UELEWA WA KURIPOTI MATUKIO YA UDHALILISHAJI WA KIJINISIA KATIKA JAMII UMEONGEZEKA, WANAMTANDAO WAPEWA MASHIRIKIANO NI BAADA YA KUANDALIWA NA TAMWA-ZANZIBAR KUIFIKIA JAMII.






Na Amina Ahmed Moh’d, Pemba  ( 0719859184). 

UELEWA katika  Kuripoti Matukio mbali mbali ya Udhalilishaji wakijinsia kwa wanawake na watoto yanapojitokeza katika Jamii kisiwani Pemba Imeelezwa kuongezeka baada ya wanachi kuendelea kutoa mashirikiano kwa wanamtandao  pamoja na kutumiaJukwaa la Habari kuripoti Matendo hayo yanapojitokeza. 

 Hayo yameelezwa na Wanamtandao wa kupinga udhalilishaji  wa Kijinsia Kisiwani Pemba katika Mkutano maalum wa kuwasilisha Ripoti ya Ufuatiliaji wa matukio ya ukatili na Udhalilishaji   walioifanya katika kipindi cha Miezi 5 kutoka maeneo mbali mbali  ya shehia za Kusini na Kaskazini Pemba.

 Wamesema  awali Jamii ilikosa Imani juu ya Mtandao huo wa kufatilia Masuala hayo Lakini kwa sasa  uelewa umeongezeka na wanaendelea kupata Mashirikiano  katika kuendeleza mapambano  hayo. 

" Jamiii, Walikuwa wanaona kama sisi hatuna nia ya kupambana na Udhalilishaji, lakini kila siku zilivyozidi waliona juhudi zetu za kupambana na Vitendo hivyo za zati  wamekuwa mstari wa mbele kutuunga Mkonona kututafuta kila inapotokea  au kuskia kesi hizo wanatutafuta"

Tunashukuru Kupitia Mashirikiano  ya wananchi  Tumeweza kutatua kwa pamoja changamoto mbali mbali za Udhalilishaji ambazo zilikuwa sugu  Kama kutorosha,na  Wahalifu kukimbizwa baada ya Kufanya matukio. Alisema Bakar Khamis Khalid Wanamtandao huo Kutoka Wilaya ya Wete. 

" Waalimu wa Madrasa  Tulikuwa Tunapata ugumu wa kuwafikia  Lakini Tumekuwanao karibu na wao wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa Mashirikiano kwa Waalimu wa Madrasa wengine katika  kutoa elimu na kuendeleza Mapambano haya" Alisema  Ustadh Juma  Said Mwanamtandao kutoka Kengeja  Wilaya ya Mkoani. 

   kwa upande mwengine  Wanamtandao hao pia   wameiomba  Taasisi ya TAMWA-Zanzibar, pamoja na Serikali Kuendelea kuwasaidia kasi ya kuripoti Matukio ya ulawiti unaoendelea kufanywa na watoto wenyewe maskulini, sambamba na kuwezesha kuundwa kambi maalum katika shehia Ambazo zitasaidia kujenga uelewa kwa Watoto wanaofanya vitendo hivyo kwa kujielewa. 
"Wimbi la watoto zaidi ya 20 wamekuwa Wakifanya mchezo huu  wa kulawitiana wenyewe kwa wenyewe, Na wimbi hili nimelibaini Katika Shehia yangu Ya kiwani nilipopita Kutoa elimu kwa wanafunzi, Tunaomba Mtusaidie kuliangalia suala hili na Shehia nyengine Ili kushibiti Mtino huu kwa wanafunzi Wadogo, wenyewe kwa wenyewe    ambao wamefundishwa mtindo huu mchafu na Mtu mzima  Anaejielewa  Alisema Mwanaidi Vuale Khatib. 

"Kamati maalum, pamoja na Maeneo maalum ambayo yatasaidia kubadili Tabia kwa watoto watukutu ambao wamekuwa wakifanya vitendo hivi kwa watoto wenzao, Serikali Pamoja na Tamwa  Zisaidie kuwepo kama sio katika kila shehia bhasi Angalau katika wilaya ili kuona tabia kwa watoto waaina kama hizi zinabadilika. Awena Salum kombo  Mwanamtandao Kutoka Kangagani. 

Aidha  wameiomba chama hicho Kuzidisha kutoa Elimu kwa Waalimu wa Madrsa ambao wamekuwa wakiona ugumu kuzungumzia Masuala haya  ya Udhalilishaji kutokana na Sababu zao binafsi   na kushindwa kutoa Mashirikiano wanapofikiwa na Wanamtandao huo. 

Kw upande wake  Mratibu wa TAMWA-Zanzibar ofisii ya Pemba  Fat-hiya Mussa Said amewataka wanamtndao hao wa Kutumia Jukwaa la Habari kumaliza  Udhalilishaji kuzidisha kasi ya Ufuataliaji  wa  Matukio hayo yanapojitokeza katika jamii ili kuzidha kasi ya  mafanikio  katika kuibua changamoto za udhalilishaji  Ili ziweze kumalizika. 

 "Wanamtandao Mnafanya kazi kubwa  Sana Kasi hii isiwe tu baada ya kumalizika kwa mradi bali iwe endelevu hata baada ya kumalizika Meadi huu tunataka kuona Mabadiliko zaidi katika kuibua kuriooti na kuchukuliwa hatua Kesi mbali mbali za Udhalilishaji Zinapotokea katika Shehia Zetu. 

 Mkutano  Huo wa Siki Moja  wa kuwasilisha Ripoti ya ufuatiliaji wa Matukio ya Udhalilishaji  kwa Wanamtandao ni katika utekelezaji wa Mradi wa Tumia Jukwaa la Haari Kumaliza Udhalilishaji unaotekelezwa na  Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar pamoja na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Nchini Denmark (DANIDA). 
Mwisho. 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI