UONGOZI WA SHEHIA WAAHIDI MASHIRIKIANO KWA WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA.

NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 

UONGOZI wa  Shehia ya Wawi wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba  umesema Utatoa mashirikiano  na wasaidizi wa Sheria   katika kutatua changamoto mbali mbali za jamii zikiwemo kero na udhalilishaji wa kijinsia   ambazo kwa muda mrefu zilikuwa zikikosa ufumbuzi na kukosa msaada  kutokana na kukosa  wasaidizi hao. 

 Aliyasema hayo Sheha wa Shehia ya Wawi Sharifa Ramadhan Abdalla Alipokuwa akifungua Mkutano Maalum wa kutoa Elimu  na Kujitambulisha kwa uongozi wa wa shehia hiyo  Msaidizi wa sheria Kutoka Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria Chake Chake Pemba. 

 Alisema  Chamgamoto mbali mbali ikiwemo kero  ambazo zinaendelea  zinajitokeza katika  vijiji vilivyomo ndani ya shehia hiyo  hukosa Msaada wa kisheria kutokana na kukosekana  ufumbuzi  na  kupelekea kuishia kienyeji bila kupatiwa ufumbuzi , hivyo ujio wa wasaidizi hao kutapelekea kupatikana suluhu ya Matukio mbali mbali yanayojitokeza. 

 "Ujio huu wa Msaidizi wa sheria  Katika Shehia hii utakuwa msaada mkubwa kwa wananchi  katika kutatua baadhi ya kesi kwani zipo kesi mbali mbali ambazo huishia kienyeji ni kutokana na kukosa msaada wa kisheria   naahidi tutashirikiana katika suala hili na kufanya kazi kwa pamoja katika kuondoa kero za jamii.  

Akizungumza katika Mkutano huo Afisa kutoka  jumuia ya wasaidizi wa sheria Chake Chake ambae  ni msaidizi mpya wa sheria katika shehia ya Wawi Haji Nassor Muhamed  Alisema kuwa  Kwa kushirikiana na Uongozi wa shehia  Msaada wa kisheria utawafikia  wananchi katika mawneo mbali mbali  kwa kuandaa vikao na kutia elimu juu ya mambo mbali mbali  . 

Aidha Afisa huyo alisema kuwa ataendelea kusimamia  vyema  na kufuatilia masuala hayo ya usaidizi wa kisheria  ili kuona haki zinapatikana  kwa mujibu wa  sheria. 
 
 Nao baadhi ya washiriki wa Mkutano huo  akiwemo Mjumbe wa sheha wa shehia hiyo  katika kijiji cha  Wawi Mtemani  Nassor  Rashid aliwataka wananchi Wa Wawi kutodharau  Viongozi wa Shehia wanapofikwa na changamoto mbali mbali  na kukimbilia vyombo vikubwa kabla kupitia katika uongozi  wa shehia ili kuepusha Mivutano isiyoya lazima. 


Katika Mkutano huo Elimu ya msaada wa kisheria juu  ya Mambo ya udhalilishaji, Haki za mtoto, Rushwa Muhali, Namna ya kutoa ushahidi, pamoja na Masuali mbali mbali ambayo yaliolizwa na washiriki qa Mkutano huo  yalitolewa ufafanuzi na Afisa huyo kutoka jumuia ya wasaidizi wa Sheria.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI