WANANCHI WAMPONGEZA KADUARA UTENDAJI WAKE JIMBONI WAAMUA KUMUITA TENA KUONGEZA KASI YA UJENZI WA MAENDELEO.

Na Amina Ahmed Moh’d Pemba (0719859184). 

WAKAAZI wa Kijiji cha Madungu Kosovo Wilaya ya Chake Chake Wamemuomba Mwakilishi wa jimbo hilo Shaibu Hassan Kaduara  Kuendeleza Ujenzi wa Barabara aliyoanza kuijenga  Na kuwa Faraja kwa wakazi wa kijiji hicho  katika kurahisisha huduma zao mbali mbali, jambo ambalo awali halikuweza kufanywa na viongozi waliopita ndani ya jimbo hilo.

 Wakizungumza baadhi ya Wakaazi hao wamesema Ujenzi  wa barabara hiyo  ulioasisiwa na Mwakilishi wao  wa jimbo la chake chake umesimama kwa Muda  huku kifusi kilichowekwa Awali kikianza kuburutwa na Maji baadhi ya Maeneo ya barabara hiyo kutokana na kusita kwa Ujenzi huo.

 Wamesema Matumaini yao ni kukamilishwa kwa kiwango cha lami Barabara hiyo  ambayo licha ya kuwahaijakamlika lakini  inaendelea kuwa faraja kwawananchi wa kjiji hicho hado sasa.
 "Mwakilishi wetu Amefanya jambo kubwa ambalo hatukuwahi kulitegemea , lakini yeye ameweza katuahidi kutuletea Barabara kijijini kwetu na  kafanya hivyo na mengi Mazuri  Tunampongeza sana, Furaha yetu ni kuona inakamlika kwa kiwango cha Lami  Barabara hii haiishii hapa ilipofika, tunamuomba Mwakilishi Wetu azidi  kuifanyia Maboresho  ili ikamilike kwa kiwango  cha lami na iweze kudumu kwa muda mrefu,"Alisema Hamadi Mbarouk mkaazi wa Kosovo Madungu. 

" Kwetu  wakaazi wa Kosovo Kaduara kawa Mkombozi   Wawakilishi waliopita walikuwa hawajui kama kuna kijiji kabisa ambacho kinahitaji barabara lakini yeye  tumekuwa tunamuona mara kwa mara anakuja Tunamweleza Changamoto zetu mbalo mbali  tunaamini atakaposikia taarifa hizi ataipa uzito jambo hili. 

, Gari zilikuwa hazijui zinafika wapi wagonjwa tulikuwa tunalazimika kuwabeba kwa vitanda mpka kufika kwenye barabara  mbali na kijiji Chetu, Harusi misiba, mizigo harakati za vifaa vya ujenzi lazima tulikuwa tunasumbuka lakini saivi Baada ya kuchongewa  baranara  tunaendesha shuvhuli hizo bila usumbufu.

"Tunaamini Majukumu Mazito ya Kiutendaji ndiyo ambayo yamemfanya ashindwe kuiendeleza hii barabara kwa hatua zilizobakia, na imani yetu atakapomaiza hayo majukumu atarudi kuliangalia hili ambalo hata yeye  ni moja kati ya vitu vya kujivunia.


Kiukweli tumeondokana na usumbufu katika harakati zetu baada ya kupata hii njia, hatua hii imeanza kutupa matumaini ya kupatikananjia ya kuingia na kutoka kijijini humo ambayo inatusaidia  tunaitumia  katika harakati mbali mbali bila usumbufu.

   Miaka mingi imepita   kijijini kwetu hakuna barabara ya uhakika  wala  hatukuwa na matumaini kama kuna siku tutaweza kupata  ufumbuzi wa suala hili lakini kwa sasa  tunamatumaini makubwa  kuweza kupata njia.

Alisema  Asha khamis Idi mkaazi wa Madungu Kossovo Hapa ilipofikia  tumeanza kuitumia.

Ombi hilo limekuja baada  ya wananchi wa kijiji hicho kuonekana katika harakati za Kujaza mchanga katika  moja ya  njia hiyo iliyoanza ujenzi wake na  Mwakilishi wa Jimbo la Chake Chake Shaib Hassan kaduara na kuonekana ikiwa tayari imeanza kuchimbuka huku ujenzi ukiwa umesimama kwa Takriban miezi Mitano Sasa. 

Harakati za  kumtafuta Mwakilishi  wa Jimbo hilo  kulizungumzia Suala hili zinaendelea. 



  
   

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI