WAANDISHI WA HABARI TAIFA LINAWASIKILIZA SANA TUMIENI FURSA HII KUSAIDIA MAKUNDI YALIOSAHAULIKA KATIKA KUSEMEA CHANGAMOTO ZAO ZIPATE UFUMBUZI.

NA  AMINA AHMED MOH’D - PEMBA

 "TUNGEPENDA  kuona kesi Za udhalilishaji kwanza Kila Mwaka zinapungua, hatutaki kabisa kudhalilishwa,wanawake, watoto na watu wenye Ulemavu ,Tuangalie ukuaji na Uwajibikaji  wa Vyombo vinavyosimamia Sheria, kwa sababu  Mwandishi wa Habari anaweza kufuatalia  mlolongo mzima wa kesi   mwanzo hadi mwisho na jamii ikaweza kuelewa, Bado kuna malalamiko katika masuala ya utolewaji wa hukumu baadhi ya watu wanakuwa huru  huku jamii ikijiuliza masuali yanayokosa majibu hivyo  waandishi tuyaone haya  katika kuandika  habari zetu".

 Ni kauli ya Mkurugenzi  Chama  Cha waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar Tamwa Dk Mzuri Issa Ali Alipokuwa Akifungua Mafuzo ya siku mbili kwa  Waandishi wa Habari wa vyombo mbali mbali Unguja na Pemba  kwa njia ya Zoom   juu ya  haki za makundi yaliyotengwa ikiwa ni pamoja na watu wenye Ulemavu, ushirikishwaji wa wanawake na vijana na wajibu wao wa kutetea mapitio au uanzishwaji wa sheria zinazohusiana na udhalilishaji wa kijinsia  na kushawishi utekelezaji wa sheria na sera  zinazoshughulikia mahitaji ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu Mapema leo  Asubuhi. 

Alisema kuwa waandishi ndio ambao wanauwezo Mkubwa wa kushawishi upatikanaji wa haki mbali mbali kupitia kalamu zao kuona  Tatizo la udhalilishaji haliongezeki Visiwani Zanzibar, pamoja na  kuzisemea ili ziweze  kupatiwa ufumbuzi Chanagamoto  za Makundi ya vijana wanwake na watu wenye ulemavu na kuweza kudai haki zao kwa lengo la kuondokana na Udhalilishaji.
   Dk Mzuri Issa Ali - Mkurugenzi Tamwa Zanzibar 

Akizungumza  na waandishi kwa upande wa kisiwani Pemba mratibu wa chama hicho Fat-hiya Mussa Said Amesema  lengo La Mafunzo hayo ni kufanyia kazi changamoto mbali mbali ziakazoibuliwa na kuzifanyia uchechemuzi  na kuona kunakuwa na Sheria moja ya udhalilishaji au kuona marekwbisho katika sheria zilizopo, pamoja na kuhamaisha utekelezwaji wa Sheria,  Ushiriki na ushirikishwaji wa wanawake, vijana pamoja na watu wenye ulemavu katika kupata fursa sawa za kimaendeleo.
 
   Fat- hiya Mussa Said- Mratibu Tamwa Pemba. 

 Mkutano huo Ulioandaliwa na Tamwa Zanzibar kwa waandishi wa habari Unguja na Pemba Ni katika utekelezaji wa mradi wa Kuhamasisha Hatua za Kitaifa dhidi ya Vitendo vya udhalilishaji Zanzibar unaotekelezwa na Tamwa Zanzibar kwa kushirikiana na Foundation for Civil Society  ambapo katika mkutano huo Mada mbali mbali  ziliwasilishwa  zilizohusu masuala  yanayigusa makundi hayo. 
 
Mwisho 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI