WANAFUNZI MADUNGU SECONDARI WAIPONGEZA TAASISI BAREFOOT COLLEGE INTERNATIONAL ZANZIBAR, KWA KUWAFANYIA MAZURI HAYA KUELEKEA SIKU YA HEDHI SALAMA , HUKU WAKIIBUA MENGINE YANAYOHITAJI MSAADA KATIKA KUIMARISHA AFYA ZAO NA KUTIMIZA MALENGO YAO WALIYOJIWEKEA. .

NA AMINA AHMED MOH’D,    PEMBA   (O719859184). 

KILA Ifikapo May  28 Dunia huadhimisha Siku Ya Hedhi Salama Ambapo Katika kuadhimisha Siku hiyo   Wanafunzi Wa Skuli ya Sekondari Madungu wameishukuru Taasisi ya Barefoot College International Zanzibar  kwa kusherehekea siku hiyo Pamoja nao  kwa kuwapatia Elimu ya Afya ya uzazi kwa Mwanamke sambamba na kuwagawia Taulo za kike, Nguo za ndani, pamoja  Sabuni ya Unga  ambapo Wanafunzi hao wamewataka  wadau wengine kuendelea kusaidia upatikanaji wa Elimu na vifaa hivyo ili kuimarisha Afya za watoto wakike katika Maskuli mbali mbali Mijini na Vijijini na kuwaondoshea usumbufu. 
 
 Wakizungumza  mara baada ya Kumalizika kwa Zoezi la utolewaji wa Elimu hiyo ya Afya, Ugawaji wa Taulo hizo Nguo za Ndani  pamoja Sabuni Baadhi ya Wanafunzi hao wamesema  iwapo Wadau kutoka taasisi na Mashirika Mengine wataungana pamoja na  Taasisi ya  Barefoot kutasaidia kuwaondoshea usumbufu wanaokumbana nao watoto wakike wengi ambao kutokana na kukosa Elimu  na Hifadhi Wanapokuwa katika kipindi hicho hupelekea kudhorota kwa ufaulu wao. 

"Tunaishukuru  Taasisi ya Barefoot  kwa Kuona umuhimu wa kutoa Elimu hii  kwetu sisi watoto wakike, Mengi tumeweza kujifunza kupitia Siku hii ya leo ambayo tulikuwa hatuyajui, Tunaomba na wadau wengine wajitokeze kwani uhitaji wa Elimu hii  pamojana Taulo  za kike ni muhimu sana hususan ni sisi wanafunzi ambao Tunakaa katika Mabweni".

Alisema  Aisha Muhammed Omar Mwanafunzi kidato cha Tano Skuli ya  Sekondari Madungu Chake Chake Kusini Pemba. 

 "Kitendo hiki  kilichofanywa na Bare foot in kwetu kitakuwa Faraja kubwa Kitasaidia kutupunguzia gharama za ununuaji wa Pedi  na Sabuni na pesa zitatusaidia kutumia matumizi mengine  ya muhimu tukiwa hapa Skuli" Alisema Nassra  Andalla Omar Mwanafunzi. 

 Aidha kupitia Siku hiyo Wanafunzi hao pia  wameiomba Serikali  kupitia Wizara  ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba  kuwasaidia Kupata huduma Ya Maji ya uhakika Katika Skuli yao,   Dampo  la kutupa Taka,  ili kuweza kuzidisha kuimarisha Matundu ya  Vyoo  ili  kudhibiti kutopata Magonjwa   ikiwemo UTI,  pamoja naMagonjwa ya ngozi kwa wanafunzi wakike ambao wanakaa katika Madahalia 

" Skuli yetu inaukosefu wa Huduma ya Maji hususan ni Sisi ambao tunakaa katika  Dahalia hili la hapa Nje ya Skuli,  Jambo ambalo linapelekea  kutumia Maji kwa umakini kutokana na Upungufu huo hivyo,  Usafi Unapungua, Maradhi yanajitokeza  Wengine wameanza Kupata maradhi ya Ngozi,  Vyoo  havifanyiwi usafi wa kutosha tunahofia kupata maradhi Ya UTI, Walisema  Asma Ameir Khamis, Awena Khamis Ali, Pamoja na Faidhat Adam Kombo baadhi ya  wanafunzi wanaosoma na kukaa katika Dahalia Skulini Hapo. 
 Awali akitoa Elimu   Juu ya Mfumo wa Afya ya Uzazi wa Mwanamke Daktari Mstaafu Kutoka Hospitali ya Wilaya Chake Chake  Mwajuma Ali Shehe Aliwataka Wanafunzi hao Kujiepusha  na vishawishi  ili kuepuka Athari ambazo zinaweza Kujitokeza  kutokana na Maumbile yao . 
        Mwajuma Ali Shehe      Dakatari Chake Chake 


  Mfumo wa uzazi wa mwanamke Ni rahisi sana  inapotokea Mtoto wakike kavunja ungo kupata Matatizo ikiwemo ujauzito hivyo niwasihi wanafunzi  msije mkajaribu  Mambo ambayo licha ya kuwa Maumbile Yenu ya Mfumo wa uzazi  yamewaruhusu lakini Kwa Umri wenu ni Athari kubwa Mzingatie, Kusoma na Endapo  mtaona dalili ambazo ni Tofaui Msisitekuwashirikisha wazazi wenu kwajili ya Usalama Zaidi". 

 Akizungumza Mkurugenzi Miradi kutoka Taasisi ya      Barefoot College International Zanzibar   Brenda Geofrey,  Amesema  kukabidhi Vifaa hivyo kwa Wanafunzi   ni katika kuadhimisha siku Ya Hedhi Salama Duniani ambapo Taasisi hiyo kwa kuushirikiana na Dnata imedhamiria kuwafikia Jumla ya Wanafunzi 300 katika Skuli Nne  Tofauti katika Maeneo mbali mbali ya Vijijini  ambapo  katika Skuli hiyo  jumla ya Wanafunzi 70 wamekabidhiwa Vifaa hivyo kwajili matumizi salama wanapokuwa katikKipindi Cha Hedhi . 

 
 Mwisho




Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI