DK MZURI ATILIA MKAZO SERA YA JINSIA KATIKA VYOMBO VYA HABARI, KUMALIZA UDHALILISHAJI MAOFISINI LAZIMA ITUMIKE IPASAVYO

NA KHAIRAT HAJI,  UNGUJA 

MKURUGENZI  wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar, Dk Mzuri Issa Ali Amesema sera ya jinsia kazini ndio chachu  ya kupunguza masuala ya udhalilishaji  maofisini. 

Dk Mzuri ameyasema wakati wa uwasilishaji ripoti za madawati ya jinsia yaliyomo ndani ya vyombo vya habari   ambavyo vilipatiwa mafunzo  na Tamwa Zanzibar, yaliofanyika huko   ofisini kwao Tunguu, Unguja. 
.

Dk Mzuri  ameongeza kuwa sera na madawati ya jinsia yanatakiwa kuwa ndio macho na masikio ya kuhakikisha  kuwa masuala ya kijinsia yanaripotiwa  vizuri maofisini. 

Aidha Dk Mzuri amesema kuwepo kwa sera ya jinsia na madawati yake katika vyombo vya habari  kutasaidia sana kuhakikisha kuwa habari za jinsia zinaripotiwa ipasavyo . 

Ndugu Husna Mohammed ambae ni mkuu wa dawati la jinsia katika gazeti la Zanzibar leo amesema  anaishukuru sana  Tamwa Zanzibar kwa kuwapatia mafunzo ya kuanzisha sera ya jinsia kwani  mafunzo hayo yamekuwa ni chachu pia ya  kuanzishwa kwa Gazeti maalum la wanawake ambalo hutolewa  kila mwisho wa mwezi. .

Said Omar kutoka Radio Jamii Mkoani Pemba, Amesema kuwa yeye kama Mhariri Mkuu wa Radio hiyo atajitahidi kuhakikisha kuwa sera hiyo  inatekelezwa ipasavyo. 

Aidha Ndugu Maryam Ame afisa mradi wa kuongeza nafasi za wanawake katika uongozi kutoka Tamwa Zanzibar amewataka wakuu na wajumbe wa madawati hayo kuzungumza  na  viongozi wao na kuona ni kwa namna  gani madawati  hayo yanakuwa na mamlaka katika utekelezaji wake kwa watendaji wa vyombo vya habari.
 Afisa Mdhamini wa Baraza la Habari Tanzania Shifaa Hassan ametoa wito kwa wahariri na watendaji wa vyombo vya Habari kuimarisha Sera ya jinsia na kamwe isibaki katika mafaili bali ifanyiwe kazi kwa vitendo. 

Sera ya jinsia katika vyombo vya habari ni muongozo wa mwenendo wa utendaji kwa wamiliki wa vyombo vya habari pamoja na wafanyakazi wote ambayo itatengeneza  mazingira mazuri salama na bora kwa ajili ya kufanya kazi ndani  ya vyombo  vya habari.

Mafunzo ya kuanzisha Sera ya Jinsia katika vyombo vya habari kwa viongozi na waandishi wa habari  yametolewa na  Tamwa  Zanzibar   mwezi Agosti mwaka 2022  kwajili ya kupunguza  masuala ya udhalilishaji na kuongeza hadhi kwa watendaji wa kike, na mpaka sasa takriban  vyombo vya  habari 6 Zanzibar  vimeshawasilisha Sera hiyo Kwa Tamwa Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI