CP ZANZIBAR AFUNGA MAFUNZO YA SAJENTI (SGT)NA OMAR HASSAN – ZANZIBAR

Na Omar Hassan Unguja

KAMISHNA wa Polisi Zanzibar CP Hamad Khamis Hamad amefunga mafunzo ya uongozi mdogo ngazi ya Sajenti na kuwataka Askari waliomaliza mafunzo hayo kufanya kazi kwa uwadilifu na haki wanapotoa huduma kwa wananchi.
Akifunga kozi nambari 1/2023 ya cheo hicho cha SGT huko Chuo cha Polisi Ziwani CP Hamad alisema mafunzo hayo yatakuwa kichocheo cha kuendeleza nidhamu, weledi, haki na uwadilifu.  
Aidha amewahimiza wahitimu hao kutumia mafunzo waliyoyapata kulisaidia jeshi na wananchi katika kukabiliana na uhalifu na wahalifu.
Akitoa tathmini ya mafunzo Mkuu wa Chuo cha Polisi Zanzibar, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Augostino Senga alisema wanafunzi 673 wamefaulu mafunzo hayo kati ya wanafunzi 679 na wanafunzi watano walishindwa kwa sababu mbali mbali.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI