WAANDISHI ANDIKENI MAZURI YANAYOFANYWA NA WANAWAKE KATIKA JAMII NA TAIFA YAPO MENGI YA MFANO.



 NA AMINA AHMED MOH’D- PEMBA. 

WAANDISHI wa habari Zanzibar  wameaswa kuwaibua na kuwandika Vizuri  wanawake wanaoendelea kufanya mambo Mazuri ya kuleta Maendeleo   katika jamii na Taifa katika nyanja  mbali mbali ili  kutoa wigo kwa wanawake wengine na  kusaidia kuongeza idadi ya viongozi wanawake ambao wataaminika katika Jamii. 
           DK  MZURI ISSA ALI -  MKURUGENZI TAMWA-ZNZ 
 
Ametoa ushauri huo Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar Dkt, Mzuri Issa Ali  alipokua akizungumza   waandishi wa habari vijana wa vyombo mbali mbali kutoka Unguja na Pemba ambao wanaendelea kupatiwa Mafunzo maalumu ya  kujengewa uwezo juu ya kuripoti habari za wanawake kushika nafasi za uongozi  katika nyanja mbali mbali sambamba na kuchochea uwajibikaji kwa maslahi ya jamii. 

Alisema kwa muda mrefu wanawake wengi wamekua wakishindwa kufikia malengo ya kushika nafasi za uongozi katika ngazi mbalimbali kutokana na kuandikwa vibaya na baadhi ya waandishi na kupelekea kujengeka  dhana Potofu  ya kwanaume Pekee ndio wanapaswa kuwa viongozi jambo ambalo ni kinyume na Mikataba yote ya kikanda na kimataifa.

‘’Nyinyi waandishi wa habari vijana muna nafasi kubwa kuibadili hali hii, sauti zenu ni kubwa zaidi ambazo mkizitumia vizuri tunaweza kufika tunapopataka  yapo mazuri tele yaliofanywa na yanayoendelea kufanywa na wanawake ambayo ni mifano ya kuigwa ’ ’alisema.

Akitoa uzoefu wa  kusaidia jamii   kupitia kazi ya uandishi wa habari   Fatma Alloo  ambae ni moja kati ya waanzishi  wa  chama cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania kuwa na  Mashirikiano  na watu mbali mbali ili kujenga  uhusiano mwema  katika utendajibkazi za kihabari. 

Aidha Aliwataka wanahabari hao kujiwekea malengo pamoja na kuwa watu wenye misimamo pale wanapoamua kutafuta jambo kwa maslahi ya wanawake na umma kwa ujumla.

Akitoa ushuhuda Mwenyekiti wa Jumuia ya kupambana na changamoto zinazowakabili wajane Zanzibar (ZAWIO) Tabia Makame alisema wanawake wanaotaka kuwa viongozi wana wajibu wa kujitambua na sio kuwa warahisi kwa kila jambo.

Alisema kuna idadi kubwa ya wanawake wanaoshindwa kufikia malengo yao kwa sababu wanashindwa  kujielewa  na kwa hali hiyo wanajikuta wanaingia kwenye mgongano na wasiopenda kuona wanawake wakipiga hatua zaidi za kimaendeleo.

‘’ Lazima tukubali ukweli udhalilishaji kwenye sehemu za kazi upo lakini ni wachache wanaoweza kukubali kuacha kazi kwa kulinda heshima yao hivyo ni lazima nyinyi vijana wadogo mjitambue’’aliongezea.

Akitoa ushuhuda mwengine Makamu wa Rais mstaafu kutoka Chuo cha Kikuu cha Zanzibar (ZU) na Waziri wa fedha Bunge la vijana Tanzania Zainab Salum Saleh alisema  wanawake wanaweza  kufikia malengo yao iwapo watajitoa katika kila jambo.


Pamoja na changamoto ambazo wanawake wanapitia  wanapoonesha dhamira yao ya kuwa viongozi lakini  kwa pamoja hawapaswi kukata tamaa na changamoto hizo badala yake wazione kama fursa za kusonga mbele.

Sambamba na hayo aliwataka vijana wenzake wanaotaka kuwa viongozi kukimbia kabisa viashiria vya rushwa pindi wanapoviona kwa sababu kuchukua sehemu hiyo ni kujiharibu pia kuikandamiza jamii yako na kufanya jambo hilo liendelee.

Jumla ya waandishi wa habari vijana 18 kutoka Unguja na Pemba wanaendelea kujengewa uwezo kupitia mradi unaotekelezwa na TAMWA-ZNZ kwa kushirikiana na shirika la “National Endowment for Democracy – NED”. 

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI