMA IPO HAJA KWA WANAWAKE WANAOPITIA  MASUALA YA UKATILI NA UDHALILISHAJI KUPATIWA   USHAURI NASAHA ILI WAWEZE KUSONGA MBELE NA MAISHA LICHA UKATILI WALIO PITIA AKIZUNGUMZA NA SPICE FM RADIO  AMESEMA WANAWAKE WENGI WANAOPITIA UKATILI HUWA WANAKUMBWA NA MSONGO WA MAWAZO  NA KUJIONA HAWANA THAMANI KATIKA JAMII AIDHA AMEITAKA JAMII  KUWAREJESHA SHULE WATOTO AMBAO WAMEKUMBANA NA UKATILI  NA   WAWACHE KUWA NYANYA PAA PAMOJA NA KUWAPA ELIMU YA KIROHO AKIFAFANUA ZAIDI  BI FATMA AMEITAKA JAMII KUWAPA MOYO WANAWAKE WALIOPITIA UKATILI NA KUWASHIRIKISHA KATIKA SHUHULI ZA KIJAMII PAMOJA NA KUWASAIDIA KUWA NA SHUHULI ZA KUJIPATIA KIOPATO ILI WAWEZE KUJITEGEMEA BI FATMA AMSEMA WENGI WA WANAWAKE AMA WATU WANAOPITIA UKATILI HUWA WANAATHIRIKA  HIVYO WASAIDIWE  KUPATA TIBA SAHIHI ABDUL LATIF...

WAANDISHI WAASWA KUSAIDIA KUTOA ELIMU KWA JAMII JUU YA MATUMIZI SAHIHI YA RISITI ZA ELEKTRONIKI NA ULIPAJI WA KODI.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA     HAFIDH ALI MUHAMED - MDHAMINI WMJJWW PEMBA.   AFISA Mdhamini wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Pemba Hafidh Ali Mohamed, amewataka waandishi wa Habari Kuisadia Serikali katika  kuelimisha jamii juu ya ulipaji wa kodi na matumizi sahihi ya risiti za elektroniki ili kuendelea kuwajengea uwelewa  kwa vile wao ndio wanaoweza kutoa ujumbe na kuweza  kufikiwa na Watu wengi kwa haraka .  Alisema kuwa, waandishi wa Habari ndio daraja la mawasiliano hivyo, ni vyema kuitumia taaluma yao ya uwandishi wa habari katika uwandaaji wa makala na vipindi vya kila siku kwa lengo la kuielimisha jamii. Aliyasema hayo alipoua akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, huko ukumbi wa TASAF Chake chake uliyoandaliwa na klabu ya waandishi wa habari wa Pemba (PPC) kwa ufadhili   Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania UTPC pamoja na M...

CP ZANZIBAR AFUNGA MAFUNZO YA SAJENTI (SGT)NA OMAR HASSAN – ZANZIBAR

Image
Na Omar Hassan Unguja KAMISHNA wa Polisi Zanzibar CP Hamad Khamis Hamad amefunga mafunzo ya uongozi mdogo ngazi ya Sajenti na kuwataka Askari waliomaliza mafunzo hayo kufanya kazi kwa uwadilifu na haki wanapotoa huduma kwa wananchi. Akifunga kozi nambari 1/2023 ya cheo hicho cha SGT huko Chuo cha Polisi Ziwani CP Hamad alisema mafunzo hayo yatakuwa kichocheo cha kuendeleza nidhamu, weledi, haki na uwadilifu .   Aidha amewahimiza wahitimu hao kutumia mafunzo waliyoyapata kulisaidia jeshi na wananchi katika kukabiliana na uhalifu na wahalifu. Akitoa tathmini ya mafunzo Mkuu wa Chuo cha Polisi Zanzibar, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Augostino Senga alisema wanafunzi 673 wamefaulu mafunzo hayo kati ya wanafunzi 679 na wanafunzi watano walishindwa kwa sababu mbali mbali.

KONDE WAMPONGEZA MWAKILISHI ZAWADI KUWASAIDIA KUPATA HUDUMA ZA KIJAMII.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D  PEMBA.  BAADHI ya Wananchi na wakaazi wa  Konde Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wamesema kasi ya Maendeleo inayoendelea kuoneshwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Zawadi Amour Nassor katika nyanja mbali mbali Ikiwemo Maendeleo ya  Elimu  pamoja na  Upatikanaji wa Huduma ya safi na Salama  imekuwa ikisaidia kuondosha Usumbufu waliokuwa wakipata Awali wao pamoja na watoto.   Wakizungumza na Habari Hizi Halima Juma  Khamis Mkaazi Wa  Matangatuani Konde Mkoa Wa Kaskazini Pemba Pamoja Na Nunu Khamis  Mkaazi wa Kiuyu kwa Manda  Wamesema Usumbufu waliokuwa Wanapata Wanafunzi wa Kijiji hicho  kufata Elimu masafa ya mbali ulikuwa ukiathiri kwa kiasi kikubwa Maendeleo yao. " Tunashukuru Mwakilishi wetu wa Jimbo la Konde Mh Zawadi kwa kutusaidia kupatikana Skuli mbili Maeneo ya karibu  ambazo zimeondosha usumbufu kwa watoto wetu, Walikuwa wanalazimika kuenda  Mgogoni jambo ambal...

WAHANDISI KUKAMILISHA MIRADI KWA WAKATI

NA HASSAN MSELLEM PEMBA.  Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar ZAWA, Balozi mstaafu na Meja Jenerali Issa Suleiman Nassor, amewataka wahandisi wa miradi ya maji Kisiwani Pemba kuhakikisha wanakamilisha miradi hiyo kwa wakati. Ametoa kauli hiyo huko katika Mradi wa tangu la maji Shumbamjini katika ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maji Kisiwani Pemba kupitia fedha za ahuweni za Uviko19, amesema azma ya Serikali ni kuhakikisha miradi hiyo inakamilika ifikapo Mwezi Julai mwaka huu ili wananchi waondokane na changamoto ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama inayowakabili. Kwa upande wake mjumbe wa bodi ya Wakurugenzi wa Maji Zanzibar ZAWA, Mheshimiwa Mohammed Aboud Mohammed, amewataka wananchi Kisiwani humo kuvitunza vyanzo vya maji ili huduma hiyo iweze kupatikana kwa urahisi. Nae Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar ZAWA Kisiwani Pemba, Bakari Mshindo, amesema kupitia miradi hiyo ya fadha za Uviko19 wamefanikiwa kuchimba visima 27 pamoja matang...

JAMII YAASWA UJUMUISHAJI WA WATU WENYE ULEMAVU HASA WANAWAKE KATIKA NAFASI ZA UONGOZI

Image
Na Masoud Juma, Unguja. Jamii imetakiwa kuwajumuisha watu wenye ulemavu hasa wanawake katika masuala mbali mbali ya maendeleo hapa nchini ikiwemo katika Nyanja za kijamii, kiuchumi.  Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Shirikisho la Jumuiya za Watu Wenye Ulemavu Zanzibar (SHIJUWAZA) bi Mwandawa Khamis wakati wa mahojiano huko katika ofisi zake zilizopo Mombasa  wilaya ya Magharibi “B” Unguja. Bi Mwandawa anasemaa kuwa watu wenye ulemavu ni watu wenye uwezo mkubwa wa kiakili na fikra, hivyo mapungufu yao yasiwakoseshe haki ya kuiletea maendeleo jamii yao ama kutengwa na kuonekana kama watu wasioweza. “ ulemavu sio ugonjwa, ni mapungufu ambayo mtu huzaliwa nayo ama humkumba wakati wa makuzi yake, hivyo ni bora jamii ikaangalia utu kwanza na kumuheshimu mtu mwenye ulemavu na kumshirikisha katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo” anasema. Bi Mwandawa ni mtu mwenye ulemavu na ni mwanaharakati wa muda mrefu wa kutetea haki za watu wenye ulemavu hapa Zanzibar na anasema...

UONGOZI WA MGENI KHATIB YAHYA UNAVYOENDELEA KUACHA ATHARI KATIKA KIPINDI KIFUPI , AWATAKA WANAWAKE KUACHA WOGA NA WAJITOSE KUTAFUTA UONGOZI ASEMA WAO NDIO CHACHU KUBWA YA MAENDELEO KWA TAIFA.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D   PEMBA  Moja kati ya Majukumu Makubwa  ni Uongozi, Uongozi  ni hali ya Mtu mmoja kuweza kuewa nyazifa ya juu  kuongoza Kundi la watu taasisi, Ambapo mtu huyo hupewa mamlaka ya kufanya maamuzi katika kuleta Maendeleo.  " Dhana hiyo ya Uongozi wenye kuleta Maendeleo kwa  Miaka mingi imejengeka akilini mwa waliowengi kuwa Mtu sahihi ambae anaweza kuleta maenedleo ni mwanaume pekee jambo ambalo halina ukweli wowote ule kikubwa kinachohitajika ni utayari na uwajibikaji tu juu ya kile kinachoongozwa na sio jinsia kama wanavyodhani wengi" .                KU LIA    NI DC MICHEWENI   MGENI KHATIB YAHYA   Ni maneno ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni khatib Yahya  alipata ku uteuzi wa nafasi hiyo ya kuongoza na kusimamia wilaya  kutoka kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi Huku akiwa ni Miongoni...

VITENDO VYA UDHALILISHAJI VINAVYOFANYWA KWA SIRI NA WANAFAMILIAKUIBULIWA NA USALAMA WETU KWANZA

Image
NA OMAR HASSAN – ZANZIBAR                                                 Mkuu wa Intelijensia ya Jinai Zanzibar, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Kombo Khamis Kombo amesema walimu wa usalama wetu wanaosomesha skuli za msingi wanaibua kesi za udhalilishaji wa watoto ambazo huwa haziripotiwi vituo vya Polisi kutokana na muhali wa wanafamilia. Akifunga mafunzo ya Usalama wetu kwanza huko Chuo cha Polisi Zanzibar amesema masomo hayo yanawafanya wanafunzi kujitambua na kuwapa ujasiri, hivyo huwa wanatoa taarifa kwa walimu Polisi endapo wamefanyiwa udhalilishaji ambapo mwaka 2022 Matukio 57 waliyaripoti wanafunzi ambayo yanaendelea kufanyiwa kazi katika Vyombo vya sheria. Mkuu wa Polisi Jamii Zanzibar, Kamishna Msaidizi wa Polisi Dkt. Egyne Emmanuel amesema Jeshi la Polisi limeanza kutoa elimu katika ngazi za awali kutokana na wahalifu walio wengi hujifunza ...