Posts

Showing posts from February, 2023

FURSA NA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI VIJANA KATIKA KUFIKIA MAENDELEO YA KUJIKOMBOA KIUCHUMI WAOMBA SERIKALI KUENDELEA KUWASAIDIA KUZIPATIA UFUMBUZI ILI KUZIDISHA KASI YA KUZIFIKIA FURSA MBALI MBALI KATIKA SIASA UCHUMI NA UONGOZI .

Image
NA  - AMINA AHMED MOH’D  -PEMBA.   MAENDELEO ya Nchi nyingi Yametokana na  nguvu kazi pamoja ma  Utendaji kazi wa vijana .    Kila Taifa linategemea Vijana kufikia Malengo mbali mbali ya kukuza Uchumi na kuleta Maendeleo.  Fursa mbali mbali ambazo vijana wamekuwa wakizitumia ndio siri pekee ya Kufikia Malengo ya kulipeleka mbele Taifa.  Moja kati ya Sifa za kufikia Fursa mbali mbali ikiwemo  Maendeleo  kwa Vijana ni kuwa Na  Elimu ambayo itasaidia kuongeza ufanisi juu ya Lile lengo lililokusudiwa la kuacha utegemezi  na kujiajiri wenyewe Kupitia Fursa  Zilizomo Katika Sekta  na nyanja Mbali mbali ikiwemo Uongozi, Uchumi, Na Siasa.    KIJANA NI NANI!  ‘ ’KIJANA ni mtu yeyote mwenye umri wa miaka 15 hadi miaka 35,’’ndivyo sera na sheria ya vijana Zanzibar inavyofafanua. Lakini kwa upande mwengine kijana ametafsiriwa kuwa ni mwanamke au mwanamme yeyote mwenye miaka katia ya 15 hadi 24...

BI ABEDA ASHAJIHISHA ELIMU YA WATU WAZIMA KATIKA SHEHIA YA KITOPE.

Image
Na RAIFFA ABDALLAH   UNGUJA  MKUFUNZI wa elimu ya watu wazima Abeda khamis Mohamed, amehimiza jamii kuyapa umuhimu masomo ya watu wazima ili waweze kujihudumia. Bi Abeda ameyasema hayo wakati akingumza na Mwandishi wa habari hizi huko katika shehia ya kitope, wilaya ya Kaskazini B,  mkoa wa kaskazini Unguja.  Amesema lengo la kuyaanzisha masomo hayo ni  kuwasaidia watu ambao hawakubahatika kupata elimu katika enzi zao za utotoni jambo ambalo linawafanya kupitia wakati mgumu sana kwani elimu ndio kila kitu katika maisha ya leo. Hata hivyo amesema , elimu hiyo itawawezesha watu kujuwa kuandika na kusoma kwani hii itafanya wawe na uelewa mzuri wa mambo ambayo yanatokea katika jamii na kuwawezesha kutoka michango ya kimawazo wakati ukihitajika.  " watu walio wengi hawajui hata kuandika majina yao na ukiwambiya waje kusoma wanakuwa hawajitokezi , darasa la kusoma watu 15 lina wanafunzi  6 na wengi wamesajili majina yao lakini hawahudhurii d...

MWANAMKE ALIEPANIA KUKUKUZA KIPAJI CHAKE KWAAJILI YA KUISAIDIA JAMII.

Image
NA      SALMA SHAALI - UNGUJA     REHEMA Ali Mzee maarufu kama Ranisha ni binti mwenye umri wa miaka ishirini na sita (26) mkaazi wa fuoni pangawe (Unguja), ambae ni mwanamke aliepania kukuza kipaji chake kwaajili ya kuisaidia jamii,ambapo anajishuhulisha na biashara ya utengenezaji wa keki za aina tofauti pamoja na mchanganyiko wa viungo mbali mbali (rosted spice) ambayo hutumika katika vyakula tofauti ikiwemo supu ya kuku,mchuzi,biriani na vyenginevyo.        Rehema aliaza kazi ya kutengeneza keki tangu alipokuwa mdogo na alikuwa hajapa darasa lolote linalohusiana na utengenezaji wa keki, Baada ya kujigundua Kuwa anakipaji akaona ni vyema kuitumia fursa hiyo ili aweze kujiletea maendeleo pamoja na kuisaidia jamii yake iondokane na tatizo la uhaba wa ajira.Rehema anasema,        ”Baada ya kujigundua kuwa nina kipaji na napenda kutengeneza keki nikaona nibora niende kwa mwalimu ili...

