Wananchi Msipuuze Chukueni Tahadhari Ugonjwa Bado Upo.

Na AMINA AHMED MOH’D- PEMBA


 WANANACHI  wa Maeneo mbali mbali Kisiwani Pemba Wameshauriwa kuendelea Kuchukua Tahadhari dhidi ya Ugonjwa Wa Malaria   kwa kuendekea kulala jatika vyandarua vilivyotiwa dawa,   kufanya vipimo vya mara kwa mara juu ya Ugonjwa huo wanapofika Hospitali, Sambamba na kuacha kutymiandawa  bila mpangilio wanapobaini  dalili za Ugonjwa.

 Ushauri huo umetolewa na  Muhamasishaji Kazi za  Malaria  Pemba Dk Yussuf Ali Juma Alipokuwa Akizungumza na  wananchi wa kisiwani Pemba kupitia Waandishi wa Habari wa Vyombo mbali mbali  katika Mkutano Maalum  wa kutoa tathimini ya  Ufuatailiaji na Mwenendo  wa Ugonjwa wa Malaria kwa Mwaka 2020 2022 Uliofanyika  katika Ukumbi wa Kitengo Cha Malaria  Wete Mkoa Wa Kaskazini Pemba.

Amesema Baadhi ya Wananchi wamekuwa wakipuuza kulala katika Vyadarua  vilivyowekwa Dawa, Kupima na kuweza kujua hali za Afya zao Pamoja na kutumia Dawa bila Mpangilio  wanapobaini Dalili za Ugonjwa wa Malaria jambo ambalo Linapelekea kuwepo kwa kesi za Malaria katika Baadhi ya Maeneo kisiwani Pemba.

 "Ugonjwa Wa Malaria Bado Upo  Kupitia Vyombo vya habari Niwaase Wananchi Maeneo Mbali mbali Kuchukua Tahadhari kwanza kulala katika vyandarua vilivyotiwa Dawa,wasivifungie kwenye Makabati tu, Kupima Afya zao wanapofika katika hospitali na vituo vya Afya na waache kutumia dawa kiholela mtu anapobaini ana dalili za Malaria  asinunue tu Dawa bila kuoata maelekezo ya Dakatari Licha Ya Asilimia  iliyopo lakini Bado Ugonjwa  Haujamaliza.
 
Aidha  Yussuf Amesema kitengo cha Malaria Pemba kinaendelea  na Mapambano dhidi ya kumaliza Ugonjwa huo kwa kufanya  uchungzi Wa Mbu wa Malaria kupitia mitego maalum , pamoja na kuendelea kutoa Vyandarua kwa Mama wajawazito, watoto,na Makundi mengine lengo ni kuweza kuwakinga Na Ugonjwa Huo .

"Mikakati yetu ni kumaliza Malaria 2023 tunawafikia Wagonjwa, kitengo kinafanya Uchunguzi kwa kubaka Mbu na kuwafanyia uchunguzi ili kuweza kujua bado wapo Mbu wanaosababisha Malaria lakini pia tunaendelea na huu mpango endelevu wa kutoa vyandarua vyenye dawa Kwa Mama wajawazito na watoto ili kuona wanaendelea kuchukua Tahadhari. 
   YUSSUF ALI JUMA - MHAMASISHAJI KAZI ZA                             MALARIA  PEMBA 
 
 Akizungumza Katika Mkutanao huo Afisa Ufuatiliaji wa Wagonjwa wa Malaria Pemba Said  Massoud Mbarouk Amewataka waandishi kufikisha ujumbe kwa jamii ili iweze kuchukua Tahadhari juu ya Ugonjwa huu kwani kwa sasa wananchi waliowengi  wamepunguza kasi katika kuendeleza Mapambano haya ya Kudhibiti na kumaliza  Malaria Zanzibar. 
            SAID MASSOUD MBAROUK - AFISA UFUATILIAJI                                      WAGONJWA MALARIA PEMBA
Kwa Upande wake  Afisa Uchunguzi Ugonjwa wa Malaria Pemba Bimkubwa  Khamis Kombo Amesema  kitengo hicho cha Malaria kitaendelea kutoa Huduma kwa Wananchi Katika Maeneno Mbali mbali kwa Kupima na kuchunguza Wagonjwa wanaofika katika hospitali na vituo vya Afya sabamba na kufuatilia wagonjwa nyumba hadi nyumba,watakaobainika kuwa na dalili za Ugonjwa huo. 

 Aidha kwa Upande wake Fatma Khamis Haji Mhamasishaji Kutoka kitengo Cha Malaria Pemba Amesema kuwa Huduma za upimaji wa malaria zinatolewa bure  Hivyo ni vyema wananchi kuendelea kuitumia fursa hiyo kufanya vipimo na watakapobainika kuanza kutumia tiba ya Malaria.
 
Mkutano huo wa siku Moja  umeandaliwa na ZAMEK kwa waandishi wa Habari ulikiwa na lengo la kueleza mikakati iliyofikiwa katika kuendeleza na  Kupambana na Ugonjwa Wa Malaria Pemba. 
Mwisho
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI