Posts

Showing posts from November, 2022

Taasisi Zapaza sauti kuelekea sikiu 16 za kupinga udhalilishaji.

Image
Na Amina Ahmed Moh’d.  TAASISI  zinazoshughulika na kupinga vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto kisiwani pemba  zimeiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuimarisha vyema mfumo wa upatikanaji wa takwimu  za matukio ya udhalilishaji  wa kijinsia ili kuonesha jamii   maendeleo yaliofikiwa  katika mapambano dhidi ya vitendo hivyo.  Akizungumza  katika Mkutano maalum na waandishi wa habari  wa vyombo mbai mbali uliofanyika  katika ofisi za Tamwa  Mkanjuni Chake Chake Pemba  Mwenyekiti wa  asasi za kiraia zinazoshughulika na Mambo ya udhalilishji Nassor Bilal Ali alisema kuimarika kwa mifumo  hiyo kutaweza kuonesha  jitihada zinazochukuliwa na serikali pamoja na Asasi hizo katika mapambano   hayo ya kupinga vitendo hivyo.  Aidha  Wanaasasi hao waliwataka waandishi wa habari Kuzidisha mashirikiano katika kutoa taarifa za ufuatiliaji na uendeshwaji wa...

UHABA WA VITUO VYA POLISI WILAYA YA CHAKE CHAKE BADO MLIMA MREFU KUDHIBITI UHALIFU VITENDO VYA UDHALILISHAJI NA UVUNJIFU WA HAKI ZA BINAADAMU.

Image
NA  AMINA AHMED MOH’D - PEMBA  CHAKE Chake ni moja kati ya  wilaya mbilizi zinazopatikana katika  Mkoa wa Kusini Pemba  Zanzibar Tanzania.  Ambayo kwa mujibu wa sensa ya  mwaka 2012  ina idadi ya wakaazi 97,249 na anuani za makazi zikiwa ni   7420   Idadi Mpya  ya wakaazi wa Chake Chake   kwa takwimu za Sensa  ya watu na makazi  ya mwaka 2022 iliyotolewa hivi karibuni  bado hazijapokelewa katika ngazi za  wilaya   ni kutokana na takwimu hizo kuikiishia  katika ngazi za Mikoa pekee jambo ambalo limewia ugumu kupatikana  idadi mpya  ya wakazi wake wa sasa.     Chake Chake ina jumla ya shehia 32 ambazo wakaazi  wake hulazimika  kutumia kituo kimoja pekee  cha polisi  katika kuripoti  matukio mbali mbali.  Matukio hayo ni pamoja uhalifu, udhalilishaji wa kijinsia wazee wanawake na watoto, wizi wa mazao , mifugo,  Pamoja na Ajali...

SOKO LA OLE LA ZINDULIWA

Image
Na Fatma Suleiman.  MWAKILISHI wa jimbo la Ole Masoud  Ali Muhammed amewataka wafanya biashara wa jimbo la ole kulitumia ipasavyo soko la mboga mboga  lililopo olee kianga  bila ya kuingiza  itikadi za kisiasa ili kuendelea kujipatia rizki za halali . Akizungumza na wana jimbo  mara baada ya uzinduzi wa soko hilo mh Massoud ambae ni waziri wanchi Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ amesema soko hilo amelijenga kwa ajili ya wanachi wote na sio la mtu binafsi hivyo ni vyema litumike kama lilivyo kusudiwa. Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya chake chake Abdala Rashid Ali amewataka wanachi wa ole kuthamini jitihada za viongozi wao pamoja na kulitunza ili liweze kutumika kwa muda mrefu . Akitoa maelezo juu ya matumizi ya soko  msimamizi wa ujenzi wa mradi huo Thabit Othman Abdalla  amesema soko hilo litatumika na wauzaji zaidi ya 20 ambapo  watauza biashara zao katika mazingira rafi...

Mkutano Maalum

Image
 HABARI NA TAMWA ZANZIBAR.  Leo November 22 TAMWA-ZNZ Kwa kushirikiana na wadau wengine Shirika la SHIJUWAZA pamoja  Shirila linalojihusisha maswala ya watu wenye ulemavu Norway (NAD) wameanza mafunzo ya siku nne kwa baadhi ya maafisa wa taasisi hizo kwa hatua ya mwisho kabla ya kuanza kutekelezwa kwa mradi mpya utakaofanyika katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba, kuwawezesha watu wenye ulemavu kutambua haki zao za kiuchumi pamoja na kuongeza ushiriki na ushirikishwaji wao katika shughuli za kiuchumi kwa lengo la kuwaongezea kipato, kupunguza umasikini na kuondokana na utegemezi.(Kijaluba iSAVE Project)

UHABA WA VITUO VYA POLISI WILAYA YA CHAKE CHAKE BADO MLIMA MREFU KUDHIBITI UHALIFU VITENDO VYA UDHALILISHAJI NA UVUNJIFU WA HAKI ZA BINAADAMU.

Image
NA  AMINA AHMED MOH’D - PEMBA  CHAKE Chake ni moja kati ya  wilaya mbilizi zinazopatikana katika  Mkoa wa Kusini Pemba  Zanzibar Tanzania.  Ambayo kwa mujibu wa sensa ya  mwaka 2012  ina idadi ya wakaazi 97,249 na anuani za makazi zikiwa ni   74200     Idadi Mpya  ya wakaazi wa Chake Chake   kwa takwimu za Sensa  ya watu na makazi  ya mwaka 2022 iliyotolewa hivi karibuni  bado hazijapokelewa katika ngazi za  wilaya   ni kutokana na takwimu hizo kuikiishia  katika ngazi za Mikoa pekee jambo ambalo limewia ugumu kupatikana  idadi mpya  ya wakazi wake wa sasa.     Chake Chake ina jumla ya shehia 32 ambazo wakaazi  wake hulazimika  kutumia kituo kimoja pekee  cha polisi  katika kuripoti  matukio mbali mbali.  Matukio hayo ni pamoja uhalifu, udhalilishaji wa kijinsia wazee wanawake na watoto, wizi wa mazao , mifu...

KAMISHNA ZANZIBAR ATOA ANGALIZO MWENYEWE KWA MADEREVA BODA BODA

NA OMAR HASSAN      KAMISHNA wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad amesema Jeshi la Polisi litawashughulikia kwa mujibu wa sheria madereva wa bodaboda wanaokiuka sheria na taratibu zilizowekwa ikiwa ni pamoja na kutojisajili kwenye vyama na Jumuiya za waendesha bodaboda.                                                                                                                CP Hamad ametoa kauli hiyo huko Paje Mkoa wa Kusini Unguja alipokua akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Paje, Bwejuu na Michamvi katika mkutano wa kusikiliza kero za wananchi zinazojitokeza katika maeneo yao.  Amesema kutofuata sheria na kutojisajili kwa waendesha bodaboda wengi kunachangia kujihusisha na vitendo v...

MASAUNI AZUNGUMZA HAYA NA WANANCHI

Image
NA OMAR HASSAN – UNGUJA                                                     WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi Mhe. Hamad Yussuf Masauni amewataka Maafisa wa Jeshi la Polisi Kamisheni ya Zanzibar kuongeza nguvu katika kuzuia na kupambana na uhalifu ili Zanzibar iendelee kuwa salama kwa wananchi na wageni. Akizungumza na Maafisa wa Jeshi hilo huko Makao Makuu ya Polisi Zanzibar amesema pamoja na kuwa takwimu zinaonesha  kupungua kwa baadhi ya Makosa ya jinai bado zipo changamoto za kiuhalifu ambazo zinawasumbua wananchi  Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad ameeleza kuwa uchache na uchakafu wa magari pamoja na uchache wa Askari ni miongoni mwa changamoto zinazokwamisha utendaji wa Jeshi hilo. Akitoa taarifa ya Uhalifu wa Makosa ya jinai kwa kipindi cha miezi tisa mwaka 2022 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mw...

Wakandarasi Miradi ya Elimu Pemba wapewa Neno

Image
NA FATMA SULEIMAN-PEMBA  KATIBU  mkuu wizara ya Elimu na mafunzo ya amali Zanzibar  Khamis Abdalah Said amewataka wasimamizi  wakuu wa   ujenzi  wa miradi ya Elimu kusimamia na kutekeleza kwa wakati ujenzi wa  skuli na madarasa mbali mbali    Ili kutimiza lengo la Serekali la kuimarisha Majengo  Ili kutoa eElimu bora  kwa wanafunzi .   Said Ameyasema hayo kwa  nyakati  tofauti katika ziara ya ya siku Moja ya kutembea miradi ya elimu inayoendelea kujengewa kisiwani Pemba. Amesema ni vyema  wakandarasi kuongeza Kasi ya utendaji kazi kwa  wafanya kazi wao ili waweze  kukabidhi miradi hiyo kwa wakati husika ikiwa imekamilika na kwa ubora uliotarajiwa. Katika hatua nyengine Katibu Mkuu amewataka walimu kutoa ushirikiano wa dhati katika kueka msingi nzuri kwa wanafunzi utakaowezesha kupata Viongozi Bora wa baadae. Kwa upande wao wakandarasi wa miradi hiyo wameelezea baadhi ya changamoto zina...

Suluhu ya Wadudu Nzi wanaothiri mazao hii hapa kutoka wizara ya kilimo.

Image
Fatma Suleiman.  Wizara ya kilimo maliasili mifugo na uvuvi imedhamiria kuondoa kabisa changamoto ya wadudu Nzi wa matunda kwa wakulima Ili waweze kujiingizia kipato kulingana na ukulima wao na kuondokana na umaskini . Akizungumza mara baada ya zoezi la ugawaji wa dawa hizo kwa wakulima   Kaimu Afisa msaidizi wa mradi wa udhibiti wa wadudu Nzi waharibifu wa matunda Pemba Fatma Nassor Sharif amesema   wizara inategemea kugawa mitego hiyo katika shehi ya zote za Pemba mara tu vitakapofika vifaa vyengine Ili kuondoa kabisa tatizo Hilo . "Kutokana na Hawa nzi waharibifu wamekua wengi na wanaathiri matunda hivyo serekali kupitia wizara imeamua ni kuwaondoa kabisa na ndio tukaamua kutoa dawa hii kwa shehia zote kisiwani Pemba Ili kuwanusuru wakulima kujikwamua kiuchumi .alisema Fatma " Sheha wa shehia ya ole shida khamis Othman  amewanasihi wakulima wa matunda uongeza umakini pamoja  kuzitumia dawa hizo ipasavyo Ili kutimiza lengo la serekali la ...

MIKAKATI YA KUDHIBITI UTORO YAZAA MATUNDA.

Image
HII HAPA MIKAKATI YA UFAULU NA KUDHIBITI UTORO SKULI ZA MSINGI MICHEWENI Na Amina Ahmed Mohamed MIKAKATI iliyobuniwa na uongozi wa wilaya ya Micheweni kudhibiti utoro skuli za msingi wilaya ya Micheweni imewezesha wilaya hiyo kuongoza kitaifa kwa ufaulu kwa miaka minne mfululizo . Mkuu wa wilaya ya Michewemi Mgeni Khatib Yahya amesema mikakati hiyo ni pamoja na   kupiga marufuku ajira za watoto maeneo yote na wananchi katika shehiza zote kwenye wilaya hiyo wameelimishwa kuzingatia umuhimu wa elimu na malezi bora, Kadhalika wilaya ya Micheweni imeunda kamati maalum katika kila shehia kufuatilia suala la suala la utoro skuli na imepepiga marufuku watoto wa skuli kushiriki dufu la usiku na kuzunguka hovyo usiku kuangalia televisheni. Tatizo la dufu linathibitishwa na mkazi wa shehia ya Majenzi Hassan Omar ambaye anasema "zamani watoto walikuwa wanachelewa kulala wanazifuata ngoma popote zinapopigwa hawakataziki lakini aliekuwa mkuu wa ...

Wizara ya kilimo yahidi neema wadudu wanaothiti mazao.

NA  FATMA SLEIMAN.  WIZARA ya kilimo maliasili mifugo na uvuvi imedhamiria kuondoa changamoto ya wadudu Nzi wa matunda kwa wakulima Ili waweze kujiingizia kipato kulingana na ukulima wao na kuondokana na umaskini . Akizungumza mara baada ya zoezi la ugawaji wa dawa hizo kwa wakulima   Kaimu Afisa msaidizi wa mradi wa udhibiti wa wadudu Nzi waharibifu wa matunda Pemba Fatma Nassor Sharif amesema   wizara inategemea kugawa mitego hiyo katika shehi ya zote za Pemba mara tu vitakapofika vifaa vyengine Ili kuondoa kabisa tatizo Hilo . Sheha wa shehia ya ole amewanasihi wakulima wa matunda uongeza umakini pamoja  kuzitumia dawa hizo ipasavyo Ili kutimiza lengo la serekali la kuhakikisha wadudu  Nzi waharibifu wanaondoka kabisa . Naao baadhi ya wakulima wameishukuru serekali kupitia mradi wa kudhibiti wadudu Nzi wa matunda kwa kuwapatia dawa  ambazo ndio kimbilio lao . Zaidi ya  Mitego 2090  ya kuulia  wadudu hao  waharibifu...

TAASISI ZA UMMA ZAASWA

Image
Na Amina Ahmed Moh’d  AFISA Mdhamini ofisi ya Rais fedha na mipango Pemba Abdul-wahab Said Abubakar amezitaka taasisi za umma kuhakikisha  zinatayarisha nyaraka zote za watumishi wanaotarajiwa kustaafu ili waweze kupata haki zao kwa haraka kupitia mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF.  Aliyasema hayo alipokuwa akifungua  mkutano maalumu kwa wastaafu watarajiwa uliofanyika katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Kisiwani Pemba.  Alisema kuwa, wastaafu wanahitaji matayarisho maalumu kwa mujibu  wa utaratibu uliowekwa kisheria ambao utasaidia kupata stahiki zao kwa wakati sahihi mara tu watakapostaafu.  "Sote tunafahamu kwamba watumishi wa umma wameitumikia serikali, na kuchangia kurithisha elimu kwa watumishi wengine sasa ni vizuri stahiki zao ziandaliwe mapema ili kuwasaidia kufikia malengo waliojiwekea baada ya kustaafu", alisema.  Aidha, Mdhamini huyo aliwataka wastaafu hao watarajiwa kuendelea kuwahimiza watumishi wengine katika maeneo...

Zijue Mbinu za Viongozi Wanawake walivyofanikisha maendeleo ya Elimu na udhibiti wa utoro kwa wanafunzi skuli za Msingi Na kupelekea kupata Mafanikio Bora katika ufaulu. .

Image
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba.   MIKAKATI  ya kudhibiti utoro skuli za msingi wilaya ya Micheweni imepelekea kuwepo kwa ufaulu mzuri miaka 4 Mfululizo  Zanzibar  ni kutokana na viongozi wa wilaya kufanya kazi kwa kushirikiana vyema na jamii .  Wilaya Ya Micheweni  ipo katika Mkoa wa kaskazini ndani ya kisiwa cha  pemba ambayo ni moja kati ya wilaya kumi za Zanzibar .   Micheweni inaongoza kwa matokeo  ya darasa la nne Zanzibar sambamba na kuvuuka lengo  liliowekwa na wizara ya Elimu  juu ya kudhibiti tatizo la  utoro na kuwarejesha skuli wanafunzi wa skuli za msingi waliotoroka.   "Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu".  Msemo huu umejidhihirisha mara  Mgeni khatib Yahya kuendeleza mikakati hiyo ni  pamoja na  kukemea   sherehe za mikusanyiko, ajira za watoto kuelimisha jamii  juu  ya umuhimu wa elimu jambo limefanikiwa kuwa bora matokeo  ya kitaifa . ...