HII HAPA SABABU YA DK MZURI MKURUGENZI WA TAMWA ZANZIBAR KUACHA KAZI IKULU.

Image
NA - YUSRA SAID   UNGUJA.  MKURUGENZI wa chama cha waandishi wa habari Tanzania TAMWA Zanzibar Dr. Mzuri Issa Amesema Tamwa itaendelea kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili kuhakikisha uwandishi wao unakuwa wa kuleta mabadiliko ya kimaendeleo hasa katika kuonyesha nafasi ya wanawake na uongozi  visiwani Zanzibar.         MZURI ISSA ALI- MKURUGENZI TAMWA ZANZIBAR.  Akizungumza na muandishi wa habari hii Mkurugenzi wa chama hicho Dr.Mzuri Issa amesema kwa kipindi kirefu kilichopita nyuma wanawake na wasichana walikuwa hawaandikwi vizuri katika vyombo vya habari jambo ambalo lilikuwa likimpa shida hivyo ameona ni vyema kuwapatia uwelewa waandishi wa habari ili waweze kuonyesha wanawake nafasi na mchango wa wanawake kwa jamii. Amesema ilifika hatua Watoto na wanawake wanafanyiwa udhalilishaji lakini hakuna mtu wa kuripoti matukio hayo ambapo ilipelekea kuzidi kufanyiwa vitendo hivyo. Aidha amesema kuwa katika Maisha ya usichana wak...

VIJANA WAASWA MAMBO HAYA KUFIKIA NAFASI ZA UONGOZI

Na MASSOUD  JUMA - UNGUJA  VIJANA  wa Zanzibar wanaotarajia kushika nafasi mbalimbali  za uongozi wameshauriwa kujikubalisha kuzikabili changamoto zote ambazo zinatokea katika uongozi na kuwa majasiri katika kutekeleza wajibu wao. Ushauri huo umetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo bi Fatma Hamad Rajab wakati akizungumzia masuala ya wanawake na uongozi huko ofisini kwake Migombani Zanzibar. Bi Fatma pia amevitaka vyama vya siasa nchini kuendelea kuwaandaa na kuwapika vijana hasa wa kike ili kuja kuwa viongozi waadilifu, wabunifu na makini na hatimae kuiletea maendeleo Zanzibar. Nae Mkurugenzi wa taasisi ya Warrior Women Foundation bi Sabra Issa Machano amewataka vijana khasa wa kike wanaotamani kushika nafasi za uongozi wawe tayari kwa kuanza chini kwa kuhudumu katika vyama mbalimbali vya siasa ambavyo wanataka kugombea kwa kutumia uwakilishi wao. Aidha, Katibu Mkuu wa wizara ya HVUM bi Fatma Rajab ameelezea umuhimu wa wanawake kujishugl...

WAKULIMA WASHAURIWA KUTUMIA MBOLEA ASILIA KUTUNZA MAZINGIRA

Image
Na UWEISIYA KHAMIS UNGUJA  WAKULIMA na wamilikk wa mashamba wametakiwa kutumia mbolea Asilia itokanayo na vinyesi,majani makavu,majani ya mjenga uwa  ili kuwawezesha kuvuna mazao yenye ubora , inayowawezesha  kulinda afya ya mlaji pamoja na kuhifadhi mazingira . Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi  Mkurugenz i Mtendaji wa kampuni ya Kilimo hai Input Arafa Hamad huko ofisini kwao Mkoa wa kaskazini wilaya ya kaskazini B shehia ya kiomba mvua  amesema Utumiaji wa mbolea Asilia ni mbolea yenye faida nyingi kwa mmea kwasababu majani ya mjenga ua yana nitrogen ya kutosha ,samadi ya ngombe ina potassium na nitrogen ambayo inasaidia kulinda afya ya mlaji kwa kuvuna mazao yenye ubora pamoja na kuhifadhi mazingira , Aidha amesema kuwa changamoto kubwa ambayo wanakutana nayo ni Uhaba wa soko na uwelewa mdogo wa wakulima juu ya utumiaji wa mbolea asilia . sambamba na hayo ameeleza jitihada ambazo anazichukua katika kuengeza uelewa wa wakulima juu ya utumiaji...

Serikali kusaidia Wanawake wajasiriamali

Image
 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kusaidia vikundi vya  kina mama ili viweze kupata mikopo na kujikwamua kimaisha.   Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ametoa kauli hiyo alipofanya mazungumzo na Uongozi wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) waliofika kujitambulisha Ofisini kwake Vuga Jijini Zanzibar.   Mhe. Hemed ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa amesema Serikali inatoa Mikopo ya gharama nafuu kwa vikundi vya wajasiriamali kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua kiuchumi na kuwaahidi kina mama kuwa Serikali inatoa kipaumbele kwa wanawake ili waondokane na utegemezi.   Mhe. Hemed ameeleza kuwa dhamira ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kutenga fedha kwa ajili ya mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali  ni  kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi.   Sambamba na hayo Mhe. Hemed ameupongeza Uongozi wa UWT kwa kuandaa mpango kazi ambao u...

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

Image
SALMA KHMIS - UNGUJA                           KATIKA Uongozi wa taifa hili viongozi ambao wako karibu na wananchi na wanapaswa kuhakikisha maendeleo yanafikiwa na yanafanyika ni Masheha. Masheha wa Wilaya ya Magharib B wamejipanga kuhakikisha maendeleo na mabadiliko yanapatikana ndani ya shehia zao. Wilaya ya Magharibi B ni miongoni mwa Wilaya tatu zilizomo katika mkoa wa mjini magharib  Unguja  ambapo Mkoa huo una jumla ya masheha 121 kati ya hao 19 ni wanawake na 101 ni wanaume. Wilaya ya Magharibi B ni Wilaya iliyotoa shehia 34 kati ya hizo shehia 6 zinaongozwa na masheha wanawake na shehia 28 zinaongwa na masheha  wanaume. Shehia ya kijitoupele na michungwani ni Shehia maarufu zilizomo katika Wilaya ya Magharib B  ambazo zinaongozwa na Masheha wanawake. Shehia hizo kwa kiasi kikubwa zimepiga hatua za kimaendeleo ikiwemo kueka mazingira safi na kupambana na vitendo vya uchimbaji wa ...

KITUO CHA HUDUMA RAFIKI CHAZINDULIWA BUMBWISUDI.

Image
NA KHAIRAT HAJI, UNGUJA.  UMOJA  wa Mataifa wa idadi ya watu UNFPA na shirika la Mfuko wa kimataifa wa watoto UNICEF wamezindua rasmi kiliniki ya huduma rafiki kwa vijana huko Bumbwisudi wilaya ya Magharibi “A” Unguja. Kliniki hiyo imezinduliwa rasmi na waziri wa afya Zanzibar Mheshmiwa Nassor Ahmed Mazrui tarehe 15/02/2023  ambapo imekarabatiwa chini ya mradi wa Wezesha Wasichana ambao unafadhiliwa na serikali ya Canada. Katika uzinduzi huo, UNFPA iliikabidhi wizara ya afya mashine mbili za ultra sound zitakazowasaidia kina mama wajawazito ili kubaini matataizo na kusaidia kupatikana kwa mimba salama. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mheshmiwa Mazrui alisema kuwa kliniki hiyo ya kituo cha huduma rafiki kwa vijana itawawezesha vijana kupata taarifa kwa wakati na huduma za kitaalam ili kupunguza madhara ya kiafya yanayosababishwa na kutumia njia za uzazi wa mpango bila ya kufuata ushauri maalum wa wataalam wa afya. Aidha, mwakilishi mkaazi wa UNFP...

DK MZURI ATILIA MKAZO SERA YA JINSIA KATIKA VYOMBO VYA HABARI, KUMALIZA UDHALILISHAJI MAOFISINI LAZIMA ITUMIKE IPASAVYO

Image
NA KHAIRAT HAJI,  UNGUJA  MKURUGENZI  wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar, Dk Mzuri Issa Ali Amesema sera ya jinsia kazini ndio chachu  ya kupunguza masuala ya udhalilishaji  maofisini.  Dk Mzuri ameyasema wakati wa uwasilishaji ripoti za madawati ya jinsia yaliyomo ndani ya vyombo vya habari   ambavyo vilipatiwa mafunzo  na Tamwa Zanzibar, yaliofanyika huko   ofisini kwao Tunguu, Unguja.  . Dk Mzuri  ameongeza kuwa sera na madawati ya jinsia yanatakiwa kuwa ndio macho na masikio ya kuhakikisha  kuwa masuala ya kijinsia yanaripotiwa  vizuri maofisini.  Aidha Dk Mzuri amesema kuwepo kwa sera ya jinsia na madawati yake katika vyombo vya habari  kutasaidia sana kuhakikisha kuwa habari za jinsia zinaripotiwa ipasavyo .  Ndugu Husna Mohammed ambae ni mkuu wa dawati la jinsia katika gazeti la Zanzibar leo amesema  anaishukuru sana  Tamwa Zanzibar kwa ku...

MWANAMKE WA MFANO ALIESHIKA NAFASI YA UWAKILISHI AWAMU 2, KUPITIA KURA ZA WANANCHI ALIELETA MAENDELEO

Image
NA ASIA MWALIM - UNGUJA  WAKATI Tanzania na Zanzibar zinatanua wigo wa demokrasia na utawala bora, juhudi za kupunguza pengo kati ya wanawake na wanaume zinaendelea na kupata mafanikio kiasi. Hilo limedhirika kutokana na nchi hizo kusaini mikataba ya kikanda na Kimataifa kwamba itazingatia usawa wa kijinsia kati ya wanawake na wanaume katika uongozi. Wakati huu wanawake wa Zanzibar wanathubutu kugombea na kushinda katika nafasi mbaali mbali za uongozi, ingawa nafasi za kuteuliwa zinaonekana  zimekua ni nyingi zaidi. Mwanaasha Khamis Juma, Mwakilishi wa Jimbo la Dimani ni miongoni mwa mwanamke wa kupigiwa mfano, kwa kushika nafasi hiyo kwa khatamu 2, kupitia uchaguzi mkuu unaofanyika kila baada ya miaka 5. Mwanamke huyo amekua mfano kwa wanawake wengine Zanzibar kutokana na harakati anazopitia katika kuhakikisha anaendelea kuwa kiongozi bila ya kubabaishwa na wale wasiopenda maendeleo ya wanawake. Alisema jitihada zake katika uongozi mara zote huwa hazimuachi nyuma,...

Haya hapa Mazuri Yaliofanywa na Mkuu wa wilaya ya Magharib B Hamida Mussa Khamis Wananchi ,Wajivunia Mabadiliko katika ukuwaji wa Maendeleo nyanja Mbali mbali

Image
NA ASIA MWALIM  "KUWA Mkuu wa wilaya ni jukumu kubwa na zaidi kwa wanawake, watu wengi hutupa changamoto kwa kuangalia jinsia zetu, lakini wanakuta tupo imara licha ya ujana jike wetu". Hayo ni maneno ya kiongozi mwanamke ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Magharibi B, Hamida Mussa Khamis(45 )aliebahatika kupata uteuzi wa nafasi hiyo kutoka kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi.   Licha ya uongozi, mwanamke huyo ni mama wa familia yenye watoto watatu 3, 1 wakiume na 2 wakike na pia anapokua nyumbani kwake anapenda zaidi kupika. Mwanamke huyo ni mfano wa kuigwa na wanawake wengine kwani ni miongoni mwa wanawake alietumika serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika awamu zilizopita na pia kuendela kupata nafasi nyengine ya uongozi katika awamu ya nane.  KABLA YA KUWA MKUU WA WILAYA YA MAGHARIBI B  Harakati za uongozi wa kuteuliwa kwa mwanamke huyo zilianza mwaka 2015, kupata nafasi ya Katibu Tawala wa wilaya ya Magharibi B, a...

UFUGAJI WA MAJONGOO BAHARI UNAVYOWANUFAISHA WANAWAKE KIUCHUMI VISIWANI.

Image
Na UWEISIYA KHAMIS- UNGUJA.  ZANZIBAR Ni njrma atakae aje sababu Mengu ni Neema Tupu ii ni baadhi ya misemo ambayo imesikika kwa wingi tangu raisi wa zanzibar wa awamu ya nane  aingie madarakani na mmoja kati ya sera ambazo alikuwa anazizungumza sana ni pamoja na suala la UCHUMI WA BULUU ikiwa lengo ni kuinua uchumi wa zanzibar kupitia rasilimali bahari.   "Uchumi wa buluu ni suala jipya katika nchi yetu tafsiri yake ni uchumi endelevu unaotokana na matumizi sahihi ya rasilimali za bahari ,kama ilivyo katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi namba 187 ikiieleza uchumi wa buluu na ambao unaweza kuajiri takriban vijana 300,ooo"  uchumi wa buluu ni dhana pana yenye kubeba maana nzima ya kutumia rasilimali itokanayo na bahari ikiwemo utalii,uvuvi,kilimo cha mwani,ufugaji wa majongoo bahari ,bandari pamoja na mafuta na gesi. Ndani ya makala hii  tutaangalia namna  UFUGAJI WA MAJONGOO BAHARI UNAVYOWANUFAISHA WANAWAKE KIUCHUMI VISIWANI ZANZIBAR,  ...