Wizara ya kilimo yahidi neema wadudu wanaothiti mazao.

NA  FATMA SLEIMAN. 

WIZARA ya kilimo maliasili mifugo na uvuvi imedhamiria kuondoa changamoto ya wadudu Nzi wa matunda kwa wakulima Ili waweze kujiingizia kipato kulingana na ukulima wao na kuondokana na umaskini .

Akizungumza mara baada ya zoezi la ugawaji wa dawa hizo kwa wakulima   Kaimu Afisa msaidizi wa mradi wa udhibiti wa wadudu Nzi waharibifu wa matunda Pemba Fatma Nassor Sharif amesema   wizara inategemea kugawa mitego hiyo katika shehi ya zote za Pemba mara tu vitakapofika vifaa vyengine Ili kuondoa kabisa tatizo Hilo .

Sheha wa shehia ya ole amewanasihi wakulima wa matunda uongeza umakini pamoja  kuzitumia dawa hizo ipasavyo Ili kutimiza lengo la serekali la kuhakikisha wadudu  Nzi waharibifu wanaondoka kabisa .

Naao baadhi ya wakulima wameishukuru serekali kupitia mradi wa kudhibiti wadudu Nzi wa matunda kwa kuwapatia dawa  ambazo ndio kimbilio lao .

Zaidi ya  Mitego 2090  ya kuulia  wadudu hao  waharibifu wa matunda , imesambazwa kisiwani Pemba   katika shehiya zote 36 za Wilaya yw  Mkoani na shehiya 3 za  Wilaya ya chake chake.
Mwisho 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI