WANANCHI PEMBA WALIA KUKOSA HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA WAOMBA WADAU NA SERIKALI KUJITOKEZA KUWASAIDIA, WADAI KUKOSA MATUMAINI NA AHADI WANAZOPEWA NA ZAWA.
Na Amina Ahmed Moh’d, Pemba- (0719859184)
BAADHI YA WANANCHI Shehia ya Gombani wilaya Ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Wamemuomba Waziri wa Maji , nishati na Madini, Zanzibar Shaib Hassan kaduara kulipatia Ufumbuzi Tatizo la ukosefu wa Huduma ya Maji Safi na Salama katika Baadhi ya Vijiji ndani ya Shehia yao kwa Muda mrefu sasa ambalo limeshindwa kupatiwa ufumbuzi.
Wakizungumza na Habari hizi baadhi ya wakaazi wa Gombani Wamesema kukosa huduma hiyo kwa muda mrefu sasa bila muelekeo wa kuoatikana ufumbuzi tatizo hilo imekuwa kukirudisha nyuma Matumaini yao katika kuipata huduma hiyo muhimu.
" Tunawaomba wahisani wanaowajengea Visima watu vijijini waje na Shehia ya Gombani wasiwekeze tu Vijijini, tunausumbufu mkubwa kwa Muda mrefu sasa waje watusaidie, au Waziri mwenye dhamana Kaduara asilichukulie masihara hili suala Wananchi wake tunasumbuka sana na Watoto, kila siku tunaambiwa kuna matenengezo wala hayamalizi tumekuwa tunadanganywa kama watoto wa kuku".
" Shehia ya Gombani ni Moja Lakini chakushangaza Baadhi wanapata Maji wengine wanakosa, mwaka huu sasa kama sio mwaka wa Pili, Mimi mtoto wangu kazaliwa ana Mwaka hajawahi kuona maji ya ZAWA Tumechoka kupiga kelele kila siku", Alisema Ilham Salum Mkaazi wa Gombani.
"Hatujui hata izo kero Tuzitolee wapi haswa mana kama ni kwenye Vyombo vya Habari tumetoa Mpka kwenye Mawio lakini hakuna mabadiliko yoyote, Mkija kutuhoji tunaona kama mnatujejea sababu hakuna kinachobadilika Maji hayatoki mifereji imeshashajiloki yenyewe, Alidai Sadam Omar.
" Mwaka huu kama sio mwaka Wa Pili mi sijaona maji kwangu wala kwa Majirani tunastiriwa na wale wasamaria wema wenye kisima chao Ndani kama sio hivyo ingekuwaje sijui “Alisema Latifa Ali Hamdan.
Akizungumzia Suala hili Sheha wa shehia ya Gombani wilaya ya Chake Chake Subira Khamis Kombo Alidai kuwa Upatikanaji wa Maji safi na salama katika shehia yake Umekuwa na ahadi zisizotekelezeka kutoka mamlka ya maji Zawa.
"Kusema kweli ndugu Mwandishi Gombani Maji ya uhakika bado hatuna najitahidi kufuatilia Suala hili lakini majibu yanakuwa yale kwa yale tu kutoka kwa mamlaka husika, huku Tatizo likizidi kuwa kubwa na la muda Mrefu, Wito wangu kwa Serikali kuu iangalie Muarubaini wa hili, wahisani pia wajitokeze kutusaidia, ili na sisi tuweze kupata Maji kama vijiji vyemgine.
Harakati za Kumtafuta Msemaji wa mamalka ya Maji Zanzibar zawa Ofisi ya Pemba juu ya Kuzungumzia Suala hili kwa mara ya Tatu zinaendelea, ambapo awali mnamo
msemaji huyo ambae ni Afisa Mahusiano mamlaka ya Maji zaaa Pemba Suleiman Anas Massoud Alizungumza na habari hizi kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mamlka ya Maji Zanzibar Zawa Ofisi ya Pemba , na kuwataka Wananchi Hao wa Shehia ya Gombani kuendelea kuwa Wastahamilivu kwani Mradi utakaonufaisha Upatikanaji wa Huduma ya Maji vijiji Vya Gombani Umefikia Hatua Nzuri.
"Matarajio Yetu tulikusudia Mwanzoni Mwa Mwezi huu Tatizo la Maji baadhi ya Vijiji Gombani libaki Historia tu Lakini Kutokana na Sababu zilizokuwa Nje ya Uwezo Wetu Mradi huo Utamaliza Mwisho wa Mwezi wa March Mwaka huu 2023.
Anass Alitaja Sababu hizo na Kusema kuwa " Baadhi ya vifaa vyao Vya Ujenzi na ulazaji Mabomba Vilizuiwa Bandarini Unguja Kwa hiyo Mafundi wakachelewa Vilikuwa havitoshi kukamilisha kwa wakati Mradi, Mabomba, Viungo, Pampu, Saruji, Kokoto, Nondo, na Magari ya Kukorogea Zege" Alisema.
Akizungumzia Suala la Utolewaji Taarifa kwa Wananchi juu ya Hatua za Ujenzi wa Mradi huo Sleiman alisema kuwa Mamlaka ilitumia vyombo vya Habari mbali mbali kuwajulisha wananchi.
" Hatukumfata kila Mtu kwake lakini katika Media ZBC Redio Tv, na Radio Jamii na baadhi na Vikao vya Masheha Wilaya zote Tumewambia nini kinaendwlwa kwa sababu Mradi wa Maji Gombani ni moja kati ya miradi inayotekelezwa kwa Fedha za ahuweni ya Uviko 19.
Aidha alisema kuwa Mamlaka imelenga kuimarisha Huduma ya Maji kwa kuongeza idadi ya Visima vya Maji vitakavyo Hudumia Chake Chake ikiwemo Gombani.
Kwa Mujibu wa Sheha wa Shehia ya Gombani jumla ya Wakaazi 4835 ambao wao ni Wanawake na Watoto wamekuwa wakishindwa kufanya shughuli zao kwa wakati kutokana na usumbufu wa kukosa Maji baadhi ya Maeneo.
Ambapo kwa Zaidi ya Miezi Saba Sasa na hulazimika kuyafata Masafa ya mbali huku baadhi ya Maeneo kupata kwa Mgao usiku usiku ambapo Mnamo siku ya Tarehe 16/12 2022 Uongozi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar zawa ofisi ya Pemba walidai kuwa Suluhu ya Usumbufu huo itakamlika Mwanzoni mwa Mwezi 12 2022, kutokana na kuendelea kwa ujenzi wa mradi visima pamoja na Ukazaji wa Mabomba yakusambazia Maji jambo ambalo limeshindwa kukamilika.
Mwisho
Comments
Post a Comment