KONDE WAMPONGEZA MWAKILISHI ZAWADI KUWASAIDIA KUPATA HUDUMA ZA KIJAMII.

NA AMINA AHMED MOH’D  PEMBA. 

BAADHI ya Wananchi na wakaazi wa  Konde Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wamesema kasi ya Maendeleo inayoendelea kuoneshwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Zawadi Amour Nassor katika nyanja mbali mbali Ikiwemo Maendeleo ya  Elimu  pamoja na  Upatikanaji wa Huduma ya safi na Salama  imekuwa ikisaidia kuondosha Usumbufu waliokuwa wakipata Awali wao pamoja na watoto. 

 Wakizungumza na Habari Hizi Halima Juma  Khamis Mkaazi Wa  Matangatuani Konde Mkoa Wa Kaskazini Pemba Pamoja Na Nunu Khamis  Mkaazi wa Kiuyu kwa Manda  Wamesema Usumbufu waliokuwa Wanapata Wanafunzi wa Kijiji hicho  kufata Elimu masafa ya mbali ulikuwa ukiathiri kwa kiasi kikubwa Maendeleo yao.

"Tunashukuru Mwakilishi wetu wa Jimbo la Konde Mh Zawadi kwa kutusaidia kupatikana Skuli mbili Maeneo ya karibu  ambazo zimeondosha usumbufu kwa watoto wetu, Walikuwa wanalazimika kuenda  Mgogoni jambo ambalo lilikuwa ni usmbufu kwao" Alisema Bi Nunu.

Hapakuwa na Skuli hapa zamani  Kila siku tulikiwa tunatoa malalamiko yetu Tulipopata Kiongozi  anaejuwa Machungu ya Kufuata mbali Elimu  Tunashukuru Ameisogeza huduma hii karibu Leo kijijini petu zimejengwa Skuli Mbili  ambazo watoto wetu wanasoma Matangatuani na Kule Meli 9 Tunashukuru sasa wanafunzi hawaendi tena mbali Mgogoni au Konde wanasoma hapa hapa".Alisema
 
 Watoto wetu wadogo miaka 4 mitano  walikuwa hatarini kutokana na kukosekana Skuli apa  kiuyu kwa Manda  Walikuwa wanatembea umabli mrefu kukatisha mabarabara,  Huku roho zilkuwa hatarini  hofu ya udhalilishaji tulikuwa tunalazimika kuvunja shughuli zetu kuwapeleka Lakini leo Adha imepungua Alidai Bi Nunu. 

Kwa upande wao Baadhi ya vijana wa jimbo hilo ambao wanaendesha Boda boda kujipatia kioato  Wamemshukuru Mwakilishi Zawadi kwa kuwasaidia kupata Elimu juu ya  Usalama  Wa Barabarani. 

Nilikuwa naendesha tu kienyeji enyeji sijasoma lolote  Mwakilishi wetu Alifanikisha Mimi na wenzangu wengi ambao tunafanya kazi hii kusoma Tulitoka hapa konde Hadi micheweni kupata Mafunzo ya udereva na leo hii yanatusaidia kudhibiti ajali za kiholela Tunamshukuru kwa mchango wakeAlisema Said Suleiman. 

 Wakizunguzia Suala La Maji Baadhi ya Wananchi Wa Jimbo hilo walisema kuwa usumbufu waliokuwa wanaupata awali  kutafuta huduma ya Maji umeondoka kutokana na Kujengewa Visima ambavyo Vinasaidia Kupatikana Maji kwa urahisi. 

 Akizungumza na Habari Hizi Mwakilishi  Wa Jimbo Hilo Zawadi Amour Nassor Amesema Maendeleo hayo Ambayo Yanaendelea Kupatikana  ndani ya Jimbo la Konde ni kutokana na Usimamizi mzuri wa Matumizi ya fedha za Mfuko Wa jimbo na Ushirikiano kutoka kwa Mashirika Mbali mbali. 

Niliahidi wakati Naomba ridhaa  kwa Wananchi kupigania Maendeleo ya jimbo la Konde , kusimamia upatikanaji wa Maji ili kuwatua ndoo Kichwani akina Mama, ni kweli kwa Kushirikianana Direct aid Nimefanikiwa kujenga na kuchimba  Visima  5  maeneo mbali mbali  vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 95, 

Aliendelea kuwa "Na kupitia Maji ya Zawa nimefanikiwa kufikisha Maji ya bomba katika shehia ya  Kifundi ambayo imekuwa  ikipeleka maji hayo na sheia jiarani. 

 Aidha Alisema Mradi unaotekelezwa na Serikali juu ya Ujenzi wa Tangi la Maji Kipange unadhamira njema ya kuondoa usumbufu kwa wananchi  wa Maeneo mbali mbali ikiwemo Makangale. 

Mwakilishi huyo alisema kuwa Furaha yake kubwa ni kuendelea kutatia Shangamoto za wananchi ndani ya jimbo hilo na kuona wanaendelea kufurahia kupata huduma bora. 

Mwisho. 


Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI