WADAU NA SERIKALI TUSHIKENI MIKONO KUTIMIZA MALENGO YETU

Na AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 

KIKUNDI   Cha Tupendane  Mkoa wa Kaskazini Pemba Wameiomba Serikali na pamoja na wadau Kuwasaidia kukamilisha ujenzi wa Eneo ambalo litakapokamilika  wataweza kulitumia  kwajili ya Shughuli wanazofanya za kimaendeleo na kuongeza  idadi ya uzalishaji wa bidhaa.

Aliyasema  hayo katibu wa kikundi hicho Time Juma Said Alipokuwa akizungumza na habari hizi  huko katika ofisi za kikundi hicho  wilaya Micheweni  Shehia ya   Majenzi ambapo kwa sasa wanaendelea kufanya shughuli zao za Ususi na Ufumaji. 

Alisema  kutokana  na wanakikundi  hao  asilimia 60 kuwa na ulemavu wa uoni Suala la   kukosa  ofisi hupeekea kusua sua kufanya shuhguli zao na wanapofanya hupelekea kubaki nazo nyumbani   jambo ambalo linarudisha nyuma  Juhudi zao za kutaka kujikomboa kiuchumi.

"Tunaiomba Serikali wadau pia Watusaidie  kumalizia ujenzi  wa ofisi yetu sisi wanakikundi cha tupendane  ni Wajasiriamali ambao tumeamua kujikomboa kuondoshea mzigo wa utegemezi Serikali, Kwa kufanya shuguhli za kujipatia maendeleo lakini Changamoto  kubwa kwa sasa imekuwa ni ofisi inayotambulika. 

Aidha Katibu huyo Amesema   kwa sasa tayari  Ujenzi huo umefika katika hatua kubwa ambapo wamepata baadhi ya vifaa ambavyo vitasaidia kusegeza mbele ujenzi huo lakini kutokana na  kukosa uwezo wamelazimika vifaa hivyo kuviwka ndani ili kusubiri msaada kutoka kwa  wahisani pamoja na Serikali. 

"Nikiwa kama Katibu nimejitahidi kuomba Msaada juu ya hili nashirikiana na Wenzangu  kila pahali  kuona kwamba   Tunapata Ofisi yetu lakini bado hatujafanikiwa kumaliza licha ya kupata msaada  wa baadhi ya vitu   tunaomba Serikali izidi kutusaidia, Serikali izidi kutuangalia bado hatujafikia malengo tuliojiwekea kama wajasirimali wenye ulemavu changamoto ni ofisi. 


Miongoni  Mwa wanankikundi hicho Ambae ni mwenye Ulemavu wa Macho Mpeta Seif   Alisema kuwa kutokana na kukosa Jengo la uhakika hulazimika kusitiaha Shuguhli zao za ufumaji wa Mashuka  ambayo kwa Asilimia kubwa yamekuwa yakiwapatia faida   kuliko bidhaa nyengine wanazozalisha. 

"Eneo tulilopo  kwa sasa sio letu  tumejiweka tu kwa mtu  tunafanya shughuli  zaidi hizi za ususi tu kwa sababu ni enwo finyu ambalo charahani zetu haziwezi kukaa  kwaio zinaharibika malengo hayafikiwi ya kujikomboa. 

Akizungumiza Juu ya sula hilo Afisa  Kutoka Baraza la  watu wenye Ulemavu wilaya ya Micheweni Ali Hassan Ali  Alisema kuwa Baraza hilo kwa kushirikian na  taasisi mbali mbali litaendelea kushighulikia  suala hilo ili kuona linapata ufumbuzi na kuwasaidia kuondokana na chagamoto hiyo. 

Kikindi hicho cha Tupendane kina jumla ya wanachama 11 Ambao Sita kati ya hao ni wanawake weye ulemavu wa Macho   Ambapo kutokana na kukosa ofisi rasmi  kunapelekea kurudisha nyuma harakati zao wanazofanya za ususi   na Ushoni wa Mashuka ambayo hutumia bidhaa hizo kwa ajili ya kujiendeleza kimaisha. 

Mwisho. 






  

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI