ZSSF PEMBA YATOA TAHADHARI KWA WASTAAFU , NI BAADA TA KUJITOKEZA MATAPELI KUTUMIA VIBAYA KAULI YA DK MWINYI KUONGEZA PENCHENI KUIINUA MGONGO.





NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA (0719859184). 

 UONGOZI wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar Zssf Pemba Umewataka Masheha  Kutoa Taarifa za uhalifu na Utapeli  zinazoendelea  Kujitokeza katika Shehia zao  Ambazo zinafanywa na baadhi ya watu ambao sio waaminifu  kwa  kutumia jina na mwamvuli wa mfuko huo  na kufanya  udanaganyifu kwa wazee wastaafu  wakidai  kuwa wanafanya usajili kwajili ya kupata Pencheni zao kwa haraka na kuwachukulia fedha .

 Akizungumza na Waandishi wa Habari Kaimu Mkurugenzi Zssf Pemba Dk. Said Salim Maalim  Amesema watu hao  ambao wamekuwa wakipita katika maeneo mbali mbali ya kisiwa cha Pemba  wakiwaeleza wazee wastaafu  kuwa wao ni Wafanya kazi kutoka Hazina Zssf  na kujitambulisha katika Uongozi wa Shehia Na hatimae kupata ruhusa ya  kuingia Mitaani kufanya udanganyifu huo  limekuwa likijitokeza katika maeneo mbali mbali  hivyo Masheha kuendelea Kuchukua Tahadhari  ili wazee na wastaafu  wasiendelee kutapeliwa.

" Matukio haya ya Udanganyifu yameanza kujitokeza takriban Shehia Nne  wilaya  zote za Pemba na   Watu hawa ambao wanafika katika uongozi wa Shehia kujitambulisha na kuingia katika majumba kufanya udanganyifu huo, Tuweke wazi kwamba Zssf haiwatambui hivyo Wananchi endeleeni kuchukua Tahadahri, kuepuka utapeli huu.

"Hawa ni watu ambao hawapendi Maendeleo na wanaitumia vibaya kauli ya Mh Rais  Wa Zanzibar Aliyoitoa Siku ya Wafanya kazi juu ya kuongeza  Pencheni  (Kiinua Mgongo) kwa Wastaafu kwa kuwafuatamajumbani  kuwarubuni na kujipatia wao kipato  kwa njia ya udanganyifu  kwa kutumia mwemvuli wa mfuko wa Zssf jambo ambalo ni kinyume na Sheria.
 
 Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo amesema tayari  Uongozi wa Zssf Pemba  umeanza kulichukulia hatua Suala hilo ikiwa ni Pamoja na kuweka taarifa  katika Vyombo vya Ulinzi na usalama Jeshi la Polisi.

 Hata hivyo Amewataka wastaafu  wote wanaopokelea pencheni Zao  Katika Mfuko Huo   kuendelea kufuata utaratibu waliowekewa na Zssf ili kuepusha Usumbufu huo. 
 " Kupitia vyombo vya habari niwasihi wastaafu muache kuamini i maneno yanayotolewa  mitaani   kutoka kwa watu watu wasiokuwa na nia njema na Serikali,Zssf ipo Na itakapobadilisha utaratibu juu ya Jambo lolote mtajuilishwa kwa utaratibu maalum   msikubali utapeli,  kwa Mabadiliko ya nyongeza za Pencheni mkarubuniwa jambo ambalo liliwekewa  utaratubu  maalum kwa wastaafu wote

 Kwa Upande de wake  Raya Hamdan Khamis  Ambaye ni Afisa uhusiano na Elimu kwa Umma ( Zssf ) Pemba  amewataka  Masheha Kutowaamini wau ambao wataingia katika shehia Bila utambulisho maalum  ikiwemo barua Rasi kutoka taasisi husika ili kuepusha kadhia  kama hizo kwa wazee.

  Udanganyifu huo  ulioripotiwa kutoka maeneo mbali mbali   Pemba  umeelezwa kuwa zaidi ya wastaafu 4   wamefanyiwa udanganyufu huo na kurubuniwa shilingi elfu 80 kila mmoja,   katika wilayaya wete,  Shehia ya Jadida, Gando, Mkoani, pamoja na Chake Chake. 

Mwisho. 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI