UONGOZI WA MGENI KHATIB YAHYA UNAVYOENDELEA KUACHA ATHARI KATIKA KIPINDI KIFUPI , AWATAKA WANAWAKE KUACHA WOGA NA WAJITOSE KUTAFUTA UONGOZI ASEMA WAO NDIO CHACHU KUBWA YA MAENDELEO KWA TAIFA.

NA AMINA AHMED MOH’D   PEMBA 

Moja kati ya Majukumu Makubwa  ni Uongozi, Uongozi  ni hali ya Mtu mmoja kuweza kuewa nyazifa ya juu  kuongoza Kundi la watu taasisi, Ambapo mtu huyo hupewa mamlaka ya kufanya maamuzi katika kuleta Maendeleo. 

"Dhana hiyo ya Uongozi wenye kuleta Maendeleo kwa  Miaka mingi imejengeka akilini mwa waliowengi kuwa Mtu sahihi ambae anaweza kuleta maenedleo ni mwanaume pekee jambo ambalo halina ukweli wowote ule kikubwa kinachohitajika ni utayari na uwajibikaji tu juu ya kile kinachoongozwa na sio jinsia kama wanavyodhani wengi".

              KULIA   NI DC MICHEWENI   MGENI KHATIB YAHYA 
Ni maneno ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni khatib Yahya  alipata ku uteuzi wa nafasi hiyo ya kuongoza na kusimamia wilaya  kutoka kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi Huku akiwa ni Miongoni mwa Wanawake wachache waliteuliwa kushika nafasi hiyo. 
 
Licha ya uongozi huo wa Wilaya ,  Mgeni Khatib  pia ni  mama wa Familia lakini pia na nk  Mke  ambae Anasimamia vyema majukumu yake kama mke na mama kwa watoto wake. 

Yapo mengi Mazuri ya kuigwa na Wanawake wengine  ambao wana malengo ya kuwa viongozi katika nyazifa mbali mbali za uongozi ikiwemo, uwajibikaji kupambana kutimiza malengo ya Maendeleo kwa jamii, kuishi vyema na jamii lakini na kutimiza malengo  na ndoto ambazo wanawake wengi wamekuwa wakijiwekea. 

Mgeni khatib yahya licha ya kuwa ni Mkuu wa wilaya ya Micheweni lakini Pia Aliwahi kuwa Mkuu wa wilaya ya Wete Kaskazini Pemba ambae ni Mtoto Wa sita kuzaliwa kati ya watoto Saba  Kutoka kwa Familia ya Mzee Khatib Yahya. 

 Kama hiyo haitoshi harakati zake za Uongozi zilianza muda mrefu mpka kufika hapo Alipo sasa   huku akidai kuwa siri kubwa ni kutokata Tamaa. 

 ALIANZAJE HARAKATI ZA UONGOZI MPKA LEO MKUU WA WILAYA 

Mgeni Khatib  kwa Sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Micheweni, ambapo katika Awamu ya nane Mwanamke  Ametumikia wilaya mbili kwa nyakati tofauti ndani ya Mkoa wa kaskazini Pemba,  Aidha kabla ya Kuwa Mkuu wa Wilaya Mgeni Khatib Aliwahi kuwa Mwalimu  katika Skuli ya Jadida, Utaani, Pamoja na Kizimbani ambapo alizaliwa Katika Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba na kusoma  Elimu yake Ya Msingi na Sekondari katika Skuli ya Miti  Ulaya PA momoja na Utaani kabla ya kuendelea na harakati zake za kutafuta Elimu ya juu  kisiwani Unguja. 



 Akiwa Mwalimu Alindelea na harakati za  Masomo katika Chuo kikuu cha Zanzibar University Katika fani ya Ualimu, Na baada ya Muda Kubadilisha Fani ya ualimu hadi kusomea fani ya Biashara na Masoko ambapo fani hiyo ilipelekea kubadilisha kutoka kuwa mwalimu na mfanyakazi wa wizara ya Elimu  hadi kuwa  Afisa Masoko katika Wizara ya Biashara Zanzibar. 

 JEE  DC  MGENI ALIFIKAJE KUWA KAIMU  TUME YA USHINDANI HALALI WA BIASHARA ? 

 Safari Ya kuwa kiongozi ilianza pale ambapo Wizara ya Biashara ilipoanzisha Tume maalum ya ushindani  halali wa Biashara na Ndipo Mkuu huyo alipoanza kupata nafasi ya kuwa kaimu Mratibu wa Tume  hiyo na kubahatika kuongoza kwa Muda mpka  mwanzoni mwa mwaka 2020. 

Akiwa katika harakati za Ualimu Dc Mgeni pia  alikuwa mwanaharakati katika masuala mbali mbali ya Maendeleo ndani ya Chama cha Mapinduzi ambapo suala hilo lilimpelekea kuhamasika na kugombania nafasi za Uongozi wa Majimbo  huku dhamira yake kubwa ikiwa  ni kuwa msaada kwa jamii yake iliyomzunguka katika kuleta Maendeleo , 

Ambapo Mgeni Khatib aligombea nafasi mbali mbali za ndani ya Chama  hadi kupata uthubutu wa kugombea nafasi ya Ubunge  mwaka 2020 Jimbo la Mtambwe  Mkoa wa Kaskazini Pemba Kupitia Chama cha Mapinduzi CCM jimbo ambalo lilikuwa na upinzani Mkubwa huku wapinzani wote walioligombania jimbo hilo kuwa ni wanaume . 


"Chama  changu cha Mapinduzi kiliniamini, nakunipatia nafasi  ya kuingia kugombania   Ubunge jimbo la Mtambwe, na niliweza kusimamisha vizuri bendera ya chama  kwa kuchuwana vikali na wenzangu bahati haikuwa ya kwangu kura hazikutosha  nilikosa kuwa mbunhe jimbo hilo  lakini sikukata tamaa, Niliendelea kukitumikia chama changu kwa moyo mmoja huku nikiendelea na kazi yangu na kukaimu nafasi katika wizara ya Biashara. 

 Baada ya Uchaguzi kumalizika nikiwa bado  ni mfanya kazi wizara ya biashara  nilipata Uteuzi  kutoka waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ  wa Kuwa Diwani wa kuteuliwa na kweli nilikuwa diwani wa kuteuliwa wakati huo huo naendelea kuwa kaimu wa tume ya ushindani halali wa Biashara na kumlinda Mtumiaji Pemba.

 Haikuishia hapo  harakati za  kutafuta  uongozi ziliendelea   
baada kuwa Diwani wa kuteuliwa Ikafika zamu ya kugombania  nafasi ya  Mwenyekiti  pamoja na katibu  ambae ataweza kuongoza madiwani wote Ndani  Wilaya ya Wete Dc Mgeni hakusita kulenga shabaha yake Kuomba nafasi hiyo. 

 "Niliomba kura  kwa Madiwani wenzangu kugombea nafasi ya uwenyekiti wa Madiwani na nilishinda na hatimae kuwa Mwenyekiti wa Madiwani Baraza la Mji  Wete. 

" Nilibahatika kuongoza nafasi hiyo kwa kipindi kifupi sana  cha mwezi Mmoja na nusu tu  na hapo ndipo namshukuru  Mh Rais wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi aliponiteuwa kwa mara ya kwanza kuwa Mkuu wa wilaya ya Wete. 

 Ni Maneno ya Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni khatib OK yahya.

Mkuu wa Wilaya ya Micheweni huanza  vyema Siku yake Kwa Kuamka Mapema Na kufanya Mazoezi ambapo hutumia takriban  Kilomita 4  kukimbia kila siku ili kuimarisha afya ya mwili wake jambo ambalo Hutumia kama mfano wa kuhamasisha  wananchi wa wilaya yake anaowaongoza. 

Lakini pia  kutembelea Wakulima, Wagonjwa Hospitali ni miongoni wa Tabia ambazo zimejengeka kama utamaduni wake wa kufata moja kati ya siku za Katika Wiki.

SERIKALI YA  AWAMU YA NANE

Mnamo Disemba 28 mwaka 2020 Harakati za Uongozi wa kuteuliwa kwa Mwanamke huyo kuwa Mkuu wa wilaya zilisikika katika Vyombo mbali mbali vya Habari  ambapo Rais wa  Zanzibar wa Awamu ya Nane  Dk Hussein Ali Mwinyi  Alipoteuwa Wakuu wa wilaya 10 za Zanzibar  Huku Mgeni Kuwa mmoja kati ya Wakuu hao na kuteuliwa Kwa mara ya kwanza kuongoza nafasi hiyo ya juu ya Uongozi na kuwa Rasmi Mkuu wa wilaya Ya Wete .

Anasema kwa mara ya kwanza alihisi Ugumu kwa kua hakua mzoefu, Wala hakutarajia kupata  nafasi hiyo, lakini kadri siku zilivyosonga mbele alizidi kuwa bora zaidi, na hilo ni kutokana na vitu alivyopewa kusimamia kwenda vizuri na kufanya kazi kwa utayari kwa kufuata misingi ya kisheria.

Licha ya kuwa Mpya katika Teuzi Alisema hakuwa na ugeni katika utendaji, baada ya kupata maelekezo  katika  majukumu yake na alifanya wajibu wake katika nafasi hiyo kwa vilealiwahi kuwa mtendaji katika nyazifa nyengine kabla ya kupata nafasi hiyo kubwa 

  Mwanamke hana Ugeni Popote , pia mama, Mwalimu pia ni kiongozi, niliendeleza ujasiri  wa kufanya kazi vizuri kama ninavyoisimama majukumu ya Familia yangu na kule ambako nimetoka kwa Mashirikiano. 
 
ALAMA ZA UONGOZI BORA NA MAENDELEO ZILIZOACHWA NA DC MGENI . 

Mkuu wa Wilaya ya Micheweni aliweza kuongoza Wilaya ya  Wete kwa kipindi cha Miezi 8 Pekee kabla ya kuongoza Wikaya ya Micheweni  lakini  Alama za Utendaji kazi wa kuketa mageuzi ya maendeleo uliochwa katika wikaya hiyo  hautosahaulika  kwa baadhi ya vijiji ambavyo kwa Jitihada na umakini wa kiongozi huyo aliuonesha. 

Mleteni, Tondooni,na vijiji Jirani ni moja kati ya Vijiji ambavyo vilikuwa na usumbufu mkubwa wa huduma za Maji safi  umeme barabara pamoja na vituo vya afya  katika kioindi kifupi cha Uongozi huo Shida hizo zilianza kuoata ufumbuzi. 

Anapokuwa katika utekelezaji wa Majukumu yake ya uongozi   Dc Mgeni hulazimika  kutenga  Muda maalum kuzungumza na wananchi wanaofika ofisini kwake kwa kusikikiza shida  changamoto na mawazo mbali mbali jambo ambalo limepikelewa  na kuongelewa kama Hadithi njema kwa wananchi wa Micheweni. 

WANANCHI WANASEMAJE. 

Kijiji Chetu cha Mleteni hatukuwa na imani kabisa juu ya kupata Maendeleo  ya aina yeyote ile Tunashukuru Awamu ya nane ilipomteuwa mama yetu  Bimgeni Ndio alikuwa kama ufunguo wetu wa maendeleo Alikuja  tukamueleza mambo mbali mbali na tunashukuru alileta Mpka kiongozi wa nchi kuja kujionea kero zetu na zinaendelea kupatiwa ufumbuzi Mpka leo licha ya kuwa yeye kaondoka. 

 Tunamkumbuka kwa Mazuri Huduma za afya hazikuwepo kabla yake Tatizo la maji safi ndio lilikuwa pasua Kichwa Mleteni Tunamkumbuka kwa wema kunakuja Miradi mbali mbali yakufungua maendeleo. 

 Ni Maneno ya Muhammed Omar Said na Saade Salumu (Mama nai) wa kijiji Cha Mleteni. 

Nassor Ali Ni mjasiriamali kutoka  kikundi cha   Jitihada Wilaya ya Micheweni Anasema Sio tu ni kiongozi bali ni Mama ambae anajenga matumaini kwa vijana katika Kufikia maendeleo.

 "Amekuwa akitusapoti Sisi wakulima wa  tulikuwa hatuna soko katusaidia, anapokuja hapa anakuja kama mtu wakawaida huwezi kuamini kama ni kiongozi anashika jembe analima anatupa mawazo mazuri ya kibiashara,Kusema kweli Mama amekubalika kwa sababu anajuwa kuishi na jamii yetu. 

Fatma Ramadhan Bakari  Mkufu   Issa na Asha Abdi Juma  ni wakaazi wa Wilaya hiyo, walisema  hatua  zilizofikiwa na Mwanamke huyo  zimeanza kuleta mabadiliko ambayo yanaboresha huduma za kijamii, kukuza maendeleo ya kiuchumi  kwa wananchi  pamoja na kuondoa usumbufu wa kufata huduma bora  nje ya wilaya hiyo na Kuimarisha harakati zao mbali mbali. 

KUNA TOFAUTI ILIOPATIKANA KATIKA MAENDELEO AWALI NA SASA KATIKA WILAYA HIYO! . 

Wilaya ya Micheweni ni moja kati ya Wilaya ambazo zimakuwa na harakati nyingi katika Sekta ya Kilimo,   biashara Pamoja na Uvuvi  ambapo kwa Asilimia kubwa harakati hizo  huendeshwa na Vijana pamoja na wanawake.
 
"Kama nilivyokueleza awali Ndugu Mwandishi nimesoma pia mambo ya Biashara na nina Degree kwaio sikai tu bure bure  nimekua nikitumia iyo elimu kuwasapoti vijana namna bora ya kuanzisha biashara  waweze kujikwamua kupitia kilimo chenye tija".

kama hiyo haitoshi Mimi pia nimewahi kuwa mwalimu naendelea kusimamia Mendeleo ya elimu kupambana na utiro kwa kushirikiana na wananchi na wizara,  Na kwa vile niliwahi kuwa mwanasiasa niko bega kwa bega na mshauri katika maabaraza ya vijana kuona tunatoa ushauri wa mambo mbali mbali ya maendeleo kwa vijana na wanawake  ikiwemo hili la  Uongozi. 


Harakati za kinamama kuimarika zikiwemo za ufinyanzi, ushoni na usarifu wa bidhaa kwa kushirikiana katika kutatua Changamoto zinazowakabili ikiwemo uoatikanaji wa soko. 


  Kusimamia malezi ya pamoja kudhibiti mmonyoko wa maadili kwa vijana walichini ya umri wa miaka 18 kwa kushirikiana na wazazi sambambana jeshi la Polisi. 

Jambo jengine alilofanikiwa Mwanamke huyo ni kusimamia ujenzi wa spitali ya wilaya katika eneo la Majenzi , pia usimamizi wa skuli mbali mbali ikiwemo skuli ya Mnarani makangale , ambayo imewakilisha vizuri suala la elimu katika wilaya hiyo .

CHANGAMOTO ALIWEZAJE KUZIFANYA KUWA FURSA YA KUFIKIA HAPO ALIPO SASA!. 

 "Napenda sana kujifunza kwa wengine ambao ni viongozi mambo mazuri nimekuwa nikipokea Ushauri kwa kiongozi wangu wa mkoa na kuiga pia mazuri yake ya utendaji ". 

"Nimeweza kushinda changamoto sababu kubwa ni kuwa tayari na kuamini kwamba changamoto haziepukiki Zipo nyingi tu lakini naendelea kuzishinda. Alisema Mgeni" .
 
DC MGENI ANASEMA FAMILIA SIO KIKWAZO BALI NI DARAJA LA KUFIKA HAPO ALIPO SASA. 

Nikiwa kama mama  Na mke pia Mumewangu  Ni msaada mkubwa katika harakati zote hizo nilizopitia Nakumbuka kipindi nagombea nafasi wakati napita  kuomba kura nilikuwa natumia usafiri wake yeye ndio ananiendeshea ananisubiri  na kila nilipohitaji sapoti alikuwa mstari wa mbele, na hadi sasa anaendelea kunisapoti  katika kuona nasimamia vyema majukumu yangu. 

MALENGO YAKE NI YAPI KATIKA KUENDELEZA SIFA ZA KUWA KIONGOZI BORA  ZAIDI WA TAIFA HILI KUHAMASISHA WENGINE  NA JEE ANA WITO GANI KWA WANAWAKE WENGINE. 

"Tunasimamiwa na kiongozi mwenye maono ya kuibadilisha Zanzibar sambamba na  kuendana na kasi ya mabadiliko kwa kuzingatia  mashirikiano hivyo naendeea , kutii maagizo kama msaidizi wa Serikali,  pia kupokea ushauri namna ya kuleta Mabadiliko  katika utendaji ambayo yataleta Maemdeleo zaidi kwa wananchi na Taifa "


" Wanawake Tunaweza  sna Asilimia 100 tulikuwa tunarudishwa nyuma kuonesha uwezo wetu kutokana na mfumo Dume kwa Miaka Mingi Lakini  sasa ni muda wa kuamka kuomesha Dunia uwezo wetu katika kuleta Maendeleo". 
 
Shughuli za Familia hazisababishi mwanamke kushindwa kuwajibika anapopewa uongozi  anaweza kuwajibika bila kuathiri familia wala uongozi hivyo Msiogope Tuendelee kujitokeza kuonesha uwezo wetu kwa kutenda mazuri tunapopata  nafasi. 

Kama ambavyo Rais wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi alivyoonesha kuwa na imani na wanawake kwakuwashirikisha katika nafasi mbali mbali tuendelee kumpa imani azidi kutuamini na kuongeza idadi katika nafasi za juu za uongozi. 

Ni Busara za Bi Mgeni  Khatib  kwa Wanawake Zanzibar kuelekea 20 -25

KATIBA YA ZANZIBAR INASEMAJE JUU YA WANAWAKE KUWA VIONGOZI. 

Kwa mfano katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, katika kifungu 21(2) kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu na yanayohusu taifa lake.

DIRA YA ZANZIBAR 2050 INATAKAJE JUU YA UONGOZI KWA WANAWAKE. 

Aidha Dira ya Zanzibar katika maazimio ya 2.5.1 hadi 2.5.9 yameeleza masuala mbali mbali ya usawa wa jinsia na kuondoa unyanyasaji wa kijinsia pamoja na kuimarisha mifumo ya uwezeshaji wanawake ikiwemo kuinua na kutoa nafasi za uongozi kwa wanawake katika jamii.

Pia kuongeza fursa na kuwawezesha katika vyombo vya kutolea maamuzi na kwenye shughuli za uchumi, kijamii, siasa katika ngazi zote za utawala na huduma za sheria.

 WANAWAKE KUONGOZA KWA MUJIBU WA SHERIA

Kwa mujibu wa Katiba Ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977,Ibara ya 5(1) mtu yeyote bila kujali jinsia (mwanaume au mwanamke) mwenye umri pm usiopungua miaka 18 ana haki ya kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi (Ibara ya 5(1). 

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI