Posts

Showing posts from January, 2023

Tume kurekebisha Sheria yaahidi Mabadiliko kufikia usawa wa kijinsia katika Uongozi.

Image
NA ASIA MWALIM-  UNGUJA TUME ya Kurekebisha sheria Zanzibar, imesema itashirikisha na Tume ya Sheria Jamhuri ya Muungano ya Tanzania katika kuzifanyia mapitio sheria zisizo zingatia jinsia katika ushiriki wa wanawake katika uongozi na ngazi za maamuzi .  Katibu wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, Mussa Kombo Bakari, aliyasema hayo wakati wa semina ya majadiliano ya sheria yaliandaliwa na shirika la Women in Law and Development Africa (WILDAF), huko Beach Resort Mazizini Unguja.  Alisema tume hizo kwa pamoja zitazingatia suala la wanawake wakati wa kufanya mapitio ya sheria ya vyama vya siasa na sheria ya taifa ya uchaguzi, ili kuona kundi hilo linakua mstari wa mbele.  Aidha alisema lengo la semina hiyo ni kujenga uwezo wanasheria ili wapate kuwakisi masuala ya wanawake wakati wa kuzipitia sheria, hatimae kutoa miongozo mizuri kwa makundi yote.  Katibu Mussa, alifahamisha kuwa, sheria za awali zilishindwa kuzingatia jinsia, ni muhimu kujenga uele...

WAANDISHI ANDIKENI MAZURI YANAYOFANYWA NA WANAWAKE KATIKA JAMII NA TAIFA YAPO MENGI YA MFANO.

Image
  NA AMINA AHMED MOH’D- PEMBA.  WAANDISHI wa habari Zanzibar  wameaswa kuwaibua na kuwandika Vizuri  wanawake wanaoendelea kufanya mambo Mazuri ya kuleta Maendeleo   katika jamii na Taifa katika nyanja  mbali mbali ili  kutoa wigo kwa wanawake wengine na  kusaidia kuongeza idadi ya viongozi wanawake ambao wataaminika katika Jamii.              DK  MZURI ISSA ALI -  MKURUGENZI TAMWA-ZNZ    Ametoa ushauri huo Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar Dkt, Mzuri Issa Ali  alipokua akizungumza   waandishi wa habari vijana wa vyombo mbali mbali kutoka Unguja na Pemba ambao wanaendelea kupatiwa Mafunzo maalumu ya  kujengewa uwezo juu ya kuripoti habari za wanawake kushika nafasi za uongozi  katika nyanja mbali mbali sambamba na kuchochea uwajibikaji kwa maslahi ya jamii.  Alisema kwa muda mrefu wanawake wengi wamekua w...

Tume ya kurekebisha Sheria Yaahidi Mashirikiano kurekebisha Sheria

NA ASIA MWALIM - UNGUJA  TUME ya Kurekebisha sheria Zanzibar, imesema itashirikisha na Tume ya Sheria Jamhuri ya Muungano ya Tanzania katika kuzifanyia mapitio sheria zisizo zingatia jinsia katika ushiriki wa wanawake katika uongozi na ngazi za maamuzi .  Katibu wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, Mussa Kombo Bakari, aliyasema hayo wakati wa semina ya majadiliano ya sheria yaliandaliwa na shirika la Women in Law and Development Africa (WILDAF), huko Beach Resort Mazizini Unguja.  Alisema tume hizo kwa pamoja zitazingatia suala la wanawake wakati wa kufanya mapitio ya sheria ya vyama vya siasa na sheria ya taifa ya uchaguzi, ili kuona kundi hilo linakua mstari wa mbele.  Aidha alisema lengo la semina hiyo ni kujenga uwezo wanasheria ili wapate kuwakisi masuala ya wanawake wakati wa kuzipitia sheria, hatimae kutoa miongozo mizuri kwa makundi yote.  Katibu alifahamisha kuwa, sheria za awali zilishindwa kuzingatia jinsia, ni muhimu kujenga uelewa kwa wanasheria ...

WAANDISHI WA HABARI TAIFA LINAWASIKILIZA SANA TUMIENI FURSA HII KUSAIDIA MAKUNDI YALIOSAHAULIKA KATIKA KUSEMEA CHANGAMOTO ZAO ZIPATE UFUMBUZI.

Image
NA  AMINA AHMED MOH’D - PEMBA  " TUNGEPENDA  kuona kesi Za udhalilishaji kwanza Kila Mwaka zinapungua, hatutaki kabisa kudhalilishwa,wanawake, watoto na watu wenye Ulemavu ,Tuangalie ukuaji na Uwajibikaji  wa Vyombo vinavyosimamia Sheria, kwa sababu  Mwandishi wa Habari anaweza kufuatalia  mlolongo mzima wa kesi   mwanzo hadi mwisho na jamii ikaweza kuelewa, Bado kuna malalamiko katika masuala ya utolewaji wa hukumu baadhi ya watu wanakuwa huru  huku jamii ikijiuliza masuali yanayokosa majibu hivyo  waandishi tuyaone haya  katika kuandika  habari zetu" .  Ni kauli ya Mkurugenzi  Chama  Cha waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar Tamwa Dk Mzuri Issa Ali Alipokuwa Akifungua Mafuzo ya siku mbili kwa  Waandishi wa Habari wa vyombo mbali mbali Unguja na Pemba  kwa njia ya Zoom   juu ya  haki za makundi yaliyotengwa ikiwa ni pamoja na watu wenye Ulemavu, ushirikishwaji wa wanawake na vijana na wa...

UONGOZI WA SHEHIA WAAHIDI MASHIRIKIANO KWA WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA.  UONGOZI wa  Shehia ya Wawi wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba  umesema Utatoa mashirikiano  na wasaidizi wa Sheria   katika kutatua changamoto mbali mbali za jamii zikiwemo kero na udhalilishaji wa kijinsia   ambazo kwa muda mrefu zilikuwa zikikosa ufumbuzi na kukosa msaada  kutokana na kukosa  wasaidizi hao.   Aliyasema hayo Sheha wa Shehia ya Wawi Sharifa Ramadhan Abdalla Alipokuwa akifungua Mkutano Maalum wa kutoa Elimu  na Kujitambulisha kwa uongozi wa wa shehia hiyo  Msaidizi wa sheria Kutoka Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria Chake Chake Pemba.   Alisema  Chamgamoto mbali mbali ikiwemo kero  ambazo zinaendelea  zinajitokeza katika  vijiji vilivyomo ndani ya shehia hiyo  hukosa Msaada wa kisheria kutokana na kukosekana  ufumbuzi  na  kupelekea kuishia kienyeji bila kupatiwa ufumbuzi , hivyo ujio wa wasaidizi hao kutapelekea kupati...

Waziti Leila Anena haya kwa wasimamizi wa miradi

Image
NA FATMA SLEIMAN ABRAHMAN PEMBA.  WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali  Lela Mohamed Mussa amewataka watendaji wa Wizara ya Elimu kutobweteka kwa sifa Walizozipata kutokana na usimamizi wa miradi ya Maendeleo na badala yake wajiandae kusimamia kwa umakini zaidi utekelezaji wa miradi katika mwaka huu wa 2023. Waziri Lela ameyasema hayo katika kikao maalumu kilichowashirikisha watendaji wa Wizara ya Elimu, kilichofanyika katika Ukumbi wa Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu Chake Chake Pemba. Amesema Serika ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi imeweka kipaombele katika swala la Elimu na kuwekeza kiwango kikubwa cha fedha hivyo  imeitaka Wizara hio  kusimamia ujenzi wa madarasa zaid ya 2000 katika mwaka 2023. Aidha  amesema katika utekelezaji wa Miradi hiyo Wizara itatoa kipaombele katika sehemu ambazo watoto wanasoma katika mazingira magumu zaidi. Nae Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Nd. Khamis Abdullah Said ame...

TRA YATAKIWA KUFANYA HAYA NA BARAZA LA WAWAKILISHI.

Na Is Haka  Muhammed Pemba.  KAMATI ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi imetaka Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kuharakisha mpango wao mkakati wa kusaidia wafanyabiashara wa kisiwani Pemba kuweza kuingiza bidhaa zao moja kwa moja kisiwani Pemba ili kupunguza gharama za bei za bidhaa kisiwani hapa na kuwaondoshea mzigo mkubwa wananchi. Kauli ya Kamati hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Abdalla Hussein Kombo wakati ilipofanya ziara katika ofisi za TRA Mkoa wa Kikodi Pemba ikiwa katika kazi zake za kawaida za kamati za kufuatilia utekelezaji wa kazi za wizara ya fedha na taasisi zake. Amesema gharama za bidhaa mbali mbali ikiwemo chakula zimekuwa za juu sana kisiwani Pemba kutokana na wafanyabiashara kutoingiza moja kwa moja bidhaa hizo kisiwani hapa na hatimae mzigo wa gharama hizo kuwaelemea wananchi. Awali akiwasilisha   taarifa ya utekelezaji wa kazi za TRA Mkoa wa Kikodi Pemba Naibu Waziri (OR) Fedha na Mipango Zanzibar Ali Suleiman Ameir amesema kuwa ufinyu kat...

WADAU NA SERIKALI TUSHIKENI MIKONO KUTIMIZA MALENGO YETU

Image
Na AMINA AHMED MOH’D - PEMBA.  KIKUNDI   Cha Tupendane  Mkoa wa Kaskazini Pemba Wameiomba Serikali na pamoja na wadau Kuwasaidia kukamilisha ujenzi wa Eneo ambalo litakapokamilika  wataweza kulitumia  kwajili ya Shughuli wanazofanya za kimaendeleo na kuongeza  idadi ya uzalishaji wa bidhaa. Aliyasema  hayo katibu wa kikundi hicho Time Juma Said Alipokuwa akizungumza na habari hizi  huko katika ofisi za kikundi hicho  wilaya Micheweni  Shehia ya   Majenzi ambapo kwa sasa wanaendelea kufanya shughuli zao za Ususi na Ufumaji.  Alisema  kutokana  na wanakikundi  hao  asilimia 60 kuwa na ulemavu wa uoni Suala la   kukosa  ofisi hupeekea kusua sua kufanya shuhguli zao na wanapofanya hupelekea kubaki nazo nyumbani   jambo ambalo linarudisha nyuma  Juhudi zao za kutaka kujikomboa kiuchumi. "Tunaiomba Serikali wadau pia Watusaidie  kumalizia ujenzi  wa ofisi yetu sisi...

59 Ya Mapinduzi Neema zinaonekana

Image
NA FATMA SULEIMAN - PEMBA.  WAZIRI wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mh. Rahma Kassim Ali amewaagiza wapiganaji wa kikosi cha kuzuia magendo (KMKM) kuimarisha ulinzi wa usafirishaji wa magendo ya karafuu ili kudhibiti uchumi wa nchi. Waziri Rahma ametowa agizo hilo wakati akizungumza na wapiganaji wa kikosi cha KMKM, viongozi wa chama na serikali na wananchi wa shehia ya Gando, baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa kambi ya KMKM Gando akiwa katika muendelezo wa shamra shamra za kuadhimisha miaka 59 ya mapinduzi ya Zanzibar. Amesema lengo la kukombolewa kwa wazanzibar ni kuhakikisha wananchi wanafaidika na huduma za kijamii bila ya ubaguzi, ambapo kwa sasa serikali inategemea zao la karafuu kupata fedha za kigeni kutekeleza miradi ya kimaendeleo. Akitowa salamu za mkoa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh. Salama Mbarouk Khatib amewashukuru wananchi wa Gando kutowa ardhi yao kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika kambi hiyo. Akisoma taarifa ya kitaalamu ...

Wananchi Msipuuze Chukueni Tahadhari Ugonjwa Bado Upo.

Image
Na AMINA AHMED MOH’D- PEMBA  WANANACHI  wa Maeneo mbali mbali Kisiwani Pemba Wameshauriwa kuendelea Kuchukua Tahadhari dhidi ya Ugonjwa Wa Malaria   kwa kuendekea kulala jatika vyandarua vilivyotiwa dawa,   kufanya vipimo vya mara kwa mara juu ya Ugonjwa huo wanapofika Hospitali, Sambamba na kuacha kutymiandawa  bila mpangilio wanapobaini  dalili za Ugonjwa.  Ushauri huo umetolewa na  Muhamasishaji Kazi za  Malaria  Pemba Dk Yussuf Ali Juma Alipokuwa Akizungumza na  wananchi wa kisiwani Pemba kupitia Waandishi wa Habari wa Vyombo mbali mbali  katika Mkutano Maalum  wa kutoa tathimini ya  Ufuatailiaji na Mwenendo  wa Ugonjwa wa Malaria kwa Mwaka 2020 2022 Uliofanyika  katika Ukumbi wa Kitengo Cha Malaria  Wete Mkoa Wa Kaskazini Pemba. Amesema Baadhi ya Wananchi wamekuwa wakipuuza kulala katika Vyadarua  vilivyowekwa Dawa, Kupima na kuweza kujua hali za Afya zao Pamoja na kutumia Dawa bila ...

MIAKA 59 YA MAPINDUZI NEEMA KWA WAZALISHAJI WA ASALI PEMBA.

Image
Na AMINA AHMED MOH’D - Pemba  WIZARA ya  Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar  imesema  itaendelea kutoa Mashirikiano  na   kuhakikisha inalipatia Soko la uhakika ndani na Nje ya Nchi   Zao  la Asali  inayozalishwa Kisiwani Pemba Pamoja na bidhaa zinazochakatwa kutokana na Zao hilo.   Akizungumza  na Wananchi  mara baada ya kufungua  Kituo cha  Usarifu  wa Mazao ya  Asali   Huko Limanda Pujini Wilaya ya Chake Chake Mkoa Wa Kusini Pemba  Waziri  Wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban   Amesema kutokana na Ubora wa Asali  itakayozalishwa kisiwani Pemba   kuwa na ubora unaohitajika katika Soko la ndani na nje ya Nchi wizara hiyo itaitangaza Asali hiyo ili kupata Soko Zaidi na kuwakomboa wajasiriamali wanaozalisha Zao hilo..  "Kwa Sababu sisi ndio wenye Jukumu la kutafuta Masoko kwa bidhaa zinazozalishwa Nda...

Waziri wa Uchumi wa Buluu Zanzibar Aahidi Mazuri haya

Image
Na Fatma Suleiman - Pemba.  WAZIRI wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Suleiman Masoud Makame amesema, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaendelea kuwawekea mazingira mazuri wafanyakazi kwa kujenga Ofisi mbali mbali, ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao wa kazi. Ameyasema hayo wakati akifungua jengo la Ofisi ya Zimamoto na Uokozi (KZU) pamoja na uwekaji wa jiwe la msingi katika Ofisi ya KMKM Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, ikiwa ni katika shamra shamra za kuadhimisha miaka 59 ya Mapinduzi Zanzibar. Amesema kuwa, lengo la Serikali ni kuhakikisha inawawekea mazingira mazuri wafanyakazi wake, ili kuimarisha utendaji wa kazi na kuongeza ufanisi. Waziri huyo alieleza kuwa, kumalizika kwa majengo hayo anaamini kwamba kutaamsha ari kwa wafanyakazi katika kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa maslahi ya Taifa. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib amesema, Serikali imejipanga kuhakikisha inaimarisha maeneo ya kazi, ili wafanyekazi kwa moyo wa imani katika kuleta maende...

Mama Mariam Atoa neno kwa Wakulima wa Mwani Pemba

Image
FATMA SULEIMAN -PEMBA. Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambae ni Muasisi na Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha bora Foundation Mama Mariam  Mwinyi amewataka Wakulima wa zao la Mwani kuwashawishi vijana kujikita katika ukulima wa zao hilo ili kuweza kujikwamua na Umaskini . Alisema zaidi ya asilimia 90 ya wakulima wa mwani ni wanawake hivyo ,waitumie mbinu ya Umama ili kuwashawishi na kuwahamasisha Vijana kuweza kulima zao hilo ,kwani ni kilimo  chenye matokeo mazuri . Mama Mariyam aliyaeleza hayo huko Kisiwani Pemba wakati alipokua akikabidhi vifaa vya ukulima wa zao hilo kwa vikundi mbalimbali vya mkoa wa Kusini Pemba  ikiwa ni ziara maalum   ya kugawa vifaa  kwa wakulima wa Mwani, Pamoja na Watu wenye Mahitaji Maalum.  Mwenyekiti huyo wa taasisi ya Zanzibar maisha bora  aliwataka Wakulima hao kuvitunza vifaa walivyopewa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa. "Nawaomba Wakulima ambao leo mumepata vifaa h...

TAARIFA KUTOKA OIFISI YA MBUNGE JIMBO LA TUMBE ,,,,

Kwa niaba ya mhe mbunge wa jimbo la tumbe Amour Khamis Mbarouk ,  tunaw ashukuruni sana viongozi wa ccm na serakali na wananchi wote kiujumla kwa mashirikiano yenu na kututia moyo katika kazi zetu  Sisi ofisi ya mbunge tutaendelea kumshauri na kumuelekeza vyema mhe mbunge mambo yote muhimu ya chama na yale yakijamii ambayo niyakimaendeleo kuyatekeleza,, Sisi tutaendelea kupokea changamoto za wananchi kwa ajili ya kuzitatua , kushauri na kuzifatilia,,, Kwa kipekee kabisa tunazishukuru ofisi za chama na serekali zilizomo ndani ya mkoa wa kaskazini Pemba pamoja na watendaji wake wote kwa ushirikiano wa dhati kabisa tunao upata kutoka kwao,,, Dhamira na malengo yetu nikuboresha miundombinu ya chama na yakijamii kwa upande wa chama kuboresha ofisi zote za ccm ndani ya jimbo la tumbe na kuhakikisha tumeweka mazingira mazuri ya vitega uchumi vya ccm ili kuweza kujiendesha kwenye utendaji wake ,,, Tutafanya mambo mengi mazuri kwa mashauri ila pale tutakapo fanya mazuri na tukasahau ku...