MIAKA 59 YA MAPINDUZI NEEMA KWA WAZALISHAJI WA ASALI PEMBA.
Na AMINA AHMED MOH’D - Pemba
WIZARA ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar imesema itaendelea kutoa Mashirikiano na kuhakikisha inalipatia Soko la uhakika ndani na Nje ya Nchi Zao la Asali inayozalishwa Kisiwani Pemba Pamoja na bidhaa zinazochakatwa kutokana na Zao hilo.
Akizungumza na Wananchi mara baada ya kufungua Kituo cha Usarifu wa Mazao ya Asali Huko Limanda Pujini Wilaya ya Chake Chake Mkoa Wa Kusini Pemba Waziri Wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban Amesema kutokana na Ubora wa Asali itakayozalishwa kisiwani Pemba kuwa na ubora unaohitajika katika Soko la ndani na nje ya Nchi wizara hiyo itaitangaza Asali hiyo ili kupata Soko Zaidi na kuwakomboa wajasiriamali wanaozalisha Zao hilo..
Akizungumza na Wananchi mara baada ya kufungua Kituo cha Usarifu wa Mazao ya Asali Huko Limanda Pujini Wilaya ya Chake Chake Mkoa Wa Kusini Pemba Waziri Wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban Amesema kutokana na Ubora wa Asali itakayozalishwa kisiwani Pemba kuwa na ubora unaohitajika katika Soko la ndani na nje ya Nchi wizara hiyo itaitangaza Asali hiyo ili kupata Soko Zaidi na kuwakomboa wajasiriamali wanaozalisha Zao hilo..
"Kwa Sababu sisi ndio wenye Jukumu la kutafuta Masoko kwa bidhaa zinazozalishwa Ndani ya nchi na kuzitangaza huko Duniani tutatoa kila uahirikiano kuhakikisha kwamba Dunia inatambua ubora na uhalisia wa Asali inayizalishwa Zanzibar Hapa Pujini."
"Miundo mbinu Imara iliyowekwa katika kituo hichi nilichokifungua rasmi Leo ndui inayohitajika katika Soko la dunia kwa ubora wa uaandaaji mpka kukamilika kwake Naahidi kwenu wajasiriamali wa Zao la Asali kulisimamia hili Suala la utafutaji wa soko nje ya Nchi kwajili ya bidhaa ya kuuza bidhaa zenu."Alisema.
Aidha Waziri Omar Amewataka Wajasirimali wa Mazao ya Asali kutoa Mashirikiano katika kukitumia kituo hicho katika kuuza na kupata Mafunzo ya Usarifu Bidhaa zitokanazo na Zao hilo , na Uzalishaji wa Nyuki, ili zifikie katika kiwango kinachohitajika katika ushindani wa Soko.
"Serikali Ya Mapinduzi ya Zanzibar imelipa Umuhimu Zao la Asali, Niwaombe Ndugu zangu Wajasiriamali mkitumie kituo hichi Kuuza bidhaa Zenu, kupata mafunzo ya kusarifu na kuzalisha Asali kwa mbinu za kisasa, lakini pia toeni Mashirikiano katika kuona kituo hichi kinakuwa endelevu katika kuzalisha Asali Bora yenye kiwango.
Akizungumza Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwekezaji Maryam Juma Sadala Alisema lengo l kujengwa kituo hicho Kisiwani Pemba ni kuwasaidia Wajasiriamali Kupata kituo maalum cha kuuza Asali yao Baada ya Mavuno pamoja na kupata Elimu ya usarifu wa Bidhaa mbali mbali zinazotokana na zao la Asali,na Uzalishaji wa Nyuki kwa Njia za kisasa.
Aidha Katibu huyo Amewashukuru Wananchi wa Kijiji cha Pujini na Wajasiriamali kwa Mashirikiano waliyatoa katika Kufanikisha ujenzi wa Kituo Hicho ambapo amewataka kuwa walinzi katika kutimiza Maelengo yaliokusudiwa.
Kwa upande wake Mkuu Wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud Ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Kwa kuyafanyia kazi Maoni yaliotolewa na wajasiriamali wa Mazao ya Asali kuwajengea kituo hicho ambapo Alisema kitasaidia kuitambulisha Asali inayozalishwa Kisiwani Pemba pamoja na kupata soko la uhakika.
Akitoa Shukurani kwa Niaba ya Wajasirimali wa Mazao ya Asali na Wafuga Nyuki Pemba Nassor Suleiman Nassor wamesema kuzinduliwa kwa kituo hicho ni chachu ya Maendeleo na Hazina itakayisaidia kukuza Mazao hayo.
"Tunamshukuru sana Rais wa Zanzibar kwa kutusaidia kupata kituo hichi kwetu ni furaha sana kutasaidia kuongeza uzalishaji wa Asali na Mazao yatokanayo na Mazao hayo.
Aidha wafanya Biashara hao waemuomba Waziri huyo kuwafukisha kilio chao kupatiwa vifaa na vitendea kazi bure kwa hatua ya awali kutokana na hali Ngumu ya kiuchumi iliyopo kwa wafuga nyuki kisiwani Pemba.
Ufunguzi wa Kituo ni Shamra Shamra Za kuelekea kutimia kwa Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambapo kituo hicho cha Usarifu wa Mazao ya Asali Pujini Limanda Wilaya ya Chake Chake Kimegharimu jumla ya Shilingi Milioni mia sita na Arobaini na moja na Themanini na tano hadi kukamilikaika ikiwa ni pamoja na ujenzi ununuzi uwekeji wa vifaa, ununuzi wa Piki piki, pamoja na ununuzi wa vitendea kazi, ambapo kitatumika kwajili ya kutoa mafunzo, kuuzabidhaa zitokanazo na Mazao hayo, kuchakata pamoja na kuto Elimu juu ya ufugaji wa Nyuki kwa Wajasirimali kikiwa Chini ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais kazi Uchumi na Uwekezaji ambapo ujenzi wa kituo hicho ulianza Mnamo Mwezi 3/ mwaka 2022 Na kuzinduliwa Rasmi leo.
Mwisho
Comments
Post a Comment